picha

Faida za kula Tango

Matunda ya zamani na ya asili, zijuwe faida za kiafya za tango

Faida za kula Tango

17.Tango (coccumber).
Tango ni katika mimea jamii ya matikiti na maboga. Tango ni katika matunda ambayo unatakiwa uyale sana kwenye maisha yako. Tafiti zinaonesha kuwa asilimia 95 ya tango ni maji. Tango lina vitamin K, B vitamins, copper, potassium, vitamin C, na madini ya manganese.

Tango lina anti-inflammatory flavonol ambayo huitwa fisetin. Hii husaidia katika kuimarisha afya ya ubongo. Hii husaidia katika kutunza kumbukumbu na kuimarisha afya ya mfumo wa fahamu pamoja na neva.

Tafiti zinaonesha kuwa tango lina polyphenols ambazo huitwa lignans (pinoresinol, lariciresinol, and secoisolariciresinol), husaidia katika kuzuia kupata aina mbalimbali za saratani (cancer) kama saratani ya kizazi kwa wanaume na wanawake.

Tango pia lina antioxidant flavonoids, kamavile quercetin, apigenin, luteolin, na kaempferol, ambazo husaidia katika kupambana na maradhi kama saratani na maradhi mengineyo.

Tango hupunguza joto tumboni, pia huondoa bajteria wanaoleta harufu mbaya mdomoni. Tafiti zinathibitisha kuwa tango husaidia katika kuondoa misongo ya mawazo na hii ni kutokana na uwepo wa vitamin B1, vitamin B5, and vitamin B7 (biotin) kwenye tango.

Tango huimarisha afya ya moyo na kupumguza shinikuizo la damu. Tanago husaidia mfumo wa kumeng’enya chakula ufanye kazi kwa ufanisi. Tango husaidia katika kuthibiti uzito wa mwili.


                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Vyakula Main: Post File: Download PDF Views 3510

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰2 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰3 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Faida za kiafya za kula maboga

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula maboga

Soma Zaidi...
Faida za kahawa mwilini.

Posti hii inahusu zaidi faida za kahawa mwilini, ni faida ambazo ujitokeza hasa kwa watumiaji wa kahawa.

Soma Zaidi...
Asili ya vyakula vya madini ya zinki

Post hii inahusu zaidi asili ya madini ya zinki, hii inaonesha sehemu gani tunaaweza kupata madini ya zinki.

Soma Zaidi...
UPUNGUFU WA VITAMIN NA MAJI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...