Viraa saba na herufi saba katika usomaji wa quran

Ni zipi hizo herufi saba, na ni vipi viraa saba katika usomaji wa Quran

Viraa saba na herufi saba.
Wataalamu wa tajwid wanaeleza kuhusu herufi saba za usomaji wa qurani. Itambulike kuwa qurani imeshuka kwa lugha ya kiarabu. Na pia itambulike kuwa waarabu wenyewe walitofautiana katika lahaja za lugha ya kiarabu. Lahaja hizi zilikuwa katika makabila saba ya kiarabu yaliyopo maka. Yaani ni kuwa waarabu walikuwa na makabila saba wakati ule. Na makabila haya ijapokuwa yalizungumza kiarabu lakini walikuwa wakitofautiana katika maneno, utamkaji na hata uandishi. Hivyo lahaja hizi zilijulikana kama herufi saba (za usomaji wa qurani).



Hivyo lahaja saba hizi ndizo chanzo za hizi herufi saba. Na hili linathibitika katika maneno ya Mtume (s.a.w) aliposema: ((Jibriyl alinisomea kwa herufi moja, nikaifanyia marudio mpaka akanifundisha nyingine, nikaendelea kumuomba nyinginezo mpaka mwishowe zikawa herufi (lahaja) saba)) (Bukhari na Ahmad).



Makabila haya yalikuwa Quraysh, Hudhayl, Thaqiyf, Hawaazin, Kinaanah, Tamiym na Yeman. Hivyo qurani ilishuka katika lahaja saba kulingana na makabila. Hivyo ikawa kila kabila linasoma qurani kwa namna ambavyo lahaja yao inawafanya waelewe. Wakawa watu wanaandika qurani kwa namna ambavyo wanaelewa wao. Kulingana na lahaja ya kabila lao. Hali hii ilifanya usomaji wa qurani utofautiaane. Mifano; “’alayhim” wengineo walitamka “’alayhimuw”, neno la “swiraatw” walitamka wengineo “zwiraatw” na wengine “siraatw”, “muumin” wengineo walitamka “muwmin” 



Amesimulia ‘Umar Ibn Al-khatab kuwa: “Nilimsikia Hishaam ibn Hakiym akisoma Suwratul-Furqaan tofuati na vile ninavyoisoma na alivyonifundisha Mtume ( ' ' ' ' B). Nilikaribia kumsimamisha (asiswalishe) lakini nikamvumilia mpaka akamaliza kisha nikamshika nguo yake shingoni na kumvuta mpaka kwa Mtume ' ' ' ') B) nikasema: “Nimesikia huyu mtu akisoma (Suwratul- Furqaan) kinyume na ulivyonifundisha”. Mtume ( ' ' ' ' B) akasema: ((Mwachie!)) Akamwambia (Hishaam): ((Soma)). Akasoma. Akasema ((Hivi ndivyo ilivyoteremshwa)). Kisha akaniambia mimi: ((Soma)). Nikasoma. Akasema: ((Hivi ndivyo ilivyoteremshwa. Hakika Qur-aan imeteremshwa kwa herufi saba, hivyo someni iliyokuwa sahali kwenu)



Uislamu ulipoenea zaidi ikawepo haja ya kuiandika qurani katika lahaja moja ambayo itasomwa. Na hii ni kutokana na kuwepo makosa katika usomaji wa qurani. Hivyo katika utawala Kikundi cha Maswahaba, kilichoongozwa na Hudhayfah bin al-Yamaaniy ambaye alikuwa Iraq, kilikuja kwa ‘Uthmaan ( ' ' ' ) na wakamsihi "auokoe ummah wa Kiislamu kabla haujatofautiana juu ya Quraan." ‘Uthmaan ( ' ' ' ) akaamrisha chini ya uongozi wa Zayd bin Thaabit ' ' ') ) nakala za Qur-aan ziandikwe na nakala zote zisizo rasmi zichomwe moto.

 

Lahaja iliyotumika kuandika Qur-aan ni ile ya ki-Quraysh na Msahafu ukajulikana kuwa ni ‘Msahafu wa ‘Uthmaan’. Nakala hizo zilisambazwa miji mikuu ya Waislamu zikiwa kama nuskhah (kopi) rasmi. Na nuskhah ya asili ikabakishwa kwa Mama wa Waumini Hafswah ( ' ' ' ). Alimwacha Zayd bin Thaabit Madiynah, ‘Abdullaah bin Swaa’ib alitumwa Makkah,Mughiyrah bin Shu’bah alitumwa Syria, Abu ‘Abdir-Rahmaan As-Sulamy alitumwa Kuwfah, ‘Aamir bin ‘Abdil-Qays alitumwa Baswrah. (www.al-hidaayah.com)



Baada ya msahafu huu kusambazwa katika dola ya kiislamu lahaja zote ambazo siorasmi zilipotea. Msahafu huu ndio chimbuko la misahafu tulionayo leo. Ijapokuwa kuna tofauti kubwa za kiuandishi kati ya misahafu ya leo na msahafu huu. Kwa m fano msahafu huu haukuwa na dot kwenye herufi za dot au irabu pia hazikuwepo. Hayo yato yalifanyika baadaye kadiri uislamu ulipoenea maeneo mbalimbali ya dunia na ikaonekana ugumu wa kutumia msahafu ule kwa watu wasiokuwa waarabu.


Viraa saba.
Viraa hivi saba ndivyo ambavyo vimetokana na lahaja ya kikurayshi ambayo ndio msahafu wa ‘Uthmani umeandikiwa. Viraa hivi wataalamu wa elimu ya tajwid wamevizungumzia katika vitabu vya elimu hii.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/10/20/Thursday - 10:09:56 am     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1521

Post zifazofanana:-

Samahani nauliza mjamzito akiwa na presha140/90 Kuna madhara?
Presha ya kupanda hypertension huweza kuzumbuwa watu kwa jinsia zote, na umri wote. Wajawazito pia wamekuwa wakisumbuliwa na presha hii mara kwa mara. Soma Zaidi...

Madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye mifupa.
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye mifupa,ni madhara ambayo utokea endapo Maambukizi kwenye mifupa yasipotibiwa kwa mda wake. Soma Zaidi...

Umuhimu wa kuvaa nguo za upasuaji.
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa nguo za upasuaji, tunajua wazi kuwa, wakati wa upasuaji tunapaswa kusafisha chumba na mazingira yake lengo ni kuhakikisha kuwa tunazuia wadudu wasisambae au kuingia kwenye mwili wa binadamu. Soma Zaidi...

Namna ya kuishi na vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuishi na vidonda vya tumbo Soma Zaidi...

Maana ya uislamu.
Kwenye kipengele hichi titajifunza maana ya uislamu,na maana nyingine tofauti. Soma Zaidi...

Jinsi ya kushusha homoni za kiume.
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza homoni za kiume kwa akina dada. Soma Zaidi...

Vipimo vya VVU
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vipimo mbalimbali vinavyotumika kupima VVU Soma Zaidi...

Madhara ya Tiba kemikali kwa wagonjwa wa saratani
Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba kemikali, ni madhara yanayotokea kwa wagonjwa wa saratani, madhara haya yanayoweza kuwa ni kwa Sababu mbalimbali kama vile kuaribika kwa seli zinazoendelea kufanya kazi kwenye mwili. Soma Zaidi...

Changamoto kubwa za tendo la ndoa kwa wanaume
Posti hii inahusu zaidi changamoto ya tendo la ndoa kwa wanaume,wanaume wamekuwa wakipata changamoto ya tendo la ndoa na kuwafanya kushindwa kujiamini na kukosa kabisa raha kwenye maisha yao Soma Zaidi...

Athari za kutokutibu minyoo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya athari zinazoweza kutokea endapo minyoo haitotibiwa Soma Zaidi...

Madhara ya kutoka kwa mimba
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutoka kwa mimba, kwa kawaida tunafahamu kwamba mimba ikitungwa na mwili mzima huwa na wajibu wa kutunza kilichotungwa kwa hiyo ikitokea mimba ikatoka usababisha madhara yafuatayo. Soma Zaidi...

Halow samahan dokta nmekuwa nikiumwa tumbo muda mwingi takriban wiki ya 3 halipon naharisha kuna muda nikila chakula hata kama kdogo tu maumivu makali,je nifanyaje msaada
Mvurugiko katika mfumo wa chakula mwilinivunaweza kusababisha maumivu ya tumbo, kuharisha, kutapika na kuchoka pia. Lakini zipo sababu nyingine kama kuwana ujauzito. Nini ufanye endapo unasumbuliwana hali hii Soma Zaidi...