Fahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya Prednisone ambayo usaidia katika kupambana na aleji.
Ifahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji
1. Prednisone ni mojawapo ya dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kwa watu wenye tatizo hili kwa sababu Kuna wale ambao Wana tatizo la aleji lakini hawawezi kutumia dawa ya hydrocortisone kwa hiyo dawa nyingine ambayo upendekezwa ni Prednisone.
2. Pamoja na kutuliza aleji ambazo zimesababishwa na dawa pamoja na vyakula dawa hii pia ufanya Kazi kwa wagonjwa wa asthma na pia kwa watu wanabanwa na kifua kwa sababu mbalimbali kwa hiyo dawa hii ni nzuri na pia imesaidia watu wengi sana.
3. Dawa hii utumika kwa mdomo mara nyingi na pia milligrams ubadilika kulingana na hali ya mgonjwa, hali ikiwa mbaya au aleji imekuwa kubwa kuzidi kiasi ya milligrams sitini inaweza kutumika na pia kadri aleji inavyopungua milligrams thelathini mpaka arobaini zinaweza kutumika, na ushauri wa wataalamu wa afya ni muhimu sana.
4. Dawa hii inapaswa kutumiwa na watu mbalimbali ila wale wenye tatizo la presha ya kupanda wanapaswa kuitumia kwa taahadhari na pia kwa wale ambao wametumia ila hawakupata nafuu wanapaswa kubadilishiwaa dawa hii na kutumia dawa nyingine ambayo inafaaa kabisa. Na kwa upande wa wagonjwa wa asthma ni vizuri kuitumia kwa uangalifu sio Mda wote kukaa wanaitumia kwa sababu inaweza kuwaletea shida kwenye mapafu.
5. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo kama vile mapigo ya moyo kwenda mbio, matatizo kwenye mapafu iwapo kama imetumika mara nyingi na kwa kiasi kikubwa na pia baada ya kupona mgonjwa anaweza kuhisi Hana nguvu na maumivu ya kichwa pia yanaweza kutokea.
6. Dawa hii inapaswa kutumiwa kulingana na wataalamu wa afya sio kuitumia kiholela.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Dapsone na kazi zake
Posti hii inahusu zaidi dawa ya Dapsone na kazi zake, hii ni dawa ambayo utumika katika kutibu ugonjwa wa ukimwi, dawa hii ufanya kazi kwa mchanganyiko wa dawa nyingine kama vile Rifampicin na clofaximine.
Soma Zaidi...Fahamu kazi ya dawa ya ampicillin inayopambana na maambukizi ya bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin
Soma Zaidi...Fahamu matumizi ya Ampicillin.
Ampicillin ni antibiotic yenye msingi wa penicillin ambayo inafanya kazi kupambana na maambukizi ya ndani ya bakteria. Ampicillin hufanya kazi ya kuharibu kuta za kinga ambazo bakteria huunda ndani ya mwili wako na kuzuia bakteria wapya kutokeza. Ampici
Soma Zaidi...Ifahamu dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi.
Soma Zaidi...