Matunda ya zamani na ya asili, zijuwe faida za kiafya za tango
17.Tango (coccumber).
Tango ni katika mimea jamii ya matikiti na maboga. Tango ni katika matunda ambayo unatakiwa uyale sana kwenye maisha yako. Tafiti zinaonesha kuwa asilimia 95 ya tango ni maji. Tango lina vitamin K, B vitamins, copper, potassium, vitamin C, na madini ya manganese.
Tango lina anti-inflammatory flavonol ambayo huitwa fisetin. Hii husaidia katika kuimarisha afya ya ubongo. Hii husaidia katika kutunza kumbukumbu na kuimarisha afya ya mfumo wa fahamu pamoja na neva.
Tafiti zinaonesha kuwa tango lina polyphenols ambazo huitwa lignans (pinoresinol, lariciresinol, and secoisolariciresinol), husaidia katika kuzuia kupata aina mbalimbali za saratani (cancer) kama saratani ya kizazi kwa wanaume na wanawake.
Tango pia lina antioxidant flavonoids, kamavile quercetin, apigenin, luteolin, na kaempferol, ambazo husaidia katika kupambana na maradhi kama saratani na maradhi mengineyo.
Tango hupunguza joto tumboni, pia huondoa bajteria wanaoleta harufu mbaya mdomoni. Tafiti zinathibitisha kuwa tango husaidia katika kuondoa misongo ya mawazo na hii ni kutokana na uwepo wa vitamin B1, vitamin B5, and vitamin B7 (biotin) kwenye tango.
Tango huimarisha afya ya moyo na kupumguza shinikuizo la damu. Tanago husaidia mfumo wa kumengβenya chakula ufanye kazi kwa ufanisi. Tango husaidia katika kuthibiti uzito wa mwili.
Umeionaje Makala hii.. ?
Hapa utajifunza sababu za kupatwa na maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Faida za kula tango japokuwa watu wengi hulipuuzia Ila Lina Faida kubwa Sana mwilini.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia maharage kwa wingi, maharage ni aina ya chakula ambacho upatikanaji wake ni rahisi na watu wengi hawajui kwa ulaji wa maharage una faida kubwa sana mwilini kwa hiyo tunapaswa kuangalia faida za maharage kama ifua
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula mihogo
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...