fahamu kuhusu vitamini B na faida zake


image


makala hii inakwenda kukupa faida, kazi na athari za vitamini B mwilini. Nini hutokea endapo utakuwa na upungufu wa vitamini B mwilini?


Fahamu vitamini B na kazi zake, Vyakula vya vitamini B na athari za upungufu wake

Vitamini B ni katika water soluble vitamin ambavyo vina kazi ya kuhakikisha kuwa michakato yote ya kikemikali mwilini inakwenda vizuri. Na hapa tunazungumzia kitaalamu metabolism. vitamini B vipo katika makundi mengi kma aB1, B2, B3, B5, B6, B7 na B12. katika makala hii nitakwenda kukueleza maana ya vitamini hivi, nini kazi zake hasa mwilini, wapi nitapata vitamini B na je ni zipi dalili za upungufu wa vitamini hivi.


 

Yaliyomo:

  1. Maana ya vitamini B
  2. Makundi ya vitamini B
  3. Kazi za vitamini B
  4. Vyakula vya vitamini B
  5. Upungufu wa vitamini B
  6. Athari za kuwa na vitamini B kupitiliza


 

Vitamini B ni nini?

Vitamini B ni katika kundi la vitamini vinavyofahamika kama water soluble vitamin. vitamini B ni kundi la vitamini ambavyo vinafanana sifa lakini vina utofauti kidogo. Vitamini B ndani ya miili yetu vinafanya kazi ya kuhakikisha kuwa michakato ya kikemikali inafanyika, michakato hiyo kitaalamu inafahamika kama metabolism.


 

Metabolism hii ni michakato ya kikemikali inayofanyika ndani ya seli kwa ajili ya mambo makuu matatu nayo ni:-

  1. Kubadili chakula kuwa nishati (nguvu)
  2. Kubadili chakula ama nishati kkuwa protein, carbohydrate, lipids na nucleic acid.
  3. Kuondoa uchafu na sumu mwilini (nitrogen waste)

Hivyobasi michakato hii yote ili ifanyike kwa ufasaha na ufanisi vitamini B vinahitajika katika miili yetu. Endelea kusoma makala hii ukaone kazi za vitamini B.


 

Makundi ya vitamini B

Makundi hayo ya vitamini B ni:

  1. B1 kitaalamu huitwa thiamine, hivi vimegunduliwa mwaka 1910 na mwanasayansi iliyeitwa Umetaro Suzuk Pia mwaka 1912 mwanasayansi aliyeitwa Casimir Funk aligundua thiamine.


 

  1. B2 kitaalamu huitwa riboflavinhivi navyo vimegunduliwa mwaka 1926 na wanasayansi wawili wanaokwenda kwa majina D.T Smith na E.G Hendrick.


 

  1. B3 pia hutambulika kama niacinau nicotinic acid kundi hili limegunduliwa mwaka 1937 na mwanasayansi anayekwenda kwa jina la Conrad Elvehjem.


 

  1. B5 na yo pia huitwa pantothenic acid, kundi hili limegunduliwa mwaka 1933 na Roger J. Williams


 

  1. B6 pia huitwa pyridoxine, pyridoxal, au pyridoxamine imegunduliwa na Paul Gyorgy mwaka 1934.


 

  1. B7 pia hufahamika kama biotinmwanasayansi aitwaye Margaret Averil Boas aliigundua vitamini hii miaka ya 1900


 

  1. B9 pia hujulikana kama folic acidMwanasayansi kwa jina la Lucy Wills aliigundua mwaka 1983


 

  1. B12 ama cobalaminshii imegunduliwa na jopo wanasayansi mbalimbali.


 

Kazi za vitamini B mwilini Na upungufu wa vitamini B mwilini

Kama tulivyoona kuwa kazi za vitamini B ni kuhakikishha kuwa mipambano ya kikemikali inafanyika ndani ya seli. Sasa hapa tutaona kazi za vitamini hivi kulingana na makundi yake:-


 

B1 hii husaidia mfumo wa fahamu (mfumo wa neva) kufanya kazi vyema. Upungufu wa vitamini hivi B1 huweza kuleta maatizo kwenye mfumo wa fahamu, moyo na mupotea kwa misuli.


 

B2 huhitajika kwa ajili ya uzalishwaji wa nishati, lipi, vitamini, madini na husaidia katika utengenezwaji wa antioxidant. Upungufu wa vitamini hivi huweza kusababisha kuvimba (imflamation) kwenye ngozi, ulimi, midomo, na matatizo kwenye mfumo wa fahamu.


 

B3 hii huhitajika katika kufanyika mchakato wa metabolism kwenye seli. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea ngozi kuwa na matatizo kama miwasho, mapele, ukurutu na kadhalika. Pia upungufu wa vitamini hivi huweza kusababisha tumbo kuvurugika na kuleta misongo ya mawazo




 

B6 hii hufanya kazi ya kuhakikisha metabolisma inayohusima katika kuchakata hamirojo asidi za amino, kuchakata hemoglobin hizi ni chembechembe za kwenye seli nyekundu za damu zinazo saidia katika kusafirisha hewa mwilini, pia katika kuthibiti kiwango cha sukari kwenye damu. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea madhara kwenye ubongo, shida kwenye fahamu ya mtu na pia ugonjwa wa anemia unaonasibiana na upungufu wa hewa ya oksijeni mwilini.


 

B9 huhusika katika kuchakata DNA, kuchakata amino acid, katika kukua na kukomaa kwa seli mwilini hasa hasa seli hai nyekundu. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea matatizo katika ukuaji, utengenezwaji na ukomaaji wa seli hai nyekundu za damu, uchovu, maumivu ya kichwa, kutokea uvimbe kwenye mdomo na hata kuathiri mtoto aliyepo tumboni.




 

B12 huhitajika kwa ajili ya utengenezwaji wa seli mpya, utengenezwaji wa damu na pia kwa ajili ya mfumo wa fahamu kufanya kazi vyema. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea kuvurugika kwa tumbo, shida kwenye mfumo wa fahamu pamoja na matatizo kwenye ulimi.


 

Vyakula vya vitamini B

Tunaweza kupata vitamini B kwenye vyakula vifuatavyo:-

  1. Nyama
  2. Nafaka kama mchele, mtama, mahindi n.k
  3. Mimea jamii ya maharagwe kama kunde
  4. Viazi
  5. Ndizi
  6. Pilipili
  7. Mayai
  8. Mimea jamii ya karanga na alizeti
  9. Mboga za majani zenye kijani iliyowiviana na kutia weusi kama spinachi
  10. Matunda kama palachichi na ndizi


 

Dalili za upungufu wa vitamini B

  1. Kupata ugonjwa wa Anaemia huu ni upungufu wa hewa ya oksijeni mwilini
  2. Matatizo kwenye ngozi
  3. Kupata vidonda kwenye mdomo, ma kupasuka kwa mdomo
  4. Misongo ya mawazo ama kuchanganyikiwa
  5. Kuharisha
  6. Kupotesa kumbukumbu kwa urahisi
  7. Misuli kupoteza ujazo
  8. Kubadilika badilika kwa mood (fikra na hisia) yaani mara umekasirika mara umefurahi


 

Athari za kuwa na vitamini b kupitiliza

  1. Kichefuchefu
  2. Kuona maluelue
  3. Kutapika
  4. Kuharisha
  5. Maumivu ya tumbo
  6. Shida kwenye ngozi
  7. Kuzidi kwa kiu


 

Makala nyingine kwa ajili yako:

  1. Vyakula vya protini
  2. Vyakula vya vitamin K
  3. Vyakula vya vitamini C
  4. Afya ya uzazi
  5. Afya na magonjwa



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Umuhimu wa kutumia maembe kiafya.
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia maembe kiafya, tunajua wazi kuwa maembe ni tunda ambalo lina umuhimu kwenye afya na uwa na vitamini C kwa hiyo tunapaswa kujua faida zake kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

image Faida za kiafya za kula magimbi/ taro roots
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula magimbi Soma Zaidi...

image Faida za mchaichai/ lemongrass
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za mchaichai Soma Zaidi...

image Vyakula vya kuongeza damu
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula vya kuongeza damu Soma Zaidi...

image Faida za vitamin C mwilini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vitamini C mwilini Soma Zaidi...

image fahamu vitamini A na kazi zake
Je na wewe i katika wale ambaowanahitaji kujuwa kuhusu Vitamini A, kazi zake na vyakula vya vitamini A. post hii inakwenda kukujuza zaidi pamoja na historia ya vitamini A. Soma Zaidi...

image Faida za kiafya za kula panzi, senene na kumbikumbi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula senene, panzi na kumbikumbi Soma Zaidi...

image Faida za kula kunde, maharage, njegere, mbaazi na njugu mawe
Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula kunde, maharage, njegere, mbaazi na njugu mawe Soma Zaidi...

image Vyakula vya fati
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu aina za vyakula vya fati na umuhimu wake mwilini Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu vitamini C na kazi zake
Makala hii itakujulisha kazi kuu za vitamini C mwilini. Hapa pia utatambuwa ni kwa nini tunahitaji vitamini C na wapi tutavipata Soma Zaidi...