Saratani (cancer)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maradhi ya cancer/saratani

SARATANI (CANCER)

Saratani ni ugonjwa unaotokana na kukuwa kwa seli ndani ya mwili bila ya mpangilio maalumu. Kukuwa huku kunashindwa kuthibitika ndani ya mwili. Seli hizi hukuwa na kusababisha kitu kinachoitwa kitaalamu tumor. Hii ni mkusanyiko wa hizi seli ambazo zimekuwa bila ya mpangilio maalumu ndani ya mwili. Hizi tumor husababisha kutokea kwa malignant tumor na hii ni mkusanyiko mkubwa wa hizi seli ambao huuwa seli nyingine za mwili na tishu. Hutokea wakati mwingine huu mkusanyiko ukawepo ila ukawa hauna madhara kwa seli nyingine, huu utaitwa benign tumor ila zikikuwa zaidi huweza kuathiri tishu za mwili. Hizi tumor zinaweza kuingia kwenye mfumo wa damu na kuenea sehemu zingine za mwili.

 

Seli za saratani ni hatari zaidi kwani zinaweza kuharibu tishu na viungo vingine vya mwili kama ubongo na maini. Kiti hatari zaidi kwenye seli hizi ni kuwa zinaweza kuhama sehemu moja ya mwili kwenda sehemu nyingine. Kwa mfano saratani ya maini inaweza kuenea kwenye ubongo na kusababisha saratani ya ubongo. Saratani ya matiti na korodani inaweza kuenea kwenye mifupa na kusababisha saratani ya mifupa.

 

Hali hii hufanya seli hizi ziwe hatari zaidi. Mchakato huu wa kuhama sehemu moja kwenda nyingine huitwa kitaalamu metastasisi.

 

Seli ya saratani ya kwanza hutokea pale gene zinapopata hitilafu. Gene ni chembechembe ambazo huhusika katika kutengenezwa kwa selimmpya. Mtu anaweza kurithi gene hizi ambazo zimeharibiwa toka kuzaliwa ama akawa anazo zimeharibiwa kwa sababi zingine. Ila mtu huyu aliyerithi gene ambazo zina hitilafu ni rahisi kwake kupata saratani zaidi kuliko huyu ambaye hajarithi. Kama tulivyoona juu kule kuna mawakala wa kueneza maradhi, hali kama hii kuna mawakala wa kusababisha saratani ambao huitwa carcinogens hawa pia huhusika katika kutia hitilafu kwenye genes. Mifano ya mawakala hawa (carcinogens ) ni ;-

1.Aina flani ya virusi kama vile papilloma virus (HPV)

2.Mionzi kama radio na ulteraviolent (UV) na mionzi mingineyo.

3.Kemikali zinazopatikana kwenye tumbaku kama arsenic, benzene na formaldehyde

4.Asbestos haya ni malighafi zinazotumika kutengezea vifaa vya umeme na vifaa vingine vya nyumba kama vya kuzuia moto.

 

Ni vigumu sana kuepukana na mawakala hawa kwenye maisha, kwani huweza kupatokana kwwenye vyakula vyetu, shuhuli zetukwenye maji na hewa. Ila tutakujaona kwamba unaweza kujiepusha na hatari za saratani kwani karibia mawakala walotajwa hapo juu hueneza saratani ila kwa uchache ila tumbaku ni kwa kiasi kikubwa sana.

 

Unaweza ukagunduwa saratani kwa kutumia vifaa vya kitaalamu kama MRI, x-rays, biospy, na DNA test. Pia unaweza ukajijua mwenyewe kama una tumor kwa kujishika sehemu husika na kuona kama kuna uvimbe wowote usio wa kawaida. Pia ijulikane kuwa zipo tiba za saratani ijapokuwa kuimaliza kabisa mwilini ni kazi mzito ila ukweli ni kuwa karibia aina zote za saratani zinaweza kutibiwa kama mtu atawahi kwa haraka.baadhi ya njia wanazotumia kupambana na saratani ni kama

A)kufanyiwa upasuaji, hufanyika kwa ufasaha zaidi kama saratani haijaenea zaidi

B)Kufanya chemotherapy ni matumizi ya dawa kwa ajili ya kuuwa seli za saratani, ila kwa bahati mbaya njia hii pia huuwa seli nyingine za mwili

C)Radiation therapy ni kutumia mionzi kwa ajili ya kuuwa seli za saratani

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1214

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Dalili za ugonjwa sugu wa Figo.

Ugonjwa sugu wa figo, pia huitwa kushindwa kwa figo sugu, huelezea upotevu wa taratibu wa utendakazi wa figo. Figo zako huchuja taka na Majimaji kupita kiasi kutoka kwa damu yako, ambayo hutolewa kwenye mkojo wako. Ugonjwa sugu wa figo unapofikia hatua

Soma Zaidi...
Vyanzo vya sumu mwilini.

Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuwepo kwa sumu mwilini, kwa sababu kuna wakati mwingine tunapata magonjwa na matatizo mbalimbali ya ki afya tunaangaika huku na huko kumbe sababu kubwa ni kuwepo kwa sumu mwilini na vyanzo vya sumu hiyo ni kama ifuatavy

Soma Zaidi...
Minyoo Ni nini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya minyoo

Soma Zaidi...
Hatua tatu anazozipitia mgonjwa wa tauni

Posti hii inahusu zaidi njia au hatua tatu muhimu anazopitia Mgonjwa wa gauni, kuanzia kwa Maambukizi mpaka kwenye hatua ya mwisho hasa kama Ugonjwa huu haujatibiwa mapema.

Soma Zaidi...
Namna ya kujikinga na VVU/UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza namna mbalimbali za kujikinga na VVU/UKIMWI

Soma Zaidi...
Ujuwe mlo sahihi kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo

Post hii itakwenda kuangalia mlo sahihi wa mwenye vidonda vya tumbo. Hata utajifunza ni vyakula vipi hapaswi kula na vipi ana paswa kula.

Soma Zaidi...
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces

Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis.

Soma Zaidi...
Dalili za tetekuwanga

Tetekuwanga (varisela) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuwasha, upele kama vile malengelenge. Tetekuwanga huambukiza sana watu ambao hawajapata ugonjwa huo wala kupewa chanjo dhidi yake. Kabla ya chanjo ya kawaida ya tetekuwanga, karibu watu

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ukoma, ni Ugonjwa unaosababishwa na mdudu anayeitwa mycobacterium leprae, mdudu huyu kwa kawaida uathiri sana sehemu za ngozi na sehemu za Neva mbalimbali za mwili

Soma Zaidi...