picha

Fahamu aina mbalimbali za Magonjwa nyemelezi ya moyo

Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za Magonjwa ya moyo,kwa kawaida tunajua wazi kuwa kuna moyo mmoja lakini moyo huo unaweza kushambuliwa na magonjwa kwa kila aina kwa mfano kuna Maambukizi kwenye mishipa ya moyo,au kubadilika kwa mapigo ya moyo na m

1. Kuathirika kwa mishipa ya moyo.

Kwa wakati mwingine kuna kuathirika kwa mishipa ya moyo ambayo kwa kitaalamu huitwa coronary artery, mishipa hii inaweza kupata Maambukizi na kushindwa kusafilisha damu kutoka kwenye moyo na kupeleka sehemu mbalimbali za mwili. Pengine mishipa inaweza kushindwa kusafilisha damu kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu na mafuta kwenye mishipa hali hii usababisha moyo kusukuma damu kwa nguvu ili kuweza kukidhi mahitaji ya mwili hali hii usababisha kuaribika kwa mishipa ya moyo.

 

Kwa hiyo tunapaswa kupunguza vyakula vyenye mafuta mengi na kuhakikisha kuachana na vyakula vyenye sumu ambavyo Usababisha kuwepo kwa mafuta kwenye mishipa na kuwepo kwa uchafu kwenye mishipa kwa kuepuka mambo hayo tutaweza kuruhusu damu kusafili zaidi na kuepuka na kuaribika kwa mishipa ya damu.

 

3.Aina nyingine ya ugonjwa wa moyo ni mapigo ya moyo kwenda tofauti.

Kwa wakati mwingine mapigo ya moyo uenda haraka na kusababisha mtu kuwa  na jasho na pengine mtu anakuwa hatulii sehemu moja . Na pia kwa wakati mwingine kuna kipindi mapigo ya moyo yanaenda taratibu sana kwa hali hii umfanya mtu kupumua kwa shida . Na kuna kipindi kingine mapigo ya moyo uenda ovyoovyo bila mpangilio hali hii ni mbaya sana inaweza kusababisha matatizo mengine makubwa kama vile kupoteza maisha.

 

4.Kwa wahudumu na ndugu wa mgonjwa baada ya kuona dalili kama hizi wanapaswa kumpeleka mgonjwa hospitalini ili aweze kupata matibabu kwa sababu hali ya kubadilika ki mapigo huwa sio nzuri hasa kwa mgonjwa yule ambaye ni mara yake ya kwanza kwa sababu anaweza kupanic na kuona kuwa ndio mwisho basi tuwafariji na kuwa pamoja nao ili waweze kupata huduma za muhimu.

 

5. Aina nyingine ni ile ya moyo kushindwa kufanya kazi.

Kuna kipindi ambapo moyo unashindwa kufanya kazi kwa sababu mbalimbali kama vile kuwepo kwa kiasi kidogo cha damu kwenye mwili au Maambukizi kwenye valve za mishipa.kwa hiyo hali  hii isipogunduliwa mapema Mgonjwa anaweza kupoteza maisha kwa watu wenye tatizo kama hili wanaweza kutumia kifaa maalum ambacho usaidia moyo ili uweze kufanya kazi na pia kifaa hicho kwa kawaida huwa kinabadilika mara kwa mara kadri ya maoni ya wataalamu wa afya.

 

6.Kuna wakati mwingine moyo ushindwa kufanya kazi kwa ghafla kwa sababu ya matukio mbalimbali na kuna huduma ambayo utolewa kwa ajili ya kushutua moyo huduma hiyo uitwa cardiopulmonary Resuscitation, hii huduma utolewa kwa wale wenye utamaalamu na mafunzo maalum kwa ajili ya kushutua moyo uliosimama ghafla.

 

7. Kuna aina nyingine t Magonjwa ya moyo ambayo huwapata watoto

Kwa wakati mwingine watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo kwa sababu kuna kesi mbalimbali zinazoonyesha kuwa mtoto amezaliwa na tundu kwenye moyo, hali hii utokea kwa sababu ya mtindo wa maisha kwa Mama wajawazito kama vile uvutaji wa sigara, utumiaji wa madawa ya kulevya wakati wa ujauzito na pia kutumia vileo vikali wakati wa ujauzito hayo yote usababisha watoto kuzaliwa na matundu kwenye Aorta.

 

8.Kwa hiyo ili kuepuka na matatizo haya wanawake wakati wa ujauzito wanapaswa kufuata mashariti ya wataalamu wa afya na kuachana na vileo, madawa ya kulevya, pombe kali na mambo kama  hayo ili kuweza kuepuka matatizo kama hayo wakati wa ujauzito, kwa hiyo akina Mama pia wahudhuria maudhurio yote ya kliniki ili kuweza kusikiliza mafundisho kwa sababu hayo mafundisho utolewa kila mwezi kipindi mama akiwa kwenye mahudhurio ya kawaida.

 

9. Aina nyingine ya Magonjwa ya moyo ni pamoja na moyo kutanuka.

Kuna kipindi ambapo moyo unataka  kusiko kwa kawaida kwa sababu ya kutanuka kwa misuli ambayo imeuzunguka moyo au kwa sababu ya kutanuka kwa kuta za moyo, kwa hiyo moyo unatumia nguvu sana kusukuma damu na kusababisha misuli yake kutanuka. Sababu kuu ambazo Usababisha moyo kutanuka ni kuwepo kwa presha kubwa juu. Kuwepo kwa Maambukizi kwenye mishipa ya moyo na mambo mengine kama hayo.

 

10. Aina nyingine ya magonjwa ya moyo ni kuwepo kwa Shinikizo la damu kwa kitaalamu huitwa blood pressure, ni hali ambayo utokea kama kuna presha iko juu kwa sababu ya moyo kutumia nguvu katika kusukuma damu au pengine kama mwili una Maambukizi vile usababisha kuwepo kwa shinikizo la damu au pengine ni kwa  sababu ya kuwepo kwa mafuta kwenye mishipa ya damu ambapo damu kidogo uruhusiwe kupita na hapo mwili unahitaji kiwango kikubwa cha damu, kwa hiyo moyo usukuma damu kwa nguvu na kusababisha shinikizo la damu.

 

11. Chembe ya moyo. Pia hii nayo ni aina ya magonjwa ya moyo kwa kawaida mgonjwa uhisi maumivu kwenye kifua hali hii inaweza kutokea kama mtu anafanya kazi au amekataa,  Maumivu pia uendana pamoja na kutokwa na jasho pia kukosa hewa safi, hasa hasa tatizo hili utokea kama mgonjwa hana damu ya kutosha mwilini.

 

12.Aina nyingine ni kufa kwa  sehemu ya misuli ya moyo.

Kuna wakati mwingine sehemu za misuli ya moyo zinakufa hali ambayo Usababisha moyo kushinwa kufanya kazi zake za kila siku na  tatizo kama halijulikana moyo unaweza kushindwa kufanya kazi zake kwa kila siku.

 

13. Aina nyingine ni damu kushindwa kusambaa.

Kuna kipindi moyo inasukuma damu na damu inashindwa kusambaa kwenye sehemu mbalimbali za mwili kwa sababu ya Maambukizi kwenye mishipa ya damu. Hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa mafuta kwenye sehemu mbalimbali za mishipa ya damu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2116

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 web hosting     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Mabadiliko ya mwili katika wiki za mwanzo za mimba

​Wiki za kwanza za ujauzito ni kipindi cha mabadiliko makubwa ya ndani na nje ya mwili wa mwanamke. Makala hii inafafanua mabadiliko hayo ili kumsaidia mama kuelewa kinachoendelea na jinsi ya kukabiliana na hali hiyo kwa usalama.Utangulizi​Wakati mwingine, mabadiliko ya mwili huanza kujitokeza hata kabla hujapima na kupata majibu chanya ya mimba. Hii inatokana na msukosuko wa homoni unaolenga kutengeneza mazingira rafiki kwa ukuaji wa kiumbe kilichotungwa. Kuelewa dalili hizi ni muhimu ili uweze kujijali na kumpa mtoto wako nafasi nzuri zaidi ya ukuaji kuanzia siku ya kwanza.​Maudhui: Mabadiliko ya Mwili katika Wiki za Mwanzo​Katika kipindi hiki, mwili wako unafanya kazi kubwa kurekebisha mfumo wake:​Mabadiliko ya Homoni: Kiwango cha homoni za estrogen na progesterone hupanda kwa kasi ili kusaidia ujauzito, hali inayoweza kubadili hisia zako (mood swings).​Mabadiliko katika Matiti: Matiti yanaweza kuwa makubwa, mazito, na yenye maumivu mepesi kutokana na kuongezeka kwa mtiririko wa damu na kujiandaa kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa.​Mabadiliko ya Mfumo wa Chakula: Unaweza kuhisi kichefuchefu, hasa asubuhi, au kupata mabadiliko ya ladha (kuchukia vyakula fulani ulivyokuwa unapenda awali).​Uchovu: Mwili hutumia nishati nyingi katika wiki za mwanzo kuunda mfumo wa kondo la nyuma (placenta), hali inayokufanya uhisi uchovu na usingizi wa mara kwa mara.​Kukojoa Mara kwa Mara: Uterasi inapoanza kukua na shinikizo la damu kuongezeka, kibofu cha mkojo hupata shinikizo zaidi, jambo linalokufanya utake kwenda chooni mara kwa mara.​Fact Check: Je, mabadiliko haya ni hatari?​Ukweli: Mabadiliko mengi unayoyahisi ni ya kawaida kabisa na ni ishara kuwa mwili wako unakubali ujauzito. Hata hivyo, si kila mwanamke anapata dalili hizi zote.​Tahadhari: Ikiwa utapata dalili hizi, unapaswa kuonana na daktari mara moja:​Maumivu makali ya tumbo (upande mmoja au sehemu ya chini).​Kutokwa na damu nyingi ukeni (vaginal bleeding).​Homa kali au maumivu wakati wa kukojoa.​Kutapika sana kiasi cha kushindwa kuhifadhi maji mwilini.​Hitimisho​Mabadiliko ya mwili katika wiki za mwanzo ni ishara ya maajabu ya kimaumbile yanayotokea ndani yako. Ingawa baadhi ya hali hizi zinaweza kuwa kero, kumbuka kuwa ni za muda mfupi. Kula mlo kamili, kunywa maji ya kutosha, na kupumzika ipasavyo kutakusaidia kupitia kipindi hiki kwa urahisi zaidi. Usisahau kuhudhuria kliniki mapema ili kupata ushauri wa kitaalamu na ufuatiliaji wa ukuaji wa mtoto wako

Soma Zaidi...
Dalili za ukimwi, unavyoenezwa na njia za kujikinga

Ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini.unasababishwa na virusi ambavyo hutokea kwa mtu mwingine kwa njia mbalimbali

Soma Zaidi...
Dalili za malaria

Malaria ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu kwa kitaalamu anaitwa Anopheles.na anasambazwa na mbu jike pale anapotafuta chakula hasa wakati akiwa na mimba. Mbu hawa hupenda kuishi kwenye mnyasi, madibwi haswa kwenye maji yaliyo simama.

Soma Zaidi...
Polio (Kilema cha utotoni): Dalili na umuhimu wa chanjo.

Ugonjwa wa Polio, unaojulikana kitaalamu kama Poliomyelitis, ni ugonjwa hatari wa kuambukiza unaosababishwa na virusi vya Polio (Poliovirus). Ugonjwa huu huathiri mfumo wa neva na unaweza kusababisha ulemavu wa kudumu au kifo ndani ya saa chache. Licha ya juhudi kubwa za kimataifa kutokomeza ugonjwa huu, bado ni tishio katika maeneo machache duniani. Makala hii inachunguza kwa kina biolojia ya ugonjwa, dalili zake, athari za muda mrefu, na umuhimu wa chanjo kama nyenzo pekee ya kuzuia maambukizi.

Soma Zaidi...
Fangasi aina ya Candida

Huu ni ugonjwa wa fangasi wanaosababishwa na mashambulizi ya fangani aia ya yeast waitwao candida.

Soma Zaidi...