Katika makala hii utajifunza faida za kuwa na udhu
1- Ni kama nusu ya iymaan:
Ni kama katika Hadiyth ya Abuu Maalik Al-Ash‘ariy (Radhi za Allaah ziwe juu yake) aliyesema: “Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((الطهور شطر الايمان))
((Twahara ni nusu ya iymaan)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (223) na wengineo.]
2- Hufuta madhambi madogo madogo:
(a) Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((إذا توضأ العبد المسلم – أو المؤمن – Ùغسل وجهه خرج من وجهه كل خطيئة نظر إليها مع قطر الماء – أو مع آخر قطر الماء-ØŒ Ùإذا غسل يديه خرجت من يديه كل خطيئة كان بطشتها يداه مع الماء – أو مع آخر قطر الماء – Ùإذا غسل رجليه خرجت كل خطيئة مشتها رجلاه مع الماء – أو مع آخر قطر الماء – Øتى يخرج نقيا من الذنوب))
((Anapotawadha mja Muislamu – au Muumini – akauosha uso wake, hutoka katika uso huo pamoja na matone ya maji kila kosa la kuangalia – au pamoja na tone la mwisho la maji - , na anapoosha mikono yake miwili, hutoka katika mikono hiyo pamoja na maji, kila kosa ambalo mikono yake imetumilia nguvu – au pamoja na tone la mwisho la maji - , na anapoosha miguu yake miwili, hutoka pamoja na maji kila kosa ambalo miguu yake ililiendea – au pamoja na tone la mwisho la maji, mpaka hutoka akiwa ametakasika kabisa na madhambi)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (244) na wengineo].
(b) Imepokelewa toka kwa ‘Uthmaan (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((من توضأ هكذا غÙر له ما تقدم من ذنبه، وكانت صلاته ومشيه إلى المسجد ناÙلة))
((Mwenye kutawadha hivi, husamehewa dhambi zake zilizopita, na Swalaah yake na kwenda kwake Msikitini huwa ni thawabu ziada. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (229) na wengineo].
Fadhila na thawabu hizi hupatikana kwa uhakika zaidi kwa mwenye kuswali moja kwa moja Swalaah ya faradhi au ya Sunnah baada ya kutawadha.
(c) Katika Hadiyth ya ‘Uthmaan akizungumzia namna wudhuu wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ulivyo, anasema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((من توضأ مثل وضوئي هذا ثم قام Ùصلى ركعتين لا ÙŠØدث Ùيهما Ù†Ùسه، غÙر له ما تقدم من ذنبه))
((Mwenye kutawadha kama ninavyotawadha mimi hivi, kisha akasimama akaswali rakaa mbili, haizungumzishi nafsi yake ndani yake, ila hufutiwa dhambi zake zilizotangulia)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (6433), Muslim (226) na wengineo].
3- Hunyanyua daraja za mja:
Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((ألا أدلكم على ما يمØÙˆ الله به الخطايا ويرÙع به الدرجات؟)) قالوا: بلى يا رسول الله! قال: ((إسباغ الوضوء على المكاره، وكثرة الخطا إلى المساجد، وانتظار الصلاة بعد الصلاة، Ùذلكم الرباط، Ùذلكم الرباط، Ùذلكم الرباط))
((Je, niwaambieni lile ambalo kwalo Allaah Huyafuta makosa na Hunyanyua kwalo daraja? Wakasema: “Tuambie, ee Rasuli wa Allaah! Akasema: Kutawadha kikamilifu pamoja na kuwepo uzito na ugumu, kukithirisha hatua kwenda Msikitini, na kusubiri Swalaah baada ya Swalaah, basi hayo ni mambo ya mtu kujifunga nayo, basi hayo ni mambo ya mtu kujifunga nayo, basi hayo ni mambo ya mtu kujifunga nayo)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (251) na wengineo].
4- Ni njia ya kuelekea peponi:
(a) Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah iwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Bilaal:
(( يا بلال! Øدثني بأرجى عمل عملته ÙÙ‰ الاسلام، إني سمعت د٠نعليك بين يدي ÙÙŠ الجنة)). قال : ((ماعملت عملا أرجى عندي من أني لم أتطهر طهورا ÙÙŠ ساعة من ليل أو نهار إلا صليت بذلك الطهور ما كتب لي أن أصلى))
((Ee Bilaal! Nielezee amali yenye matarajio zaidi uliyoifanya katika Uislamu, kwani mimi nimesikia mtaharuki wa viatu vyako mbele yangu huko peponi)).
Bilaal akasema: “Sikufanya amali yoyote yenye matarajio makubwa kwangu zaidi ya kuwa sikupata kujitwaharisha wakati wowote wa usiku au mchana, ila huswali kwa twahara hiyo kile nilichoandikiwa kukiswali”. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (1149), Muslim (2458) na wengineo].
(b) Imepokelewa toka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir (Radhi za Allaah ziwe juu yake) akisema: “Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:
((من توضأ ÙØ£Øسن الوضوء ثم صلى ركعتين، يقبل عليهما بقلبه ووجهه، وجبت له الجنة))
((Mwenye kutawadha, akaukamilisha vyema wudhuu wake kama inavyotakikana, kisha akaswali rakaa mbili, akafanya khushui kwa moyo wake na uso wake (viungo vyake), basi ni lazima aingie peponi)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (234) An-Nasaaiy (1/80) na wengineo].
(5) Utakuwa ni alama itakayoupambanua Ummah huu wakati wa kupita kwenye hawdh:
Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikwenda makaburini akasema:
((السلام عليكم دار قوم مؤمنين وإنا- إن شاء الله- بكم عن قريب لاØقون، وددت لو أنا قد رأينا إخواننا)) قالوا: أو لسنا إخوانك يا رسول الله؟ قال: ((أنتم أصØابي، وإخواننا الذين لم يأتوا بعد)) Ùقالوا: كي٠تعر٠من لم يأت من أمتك يا رسو Ù„ الله؟ قال: (( أرأيت لو أن رجلا له خيل غر Ù…Øجلة بين ظهري خيل دهم بهم ألا يعر٠خيله؟)) قالوا: بلى يا رسول الله، قال: ((Ùإنهم يأتون غرا Ù…Øجلين من الوضوء، وأنا Ùرطهم على الØوض، ألا ليذادن رجال عن Øوضى كما يذاد البعير الضال أناديهم ألا هلم Ùيقال: إنهم قد بدلوا بعدك، Ùأقول: سØقا سØقا))
((Amani iwe juu yenu nyumba ya jamaa ya Waumini. Na sisi bila shaka Apendapo Allaah tutakuwa nanyi hivi karibuni. Ningependa lau sisi tungeliwaona ndugu zetu)). Wakasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Je, sisi sio ndugu zako”? Akasema:
((Nyinyi ni Maswahaba zangu. Ama ndugu zangu, hao ni wale ambao hawajakuja bado)). Wakasema: “Ni vipi utamtambua yule ambaye bado hajakuja katika umati wako ee Rasuli wa Allaah?”. Akasema: ((Niambieni, lau kama mtu ana farasi wenye alama usoni na miguuni wakawa baina ya farasi weusi wasio na mabaka, je hawezi kuwatambua farasi wake?)). Wakasema: “Ndio, atawatambua ee Rasuli wa Allaah”. Akasema: ((Basi wao watakuja nailhali wana nuru nyusoni, miguuni na mikononi kutokana na wudhuu. Na mimi ndiye nitakayewatangulia kwenye hawdh. Basi jueni kwa yakini kwamba watu watazuiliwa na kufukuzwa wasije kwenye hawdh langu kama wanavyozuiliwa ngamia wasio na mchunga. Nitawaita: Haya njooni! Patasemwa: “Hakika hao walibadili baada yako”. Nitawaambia: Poteleeni mbali kabisa)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (234), An-Nasaaiy (1/80) na wengineo].
(6) Ni nuru kwa mja siku ya Qiyaamah:
Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) akisema: “Nimemsikia Kipenzi changu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:
((تبلغ الØلية من المؤمنين Øيث يبلغ الوضوء))
((Nuru ya Waumini itafikilia pale wudhuu unapofikilia)).
(7) Unafungua kifundo cha shaytwaan:
Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((يعقد الشيطان على قاÙية رأس Ø£Øدكم إذا هو نام ثلاث عقد يضرب كل عقدة: عليك ليل طويل Ùارقد، Ùإن استيقظ Ùذكر الله انØلت عقدة، Ùإن توضأ انØلت عقدة، Ùإن صلى انØلت عقدة، ÙØ£ØµØ¨Ø Ù†Ø´ÙŠØ·Ø§ طيب النÙس، وإلا Ø£ØµØ¨Ø Ø®Ø¨ÙŠØ« النÙس كسلان))
((Anapolala mmoja wenu, shaytwaan hufunga kisogoni mwake vifundo vitatu. Hupiga kila kifundo (kumwambia): Umebakiwa na usiku mrefu, basi lala. Anapoamka akamtaja Allaah, kifundo kimoja hufunguka. Anapotawadha, hufunguka kingine, na anaposwali cha tatu hufunguka. Hapo huwa mchangamfu na mwenye nafsi nzuri, na kama si hivyo, huwa na nafsi mbaya na mvivu)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (1142) na Muslim (776)].
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 1659
Sponsored links
👉1
Kitabu cha Afya
👉2
Kitau cha Fiqh
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉5
Madrasa kiganjani
👉6
Simulizi za Hadithi Audio
Usiku wa lailat al qadir maana yake na fadhila zake. Nini ufanye katika usiku wa lailat al-qadir
Soma Zaidi...
Al-Arba'uwn An-Nawawiyyah hadithi ya 1: Nia
huu ni mwanzo wa kitabu hiki cha Matn arbaina Naway Soma Zaidi...
BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU
BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU. Soma Zaidi...
SHUGHULI ZA KILA SIKU
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...
Hadithi Ya 31: Upe Ulimwengu Kisogo Allaah Atakupenda
Soma Zaidi...
HUU NDIO USIA WA MTUME KWA WAISLAMU
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَجُلًا قَالَ لِلنَّبِيِّ صلى الله عليه و سلم أَوْصِنِي. Soma Zaidi...
KUINGIA KWA WAGENI
Download kitabu Hiki Bofya hapa KUINGIA KWA WAGENI Amina na Sadie walimuonea huruma wakamuomba Zubeid amruhusu abakie. Soma Zaidi...
DUA YA 1 - 10
1. Soma Zaidi...