Saratani (cancer)
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maradhi ya cancer/saratani
SARATANI (CANCER)
Saratani ni ugonjwa unaotokana na kukuwa kwa seli ndani ya mwili bila ya mpangilio maalumu. Kukuwa huku kunashindwa kuthibitika ndani ya mwili. Seli hizi hukuwa na kusababisha kitu kinachoitwa kitaalamu tumor. Hii ni mkusanyiko wa hizi seli ambazo zimekuwa bila ya mpangilio maalumu ndani ya mwili. Hizi tumor husababisha kutokea kwa malignant tumor na hii ni mkusanyiko mkubwa wa hizi seli ambao huuwa seli nyingine za mwili na tishu. Hutokea wakati mwingine huu mkusanyiko ukawepo ila ukawa hauna madhara kwa seli nyingine, huu utaitwa benign tumor ila zikikuwa zaidi huweza kuathiri tishu za mwili. Hizi tumor zinaweza kuingia kwenye mfumo wa damu na kuenea sehemu zingine za mwili.
Seli za saratani ni hatari zaidi kwani zinaweza kuharibu tishu na viungo vingine vya mwili kama ubongo na maini. Kiti hatari zaidi kwenye seli hizi ni kuwa zinaweza kuhama sehemu moja ya mwili kwenda sehemu nyingine. Kwa mfano saratani ya maini inaweza kuenea kwenye ubongo na kusababisha saratani ya ubongo. Saratani ya matiti na korodani inaweza kuenea kwenye mifupa na kusababisha saratani ya mifupa.
Hali hii hufanya seli hizi ziwe hatari zaidi. Mchakato huu wa kuhama sehemu moja kwenda nyingine huitwa kitaalamu metastasisi.
Seli ya saratani ya kwanza hutokea pale gene zinapopata hitilafu. Gene ni chembechembe ambazo huhusika katika kutengenezwa kwa selimmpya. Mtu anaweza kurithi gene hizi ambazo zimeharibiwa toka kuzaliwa ama akawa anazo zimeharibiwa kwa sababi zingine. Ila mtu huyu aliyerithi gene ambazo zina hitilafu ni rahisi kwake kupata saratani zaidi kuliko huyu ambaye hajarithi. Kama tulivyoona juu kule kuna mawakala wa kueneza maradhi, hali kama hii kuna mawakala wa kusababisha saratani ambao huitwa carcinogens hawa pia huhusika katika kutia hitilafu kwenye genes. Mifano ya mawakala hawa (carcinogens ) ni ;-
1.Aina flani ya virusi kama vile papilloma virus (HPV)
2.Mionzi kama radio na ulteraviolent (UV) na mionzi mingineyo.
3.Kemikali zinazopatikana kwenye tumbaku kama arsenic, benzene na formaldehyde
4.Asbestos haya ni malighafi zinazotumika kutengezea vifaa vya umeme na vifaa vingine vya nyumba kama vya kuzuia moto.
Ni vigumu sana kuepukana na mawakala hawa kwenye maisha, kwani huweza kupatokana kwwenye vyakula vyetu, shuhuli zetukwenye maji na hewa. Ila tutakujaona kwamba unaweza kujiepusha na hatari za saratani kwani karibia mawakala walotajwa hapo juu hueneza saratani ila kwa uchache ila tumbaku ni kwa kiasi kikubwa sana.
Unaweza ukagunduwa saratani kwa kutumia vifaa vya kitaalamu kama MRI, x-rays, biospy, na DNA test. Pia unaweza ukajijua mwenyewe kama una tumor kwa kujishika sehemu husika na kuona kama kuna uvimbe wowote usio wa kawaida. Pia ijulikane kuwa zipo tiba za saratani ijapokuwa kuimaliza kabisa mwilini ni kazi mzito ila ukweli ni kuwa karibia aina zote za saratani zinaweza kutibiwa kama mtu atawahi kwa haraka.baadhi ya njia wanazotumia kupambana na saratani ni kama
A)kufanyiwa upasuaji, hufanyika kwa ufasaha zaidi kama saratani haijaenea zaidi
B)Kufanya chemotherapy ni matumizi ya dawa kwa ajili ya kuuwa seli za saratani, ila kwa bahati mbaya njia hii pia huuwa seli nyingine za mwili
C)Radiation therapy ni kutumia mionzi kwa ajili ya kuuwa seli za saratani
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 ai web app π2 web hosting π3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π4 Madrasa kiganjani π5 Dua za Mitume na Manabii π6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Samahan naomb kujua staili za tendo la ndoa
Post hii inakwenda kujibu swali la muulizaji. Kuhusu syyle za tendo la ndoa
Soma Zaidi...Gout (Ugonjwa wa baridi ya yabisi): Dalili na vyakula vya kuepuka.
Gout ni aina ngumu ya ugonjwa wa baridi ya yabisi (arthritis) inayojulikana kwa kusababisha maumivu makali ya ghafla, uvimbe, na wekundu kwenye viungo, hasa kidole gumba cha mguu. Hali hii husababishwa na mrundikano wa asidi ya uric (uric acid) kwenye damu, ambayo huunda fuwele (crystals) ndogo zinazochoma viungo. Makala haya yanakupa mwongozo wa kina kuhusu namna ya kutambua dalili za gout na hatua za lishe za kuchukua ili kudhibiti maumivu na kuzuia mashambulizi ya mara kwa mara.
Soma Zaidi...KAMA UNASUMBULIWA NA FANGASI
Post hii fupi inakwenda kukujuza juu ya tatizo la fangasi na nini ufanye.
Soma Zaidi...DALILI ZA MINYOO: maumivu ya tumbo, kichwa, kuwashwa, kutapika damu, moyo kuumwa, ukuaji hafifu, udhaifu na kuchoka
DALILI ZA MINYOO Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa ngozi (Eczema): Sababu na jinsi ya kutunza ngozi.
βMuhtasari βEczema, inayofahamika kitaalamu kama atopic dermatitis, ni hali ya ngozi kuwa kavu, kuwasha, na kupata vipele vinavyoweza kujitokeza mara kwa mara. Makala haya yameandaliwa kwa kina kuchunguza visababishi vya eczema, vichochezi vyake, na kutoa mwongozo wa kitaalamu wa jinsi ya kutunza ngozi ili kudhibiti hali hii na kuboresha maisha ya kila siku.
Soma Zaidi...Saratani ya Matiti ya wanaume.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Saratani ya matiti ya Mwanaume ni Saratani nadra ambayo hutokea katika tishu za matiti za wanaume. Ingawa saratani ya matiti hufikiriwa zaidi kuwa ugonjwa wa wanawake, saratani ya matiti ya mwanaume hutokea. Saratani y
Soma Zaidi...