picha

Fahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji

Post hii inahusu zaidi dawa ya Prednisone ambayo usaidia katika kupambana na aleji.

Ifahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji 

1. Prednisone ni mojawapo ya dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kwa watu wenye tatizo hili kwa sababu Kuna wale ambao Wana tatizo la aleji lakini hawawezi kutumia dawa ya hydrocortisone kwa hiyo dawa nyingine ambayo upendekezwa ni Prednisone.

 

2. Pamoja na kutuliza aleji ambazo zimesababishwa na dawa pamoja na vyakula dawa hii pia ufanya Kazi kwa wagonjwa wa asthma na pia kwa watu wanabanwa na kifua kwa sababu mbalimbali kwa hiyo dawa hii ni nzuri na pia imesaidia watu wengi sana.

 

3. Dawa hii utumika kwa mdomo mara nyingi na pia milligrams ubadilika kulingana na hali ya mgonjwa, hali ikiwa mbaya au aleji imekuwa kubwa kuzidi kiasi ya milligrams sitini inaweza kutumika na pia kadri aleji inavyopungua milligrams thelathini mpaka arobaini zinaweza kutumika, na ushauri wa wataalamu wa afya ni muhimu sana.

 

4. Dawa hii inapaswa kutumiwa na watu mbalimbali ila wale wenye tatizo la presha ya kupanda wanapaswa kuitumia kwa taahadhari na pia kwa wale ambao wametumia ila hawakupata nafuu wanapaswa kubadilishiwaa dawa hii na kutumia dawa nyingine ambayo inafaaa kabisa. Na kwa upande wa wagonjwa wa asthma ni vizuri kuitumia kwa uangalifu sio Mda wote kukaa wanaitumia kwa sababu inaweza kuwaletea shida kwenye mapafu.

 

5. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo kama vile mapigo ya moyo kwenda mbio, matatizo kwenye mapafu iwapo kama imetumika mara nyingi na kwa kiasi kikubwa na pia baada ya kupona mgonjwa anaweza kuhisi Hana nguvu na maumivu ya kichwa pia yanaweza kutokea.

 

6. Dawa hii inapaswa kutumiwa kulingana na wataalamu wa afya sio kuitumia kiholela.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 9212

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Ni dawa gani hatari kwa mjamzito?

Ukiwa mjamzito uwe makini sana katika kuchagua matumizi ya dawa. Vinginevyobinawwza kuwa hatari. Hapa nitakujuza dawa ambazo ni hatari kutumia kwa ujauzito wako.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya loperamide dawa ya kuzuia kuharusha

Post hii inahusu zaidi dawa ya loperamide ni dawa ambayo inazuia kuharisha ni dawa inayofanya kazi kuanzia kwenye utumbo na pia usaidia kutuliza maumivu ya tumbo

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya potassium sparing

Post hii inahusu zaidi dawa ya potassium sparing katika matibabu ya magonjwa ya moyo.

Soma Zaidi...
Dawa za kutibu kiungulia

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za kutibu kiungulia

Soma Zaidi...
Dawa ya chango na maumivu ya hedhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya chango na dawa ya maumivu ya hedhi

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya mebendazole

Post hii inahusu zaidi dawa ya mebendazole ni dawa ambayo utumika kutibu minyoo ambayo utokea kwa watoto na watu wazima.

Soma Zaidi...