image

DUA 11 - 20

11.

DUA 11 - 20


11.Allahumma inniy a'uudhubika minal-kufri, walfaq-ri, waa'uudhubika min'adhaabil-qabri, Laailaha illa anta. (mara tatu) Ee! Allah hakika mimi najilinda kwako kutokana na ukafiri; na ufakiri; na najilinda kwako kutokana na adhabu ya kabri; Hapana Mola ila wewe." (Mara 3)

12.“Has-biyallahu laailaha illaahuwa 'alayhi tawakkal-tu wahuwa rabbul-'arshil-adhiimi. (Mara saba asubuhi na jioni). Allah ananitosha, hapana Mola ila yeye. Kwake yeye ninategemea, na yeye ni Mola wa arshi tukufu (mara saba asubuhi na jioni).

13.“A'uudhubikalimaatillaahi ttaammaati min-sharri maa khalaqa." (mara tatu jioni) “Najikinga kwa maneno timilifu ya Allah kutokana na shari ya alivyoviumba" (mara tatu jioni).

14.“Bismillahi lladhii laayadhurru ma'asmihi shay-un fiyl-ardhi walaa fissamaai wahuwas-samii'ul-'aliimu. (mara tatu). “Kwa jina la Allah ambaye hakidhuru kwa jina lake kitu chochote kile kilichoko ardhini wala mbinguni, naye ni Msikivu Mjuzi.

15."Sub-haanallahi wabihamdihi, 'adadakhalqihi, waridhwaa nafsihi wazinata ‘arshihi wamidaada kalimatihi, (Mara tatu) “metakasika Allah na sifa zote njema ni zake kwa hisabu ya viumbe vyake, na radhi yake (mara tatu kila asubuhi)

16.“Allahumma inny as-aluka 'il-man-naafiaa, wariz-qan twayyiba, wa-'amalan mutaqabbala". “Ee! Allah nakuomba unipe elimu yenye manufaa, na riziki iliyo nzuri na amali (ibada) yenye kukubaliwa.

17." Sub-hanallahi wabihamdihi." (mara mia) Ametakasika Allah na sifa zote njema ni zake.

18.“Laailaha illallahu, wah-dahu laa sharikalahu, lahul-mul-ku walahul-hamdu wahuwa 'alaa kulli shay-in qadiiru" (mara mia) “Hapana Mola ila Allah, mpweke, asiye na mshirika, ni wake ufalme na ni zake sifa njema zote, na yeye yuko juu ya kila kitu.

19.Mwenye kusoma Ayatul-Kurisiyy (2:255) pindi anapoamka atalindwa kutokana na mashetani (majini) mpaka jioni, na atakayesoma jioni atalindwa nayo mpaka asubuhi. Mwenyezi Mungu hakuna Mola ila Yeye, (na) ndiye Mwenye uhai wa maisha, Msimamia kila jambo. Kusinzia hakumshiki wala kulala.

Ni Vyake (peke yake vyote) vilivyomo mbinguni na vilivyomo katika ardhi. Na nani huyo awezaye kuombea mbele Yake (Allah) bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao (viumbe) na (yajayo) nyuma yao; wala (hao viumbe) hawalijui lo lote katika yaliyo katika ilimu Yake (Mwenyezi Mungu) ila kwa alipendalo (Mwenyewe). Enzi yake imeenea mbingu; na ardhi; wala kuvilinda hivyo hakumshindi; na Yeye (peke yake) ndiye aliye juu na ndiye aliye Mkuu. (2:255) 20.Mwenye kuzisoma mara tatu asubuhi na jioni sura zifuatazo zinamtosheleza na kila kitu:


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 286


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Hadithi Ya 42: Ewe Mwana Wa Adam, Utakaponiomba Na Kuweka Matumaini Kwangu Basi Nitakusamehe
Soma Zaidi...

HADITHI 40 ZA IMAM NAWAW AROBAIN AN-NAWAWIY
Soma Zaidi...

DUA 51 - 60
51. Soma Zaidi...

Matamshi ambayo ukimwambia Allah kwenye dua yako basi hujibiwa kwa haraka dua hiyo
Post hii inakwenda kukufundisha matamshi ambayo mtu akiyatamka Allah hujibu dua hiyo kwa urahisi. Soma Zaidi...

DUA 85 - 93
SWALA YA MTUME 85. Soma Zaidi...

dua ya kuomba jambo ufanikiwe
hii ni damna ya kuomba dua ukubaliwe, dua ya kuomba jambo ufanikiwe Soma Zaidi...

Hadithi ya tatu:ukarimu na kusaidiana
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Historia ya uandishi wa Hadithi, na ni kwa nini wakati wa Mtunme hakukuwa na uandishibmkubwa wa hadithi
Hapa utakwendabkuijuwabhistoria ya uandishi wa hadithi. Pia utaijuwa sababu iliyopelekea uandishi wa hadithi kuwa mdogo . Soma Zaidi...

Hadithi inayotaja nguzo tano za uislamu
عَنْ أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عُمَرَ بْنِ الْخَطَّابِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صل?... Soma Zaidi...

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU
BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU. Soma Zaidi...

Faida za swala ya Mtume
Hapa utajifunza fadhila za kumswalia Mtume (s.a.w) Soma Zaidi...

DUA 120
Soma Zaidi...