Katika makala hii utajifunza faida za kuwa na udhu
1- Ni kama nusu ya iymaan:
Ni kama katika Hadiyth ya Abuu Maalik Al-Ash‘ariy (Radhi za Allaah ziwe juu yake) aliyesema: “Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((الطهور شطر الايمان))
((Twahara ni nusu ya iymaan)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (223) na wengineo.]
2- Hufuta madhambi madogo madogo:
(a) Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((إذا توضأ العبد المسلم – أو المؤمن – ÙØºØ³Ù„ وجهه خرج من وجهه كل خطيئة نظر إليها مع قطر الماء – أو مع آخر قطر الماء-ØŒ ÙØ¥Ø°Ø§ غسل يديه خرجت من يديه كل خطيئة كان بطشتها يداه مع الماء – أو مع آخر قطر الماء – ÙØ¥Ø°Ø§ غسل رجليه خرجت كل خطيئة مشتها رجلاه مع الماء – أو مع آخر قطر الماء – ØØªÙ‰ يخرج نقيا من الذنوب))
((Anapotawadha mja Muislamu – au Muumini – akauosha uso wake, hutoka katika uso huo pamoja na matone ya maji kila kosa la kuangalia – au pamoja na tone la mwisho la maji - , na anapoosha mikono yake miwili, hutoka katika mikono hiyo pamoja na maji, kila kosa ambalo mikono yake imetumilia nguvu – au pamoja na tone la mwisho la maji - , na anapoosha miguu yake miwili, hutoka pamoja na maji kila kosa ambalo miguu yake ililiendea – au pamoja na tone la mwisho la maji, mpaka hutoka akiwa ametakasika kabisa na madhambi)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (244) na wengineo].
(b) Imepokelewa toka kwa ‘Uthmaan (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((من توضأ هكذا ØºÙØ± له ما تقدم من ذنبه، وكانت صلاته ومشيه إلى المسجد ناÙلة))
((Mwenye kutawadha hivi, husamehewa dhambi zake zilizopita, na Swalaah yake na kwenda kwake Msikitini huwa ni thawabu ziada. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (229) na wengineo].
Fadhila na thawabu hizi hupatikana kwa uhakika zaidi kwa mwenye kuswali moja kwa moja Swalaah ya faradhi au ya Sunnah baada ya kutawadha.
(c) Katika Hadiyth ya ‘Uthmaan akizungumzia namna wudhuu wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ulivyo, anasema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((من توضأ مثل وضوئي هذا ثم قام ÙØµÙ„Ù‰ ركعتين لا ÙŠØØ¯Ø« Ùيهما Ù†ÙØ³Ù‡ØŒ ØºÙØ± له ما تقدم من ذنبه))
((Mwenye kutawadha kama ninavyotawadha mimi hivi, kisha akasimama akaswali rakaa mbili, haizungumzishi nafsi yake ndani yake, ila hufutiwa dhambi zake zilizotangulia)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (6433), Muslim (226) na wengineo].
3- Hunyanyua daraja za mja:
Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((ألا أدلكم على ما يمØÙˆ الله به الخطايا ÙˆÙŠØ±ÙØ¹ به الدرجات؟)) قالوا: بلى يا رسول الله! قال: ((إسباغ الوضوء على المكاره، وكثرة الخطا إلى المساجد، وانتظار الصلاة بعد الصلاة، ÙØ°Ù„كم الرباط، ÙØ°Ù„كم الرباط، ÙØ°Ù„كم الرباط))
((Je, niwaambieni lile ambalo kwalo Allaah Huyafuta makosa na Hunyanyua kwalo daraja? Wakasema: “Tuambie, ee Rasuli wa Allaah! Akasema: Kutawadha kikamilifu pamoja na kuwepo uzito na ugumu, kukithirisha hatua kwenda Msikitini, na kusubiri Swalaah baada ya Swalaah, basi hayo ni mambo ya mtu kujifunga nayo, basi hayo ni mambo ya mtu kujifunga nayo, basi hayo ni mambo ya mtu kujifunga nayo)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (251) na wengineo].
4- Ni njia ya kuelekea peponi:
(a) Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah iwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Bilaal:
(( يا بلال! ØØ¯Ø«Ù†ÙŠ Ø¨Ø£Ø±Ø¬Ù‰ عمل عملته ÙÙ‰ الاسلام، إني سمعت د٠نعليك بين يدي ÙÙŠ الجنة)). قال : ((ماعملت عملا أرجى عندي من أني لم أتطهر طهورا ÙÙŠ ساعة من ليل أو نهار إلا صليت بذلك الطهور ما كتب لي أن أصلى))
((Ee Bilaal! Nielezee amali yenye matarajio zaidi uliyoifanya katika Uislamu, kwani mimi nimesikia mtaharuki wa viatu vyako mbele yangu huko peponi)).
Bilaal akasema: “Sikufanya amali yoyote yenye matarajio makubwa kwangu zaidi ya kuwa sikupata kujitwaharisha wakati wowote wa usiku au mchana, ila huswali kwa twahara hiyo kile nilichoandikiwa kukiswali”. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (1149), Muslim (2458) na wengineo].
(b) Imepokelewa toka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir (Radhi za Allaah ziwe juu yake) akisema: “Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:
((من توضأ ÙØ£ØØ³Ù† الوضوء ثم صلى ركعتين، يقبل عليهما بقلبه ووجهه، وجبت له الجنة))
((Mwenye kutawadha, akaukamilisha vyema wudhuu wake kama inavyotakikana, kisha akaswali rakaa mbili, akafanya khushui kwa moyo wake na uso wake (viungo vyake), basi ni lazima aingie peponi)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (234) An-Nasaaiy (1/80) na wengineo].
(5) Utakuwa ni alama itakayoupambanua Ummah huu wakati wa kupita kwenye hawdh:
Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikwenda makaburini akasema:
((السلام عليكم دار قوم مؤمنين وإنا- إن شاء الله- بكم عن قريب لاØÙ‚ون، وددت لو أنا قد رأينا إخواننا)) قالوا: أو لسنا إخوانك يا رسول الله؟ قال: ((أنتم Ø£ØµØØ§Ø¨ÙŠØŒ وإخواننا الذين لم يأتوا بعد)) Ùقالوا: كي٠تعر٠من لم يأت من أمتك يا رسو Ù„ الله؟ قال: (( أرأيت لو أن رجلا له خيل غر Ù…ØØ¬Ù„Ø© بين ظهري خيل دهم بهم ألا يعر٠خيله؟)) قالوا: بلى يا رسول الله، قال: ((ÙØ¥Ù†Ù‡Ù… يأتون غرا Ù…ØØ¬Ù„ين من الوضوء، وأنا ÙØ±Ø·Ù‡Ù… على الØÙˆØ¶ØŒ ألا ليذادن رجال عن ØÙˆØ¶Ù‰ كما يذاد البعير الضال أناديهم ألا هلم Ùيقال: إنهم قد بدلوا بعدك، ÙØ£Ù‚ول: سØÙ‚ا سØÙ‚ا))
((Amani iwe juu yenu nyumba ya jamaa ya Waumini. Na sisi bila shaka Apendapo Allaah tutakuwa nanyi hivi karibuni. Ningependa lau sisi tungeliwaona ndugu zetu)). Wakasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Je, sisi sio ndugu zako”? Akasema:
((Nyinyi ni Maswahaba zangu. Ama ndugu zangu, hao ni wale ambao hawajakuja bado)). Wakasema: “Ni vipi utamtambua yule ambaye bado hajakuja katika umati wako ee Rasuli wa Allaah?”. Akasema: ((Niambieni, lau kama mtu ana farasi wenye alama usoni na miguuni wakawa baina ya farasi weusi wasio na mabaka, je hawezi kuwatambua farasi wake?)). Wakasema: “Ndio, atawatambua ee Rasuli wa Allaah”. Akasema: ((Basi wao watakuja nailhali wana nuru nyusoni, miguuni na mikononi kutokana na wudhuu. Na mimi ndiye nitakayewatangulia kwenye hawdh. Basi jueni kwa yakini kwamba watu watazuiliwa na kufukuzwa wasije kwenye hawdh langu kama wanavyozuiliwa ngamia wasio na mchunga. Nitawaita: Haya njooni! Patasemwa: “Hakika hao walibadili baada yako”. Nitawaambia: Poteleeni mbali kabisa)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (234), An-Nasaaiy (1/80) na wengineo].
(6) Ni nuru kwa mja siku ya Qiyaamah:
Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) akisema: “Nimemsikia Kipenzi changu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:
((تبلغ الØÙ„ية من المؤمنين ØÙŠØ« يبلغ الوضوء))
((Nuru ya Waumini itafikilia pale wudhuu unapofikilia)).
(7) Unafungua kifundo cha shaytwaan:
Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((يعقد الشيطان على قاÙية رأس Ø£ØØ¯ÙƒÙ… إذا هو نام ثلاث عقد يضرب كل عقدة: عليك ليل طويل ÙØ§Ø±Ù‚د، ÙØ¥Ù† استيقظ ÙØ°ÙƒØ± الله انØÙ„ت عقدة، ÙØ¥Ù† توضأ انØÙ„ت عقدة، ÙØ¥Ù† صلى انØÙ„ت عقدة، ÙØ£ØµØ¨Ø نشيطا طيب Ø§Ù„Ù†ÙØ³ØŒ وإلا Ø£ØµØ¨Ø Ø®Ø¨ÙŠØ« Ø§Ù„Ù†ÙØ³ كسلان))
((Anapolala mmoja wenu, shaytwaan hufunga kisogoni mwake vifundo vitatu. Hupiga kila kifundo (kumwambia): Umebakiwa na usiku mrefu, basi lala. Anapoamka akamtaja Allaah, kifundo kimoja hufunguka. Anapotawadha, hufunguka kingine, na anaposwali cha tatu hufunguka. Hapo huwa mchangamfu na mwenye nafsi nzuri, na kama si hivyo, huwa na nafsi mbaya na mvivu)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (1142) na Muslim (776)].
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Hii ni historia ya uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina. Yaani wafuasi wa wale wafuasi wa Masahaba
Soma Zaidi...عَنْ أُمِّ الْمُؤْمِنِينَ أُمِّ عَبْدِ اللَّهِ عَائِشَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا، قَالَتْ: قَالَ: رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم "...
Soma Zaidi...Hapa nitakuletea baadhi tu ya adhkari ambazo ni muhimu kwa muislamu
Soma Zaidi...Hapa utajifunza nafasi ya kufuata suna katika Uislamu
Soma Zaidi...