Hadhi na haki za Mwanamke katika jamii za Mashariki ya Kati bara la arabu hapo zamani
(c) Mashariki ya kati
Uarabuni kabla ya Ujumbe wa Mtume Muhammad (s.a.w) mwanamke alionekana kitu duni na nuksi kwa jamii. Baba akipewa habari ya kuzaliwa mtoto wa kike alijinyonga nyonga na kuhuzunika sana. Wanaume walikuwa wakitafuta kila njia ya kujiokoa na aibu hiyo ya kupata mtoto wa kike. Ilikuwa kuchagua moja katika njia mbili: Ama amzike binti huyo mzima mzima akiwa hai au aendelee kuishi maisha ya aibu na fedheha kwa kumbakisha hai.
Mara nyingine wanaume walikuwa wakiwalazimisha wake zao wanapoanza mwezi wa tisa wa ujauzito wa kuchimba shimo uvungni mwa kitanda. Shimo likiwa tayari mume anamuagiza mkewe: "Ukimzaa mtoto mwanake basi haraka sana mfukie mwenyewe katika shimo hii kabla sijaja." Qur'an inatufahamisha tabia ya Waarabu dhidi ya watoto wa kike katika aya zifuatazo:
Na mmoja wao anapopewa habari ya (kuzaliwa) mtoto wa kike, husawajika uso wake, akajaa sikitiko (akawa) anajflcha na watu kwa sababu ya ha bar mbaya ile aliyoambiwa (anafanya shauri) Je, akae nayejuu yafedheha hiyo au amfukie udongoni (akiwa hai). Sikilizeni! Ni mbaya mno hukumu yao hiyo. (1 6:58-59).
Wanawake baada ya kufiwa na waume zao, walirithiwa na wanawe wa kambo au shemeji zao. Walikuwa hawaruhusiwi kuolewa tena. Qur'an inakataza tabia hii kama ifuatavyo:
Enyi mlioamini! Si halali kwenu kurithi wanawake kwa jeuri. Wala msiwazuie (kuolewa na wanaume wengine) iii mpate kuwanyang 'anya baadhiya vile mlivyo wapa... (4:19).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 ai web app π2 kitabu cha Simulizi π3 web hosting π4 Kitabu cha Afya π5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Kuendeshwa kwa dola ya kiislamu, Uchumi, ulinzi, haki na sheria, siasa na vikao vya shura
Uendeshaji wa Dola ya Kiislamu Madinah.
Soma Zaidi...Uchaguzi wa Omar (Umar) kuwa khalifa wa Pili baada ya Mtume
Uchaguzi wa βUmar bin Khattab kuwa Khalifa wa Pili.
Soma Zaidi...