11.
11.Allahumma inniy a'uudhubika minal-kufri, walfaq-ri, waa'uudhubika min'adhaabil-qabri, Laailaha illa anta. (mara tatu) Ee! Allah hakika mimi najilinda kwako kutokana na ukafiri; na ufakiri; na najilinda kwako kutokana na adhabu ya kabri; Hapana Mola ila wewe." (Mara 3)
12.โHas-biyallahu laailaha illaahuwa 'alayhi tawakkal-tu wahuwa rabbul-'arshil-adhiimi. (Mara saba asubuhi na jioni). Allah ananitosha, hapana Mola ila yeye. Kwake yeye ninategemea, na yeye ni Mola wa arshi tukufu (mara saba asubuhi na jioni).
13.โA'uudhubikalimaatillaahi ttaammaati min-sharri maa khalaqa." (mara tatu jioni) โNajikinga kwa maneno timilifu ya Allah kutokana na shari ya alivyoviumba" (mara tatu jioni).
14.โBismillahi lladhii laayadhurru ma'asmihi shay-un fiyl-ardhi walaa fissamaai wahuwas-samii'ul-'aliimu. (mara tatu). โKwa jina la Allah ambaye hakidhuru kwa jina lake kitu chochote kile kilichoko ardhini wala mbinguni, naye ni Msikivu Mjuzi.
15."Sub-haanallahi wabihamdihi, 'adadakhalqihi, waridhwaa nafsihi wazinata โarshihi wamidaada kalimatihi, (Mara tatu) โmetakasika Allah na sifa zote njema ni zake kwa hisabu ya viumbe vyake, na radhi yake (mara tatu kila asubuhi)
16.โAllahumma inny as-aluka 'il-man-naafiaa, wariz-qan twayyiba, wa-'amalan mutaqabbala". โEe! Allah nakuomba unipe elimu yenye manufaa, na riziki iliyo nzuri na amali (ibada) yenye kukubaliwa.
17." Sub-hanallahi wabihamdihi." (mara mia) Ametakasika Allah na sifa zote njema ni zake.
18.โLaailaha illallahu, wah-dahu laa sharikalahu, lahul-mul-ku walahul-hamdu wahuwa 'alaa kulli shay-in qadiiru" (mara mia) โHapana Mola ila Allah, mpweke, asiye na mshirika, ni wake ufalme na ni zake sifa njema zote, na yeye yuko juu ya kila kitu.
19.Mwenye kusoma Ayatul-Kurisiyy (2:255) pindi anapoamka atalindwa kutokana na mashetani (majini) mpaka jioni, na atakayesoma jioni atalindwa nayo mpaka asubuhi. Mwenyezi Mungu hakuna Mola ila Yeye, (na) ndiye Mwenye uhai wa maisha, Msimamia kila jambo. Kusinzia hakumshiki wala kulala.
Ni Vyake (peke yake vyote) vilivyomo mbinguni na vilivyomo katika ardhi. Na nani huyo awezaye kuombea mbele Yake (Allah) bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao (viumbe) na (yajayo) nyuma yao; wala (hao viumbe) hawalijui lo lote katika yaliyo katika ilimu Yake (Mwenyezi Mungu) ila kwa alipendalo (Mwenyewe). Enzi yake imeenea mbingu; na ardhi; wala kuvilinda hivyo hakumshindi; na Yeye (peke yake) ndiye aliye juu na ndiye aliye Mkuu. (2:255) 20.Mwenye kuzisoma mara tatu asubuhi na jioni sura zifuatazo zinamtosheleza na kila kitu:
Umeionaje Makala hii.. ?
Zijue fadhila za kuomba dua, tambua umuhimu na mahimizo juu ya kuomba dua?
Soma Zaidi...ุนููู ุฃูุจูู ู ูุญูู ููุฏู ุงููุญูุณููู ุจููู ุนูููููู ุจููู ุฃูุจูู ุทูุงููุจู ุณูุจูุทู ุฑูุณูููู ุงูููููู ุตูู ุงููู ุนููู ู ุณูู ููุฑูููุญูุงููุชููู ุฑูุถููู ุงููู...
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha matamshi ambayo mtu akiyatamka Allah hujibu dua hiyo kwa urahisi.
Soma Zaidi...Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe.
Soma Zaidi...Posti hii inakwenda kukupa orodha ya dua 10 ambazo unaweza kuziomba kila siku.
Soma Zaidi...hii ni orodha ya dua mbalimbali kutoka kwenye quran. Unaweza kuzitumia dua hizi kujipendekeza kwa Allah na kupata msamaha, neema na mengineyo.
Soma Zaidi...