picha

Saratani (cancer)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maradhi ya cancer/saratani

SARATANI (CANCER)

Saratani ni ugonjwa unaotokana na kukuwa kwa seli ndani ya mwili bila ya mpangilio maalumu. Kukuwa huku kunashindwa kuthibitika ndani ya mwili. Seli hizi hukuwa na kusababisha kitu kinachoitwa kitaalamu tumor. Hii ni mkusanyiko wa hizi seli ambazo zimekuwa bila ya mpangilio maalumu ndani ya mwili. Hizi tumor husababisha kutokea kwa malignant tumor na hii ni mkusanyiko mkubwa wa hizi seli ambao huuwa seli nyingine za mwili na tishu. Hutokea wakati mwingine huu mkusanyiko ukawepo ila ukawa hauna madhara kwa seli nyingine, huu utaitwa benign tumor ila zikikuwa zaidi huweza kuathiri tishu za mwili. Hizi tumor zinaweza kuingia kwenye mfumo wa damu na kuenea sehemu zingine za mwili.

 

Seli za saratani ni hatari zaidi kwani zinaweza kuharibu tishu na viungo vingine vya mwili kama ubongo na maini. Kiti hatari zaidi kwenye seli hizi ni kuwa zinaweza kuhama sehemu moja ya mwili kwenda sehemu nyingine. Kwa mfano saratani ya maini inaweza kuenea kwenye ubongo na kusababisha saratani ya ubongo. Saratani ya matiti na korodani inaweza kuenea kwenye mifupa na kusababisha saratani ya mifupa.

 

Hali hii hufanya seli hizi ziwe hatari zaidi. Mchakato huu wa kuhama sehemu moja kwenda nyingine huitwa kitaalamu metastasisi.

 

Seli ya saratani ya kwanza hutokea pale gene zinapopata hitilafu. Gene ni chembechembe ambazo huhusika katika kutengenezwa kwa selimmpya. Mtu anaweza kurithi gene hizi ambazo zimeharibiwa toka kuzaliwa ama akawa anazo zimeharibiwa kwa sababi zingine. Ila mtu huyu aliyerithi gene ambazo zina hitilafu ni rahisi kwake kupata saratani zaidi kuliko huyu ambaye hajarithi. Kama tulivyoona juu kule kuna mawakala wa kueneza maradhi, hali kama hii kuna mawakala wa kusababisha saratani ambao huitwa carcinogens hawa pia huhusika katika kutia hitilafu kwenye genes. Mifano ya mawakala hawa (carcinogens ) ni ;-

1.Aina flani ya virusi kama vile papilloma virus (HPV)

2.Mionzi kama radio na ulteraviolent (UV) na mionzi mingineyo.

3.Kemikali zinazopatikana kwenye tumbaku kama arsenic, benzene na formaldehyde

4.Asbestos haya ni malighafi zinazotumika kutengezea vifaa vya umeme na vifaa vingine vya nyumba kama vya kuzuia moto.

 

Ni vigumu sana kuepukana na mawakala hawa kwenye maisha, kwani huweza kupatokana kwwenye vyakula vyetu, shuhuli zetukwenye maji na hewa. Ila tutakujaona kwamba unaweza kujiepusha na hatari za saratani kwani karibia mawakala walotajwa hapo juu hueneza saratani ila kwa uchache ila tumbaku ni kwa kiasi kikubwa sana.

 

Unaweza ukagunduwa saratani kwa kutumia vifaa vya kitaalamu kama MRI, x-rays, biospy, na DNA test. Pia unaweza ukajijua mwenyewe kama una tumor kwa kujishika sehemu husika na kuona kama kuna uvimbe wowote usio wa kawaida. Pia ijulikane kuwa zipo tiba za saratani ijapokuwa kuimaliza kabisa mwilini ni kazi mzito ila ukweli ni kuwa karibia aina zote za saratani zinaweza kutibiwa kama mtu atawahi kwa haraka.baadhi ya njia wanazotumia kupambana na saratani ni kama

A)kufanyiwa upasuaji, hufanyika kwa ufasaha zaidi kama saratani haijaenea zaidi

B)Kufanya chemotherapy ni matumizi ya dawa kwa ajili ya kuuwa seli za saratani, ila kwa bahati mbaya njia hii pia huuwa seli nyingine za mwili

C)Radiation therapy ni kutumia mionzi kwa ajili ya kuuwa seli za saratani

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1925

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 web hosting     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa macho

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa macho, ni ugonjwa ambao ushambulia zaidi sehemu za nje za macho ambazo kwa kawaida uitwa conjunctiva na cornea hizi sehemu zikipata maambukizi zisipotibiwa mapema uweza kusababisha upofu kwa mgonjwa.

Soma Zaidi...
Mazoezi 5 rahisi ya kupunguza uzito na kuimarisha moyo.

Mazoezi ya moyo (cardio) ni ufunguo wa kuchoma mafuta, kuimarisha misuli ya moyo, na kuboresha mfumo mzima wa mzunguko wa damu. Sio lazima uwe na vifaa vya gharama au kujiunga na ukumbi wa mazoezi ili uweze kufanya mazoezi yenye tija. Makala haya yanakuletea mazoezi 5 rahisi, yanayopatikana, na yenye ufanisi mkubwa ambayo unaweza kuyafanya popote pale ili kuanza safari yako ya kupunguza uzito na kulinda afya ya moyo wako.

Soma Zaidi...
Dalili za selulitis.

Selulitis ni maambukizi ya ngozi ya bakteria ya kawaida, ambayo yanaweza kuwa mbaya. Cellulitis inaonekana kama sehemu nyekundu ya ngozi iliyovimba na inahisi joto na laini. Inaweza kuenea kwa kasi kwa sehemu nyingine za mwili. Cellulitis haienei kuto

Soma Zaidi...
Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Hofu ya kufanya makosa (Perfectionism) na jinsi ya kuikabili.

​Katika ulimwengu wa ushindani na mitandao ya kijamii, wengi wetu tunajikuta tukinyongwa na mzigo wa kutaka kila kitu kiwe "kamilifu." Makala hii inachunguza kwa kina dhana ya perfectionism—hofu inayozuia ubunifu na maendeleo. Tutachambua kwa nini tunahofu kufanya makosa, athari zake katika afya ya akili na tija, na kutoa mwongozo wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kuachana na tabia hii ili kufikia mafanikio ya kweli kupitia kukubali mapungufu.

Soma Zaidi...
Dalili za Fangasi Ukeni kwa Mwanamke

​Makala hii inaangazia maambukizi ya fangasi ukeni (vaginal yeast infection), hali inayowapata wanawake wengi katika hatua mbalimbali za maisha. Tutaangalia dalili kuu za utambuzi, sababu zinazochangia maambukizi haya, na ukweli wa kisayansi kuhusu jinsi ya kuyashughulikia.

Soma Zaidi...