Fahamu dawa ya aminophylline kutibi maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji
Post hii inahusu zaidi dawa ya aminophylline katika kutuliza maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji.
Fahamu dawa ya kutibu au kutuliza maumivu kwenye mfumo wa upumuaji.
1. Aminophylline ni mojawapo ya dawa ambayo ufanya kazi katika mfumo wa upumuaji kwa matibabu hasa ya asthma na pia kwa watu wenye tabia ya kubanwa na vifua wakati hali ya hewa inapobadilika na matatizo ya upumuaji kwa ujumla pia dawa hii utolewa kwa kupitia kwenye mishipa ya damu Ili kuweza kufanya kazi kwa haraka kwa mgonjwa.
2. Pia kwa mara chache huwa kwenye mfumo wa vidonge na pia wakati mwingine uweza kutolewa kwa kupitia kwenye matako na paja ila kwa upande wa matako na paja usababisha maupeke na maumivu na pia kwa kupitia kwenye damu utolewa taratibu walau kwa mda wa dakika ishilini au zaidi kidogo.
3. Dawa hii Ina kuwa na milligrams mia mbili hamsini na pia mills kumi na utolewa kwa utaratibu na pia dozi ubadilika kulingana na umri pamoja na Uzito.
4. Dawa hii huwa na maudhi madogo madogo kama vile kichefuchefu na kutapika, kizunguzungu, mapigo ya moyo kwenda mbio na pia inawezekana kuwepo kwa degedege hasa kwa watoto wadogo na kwa watu wazima ni mara chache sana
5. Iwapo kama Kuna matokeo ya kuwepo kwa degedege ni vizuri kutumia dawa ya diazepam Ili kuweza kutuliza hiyo degedege, kwa hiyo dawa hii inapaswa kueleweka kwamba Kuna watu ambao hawapaswi kutumia dawa hii ni wale wenye aleji na dawa hii na pia kwa wale wenye tatizo la kifafa wanapaswa kuitumia dawa hii kwa uangalizi maalumu na ikibidi wanapaswa kuitumia kwa uangalizi Fulani.
6. Pia dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela au kwa mazoea Bali kwa utaratibu wa wataalamu wa afya Ili kuepuka madhara zaidi ambayo yanaweza kutokea.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 web hosting 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 ai web app 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Ijue Dawa ya lignocaine
Posti hii inahusu zaidi dawa ya lignocaine kama mojawapo ya Dawa ambayo utumika wakati wa upasuaji.
Soma Zaidi...Fahamu zaidi kuhusiana na Dawa inayotibu shinikizo la damu. iitwayo LASIX
Lasix (Furosemide) iko katika kundi la dawa zinazoitwa vidonge vya maji (loop diuretics) vidonge vya maji. Lasix hutumiwa kupunguza uvimbe mwilini unaosababishwa na kushindwa kwa moyo, ugonjwa wa ini, au ugonjwa wa figo. Kwa matibabu ya dalili nyingi.La
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu
Post hii inahusu dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu kifua kikuu, kwanza kabisa kabla ya kuanza kufahamu dawa hizo ni vizuri kabisa kufahamu kifua kikuu nini hili kuweza pia kufahamu dawa zake.
Soma Zaidi...Ifahamu dawa ya kutibu kifua kikuu
Post hii inahusu zaidi dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu.
Soma Zaidi...Tiba mbadala za vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukuletea tiba mbadala za vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...