Faida za tangawizi
Somo Hili linakwenda kukuletea faida za tangawizi
FAIDA ZA TANGAIZI
Tangaizi ni katika mimea yenye asili na bara la asia hususan nchi ya China. Mmea huu hutambulika kwa faida zake za kitiba toka zamani sana. Na karibia dunia nzima hutumia tangaizi kama tiba na kama kinywaji. Ndani ya tangaizi kuna chembechembe ziitwazo gingerol, hizi ndizo huipa tangaizi uwezo wake wa kitiba.
Unaweza kutumia tangaizi kwa kutafuna vipande vidogovidogo au kwa kutia kwenye mboga. Pia unaweza kuweka kwenye chai ikiwa vipande vidogo au ikiwa imekauchwa na kusagwa kama ungaunga. Zipo njia nyingi za kutumia tangaizi. Zifuatazo ni katika baadhi ya faida za tangaizi iafya:-
1. Tangaizi ni mujarabu sana katika kutibu kichefuchefu. Hususani kichefuchefu cha mimba. Kwa ujumla kichefuchefu huwapata sana wajawazito, na watu walofanyiwa upasuaji wa ndani. Lakini kinaweza kumpata mtu yeyote. Unaweza kutumia tangaizi kwenye chai, ama kutafuna vipande vidogo. Hakikisha unakula japo gram moja.
2. Hupunguza maumivu ya misuli
3. Hupunguza maumivu ya viungo
4. Husaidia katika kushusha kiwango cha sukari. Hususan kwa wenye kisukari type 2. kwa kufanya hivi pia hupunguza athari ya kupata maradhi ya moyo
5. Husaidia kwa wenye tatizo la kutokupata choo na kukosa hamu ya kula.
6. Hupunguza maumivu ya tumbo la chango kwa wanawake.
7. Hupunguza hatari ya kupata ugonjwa wa saratani (cancer)
8. Huimarisha afya ya ubongo
9. Husaidia katika kuimarisha mfumo wa kinga za mwili.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 web hosting π2 Kitau cha Fiqh π3 Madrasa kiganjani π4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume
Vijuwe vyakula vya kyongeza nguvu za kiume na mambo yanayopunguza nguvu za kiume
Soma Zaidi...Faida za kula limao
Usiwashangae wanaokula lima, kwa hakika kuna faida kubwa kiafya kula limao, je unazijuwa faida hizo
Soma Zaidi...Tufaha (apple)
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula apple/tufaha
Soma Zaidi...VYAKULA VYA VITAMIN NA MAJI
Zitambue aina zote za vyakule na ufanye maamuzi yaliyo kuwa sahihi katika uandaaji wa chakula chako
Soma Zaidi...Vyakula bora kwa ajili ya afya ya macho.
βMacho ni moja ya viungo muhimu zaidi vinavyokuunganisha na ulimwengu, lakini mara nyingi tunayasahau hadi pale tunapoanza kupata changamoto za kuona. Kama ilivyo viungo vingine, macho yanahitaji virutubisho maalum ili yasibadilike ubora kadiri umri unavyosonga mbele. Makala haya yanakupa orodha ya vyakula bora unayoweza kuingiza kwenye sahani yako leo ili kuimarisha uwezo wako wa kuona
Soma Zaidi...