Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za ukwaju
. Faida za ukwaju (Tamarind)
Ukwajju ni katika mimea ambayo matunda yake yanatumika katika kutengenezea madawa ya hospitali. Kinywaji cha ukwaju hutumika katika kutibu kuharisha, kukosa choo, homa na aina za vidonda vya tumbo. Tofauti na matunda pia majani na maganda ya mti huu pia hutumika katika kutibu vidonda. Wataalamu wa afya bado wanaendelea kuuchunguza mti huu kwa ajili ya kupata tiba zaidi.
Antioxidant ambayo ipo kwenye ukwaju husaidia katika kudhibiti na kulinda mwili dhidi ya maradhi ya moyo, saratani na kisukari. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa ukwaju husaidia katika kushusha kiwango cha sukari kwenye damu. Pia kwa watu wenye kutaka kupunguza uzito, ukwaju pia husaidia.
Ukwaju una virutubisho vingi sana kama vile:- madini ya magnesium, potassium, chuma, calcium na phosphorous. Pia kuna vitamin B1 (thiamin), vitamin B2 (riboflavin), vitamin B3 (niacin). pia kuna vitamin C, k na B6 na B5. kwa ufupi ukwaju ni katika matunda ya asili yalotumiwa na watu toka zamani sana.
Katika ukwaju kuna polyphenols kama vile flavonoids ambayo husaidia katika kudhibiti kiwango cha cholesterol na triglycerides. Antioxidant zilizomo kwenye tunda hili husaidia katika kulinda mwili dhidi ya maradhi ya moyo. Pia ukwaju husaidia katika kutengeneza dawa za malaria.
Tafiti za kisayansi zinaonesha kuwa ukwaju husaidia katika kupunguza uzito. Itambulike kuwa kuzidi uzito mwilini kunahusianishwa sana na maradhi ya moyo, ini, na figo. Hivyo ukwaju husaidia katika kupunguza choloesterol mbaya (LDL) na husaidia katika kuongeza cholesterol nzuri (HDL).
Ukwaju una potassium bitartipate ambayo hii husaidia katika upatikanaji wa choo na kuzuia kuganda kwa choo. Mizizi na maganda ya mkwaju husaidia sana kwa maumivu ya tumbo. Uw.epo wa procyanidins kwenye ukwaju husaidia katika kulinda ini dhidi ya uharibifu. Pia ukwaju hutumika katika kutibu along’atwa na nyoka
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula nanasi
Soma Zaidi...Kuna faida kubwa za kiafya kwa kula ndizi, soma makala hii mpaka mwisho
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna nzuri ya kuandaa mchai chai kwa ajili ya matumizi mbalimbali, Ili kutumia mmea wa mchai chai zifuatazo ni mbinu za kuandaa mmea huu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi juu ya madini ya zinki na faida zake katika mwili wa binadamu,
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Ukosefu wa madini ya Shaba mwilini, ni Ukosefu wa madini ya Shaba mwilini ambao usababisha madhara kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Posti hii itakwende kukueleza kuhusu faida za kula apple na umuhimu wake kiafya
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida za majani ya mstafeli,ni majani ambayo utibu magonjwa mbalimbali hasa saratani, kwa hiyo tunapaswa kuyatumia ili tuweze kupata matibabu ya kansa mbalimbali.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu upungufu wa protini na dalili zake
Soma Zaidi...