Kuepuka Maongezi yasiyo na Maana

12.

Kuepuka Maongezi yasiyo na Maana

12. Kuepuka Maongezi yasiyo na Maana


Maongezi au mazungumzo yasiyo na maana ni yale yasiyoleta manufaa au kheri yoyote ila hasara tu. Mazungumzo haya yapo katika kupiga soga, kupiga porojo, kupiga hadithi za pauka pakawa, kutaniana, kubishana, na mengine ya namna hiyo. Mara zote mazungumzo ya aina hii huwapelekea watu kusengenya, kusema uwongo, kufitinisha, kugombana na kupoteza muda. Aidha mazungumzo ya aina hii huwasahaulisha watu kumkumbuka Allah (s.w).
Muumini hana budi kujiepusha na tabia hii ya kujiingiza kwenye mazungumzo ya upuuzi. Miongoni mwa sifa za waumini ni pamoja na kujiepusha na mambo ya upuuzi kama tunavyojifunza katika Quran:


“Hakika wamefuzu Waumini. Ambao katika Sw ala zao ni wanyenyekevu. Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi”. (23:1-3).
Waja wema mbele ya Allah ni pamoja:

“Na wale ambao hawashuhudii uwongo na wanapopita penye upuuzi hupita kwa heshima (zao). (25:72).
Muislamu anashauriwa daima abaki kimya kama hana la maana la kuzungumza. Mtume (s.a.w) ametuusia:
“Kuwa kimya. Hii ni njia ya kumfukuza shetani na kuimarisha dini yako” (Ahm ad).

“Anayekuwa kimya (anayenyamaza wakati hana la maana la kuzungumza) atakuw a salama ”. (Ahmad, tirmidh).
“Ni jambo bora mno kwa Muumini kuacha yasiyomhusu” (Ma lik, Ahm ad, Tirm idh).
“Ni katika ubora wa Imani ya mtu kwa kuacha kujihusisha na mambo ya upuuzi”. (Tirm idh).



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1254

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 web hosting    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU.

Soma Zaidi...
HALI AMBAZO MTU AKIOMBA DUA HUJIBIWA

HALI AMBAZO MTU AKIOMBA DUA ITAJIBIWA.

Soma Zaidi...
NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU

Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
UHAKIKI WA HADITHI

Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.

Soma Zaidi...
Dua Sehemu ya 01

Zijue fadhila za kuomba dua, tambua umuhimu na mahimizo juu ya kuomba dua?

Soma Zaidi...
Hadithi Ya 32: Kusiwe Na Kudhuriana Wala Kulipiza Dhara

الحديث الثاني والثلاثون "لا ضرر ولا ضرار" عَنْ أَبىِ سَعيدٍ سَعْدِ بْن مَالكِ بْن سِنَانٍ الْخُدريِّ رضي الله عنه  أَنَّ رَسُولَ اللّ?...

Soma Zaidi...
hadithi ya 8

عَنْ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "أُمِرْتُ أَنْ أُقَاتِلَ النَّاسَ حَتَّى ?...

Soma Zaidi...
Mzazi na msafiri na mwenye kudhulumiwa dua zao hujibiwa kwa haraka

Wapo watu kadhaa ambao waliomba dua hazirudi. Hapa nitakueleza wawili ambao ni mzazi na msafiri.

Soma Zaidi...
SWALA YA MTUME (s.a.w)

SWALA YA MTUME Kumswalia Mtume (s.

Soma Zaidi...