picha

Fahamu aina mbalimbali za Magonjwa nyemelezi ya moyo

Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za Magonjwa ya moyo,kwa kawaida tunajua wazi kuwa kuna moyo mmoja lakini moyo huo unaweza kushambuliwa na magonjwa kwa kila aina kwa mfano kuna Maambukizi kwenye mishipa ya moyo,au kubadilika kwa mapigo ya moyo na m

1. Kuathirika kwa mishipa ya moyo.

Kwa wakati mwingine kuna kuathirika kwa mishipa ya moyo ambayo kwa kitaalamu huitwa coronary artery, mishipa hii inaweza kupata Maambukizi na kushindwa kusafilisha damu kutoka kwenye moyo na kupeleka sehemu mbalimbali za mwili. Pengine mishipa inaweza kushindwa kusafilisha damu kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu na mafuta kwenye mishipa hali hii usababisha moyo kusukuma damu kwa nguvu ili kuweza kukidhi mahitaji ya mwili hali hii usababisha kuaribika kwa mishipa ya moyo.

 

Kwa hiyo tunapaswa kupunguza vyakula vyenye mafuta mengi na kuhakikisha kuachana na vyakula vyenye sumu ambavyo Usababisha kuwepo kwa mafuta kwenye mishipa na kuwepo kwa uchafu kwenye mishipa kwa kuepuka mambo hayo tutaweza kuruhusu damu kusafili zaidi na kuepuka na kuaribika kwa mishipa ya damu.

 

3.Aina nyingine ya ugonjwa wa moyo ni mapigo ya moyo kwenda tofauti.

Kwa wakati mwingine mapigo ya moyo uenda haraka na kusababisha mtu kuwa  na jasho na pengine mtu anakuwa hatulii sehemu moja . Na pia kwa wakati mwingine kuna kipindi mapigo ya moyo yanaenda taratibu sana kwa hali hii umfanya mtu kupumua kwa shida . Na kuna kipindi kingine mapigo ya moyo uenda ovyoovyo bila mpangilio hali hii ni mbaya sana inaweza kusababisha matatizo mengine makubwa kama vile kupoteza maisha.

 

4.Kwa wahudumu na ndugu wa mgonjwa baada ya kuona dalili kama hizi wanapaswa kumpeleka mgonjwa hospitalini ili aweze kupata matibabu kwa sababu hali ya kubadilika ki mapigo huwa sio nzuri hasa kwa mgonjwa yule ambaye ni mara yake ya kwanza kwa sababu anaweza kupanic na kuona kuwa ndio mwisho basi tuwafariji na kuwa pamoja nao ili waweze kupata huduma za muhimu.

 

5. Aina nyingine ni ile ya moyo kushindwa kufanya kazi.

Kuna kipindi ambapo moyo unashindwa kufanya kazi kwa sababu mbalimbali kama vile kuwepo kwa kiasi kidogo cha damu kwenye mwili au Maambukizi kwenye valve za mishipa.kwa hiyo hali  hii isipogunduliwa mapema Mgonjwa anaweza kupoteza maisha kwa watu wenye tatizo kama hili wanaweza kutumia kifaa maalum ambacho usaidia moyo ili uweze kufanya kazi na pia kifaa hicho kwa kawaida huwa kinabadilika mara kwa mara kadri ya maoni ya wataalamu wa afya.

 

6.Kuna wakati mwingine moyo ushindwa kufanya kazi kwa ghafla kwa sababu ya matukio mbalimbali na kuna huduma ambayo utolewa kwa ajili ya kushutua moyo huduma hiyo uitwa cardiopulmonary Resuscitation, hii huduma utolewa kwa wale wenye utamaalamu na mafunzo maalum kwa ajili ya kushutua moyo uliosimama ghafla.

 

7. Kuna aina nyingine t Magonjwa ya moyo ambayo huwapata watoto

Kwa wakati mwingine watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo kwa sababu kuna kesi mbalimbali zinazoonyesha kuwa mtoto amezaliwa na tundu kwenye moyo, hali hii utokea kwa sababu ya mtindo wa maisha kwa Mama wajawazito kama vile uvutaji wa sigara, utumiaji wa madawa ya kulevya wakati wa ujauzito na pia kutumia vileo vikali wakati wa ujauzito hayo yote usababisha watoto kuzaliwa na matundu kwenye Aorta.

 

8.Kwa hiyo ili kuepuka na matatizo haya wanawake wakati wa ujauzito wanapaswa kufuata mashariti ya wataalamu wa afya na kuachana na vileo, madawa ya kulevya, pombe kali na mambo kama  hayo ili kuweza kuepuka matatizo kama hayo wakati wa ujauzito, kwa hiyo akina Mama pia wahudhuria maudhurio yote ya kliniki ili kuweza kusikiliza mafundisho kwa sababu hayo mafundisho utolewa kila mwezi kipindi mama akiwa kwenye mahudhurio ya kawaida.

 

9. Aina nyingine ya Magonjwa ya moyo ni pamoja na moyo kutanuka.

Kuna kipindi ambapo moyo unataka  kusiko kwa kawaida kwa sababu ya kutanuka kwa misuli ambayo imeuzunguka moyo au kwa sababu ya kutanuka kwa kuta za moyo, kwa hiyo moyo unatumia nguvu sana kusukuma damu na kusababisha misuli yake kutanuka. Sababu kuu ambazo Usababisha moyo kutanuka ni kuwepo kwa presha kubwa juu. Kuwepo kwa Maambukizi kwenye mishipa ya moyo na mambo mengine kama hayo.

 

10. Aina nyingine ya magonjwa ya moyo ni kuwepo kwa Shinikizo la damu kwa kitaalamu huitwa blood pressure, ni hali ambayo utokea kama kuna presha iko juu kwa sababu ya moyo kutumia nguvu katika kusukuma damu au pengine kama mwili una Maambukizi vile usababisha kuwepo kwa shinikizo la damu au pengine ni kwa  sababu ya kuwepo kwa mafuta kwenye mishipa ya damu ambapo damu kidogo uruhusiwe kupita na hapo mwili unahitaji kiwango kikubwa cha damu, kwa hiyo moyo usukuma damu kwa nguvu na kusababisha shinikizo la damu.

 

11. Chembe ya moyo. Pia hii nayo ni aina ya magonjwa ya moyo kwa kawaida mgonjwa uhisi maumivu kwenye kifua hali hii inaweza kutokea kama mtu anafanya kazi au amekataa,  Maumivu pia uendana pamoja na kutokwa na jasho pia kukosa hewa safi, hasa hasa tatizo hili utokea kama mgonjwa hana damu ya kutosha mwilini.

 

12.Aina nyingine ni kufa kwa  sehemu ya misuli ya moyo.

Kuna wakati mwingine sehemu za misuli ya moyo zinakufa hali ambayo Usababisha moyo kushinwa kufanya kazi zake za kila siku na  tatizo kama halijulikana moyo unaweza kushindwa kufanya kazi zake kwa kila siku.

 

13. Aina nyingine ni damu kushindwa kusambaa.

Kuna kipindi moyo inasukuma damu na damu inashindwa kusambaa kwenye sehemu mbalimbali za mwili kwa sababu ya Maambukizi kwenye mishipa ya damu. Hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa mafuta kwenye sehemu mbalimbali za mishipa ya damu.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/03/11/Friday - 09:07:27 pm Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1941

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 ai web app    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Madhara ya Tiba homoni kwa wagonjwa wa saratani

Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba homoni, ni madhara- ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia homoni kama Tiba kwenye kutibu saratani.

Soma Zaidi...
nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ?

mm nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ?

Soma Zaidi...
Dalili za minyoo na sababu zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo na sababu zake

Soma Zaidi...
Madhara ya minyoo

Posti hii inaonyesha kiufupi kabisa madhara ya minyoo kwenye mwili wa binadamu. Yafuatayo Ni madhara ya minyoo;

Soma Zaidi...
Madhara ya maumivu kwenye nyonga na kiuno.

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa matibabu kwenye nyonga na kiuno hayatafanyika.

Soma Zaidi...
MALARIA NI NINI? NI WATU WANGAPI WANAKUFA KWA MALARIA DUNIANI

Malaria ni katika maradhi yanayosumbua sana na kusababisha maradhi ya watu wengi sana duniani.

Soma Zaidi...
MAMBO HATARI KWA MWENYE VIDONDA VYA TUMBO

MAMBO HATARI KWA MWENYE VIDONDA VYA TUMBO Tukiachia mbali kuchukua dawa aina ya NSAIDs, unaweza kuwa na hatari ya kuongezeka kwa vidonda vya tumbo ikiwa: Utakuwa ni mvutaji wa sigara.

Soma Zaidi...
Ni zipi dalili za awali za pumu

Kabla ya kubanwa zaidi na pumu, kuna dalili za awali zinzznza kujitokeza, na hapo ndipo utakapoanza kuchukuwa tahadhari. Makala hii itakwenda kukujulisha zaidi kuhusu dalili hizo.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za kuvimba kope.

Posti hii inaonyesha Dalili na ishara za kuvimba kope ambayo kitaalamu hujulikana Kama blepharitis.

Soma Zaidi...