image

Dawa ya quinenes katika kutibu Malaria

Post hii inahusu zaidi dawa e quinine katika kutibu Malaria ni dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria ikiwa dawa nyingine zimeshindwa kufanya kazi.

Kazi ya quinine Katika kutibu Malaria.

1.quinine ni dawa inayotumiwa kutibu malaria dawa hii utumika kutibu Malaria ikiwa mgonjwa vametumia dawa nyingine lakini hakufanikiwa kupona kwa hiyo dawa hii utumika kwa wagonjwa wa Aina hii, kwa hiyo ni dawa yenye nguvu kwa namna Moja au nyingine na inapotumika hutumiwa kwa tahadhari na kwa  uangalifu.

 

2. Dawa hii huwa kwenye mfumo wa vidonge na kwenye mfumo wa Maji maji ambapo dawa ambayo Iko kwenye mfumo wa Maji maji huweza kutumika kwa mgonjwa kwa kuchanganya kwenye drip kwa kipimo fulani na kwa uangalifu mkubwa, ikiwa quinine haijachanganywa na maji na mtu akitumia kupitia kwenye mishipa mgonjwa anaweza kupoteza maisha kwa hiyo dawa hii inabidi kutumiwa kwa uangalifu sana na kwa mtu anayeitoa uhakikisha kuwa inaenda vizuri, hii dawa uangaliwa kwa makini kwa Sababu Ina Tabia ya kumaliza sukari mwilini.

 

3.Dawa hii pia huwa na matokea au maudhi ambayo uweza kutokea kama vile kutapika kwa mgonjwa pale anapokuwa anatumia dawa, kizunguzungu utokea kwa kwa wagonjwa wakati mwingine mgonjwa uziba masikio kwa sababu ya dawa zile anazozitumia na pengine mgonjwa uona shida katika kuona kwa sababu hiyo anaanza kuhangaika wakati wa kuona , na kwa wagonjwa wengine wanashindwa kutulia kwenye sehemu Moja uhangaika sana kwa sababu ya maumivu wanayopata kutokana na dawa hii ya maumivu  kwa hiyo tuwe makini katika kuwahudumia.

 

4.kwa hiyo dawa hii ya quinine Ina nguvu sana haipaswi kutumiwa na watu ambao hawana shida maalumu kama vile allergies kwa dawa nyingine za malaria wanapaswa kutumia wale tu ambao wameitumia dawa nyingine za malaria na hawakupata nafuu na katika kutumia dawa nyingine za malaria kwa hiyo tunapaswa kuwa waangalifu katika kutumia dawa hii ya quinine  na watu wale wanaopungukiwa sukari mara kwa mara hawapaswi kutumia dawa hii au wakitumia waitumie kwa uangalifu mkubwa sana.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1502


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Dawa ya fangasi kwenye mdomo na ulimi
Utajifunza dalili za fangasi mdomoni na ulimini, sababu za fangasi wa mdomoni na ulimini, matibabu yeke na njia za kukabiliana nao Soma Zaidi...

Fahamu antibiotics ya asili.
Post hii inahusu zaidi antibiotics ya asili, ni antibiotics inayotumia vitu vya kila siku na ya kawaida na mtu akaweza kupona kabisa na kufanya kazi kama antibiotics ya vidonge vya kawaida. Soma Zaidi...

Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo Aspirin.
Aspirini Ni dawa ya kutuliza maumivu.Majina yanayoaminika zaidi katika kutuliza maumivu sasa yanapatikana kwa njia mbadala inayookoa gharama kwa kutumia Aspirini. Aspirini inayopendwa na familia kwa miongo kadhaa, mara nyingi hutumiwa kupunguza maumivu y Soma Zaidi...

Vyakula vya wanga
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya wanga Soma Zaidi...

Fahamu dawa za cyclophosphamide na mustargen.
Post hii inahusu zaidi dawa za cyclophosphamide na mustargen katika kupambana na ugonjwa wa Kansa. Soma Zaidi...

Nani anapaswa kutumia vidonge vya zamiconal.
Posti hii inahusu zaidi watu ambao wana uwezo wa kutumia vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya watu au makundi yanayoweza kutumia vidonge hivi. Soma Zaidi...

Dawa za kutibu kiungulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za kutibu kiungulia Soma Zaidi...

Namna ya kutumia tiba ya jino.
Posti hii inahusu zaidi namna au njia ya kufanya Ili kuweza kutumia tiba hii ya jino, kwa sababu ya mchanganyiko ambao umekwisha kuwepo kwa hiyo unachumua mchanganyiko unafanya kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Dawa ya kutibu ugonjwa wa PID
PID ni mashambulizi ya bakteria kwenye mfumo wa uzazi kwa wanawake. Hapa nitakujulisha dawa Soma Zaidi...

Dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU
Somo hili linakwenda kukuletea dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU Soma Zaidi...

Fahamu dawa ambazo uchangia kupungua kwa nguvu za kiume
Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali ambazo uchangia katika kupunguza nguvu za kiume , hii ni kwa sababu ya wataalamu mbalimbali wanavyosema Soma Zaidi...

Mgawanyo wa tiba ya kifua kikuu
Post hii inahusu zaidi mgawanyiko wa tiba ya kifua kikuu, kwa kawaida tiba hii imegawanyika katika sehemu kuu mbili. Soma Zaidi...