FAHAMU DAWA YA PREDNISONE KATIKA KUPAMBANA NA ALEJI


image


Post hii inahusu zaidi dawa ya Prednisone ambayo usaidia katika kupambana na aleji.


Ifahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji 

1. Prednisone ni mojawapo ya dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kwa watu wenye tatizo hili kwa sababu Kuna wale ambao Wana tatizo la aleji lakini hawawezi kutumia dawa ya hydrocortisone kwa hiyo dawa nyingine ambayo upendekezwa ni Prednisone.

 

2. Pamoja na kutuliza aleji ambazo zimesababishwa na dawa pamoja na vyakula dawa hii pia ufanya Kazi kwa wagonjwa wa asthma na pia kwa watu wanabanwa na kifua kwa sababu mbalimbali kwa hiyo dawa hii ni nzuri na pia imesaidia watu wengi sana.

 

3. Dawa hii utumika kwa mdomo mara nyingi na pia milligrams ubadilika kulingana na hali ya mgonjwa, hali ikiwa mbaya au aleji imekuwa kubwa kuzidi kiasi ya milligrams sitini inaweza kutumika na pia kadri aleji inavyopungua milligrams thelathini mpaka arobaini zinaweza kutumika, na ushauri wa wataalamu wa afya ni muhimu sana.

 

4. Dawa hii inapaswa kutumiwa na watu mbalimbali ila wale wenye tatizo la presha ya kupanda wanapaswa kuitumia kwa taahadhari na pia kwa wale ambao wametumia ila hawakupata nafuu wanapaswa kubadilishiwaa dawa hii na kutumia dawa nyingine ambayo inafaaa kabisa. Na kwa upande wa wagonjwa wa asthma ni vizuri kuitumia kwa uangalifu sio Mda wote kukaa wanaitumia kwa sababu inaweza kuwaletea shida kwenye mapafu.

 

5. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo kama vile mapigo ya moyo kwenda mbio, matatizo kwenye mapafu iwapo kama imetumika mara nyingi na kwa kiasi kikubwa na pia baada ya kupona mgonjwa anaweza kuhisi Hana nguvu na maumivu ya kichwa pia yanaweza kutokea.

 

6. Dawa hii inapaswa kutumiwa kulingana na wataalamu wa afya sio kuitumia kiholela.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    2 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    3 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    5 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    6 Magonjwa na afya    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Fahamu tiba ya jino
Post hii inahusu zaidi tiba ya jino,ni tiba ya kawaida kwa watu walio na matatizo ya meno, kwa kawaida tunafahamu kwamba jino huwa halina dawa ila dawa yake huwa ni kungoa lakini Leo nawaletea habari njema kwamba jino sio kungoa tena ila Kuna tiba ambayo utolewa na jino haliwezi kuuma , kufa ganzi au kutoboka kwa hiyo ifuatavyo ni tiba ya jino. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo, ni dawa ambayo imo kwenye kundi la vasodilators na ufanya Kazi mbalimbali zinazousu magonjwa ya moyo. Soma Zaidi...

image Wanaopasawa kutumia PEP
PEP Ni dawa ambazo utumiwa na watu wanaojamiiana na watu wenye virus vya ukimwi ila wenyewe hawawezi kupata kwa sababu ya kutumia dawa hizo. Soma Zaidi...

image Matibabu ya vidonda vya tumbo nyumbani
Post hii inahusu zaidi matibabu ya vidonda vya tumbo nyumbani, ni njia ya kawaida ya kujitibu vidonda vya tumbo kama tulivyoona. Soma Zaidi...

image Ifahamu dawa ya isoniazid katika kupambana na ugonjwa wa TB
Post hii inahusu zaidi dawa ya isoniazid katika mapambano na kifua kikuu, tunafahamu kabisa kwamba kifua kikuu ni hatari katika jamii kwa hiyo dawa ya isoniazid ni mkombozi katika mapambano na kifua kikuu. Soma Zaidi...

image IJUE DAWA YA AMOXLINE (antibiotic) NA MATUMIZI YAKE
Posti hii inahusu zaidi dawa ya amoxline .jinsi inavyofanya kazi mwilini.pamoja na matumizi yake. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu dawa ya Albendazole
Post hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole ni mojawapo ya dawa ambazo usaidia kutibu minyoo, na pia imefanikiwa sana kadri ya watumiaji wa dawa hiyo. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu dawa ya potassium sparing
Post hii inahusu zaidi dawa ya potassium sparing katika matibabu ya magonjwa ya moyo. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ya kutuliza mishutuko.
Post hii inahusu zaidi dawa ya phenytoin,ni dawa inayotuliza mishutuko mbalimbali inayoweza kutokea kwenye mwili na kutokana na mishutuko hiyo tunaweza kupata kifafa. Soma Zaidi...

image Faida za dawa za NMN
Posti hii inahusu zaidi faida za dawa za NMN maana yake ni Nicotinamide mononucleotide ni dawa ambazo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali kama vile. Soma Zaidi...