Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za Magonjwa ya moyo,kwa kawaida tunajua wazi kuwa kuna moyo mmoja lakini moyo huo unaweza kushambuliwa na magonjwa kwa kila aina kwa mfano kuna Maambukizi kwenye mishipa ya moyo,au kubadilika kwa mapigo ya moyo na m
1. Kuathirika kwa mishipa ya moyo.
Kwa wakati mwingine kuna kuathirika kwa mishipa ya moyo ambayo kwa kitaalamu huitwa coronary artery, mishipa hii inaweza kupata Maambukizi na kushindwa kusafilisha damu kutoka kwenye moyo na kupeleka sehemu mbalimbali za mwili. Pengine mishipa inaweza kushindwa kusafilisha damu kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu na mafuta kwenye mishipa hali hii usababisha moyo kusukuma damu kwa nguvu ili kuweza kukidhi mahitaji ya mwili hali hii usababisha kuaribika kwa mishipa ya moyo.
Kwa hiyo tunapaswa kupunguza vyakula vyenye mafuta mengi na kuhakikisha kuachana na vyakula vyenye sumu ambavyo Usababisha kuwepo kwa mafuta kwenye mishipa na kuwepo kwa uchafu kwenye mishipa kwa kuepuka mambo hayo tutaweza kuruhusu damu kusafili zaidi na kuepuka na kuaribika kwa mishipa ya damu.
3.Aina nyingine ya ugonjwa wa moyo ni mapigo ya moyo kwenda tofauti.
Kwa wakati mwingine mapigo ya moyo uenda haraka na kusababisha mtu kuwa na jasho na pengine mtu anakuwa hatulii sehemu moja . Na pia kwa wakati mwingine kuna kipindi mapigo ya moyo yanaenda taratibu sana kwa hali hii umfanya mtu kupumua kwa shida . Na kuna kipindi kingine mapigo ya moyo uenda ovyoovyo bila mpangilio hali hii ni mbaya sana inaweza kusababisha matatizo mengine makubwa kama vile kupoteza maisha.
4.Kwa wahudumu na ndugu wa mgonjwa baada ya kuona dalili kama hizi wanapaswa kumpeleka mgonjwa hospitalini ili aweze kupata matibabu kwa sababu hali ya kubadilika ki mapigo huwa sio nzuri hasa kwa mgonjwa yule ambaye ni mara yake ya kwanza kwa sababu anaweza kupanic na kuona kuwa ndio mwisho basi tuwafariji na kuwa pamoja nao ili waweze kupata huduma za muhimu.
5. Aina nyingine ni ile ya moyo kushindwa kufanya kazi.
Kuna kipindi ambapo moyo unashindwa kufanya kazi kwa sababu mbalimbali kama vile kuwepo kwa kiasi kidogo cha damu kwenye mwili au Maambukizi kwenye valve za mishipa.kwa hiyo hali hii isipogunduliwa mapema Mgonjwa anaweza kupoteza maisha kwa watu wenye tatizo kama hili wanaweza kutumia kifaa maalum ambacho usaidia moyo ili uweze kufanya kazi na pia kifaa hicho kwa kawaida huwa kinabadilika mara kwa mara kadri ya maoni ya wataalamu wa afya.
6.Kuna wakati mwingine moyo ushindwa kufanya kazi kwa ghafla kwa sababu ya matukio mbalimbali na kuna huduma ambayo utolewa kwa ajili ya kushutua moyo huduma hiyo uitwa cardiopulmonary Resuscitation, hii huduma utolewa kwa wale wenye utamaalamu na mafunzo maalum kwa ajili ya kushutua moyo uliosimama ghafla.
7. Kuna aina nyingine t Magonjwa ya moyo ambayo huwapata watoto
Kwa wakati mwingine watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo kwa sababu kuna kesi mbalimbali zinazoonyesha kuwa mtoto amezaliwa na tundu kwenye moyo, hali hii utokea kwa sababu ya mtindo wa maisha kwa Mama wajawazito kama vile uvutaji wa sigara, utumiaji wa madawa ya kulevya wakati wa ujauzito na pia kutumia vileo vikali wakati wa ujauzito hayo yote usababisha watoto kuzaliwa na matundu kwenye Aorta.
8.Kwa hiyo ili kuepuka na matatizo haya wanawake wakati wa ujauzito wanapaswa kufuata mashariti ya wataalamu wa afya na kuachana na vileo, madawa ya kulevya, pombe kali na mambo kama hayo ili kuweza kuepuka matatizo kama hayo wakati wa ujauzito, kwa hiyo akina Mama pia wahudhuria maudhurio yote ya kliniki ili kuweza kusikiliza mafundisho kwa sababu hayo mafundisho utolewa kila mwezi kipindi mama akiwa kwenye mahudhurio ya kawaida.
9. Aina nyingine ya Magonjwa ya moyo ni pamoja na moyo kutanuka.
Kuna kipindi ambapo moyo unataka kusiko kwa kawaida kwa sababu ya kutanuka kwa misuli ambayo imeuzunguka moyo au kwa sababu ya kutanuka kwa kuta za moyo, kwa hiyo moyo unatumia nguvu sana kusukuma damu na kusababisha misuli yake kutanuka. Sababu kuu ambazo Usababisha moyo kutanuka ni kuwepo kwa presha kubwa juu. Kuwepo kwa Maambukizi kwenye mishipa ya moyo na mambo mengine kama hayo.
10. Aina nyingine ya magonjwa ya moyo ni kuwepo kwa Shinikizo la damu kwa kitaalamu huitwa blood pressure, ni hali ambayo utokea kama kuna presha iko juu kwa sababu ya moyo kutumia nguvu katika kusukuma damu au pengine kama mwili una Maambukizi vile usababisha kuwepo kwa shinikizo la damu au pengine ni kwa sababu ya kuwepo kwa mafuta kwenye mishipa ya damu ambapo damu kidogo uruhusiwe kupita na hapo mwili unahitaji kiwango kikubwa cha damu, kwa hiyo moyo usukuma damu kwa nguvu na kusababisha shinikizo la damu.
11. Chembe ya moyo. Pia hii nayo ni aina ya magonjwa ya moyo kwa kawaida mgonjwa uhisi maumivu kwenye kifua hali hii inaweza kutokea kama mtu anafanya kazi au amekataa, Maumivu pia uendana pamoja na kutokwa na jasho pia kukosa hewa safi, hasa hasa tatizo hili utokea kama mgonjwa hana damu ya kutosha mwilini.
12.Aina nyingine ni kufa kwa sehemu ya misuli ya moyo.
Kuna wakati mwingine sehemu za misuli ya moyo zinakufa hali ambayo Usababisha moyo kushinwa kufanya kazi zake za kila siku na tatizo kama halijulikana moyo unaweza kushindwa kufanya kazi zake kwa kila siku.
13. Aina nyingine ni damu kushindwa kusambaa.
Kuna kipindi moyo inasukuma damu na damu inashindwa kusambaa kwenye sehemu mbalimbali za mwili kwa sababu ya Maambukizi kwenye mishipa ya damu. Hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa mafuta kwenye sehemu mbalimbali za mishipa ya damu.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Hapa utajifunza sababu za kuwepo na maumovu ya tumbe kitomvuni.
Soma Zaidi...Watoto wachanga ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano, watoto hawa hushambulia na maginjwa mara kwa mara na kusababisha ukuaji wao kuwa dunk,
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili na Sababu za Homa ya manjano ya watoto wachanga ni kubadilika rangi kwa manjano katika ngozi na macho ya mtoto mchanga. Homa ya manjano ya mtoto hutokea kwa sababu damu ya mtoto ina ziada ya rangi ya
Soma Zaidi...Kama unahisi maumivu ya tumbo huwenda umejiuliza swali hili ukiwa kama mwanamke "Je maumivu juu ya kitovu ni miongoni mwa dalili za mimba?". Post hii inakwenda kujibu swali hili
Soma Zaidi...Post hii inahusu dalili za mtu Mwenye ugonjwa wa kisukari, dalili hizi zinaweza kujitokeza Moja kwa Moja mtu akagundua kuwa ana Ugonjwa wa kisukari.zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kisukari.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia ugonjwa wa Homa ya inni, ni njia ambazo utumiwa Ili kuepuka kusambaa kwa ugonjwa wa Homa ya inni kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine,
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo
Soma Zaidi...Post hii inahusu Zaidi tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,ni tatizo ambalo usababishwa na bakteria ambao uingia kwenye mapafu na kusababisha madhara na hatimaye mapafu kuwa na usaha .
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hatua mbalimbali za Ugonjwa wa Ukimwi, kawaida Ugonjwa huu huwa na hatua kuu nne ila kila hatua huwa na sifa zake kwa hiyo tunapaswa kujua hatua za Ugonjwa huu na kujaribu kuzuia maambukizi yasisambae kabisa.
Soma Zaidi...Malaria ni katika maradhi yanayosumbua sana na kusababisha maradhi ya watu wengi sana duniani.
Soma Zaidi...