Hukumu ya Talaka kabla ya kufanya jimai
Talaka Kabla ya Jimai:Mwanamume au mwanamke anaweza kughairi na kuamua kuvunja ndoa mapema kabla ya kufanya tendo Ia ndoa.
Talaka Kabla ya Jimai:
Mwanamume au mwanamke anaweza kughairi na kuamua kuvunja ndoa mapema kabla ya kufanya tendo Ia ndoa. Mwanamume atatoa talaka na mkewe ataachika hapo hapo bila ya kukaa eda. Kama mwanamume ameshatoa mahari hatadai chochote kama yeye ndiye aliyeamua kumuacha mkewe bali atalazimika kumpa kiliwazo (kitoka nyumba). Ikiwa hajatoa mahari atalazimika kutoa nusu ya mahari. Kama mke ndiye aliyedai talaka atalazimika kumrudishia mumewe mahari aliyompa. Hukumu ya talaka ya ama hii inabainika katika aya zifuatazo:
Si dhambi kwenu kama mkiwapa wanawake talaka ambao hamjawagusa au kuwabainishia mahari (yao). Lakini wapeni cha kuwaliwaza (kitoka nyumba); mwenye wasaa kadiri awezavyo, na mwenye dhiki kadiri awezavyo. Matumizi hayo (wanayopewa) yawe kama inavyosema Sharia. Ndio wajibu kwa wafanyao mema. (2:236)
Na kama mkiwapa talaka kabla ya kuwagusa na mmekwisha wawekea hayo mahari (basi (wapeni) nusu ya hayo mahari mliyoagana, isipokuwa wanawake wenyewe waache (wasitake kitu), au yule (mume) ambaye kifungo cha ndoa ki mikononi mwake aache (haki yake kwa kumpa mahari kamili). Na kuachiana ndiyo kunakomkurubisha mtu sana na kumcha Mungu. Wala msisahau kufanyiana ihsani baina yenu; hakika Mwenyezi Mungu anayaona yote mnayoyafanya. (2:237)
Talaka ya Aliyerukwa na akili na aliyetenzwa nguvu
Talaka si jambo Ia kulifanyia maskhara Muislamu anatakiwa awe hadhiri wakati wa kutoa talaka. Ahakikishe kuwa wakati anaamua kutoa talaka akili yake iko katika hali ya utulivu. Talaka ya aliyerukwa na akili haiswihi kama tunavyojifunza katika Hadith:
Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Kila talaka ni halali isipokuwa talaka ya punguani na mwenye kurukwa na akili". (Tirmidh).
Pia mtu akilazimishwa kutoa talaka pasina sababu za kisheria au mume na mke wakitalakishwa kwa nguvu huku bado wanapendana katika mipaka ya Allah (s.w), talaka hiyo haitaswihi kama tunavyojifunza katika Hadithi:
Aysha (r.a) ameeleza kuwa amemsikia Mtume wa Allah akisema: "Hakuna talaka wala hakuna kumwacha huru mtumwa kwa nguvu ". (Tirmidh).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Dua za Mitume na Manabii ๐2 ai web app ๐3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina ๐4 Kitau cha Fiqh ๐5 Madrasa kiganjani ๐6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Hatua za kinga za ugumba na Utasa.
Ugumba ni รขโฌลugonjwa wa mfumo wa uzazi unaofafanuliwa kwa kushindwa kupata ujauzito baada ya miezi 12 au zaidi ya kujamiiana bila kinga mara kwa mara. Utasaรย kutoweza kwa kiumbe hai kufanya uzazi wa ngono au kutoweza kupata mimba au kuchangia mimba.
Soma Zaidi...Taratibi za malezi ya watoto wadogo baada ya talaka katika uislamu
Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?
Soma Zaidi...Jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi.
Soma Zaidi...Taratibu za kutaliki katika uislamu.
Hapa utajifunza taratibu zinazofuatwa wakati wa kukusudia kumuacha mke. Pia utajifunza sababu za kiwepo kwa eda baada ya kuachwa mwanamke.
Soma Zaidi...Kumkafini (kumvisha sanda maiti)
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...