Menu



fahamu kuhusu vitamini B na faida zake

makala hii inakwenda kukupa faida, kazi na athari za vitamini B mwilini. Nini hutokea endapo utakuwa na upungufu wa vitamini B mwilini?

Fahamu vitamini B na kazi zake, Vyakula vya vitamini B na athari za upungufu wake

Vitamini B ni katika water soluble vitamin ambavyo vina kazi ya kuhakikisha kuwa michakato yote ya kikemikali mwilini inakwenda vizuri. Na hapa tunazungumzia kitaalamu metabolism. vitamini B vipo katika makundi mengi kma aB1, B2, B3, B5, B6, B7 na B12. katika makala hii nitakwenda kukueleza maana ya vitamini hivi, nini kazi zake hasa mwilini, wapi nitapata vitamini B na je ni zipi dalili za upungufu wa vitamini hivi.


 

Yaliyomo:

  1. Maana ya vitamini B
  2. Makundi ya vitamini B
  3. Kazi za vitamini B
  4. Vyakula vya vitamini B
  5. Upungufu wa vitamini B
  6. Athari za kuwa na vitamini B kupitiliza


 

Vitamini B ni nini?

Vitamini B ni katika kundi la vitamini vinavyofahamika kama water soluble vitamin. vitamini B ni kundi la vitamini ambavyo vinafanana sifa lakini vina utofauti kidogo. Vitamini B ndani ya miili yetu vinafanya kazi ya kuhakikisha kuwa michakato ya kikemikali inafanyika, michakato hiyo kitaalamu inafahamika kama metabolism.


 

Metabolism hii ni michakato ya kikemikali inayofanyika ndani ya seli kwa ajili ya mambo makuu matatu nayo ni:-

  1. Kubadili chakula kuwa nishati (nguvu)
  2. Kubadili chakula ama nishati kkuwa protein, carbohydrate, lipids na nucleic acid.
  3. Kuondoa uchafu na sumu mwilini (nitrogen waste)

Hivyobasi michakato hii yote ili ifanyike kwa ufasaha na ufanisi vitamini B vinahitajika katika miili yetu. Endelea kusoma makala hii ukaone kazi za vitamini B.


 

Makundi ya vitamini B

Makundi hayo ya vitamini B ni:

  1. B1 kitaalamu huitwa thiamine, hivi vimegunduliwa mwaka 1910 na mwanasayansi iliyeitwa Umetaro Suzuk Pia mwaka 1912 mwanasayansi aliyeitwa Casimir Funk aligundua thiamine.


 

  1. B2 kitaalamu huitwa riboflavinhivi navyo vimegunduliwa mwaka 1926 na wanasayansi wawili wanaokwenda kwa majina D.T Smith na E.G Hendrick.


 

  1. B3 pia hutambulika kama niacinau nicotinic acid kundi hili limegunduliwa mwaka 1937 na mwanasayansi anayekwenda kwa jina la Conrad Elvehjem.


 

  1. B5 na yo pia huitwa pantothenic acid, kundi hili limegunduliwa mwaka 1933 na Roger J. Williams


 

  1. B6 pia huitwa pyridoxine, pyridoxal, au pyridoxamine imegunduliwa na Paul Gyorgy mwaka 1934.


 

  1. B7 pia hufahamika kama biotinmwanasayansi aitwaye Margaret Averil Boas aliigundua vitamini hii miaka ya 1900


 

  1. B9 pia hujulikana kama folic acidMwanasayansi kwa jina la Lucy Wills aliigundua mwaka 1983


 

  1. B12 ama cobalaminshii imegunduliwa na jopo wanasayansi mbalimbali.


 

Kazi za vitamini B mwilini Na upungufu wa vitamini B mwilini

Kama tulivyoona kuwa kazi za vitamini B ni kuhakikishha kuwa mipambano ya kikemikali inafanyika ndani ya seli. Sasa hapa tutaona kazi za vitamini hivi kulingana na makundi yake:-


 

B1 hii husaidia mfumo wa fahamu (mfumo wa neva) kufanya kazi vyema. Upungufu wa vitamini hivi B1 huweza kuleta maatizo kwenye mfumo wa fahamu, moyo na mupotea kwa misuli.


 

B2 huhitajika kwa ajili ya uzalishwaji wa nishati, lipi, vitamini, madini na husaidia katika utengenezwaji wa antioxidant. Upungufu wa vitamini hivi huweza kusababisha kuvimba (imflamation) kwenye ngozi, ulimi, midomo, na matatizo kwenye mfumo wa fahamu.


 

B3 hii huhitajika katika kufanyika mchakato wa metabolism kwenye seli. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea ngozi kuwa na matatizo kama miwasho, mapele, ukurutu na kadhalika. Pia upungufu wa vitamini hivi huweza kusababisha tumbo kuvurugika na kuleta misongo ya mawazo




 

B6 hii hufanya kazi ya kuhakikisha metabolisma inayohusima katika kuchakata hamirojo asidi za amino, kuchakata hemoglobin hizi ni chembechembe za kwenye seli nyekundu za damu zinazo saidia katika kusafirisha hewa mwilini, pia katika kuthibiti kiwango cha sukari kwenye damu. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea madhara kwenye ubongo, shida kwenye fahamu ya mtu na pia ugonjwa wa anemia unaonasibiana na upungufu wa hewa ya oksijeni mwilini.


 

B9 huhusika katika kuchakata DNA, kuchakata amino acid, katika kukua na kukomaa kwa seli mwilini hasa hasa seli hai nyekundu. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea matatizo katika ukuaji, utengenezwaji na ukomaaji wa seli hai nyekundu za damu, uchovu, maumivu ya kichwa, kutokea uvimbe kwenye mdomo na hata kuathiri mtoto aliyepo tumboni.




 

B12 huhitajika kwa ajili ya utengenezwaji wa seli mpya, utengenezwaji wa damu na pia kwa ajili ya mfumo wa fahamu kufanya kazi vyema. Upungufu wa vitamini hivi huweza kupelekea kuvurugika kwa tumbo, shida kwenye mfumo wa fahamu pamoja na matatizo kwenye ulimi.


 

Vyakula vya vitamini B

Tunaweza kupata vitamini B kwenye vyakula vifuatavyo:-

  1. Nyama
  2. Nafaka kama mchele, mtama, mahindi n.k
  3. Mimea jamii ya maharagwe kama kunde
  4. Viazi
  5. Ndizi
  6. Pilipili
  7. Mayai
  8. Mimea jamii ya karanga na alizeti
  9. Mboga za majani zenye kijani iliyowiviana na kutia weusi kama spinachi
  10. Matunda kama palachichi na ndizi


 

Dalili za upungufu wa vitamini B

  1. Kupata ugonjwa wa Anaemia huu ni upungufu wa hewa ya oksijeni mwilini
  2. Matatizo kwenye ngozi
  3. Kupata vidonda kwenye mdomo, ma kupasuka kwa mdomo
  4. Misongo ya mawazo ama kuchanganyikiwa
  5. Kuharisha
  6. Kupotesa kumbukumbu kwa urahisi
  7. Misuli kupoteza ujazo
  8. Kubadilika badilika kwa mood (fikra na hisia) yaani mara umekasirika mara umefurahi


 

Athari za kuwa na vitamini b kupitiliza

  1. Kichefuchefu
  2. Kuona maluelue
  3. Kutapika
  4. Kuharisha
  5. Maumivu ya tumbo
  6. Shida kwenye ngozi
  7. Kuzidi kwa kiu


 

Makala nyingine kwa ajili yako:

  1. Vyakula vya protini
  2. Vyakula vya vitamin K
  3. Vyakula vya vitamini C
  4. Afya ya uzazi
  5. Afya na magonjwa

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1870


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Utaratibu wa maisha kwa aliye athirika
Somo hili linakwenda kukuletea utaratibu wa maisha kwa aliye athirika Soma Zaidi...

Maana ya afya
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya afya Soma Zaidi...

Mzunguko wa mwezi kwa mwanamke
Posti hii inahusu zaidi mzunguko wa mwezi kwa mwanamke, ni mzunguko ambao huchukua siku ishilini na nane kwa kawaida Ila lla ubadilika kulingana na mtu, Ila ngoja tuangalie siku ishilini na nane tu. Soma Zaidi...

Faida za kusafisha vidonda.
Posti hii inahusu zaidi faida za kusafisha vidonda, ni faida ambazo Mgonjwa mwenye vidonge uzipata kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Upungufu wa vyakula na madhara yake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula Soma Zaidi...

Kwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?
Swali languKwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe? Soma Zaidi...

Mbinu za kupunguza magonjwa yanayohusiana na figo
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa figo. Ni ugonjwa unaotokana pale figo linaposhindwa kufanya kazi, tuone mbinu za kufanya Ili kuepuka na tatizo hilo. Soma Zaidi...

Huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi
Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wagonjwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi wanaweza kupata, huduma hii utolewa hasa kwa wale ambao wamejitokeza kupima afya zao na kujua wazi hali zao na kwa wale wanaofatilia huduma hii wanaweza kuishi vizu Soma Zaidi...

Njia za kufuata unapohudumia watu waliopata ajali
Post hii inahusu zaidi namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa watu waliopata ajali. Ajali ni tukio lisilotarajiwa ambalo kinaweza kumkuta mtu yeyote, tunapotoa huduma ya kwanza tnazingatia rangi ambazo huwakilisha jinsi watu walivyoumia. Soma Zaidi...

Makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika, Ni magroup manne ya damu ambayo husaidia kuongeza damu kwa mtu ambaye amepungukiwa damu Soma Zaidi...