Hadhi na haki za Mwanamke katika jamii za Mashariki ya Kati bara la arabu hapo zamani

Hadhi na haki za Mwanamke katika jamii za Mashariki ya Kati bara la arabu hapo zamani

Hadhi na haki za Mwanamke katika jamii za Mashariki ya Kati bara la arabu hapo zamani

(c) Mashariki ya kati



Uarabuni kabla ya Ujumbe wa Mtume Muhammad (s.a.w) mwanamke alionekana kitu duni na nuksi kwa jamii. Baba akipewa habari ya kuzaliwa mtoto wa kike alijinyonga nyonga na kuhuzunika sana. Wanaume walikuwa wakitafuta kila njia ya kujiokoa na aibu hiyo ya kupata mtoto wa kike. Ilikuwa kuchagua moja katika njia mbili: Ama amzike binti huyo mzima mzima akiwa hai au aendelee kuishi maisha ya aibu na fedheha kwa kumbakisha hai.


Mara nyingine wanaume walikuwa wakiwalazimisha wake zao wanapoanza mwezi wa tisa wa ujauzito wa kuchimba shimo uvungni mwa kitanda. Shimo likiwa tayari mume anamuagiza mkewe: "Ukimzaa mtoto mwanake basi haraka sana mfukie mwenyewe katika shimo hii kabla sijaja." Qur'an inatufahamisha tabia ya Waarabu dhidi ya watoto wa kike katika aya zifuatazo:


Na mmoja wao anapopewa habari ya (kuzaliwa) mtoto wa kike, husawajika uso wake, akajaa sikitiko (akawa) anajflcha na watu kwa sababu ya ha bar mbaya ile aliyoambiwa (anafanya shauri) Je, akae nayejuu yafedheha hiyo au amfukie udongoni (akiwa hai). Sikilizeni! Ni mbaya mno hukumu yao hiyo. (1 6:58-59).



Wanawake baada ya kufiwa na waume zao, walirithiwa na wanawe wa kambo au shemeji zao. Walikuwa hawaruhusiwi kuolewa tena. Qur'an inakataza tabia hii kama ifuatavyo:


Enyi mlioamini! Si halali kwenu kurithi wanawake kwa jeuri. Wala msiwazuie (kuolewa na wanaume wengine) iii mpate kuwanyang 'anya baadhiya vile mlivyo wapa... (4:19).




                   


Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views: 1360

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu

KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S.

Soma Zaidi...
Watu waliovunja amri ya kuheshimu siku ya Jumamosi.

Katika zama za kale Mayahudi walikatazwa kufanya kazi siku ya Jumamosi.

Soma Zaidi...
MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KULELEWA NA BABA YAKE MDOGO MTUME (ABU TALIB)

KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake.

Soma Zaidi...