DUA 11 - 20

DUA 11 - 20

11.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

DUA 11 - 20


11.Allahumma inniy a'uudhubika minal-kufri, walfaq-ri, waa'uudhubika min'adhaabil-qabri, Laailaha illa anta. (mara tatu) Ee! Allah hakika mimi najilinda kwako kutokana na ukafiri; na ufakiri; na najilinda kwako kutokana na adhabu ya kabri; Hapana Mola ila wewe." (Mara 3)

12.“Has-biyallahu laailaha illaahuwa 'alayhi tawakkal-tu wahuwa rabbul-'arshil-adhiimi. (Mara saba asubuhi na jioni). Allah ananitosha, hapana Mola ila yeye. Kwake yeye ninategemea, na yeye ni Mola wa arshi tukufu (mara saba asubuhi na jioni).

13.“A'uudhubikalimaatillaahi ttaammaati min-sharri maa khalaqa." (mara tatu jioni) “Najikinga kwa maneno timilifu ya Allah kutokana na shari ya alivyoviumba" (mara tatu jioni).

14.“Bismillahi lladhii laayadhurru ma'asmihi shay-un fiyl-ardhi walaa fissamaai wahuwas-samii'ul-'aliimu. (mara tatu). “Kwa jina la Allah ambaye hakidhuru kwa jina lake kitu chochote kile kilichoko ardhini wala mbinguni, naye ni Msikivu Mjuzi.

15."Sub-haanallahi wabihamdihi, 'adadakhalqihi, waridhwaa nafsihi wazinata ‘arshihi wamidaada kalimatihi, (Mara tatu) “metakasika Allah na sifa zote njema ni zake kwa hisabu ya viumbe vyake, na radhi yake (mara tatu kila asubuhi)

16.“Allahumma inny as-aluka 'il-man-naafiaa, wariz-qan twayyiba, wa-'amalan mutaqabbala". “Ee! Allah nakuomba unipe elimu yenye manufaa, na riziki iliyo nzuri na amali (ibada) yenye kukubaliwa.

17." Sub-hanallahi wabihamdihi." (mara mia) Ametakasika Allah na sifa zote njema ni zake.

18.“Laailaha illallahu, wah-dahu laa sharikalahu, lahul-mul-ku walahul-hamdu wahuwa 'alaa kulli shay-in qadiiru" (mara mia) “Hapana Mola ila Allah, mpweke, asiye na mshirika, ni wake ufalme na ni zake sifa njema zote, na yeye yuko juu ya kila kitu.

19.Mwenye kusoma Ayatul-Kurisiyy (2:255) pindi anapoamka atalindwa kutokana na mashetani (majini) mpaka jioni, na atakayesoma jioni atalindwa nayo mpaka asubuhi. Mwenyezi Mungu hakuna Mola ila Yeye, (na) ndiye Mwenye uhai wa maisha, Msimamia kila jambo. Kusinzia hakumshiki wala kulala.

Ni Vyake (peke yake vyote) vilivyomo mbinguni na vilivyomo katika ardhi. Na nani huyo awezaye kuombea mbele Yake (Allah) bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao (viumbe) na (yajayo) nyuma yao; wala (hao viumbe) hawalijui lo lote katika yaliyo katika ilimu Yake (Mwenyezi Mungu) ila kwa alipendalo (Mwenyewe). Enzi yake imeenea mbingu; na ardhi; wala kuvilinda hivyo hakumshindi; na Yeye (peke yake) ndiye aliye juu na ndiye aliye Mkuu. (2:255) 20.Mwenye kuzisoma mara tatu asubuhi na jioni sura zifuatazo zinamtosheleza na kila kitu:


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 657

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

 WACHA KILE ULICHO NA SHAKA NACHO NA FANYA USICHO NA SHAKA NACHO
WACHA KILE ULICHO NA SHAKA NACHO NA FANYA USICHO NA SHAKA NACHO

عَنْ أَبِي مُحَمَّدٍ الْحَسَنِ بْنِ عَلِيِّ بْنِ أَبِي طَالِبٍ سِبْطِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم وَرَيْحَانَتِهِ رَضِيَ اللَ...

Soma Zaidi...
MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA
MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA

MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA.

Soma Zaidi...
DUA DHIDI YA WASIWASI, UCHAWI NA MASHETANI
DUA DHIDI YA WASIWASI, UCHAWI NA MASHETANI

DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 1.

Soma Zaidi...