Home Afya Shule ICT Burudani Dini Maktaba Maswali Madrasa Apps Blog Legacy Login

FAIDA ZA UKWAJU (TAMARIND)


image


Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za ukwaju


. Faida za ukwaju (Tamarind)

Ukwajju ni katika mimea ambayo matunda yake yanatumika katika kutengenezea madawa ya hospitali. Kinywaji cha ukwaju hutumika katika kutibu kuharisha, kukosa choo, homa na aina za vidonda vya tumbo. Tofauti na matunda pia majani na maganda ya mti huu pia hutumika katika kutibu vidonda. Wataalamu wa afya bado wanaendelea kuuchunguza mti huu kwa ajili ya kupata tiba zaidi.

 

Antioxidant ambayo ipo kwenye ukwaju husaidia katika kudhibiti na kulinda mwili dhidi ya maradhi ya moyo, saratani na kisukari. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa ukwaju husaidia katika kushusha kiwango cha sukari kwenye damu. Pia kwa watu wenye kutaka kupunguza uzito, ukwaju pia husaidia.

 

Ukwaju una virutubisho vingi sana kama vile:- madini ya magnesium, potassium, chuma, calcium na phosphorous. Pia kuna vitamin B1 (thiamin), vitamin B2 (riboflavin), vitamin B3 (niacin). pia kuna vitamin C, k na B6 na B5. kwa ufupi ukwaju ni katika matunda ya asili yalotumiwa na watu toka zamani sana.

 

Katika ukwaju kuna polyphenols kama vile flavonoids ambayo husaidia katika kudhibiti kiwango cha cholesterol na triglycerides. Antioxidant zilizomo kwenye tunda hili husaidia katika kulinda mwili dhidi ya maradhi ya moyo. Pia ukwaju husaidia katika kutengeneza dawa za malaria.

 

Tafiti za kisayansi zinaonesha kuwa ukwaju husaidia katika kupunguza uzito. Itambulike kuwa kuzidi uzito mwilini kunahusianishwa sana na maradhi ya moyo, ini, na figo. Hivyo ukwaju husaidia katika kupunguza choloesterol mbaya (LDL) na husaidia katika kuongeza cholesterol nzuri (HDL).

 

Ukwaju una potassium bitartipate ambayo hii husaidia katika upatikanaji wa choo na kuzuia kuganda kwa choo. Mizizi na maganda ya mkwaju husaidia sana kwa maumivu ya tumbo. Uw.epo wa procyanidins kwenye ukwaju husaidia katika kulinda ini dhidi ya uharibifu. Pia ukwaju hutumika katika kutibu along’atwa na nyoka



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    2 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    3 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    5 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    6 ICT    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS

Imeandikwa na Bongoclass Tags AFYA , Matunda , ALL , Tarehe 2021-10-30     Share On facebook or WhatsApp Topic school Zaidi Dini AFYA ICT Burudani Tags Uzazi maswali Afya mengineyo dini HIV Sira vyakula Matunda HTML php Alif Lela 1 Alif Lela 2 FANGASI Dawa SQL Tips Quran Sunnah fiqh DARSA Magonjwa Tajwid tawhid simulizi Dua Academy Wahenga chemshabongo WAJUWA Michezo ICT Imesomwa mara 1869



Post Nyingine


image Faida za kiafya za stafeli/soursop
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za stafeli ama soursop Soma Zaidi...

image Faida za mbegu za papai
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za mbegu za papai na umuhimu wake kiafya Soma Zaidi...

image Faida za kula stafeli/soursop
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za stafel/soursop Soma Zaidi...

image Faida za kula bamia
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula bamia Soma Zaidi...

image Faida za kiafya za peaz/ peas
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula peazi Soma Zaidi...

image Faida za kiafya za parachichi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula parachichi Soma Zaidi...

image Matunda yenye vitamin C kwa wingi
Somo hili linakwenda kukuletea matunda yenye vitamin C kwa wingi Soma Zaidi...

image Faida za limao au ndimu
Post hii itakwenda kukueleza umuhimu wa limao kiafya Soma Zaidi...

image Faida za pilipili
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za pilipili Soma Zaidi...

image Faida za kiafya za kula bamia
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula bamia Soma Zaidi...