picha

DUA 11 - 20

11.

DUA 11 - 20


11.Allahumma inniy a'uudhubika minal-kufri, walfaq-ri, waa'uudhubika min'adhaabil-qabri, Laailaha illa anta. (mara tatu) Ee! Allah hakika mimi najilinda kwako kutokana na ukafiri; na ufakiri; na najilinda kwako kutokana na adhabu ya kabri; Hapana Mola ila wewe." (Mara 3)

12.“Has-biyallahu laailaha illaahuwa 'alayhi tawakkal-tu wahuwa rabbul-'arshil-adhiimi. (Mara saba asubuhi na jioni). Allah ananitosha, hapana Mola ila yeye. Kwake yeye ninategemea, na yeye ni Mola wa arshi tukufu (mara saba asubuhi na jioni).

13.“A'uudhubikalimaatillaahi ttaammaati min-sharri maa khalaqa." (mara tatu jioni) “Najikinga kwa maneno timilifu ya Allah kutokana na shari ya alivyoviumba" (mara tatu jioni).

14.“Bismillahi lladhii laayadhurru ma'asmihi shay-un fiyl-ardhi walaa fissamaai wahuwas-samii'ul-'aliimu. (mara tatu). “Kwa jina la Allah ambaye hakidhuru kwa jina lake kitu chochote kile kilichoko ardhini wala mbinguni, naye ni Msikivu Mjuzi.

15."Sub-haanallahi wabihamdihi, 'adadakhalqihi, waridhwaa nafsihi wazinata ‘arshihi wamidaada kalimatihi, (Mara tatu) “metakasika Allah na sifa zote njema ni zake kwa hisabu ya viumbe vyake, na radhi yake (mara tatu kila asubuhi)

16.“Allahumma inny as-aluka 'il-man-naafiaa, wariz-qan twayyiba, wa-'amalan mutaqabbala". “Ee! Allah nakuomba unipe elimu yenye manufaa, na riziki iliyo nzuri na amali (ibada) yenye kukubaliwa.

17." Sub-hanallahi wabihamdihi." (mara mia) Ametakasika Allah na sifa zote njema ni zake.

18.“Laailaha illallahu, wah-dahu laa sharikalahu, lahul-mul-ku walahul-hamdu wahuwa 'alaa kulli shay-in qadiiru" (mara mia) “Hapana Mola ila Allah, mpweke, asiye na mshirika, ni wake ufalme na ni zake sifa njema zote, na yeye yuko juu ya kila kitu.

19.Mwenye kusoma Ayatul-Kurisiyy (2:255) pindi anapoamka atalindwa kutokana na mashetani (majini) mpaka jioni, na atakayesoma jioni atalindwa nayo mpaka asubuhi. Mwenyezi Mungu hakuna Mola ila Yeye, (na) ndiye Mwenye uhai wa maisha, Msimamia kila jambo. Kusinzia hakumshiki wala kulala.

Ni Vyake (peke yake vyote) vilivyomo mbinguni na vilivyomo katika ardhi. Na nani huyo awezaye kuombea mbele Yake (Allah) bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao (viumbe) na (yajayo) nyuma yao; wala (hao viumbe) hawalijui lo lote katika yaliyo katika ilimu Yake (Mwenyezi Mungu) ila kwa alipendalo (Mwenyewe). Enzi yake imeenea mbingu; na ardhi; wala kuvilinda hivyo hakumshindi; na Yeye (peke yake) ndiye aliye juu na ndiye aliye Mkuu. (2:255) 20.Mwenye kuzisoma mara tatu asubuhi na jioni sura zifuatazo zinamtosheleza na kila kitu:


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Jiunge nasi WhatsApp
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1082

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Dua za wakati wa shida na taabu

Hizi ni Dua ambazo unatakiwa uziombe wakati wa shida na taabu

Soma Zaidi...
DUA 113 - 126

DUA ZA WAKATI WA SHIDA Dua ya wakati wa taabu “LAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-’ADHIMUL-HALIIMU.

Soma Zaidi...
Je! inajuzu wanawake kuzuru makaburi?

As salaam alaykum warahmatullah wabarakatuh, nauliza inajuzu wanawake kuzuru makaburi?

Soma Zaidi...
SHUGHULI ZA KILA SIKU

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
KAMA HUNA HAYA BASI FAJA UNACHOTAKA

عَنْ أَبِي مَسْعُودٍ عُقْبَةَ بْنِ عَمْرٍو الْأَنْصَارِيِّ الْبَدْرِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عل?...

Soma Zaidi...
MAANA YA HADITHI SUNNAH

Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila.

Soma Zaidi...
Al-Arba uwn An-Nawawiyyah hadithi ya 7: Nasaha katika dini

Post hii itakufundisha umuhimu wa nasaha katika dini

Soma Zaidi...