Haki na Hadhi za Mwanamke katika jamii za mashariki: China, India na Japani hapo zamani

2.

Haki na Hadhi za Mwanamke katika jamii za mashariki: China, India na Japani hapo zamani

2. JAMII ZA MASHARIKI



Kila jamii utakayoichunguza utakuta kunyanyaswa na kudhalilishwa kwa mwanamke kuko pale pale. Ukichunguza hata zile nchi zilizohesabika katika historia kuwa mbele katika maendeleo ya mwanaadamu kama vile China, India, Iraq na Iran, utasikitishwa na vitimbwi alivyokuwa akifanyiwa mwanamke. Hebu tuanglie baadhi ya jamii chache za nchi za Mashariki.



Uchina
Mwanamke wa Uchina alikuwa hana haki yoyote katika jamii. Hata watoto wake aliowazaa mwenyewe hakuwa na haki nao. Mume wake aliweza kuuza mwili wake kwa mume mwingine. Baada ya mumewe kufariki alirithiwa kama mali na ndugu wa mumewe na haikuwezekana kwake kuolewa tena. Juu ya yote hayo, wanawake waliuzwa na kufanywa watumwa. Mpaka kufikia 1937, Uchina ilikuwa na wasichana watumwa milioni mbili.



Katika kitabu chao kiitwacho, Marriage East and West (New York, 1960) David na Mace wanasema hadhi ya mwanamke huko Uchina ilikuwa duni sana. Mshairi mashuhuri wa China aliyeitwa Xuan,(100B.C) aliandika katika shairi moja:



Ni huzuni ilioje kuwa mwanamke Duniani hakuna kilicho duni Duniani hakuna kilicho duni kuliko mwanamke.
Mwana falsafa wao mkubwa, Bwana Confusious ambaye alikuwa pia kiongozi wa kidini aliwafundisha watu kuwa wajibu mkuu wa mwanamke ni utii. Akiwa mototo amtii baba yake, akiolewa amtii mumewe na akifiwa na mumewe basi amtii mwanawe wa kiume. Na atii kila kitu bila kuhoji. Wachina pia waliamini kuwa mtu akipata mtoto wa kiume amepata hidaya kutoka kwa Mwenyezi Mungu lakini akipata binti, basi ni nuksi.



India
Katika jamii ya India mwanamke hakuthaminiwa kabisa. Mwanamke alihesabiwa kama mashine ya uzazi. Iwapo mwanamke hakujaaliwa kupata mtoto wa kiume kwa mume aliyemuoa, alilazimishwa azini na mume asiyemjua iii apate mtoto wa kiume.



Budha, kiongozi wa kidini huko India aliwafundisha wafuasi wake kuwa mwanamke ni kiumbe duni aliyejawa na dhambi. Hakuna kiumbe anayefaa kuhofiwa na kuepukwa kama mwanamke. Na kwa mujibu wa sheria ya Manu wa huko huko India, wanawake ni lazima wabanwe na kudhibitiwa vikali kwani wao ndio chanzo cha madhambi yote na ufisadi.



Mwanamke hakuna na haki ya urithi bali urithi ulikuwa ni haki ya watoto wa kiume tu. Mke alitakiwa amwite mume wake ama Bwana wangu au Mungu wangu kwani mume alihesabiwa kuwa ni mungu wake hapa duniani. Ilikuwa marufuku mke kula pamoja na mumewe. Jimai hata kati ya mtu na mkewe ilihesabika kuwa ni kitu kiovu na kichafu. Mke mwema alikuwa yule ambaye akili zake, kauli yake na mwili wake si huru. Mke hakuruhusiwa kuolewa tena pindi mumewe akifariki. Ilibidi afanye moja katika mawili, ama ajichome moto ili afe na kumfuata mumewe au awe mtumishi wa shemeji zake hadi atakapo fariki. Mwenendo huu wa kujichoma moto au kuchomwa moto na mashemeji zake bado unaendelea hadi leo. Gazeti liitwalo "The Economist" 27 August - 2 September 1983 liliandika hivi:



The grisly practice of wife burning in India shows no sign of succumbing on its own to modern ideas about the value of a womans ' life. Many women are donsed with kerosene and set aflame by in-laws greedy for more dowries... The official figures shows 610 burnings in 1982.



Tafsiri:
Mwenendo wa kutisha wa kuwachoma moto wanawake huko India hauonyeshi dalili za kukoma kutokana na fikra za kisasa juu ya thamani ya uhai wa mwanamke. Wanawake wengi humwagiwa mafuta ya taa na kuchomwa moto na mashemeji kwa uroho wa kutafuta mahari nyingine. Taarifa rasmi ya serikali yaonyesha kuwa wanawake 610 walichomwa moto mwaka 1982. Hali ilikuwa hivyo hivyo huko Japan.




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 99

Post zifazofanana:-

VOCABULARY TEXT 05
learn English Vocabulary Soma Zaidi...

ENGLISH TENSES
Soma Zaidi...

ITAMBUE SARATANI CHANZO CHAKE, DALILI NA KUKABILIANA NAYO
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

Harun(a.s), Achaguliwa Kuwa Msaidizi Musa(a.s) na kumkabili (kumlingania) firauni
Nabii Musa(a. Soma Zaidi...

Historia ya kujengwa kwa Alkabah (Maka)
Kama tulivyoona katika maisha ya Mtume Ibrahim(a. Soma Zaidi...

Fangasi watambulikao kama invasive candidiasis
Hawa huweza kuingia kwenye mfumo wa damu na kuenda maeneo mengine nyeti sana ya mwili. Soma Zaidi...

HUKUMU ZA KUSOMA QURAN, HUKUMU ZA TAJWID, HUKUMU ZA NUN SAKINA, MIM SAKINA, QLQALA NA IQLAB, TANWIN NA MADA
Soma Zaidi...

darasa la lishe
Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe Soma Zaidi...

MUDA WA KUCHAJI SIMU YAKO AMA MUDA WA KUCHAJI BETRI YAKO
Wwatu wengi wamekuwa wakijiuliza ni muda gani hasa inapasa kuchaji simu, je nisubiri mpaka chaji iishe kabisa, ama nichaji ikiwa na asilimia ngap? Soma Zaidi...

Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.
Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah. Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA
SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i'rab ( '). Soma Zaidi...

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Munaafiqun
Wanapokujia wanafiki, husema: "Tunashuhudia ya kuwa kwa yakini wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Soma Zaidi...