Fahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya Prednisone ambayo usaidia katika kupambana na aleji.
Ifahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji
1. Prednisone ni mojawapo ya dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kwa watu wenye tatizo hili kwa sababu Kuna wale ambao Wana tatizo la aleji lakini hawawezi kutumia dawa ya hydrocortisone kwa hiyo dawa nyingine ambayo upendekezwa ni Prednisone.
2. Pamoja na kutuliza aleji ambazo zimesababishwa na dawa pamoja na vyakula dawa hii pia ufanya Kazi kwa wagonjwa wa asthma na pia kwa watu wanabanwa na kifua kwa sababu mbalimbali kwa hiyo dawa hii ni nzuri na pia imesaidia watu wengi sana.
3. Dawa hii utumika kwa mdomo mara nyingi na pia milligrams ubadilika kulingana na hali ya mgonjwa, hali ikiwa mbaya au aleji imekuwa kubwa kuzidi kiasi ya milligrams sitini inaweza kutumika na pia kadri aleji inavyopungua milligrams thelathini mpaka arobaini zinaweza kutumika, na ushauri wa wataalamu wa afya ni muhimu sana.
4. Dawa hii inapaswa kutumiwa na watu mbalimbali ila wale wenye tatizo la presha ya kupanda wanapaswa kuitumia kwa taahadhari na pia kwa wale ambao wametumia ila hawakupata nafuu wanapaswa kubadilishiwaa dawa hii na kutumia dawa nyingine ambayo inafaaa kabisa. Na kwa upande wa wagonjwa wa asthma ni vizuri kuitumia kwa uangalifu sio Mda wote kukaa wanaitumia kwa sababu inaweza kuwaletea shida kwenye mapafu.
5. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo kama vile mapigo ya moyo kwenda mbio, matatizo kwenye mapafu iwapo kama imetumika mara nyingi na kwa kiasi kikubwa na pia baada ya kupona mgonjwa anaweza kuhisi Hana nguvu na maumivu ya kichwa pia yanaweza kutokea.
6. Dawa hii inapaswa kutumiwa kulingana na wataalamu wa afya sio kuitumia kiholela.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 ai web app 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 web hosting 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Ni dawa gani hatari kwa mjamzito?
Ukiwa mjamzito uwe makini sana katika kuchagua matumizi ya dawa. Vinginevyobinawwza kuwa hatari. Hapa nitakujuza dawa ambazo ni hatari kutumia kwa ujauzito wako.
Soma Zaidi...Matibabu ya Fangasi ukeni na dawa za fangasi wanaoshambulia uke.
Fangasi wanaweza kushambulia uke, kwa juu kwenye mashhav ya uke ama kwa ndani. Hali hii inaweza kusababisha miwasho na maumivu pia. Inaweza kusababisha michubuko na kutofurahia tendo la ndoa. Makala hii inakwenda kukujuza dawa na matibabu ya fangasi ukeni
Soma Zaidi...Fahamu dawa zinazotumika kwenye matibabu ya kansa
Post hii inahusu zaidi dawa ambazo zinatumika kwenye matibabu ya kansa, dawa hizi usaidia kuharibu seli ambazo ambazo hazistahili kwa kitaalamu huitwa malignant seli.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya ibuprofen katika kutuliza maumivu
Post hii inahusu zaidi dawa ibuprofen katika kutuliza maumivu, ni aina mojawapo ya dawa na yenyewe ufanya kazi kama aspirin na paracetamol
Soma Zaidi...Kazi za Dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria
Posti hii inahusu zaidi kazi za dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria kali, ni dawa ambayo inatumika sana kutibu Malaria kali.
Soma Zaidi...