Dawa za fangasi ukeni
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za fangasi ukeni
DAWA YA FANGASI UKENIFangasi ukeni wanaweza kuwa ni tatizo kubwa na wakati mwengine wanaweza kuleta aina, madhara na kupoteza ladha ya mapenzi. Fangasi ukeni ni rahisi kutibika kama mwanamke atatumia dawa kwa uangalifu. Unaweza kutibu fangasi ukeni kwa kutumia dawa za kupata kutoka katika maduka ya dawa. Kama hali haina nafuu muonedaktari anaweza kukuandikia dawa za kumeza ama sindano ikibidi. Kunawada nyingine si za kupaka ila ni vidonge, hivi mwanamke ataweza ukeni na kitamumunyika chenyewe.
Makala hii inakwenda kukuletea tiba na dawa za fangasi ukeni, sababu zake, namna ya kupambana na fangasi hawa na dalili za fangasi ukeni. Pia tutaona madhara ya fangasi ukeni endapo watachelewa kutibiwa. Soma mkala hii hadi mwisho huwenda ikakusaidia sana.
1.Dawa ya fangasi ukeni ya kupakaA.ClotrimazoleB.MiconazoleC.TioconazoleD.TerconazoleE.Butoconazole
Ni vyema kumuona daktari kwanza kabla hujatumia dawa hizi. Kwa mfano terconazole na butoconazole zinahitaji maelezo kutoka kwa daktari kwa usalama zaidi wa afya yako.
2.Dawa ya fangasi ukeni ya kumezaEndapo dawa za kupaka hazikuonyesha ahueni, mgonjwa atabadilishiwa dawa na kupewa za kumeza ama sindano.fluconazoe (diflucan) hii ni nzuri sana kwa wenye fangasi silizoshindikana kwa dawa za kupaka. Pata kwa nza maelezo ya daktari kabla ya kutumia. Dawa hii haitumiwi na wajawazito. Ukitumia dawa hii unaweza kuona mabadiliko kama maumivu ya tumbo au tumbo kuvurugika na maumivu ya kichwa.
3.Dawa ya fangasi ukeni walio sugu (azole resistant therapy).Dawa hii sio ya kumeza, maana ni hatari sana. Napi asio ya kupaka. Dawa hii hutumika endapo ddawa za hapo juu zimeshindikana. Kwanamke atapewa dawa hii aiingize kwenye uke wake.
Nini kinasababisha fangasi ukeni?Fangasi ukeni husababishwa na ina ya fangasi wanaoitwa candida albican. Kikawaida ukeni kuna bakteria na fangasi aina ya candida kwa kiwango maalumu. Pia kuna aina ya fangasi waitwao lactobacillus hawa huzuia ongezeko la fangasi candida wasiwe wengi kupitiliza. Sasa endapo fangasi candida wakizaliana kwa wingi na kupitiliza kiwango ndipo madhara yanaanza kuonekana. Swali la kijuliza hapa inakuwaje fangasi hawa wanazaliana zaidi?
Sababu za kuzaliana fangasi ukeni kwa wingi:A.Kama mwanamke anatumia dawa za antibioticsB.Kama mwanamke ana mimbaC.Kisukari kilichoshindwa kudhibitiwaD.Mfumo wa kinga kudhoofuE.Kutumia dawa za kudhibiti uzazi wa mpango dawa za kumeza.
Namna ya kujilinda na fangasi wa ukeni
1.Jiepushe kuvaa nguo za ndani zilizobana sana
2.Jizuie kusafisha uke kwa kemikali
3.Jiepushe na baadhi ya vifaa vya wanawake vilivyowekewa manukato kama pedi zenye manukato, badhi ya sabuni zenye manukato za kusafishia uke n.k
4.Kama huna ulazima wa kutumia antibiotics wacha kutumia
5.Usivae nguo zenye majimaji, hakikisha nguo zako ni kavu, ni vuema zile za ndani zikawa ni za pamba.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 web hosting 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Dawa ya vidonda vya tumbo
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Dawa ya Panadol au paracetamol katika kutuliza maumivu
Posti hii inahusu zaidi kazi ya paracetamol katika kutuliza maumivu, ni Aina ya dawa ambayo utumiwa sana katika kutuliza maumivu kwa wagonjwa.
Soma Zaidi...Fahamu kundi la veta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
Post hii inahusu zaidi kundi la beta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo,hili kundi lina dawa mbalimbali ambazo utumika katika matibabu ya magonjwa ya moyo na kila dawa tutaiongelea tofauti tofauti ili kuweza kujua kazi zake.
Soma Zaidi...Penicillin dawa ya kutibu maambukizi ya bakteria mwilini
Post hii Inahusu zaidi dawa za kutibu maambukizi yoyote Yale yanayosababishwa na bakteria dawa hizi kwa kitaamu huiitwa antibiotics Kuna dawa mbalimbali zinazotibu maambukizi ya bakteria leo tutaanza na dawa ambayo inaitwa penicillin.
Soma Zaidi...