Mifumo ya benki ya kiislamu.


image


Hapa utajifunza njia ambazo nenk ya kiislamu hutumia ili kujiendesha


Benki za Kiislamu
Benki za Kiislamu ambazo hutoa huduma kama benki nyingine zinaendeshwa katika msingi wa biashara na sio ule wa riba. Benki za Kiislamu badala ya kukopesha kwa riba, hutumia rasilimali zake kwa zenyewe kujihusisha katika uzalishaji kwa kufuata misingi inayokubalika katika Uislamu. Miongoni mwa misingi inayokubalika kwa Muislamu au Benki ya Kiislamu kuingiza fedha zake katika miradi ya biashara au uzalishaji ni hii ifuatayo:

 

(i)Mudharabah
Mudharabah ni makubaliano kati ya watu wawili au zaidi ambapo mmoja au zaidi kati ya hao anatoa mtaji na mwingine hushiriki kwa ukamilifu katika kuendesha na kuongoza mradi wa uchumi. Faida itakayopatikana katika mradi huo itagawanywa kulingana na makubaliano yao. Hasara itakayotokana na mradi huo itakuwa ni ya mwenye kutoa mtaji. Wengine hawatoi chochote kusaidia hasara kwa sababu wameshatoa mchango wao wa hasara hiyo kwa jasho walilolitoa katika shughuli ambayo haikuzaa matunda bali hasara.

 


Benki za Kiislamu zinaingiza fedha zake katika miradi ya uchumi kwa njia hii ya Mudharabah ambapo benki hutoa mtaji kwa ajili ya miradi mbali mbali ya uchumi kwa mapatano ya kupata kiasi (asilimia) fulani cha faida itakayopatikana na kuwa tayari kulipa hasara itakayopatikan a.

 

(ii)Musharikah
Musharikah ni ushiriki kati ya watu wawili ambapo, tofauti na Mudharabah wote wawili wanachangia mtaji na kushiriki katika uendeshaji wa shughuli ya kiuchumi, lakini si lazima watoe hisa sawa sawa, kwa makubaliano ya kugawana faida na hasara kulingana na kiasi cha hisa alichotoa kila mmoja wao. Kwa mtindo huu wa “Musharikah” Benki ya Kiislamu inaingia katika kuchangia mtaji, kuendesha na kusimamia mradi wa uchumi na watagawana (faida au hasara) kulingana na kiasi cha mtaji kila mmoja alichotoa.

 


(iii)Ijara-Uara wa Iktina
Huu ni utaratibu mwingine unaokubalika kisheria ambapo mtu au benki inatumia fedha zake katika kukodi vitu kama vile magari, majumba, ardhi, na kadhalika, ambavyo vikifanyiwa kazi huzalisha mali na kutoa faida. Benki za Kiislamu hujipatia faida kubwa kutokana na mtindo huu.

 


(iv)Murabah
Huu ni utaratibu unaotumiwa katika kununua bidhaa kwa wingi kwa ajili ya kuwauzia wafanya biashara ambao waliofikiana kuwa bidhaa hizo zinunuliwe kwa ajili yao. Benki kutokana na uwezo wake inapanga na wafanya biashara kuwa inunue bidhaa nyingi kutoka ndani na nje ya nchi kwa jina lake kisha iwauzie wafanyabiashara hao kwa bei itakayoipatia benki faida. Pia benki kwa mtindo huu inaweza kununua mazao ya wakulima na kuyauza kwa walaji kwa faida.

 


(v)Muqaradha
Mtindo huu wa Muqaradha humruhusu mtu au benki kununua “share” au “bonds” katika kampuni ya uzalishaji kwa mapatano ya kugawana faida au hasara kulingana na kiasi cha “share”.

 

Kwa kufuata mitindo hii katika kuingiza fedha zake katika miradi ya uchumi, Benki za Kiislamu hupata faida kubwa hata zaidi ya kipato cha riba kinachopatikana katika benki za riba. Benki za Kiislamu nazo hugawa faida inayopatikana kwa wateja wake walioweka fedha zao kwenye benki.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Nini kifanyike baada ya mazishi ya kiislamu
Huu ni utaratibu unaotakiwa kufanyika baada ya kuzika. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf Soma Zaidi...

image Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume. Soma Zaidi...

image Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii
Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake? Soma Zaidi...

image mambo yanayofungua swaumu
post hii ijakwenda kukufundisha mambo yanayoharibu funga Soma Zaidi...

image Nguzo za swaumu (kufinga)
Hapa utajifunza nguzo kuu za swaumu. Kama hazitatimia nguzo hizi basi swaumu itakuwa ni batili. Soma Zaidi...

image Hadathi ya kati na kati
Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati. Soma Zaidi...

image Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja
Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja. Soma Zaidi...

image Sifa za imamu wa swala ya jamaa
Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii. Soma Zaidi...

image Swala ya jamaa na taratibu zake
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya jamaa na taratibu zake. Soma Zaidi...