picha

DUA 21 - 31

21.

DUA 21 - 31


21.Suratul-Ikhlas (112:1-4) Sema, Yeye ni Allah aliye mmoja tu Allah ndiye anayestahiki 475 kukusudiwa (na viumbe vyote). Hakuzaa wala hakuzaliwa. Hakuna hata mmoja anayefanana naye." (112:1-4)

22.Suratul-Falaq (113:1-5) Sema: Ninajikinga kwa Mola wa ulimwengu wote.Na shari ya Alivyoviumba. Na shari ya giza la usiku liingiapo.Na shari ya wale wanaopulizia mafundoni.Na shari ya hasidi anapohusudu. (113:1-5)

23.Suratun-Naas (114:1-6) Sema: Ninajikinga kwa Bwana Mwenye kuwalea watu. Mfalme wa watu. Muabudiwa wa watu. Na shari ya mwenye kutia wasiwasi mwenye kurejea nyuma. Atiaye wasi wasi nyoyoni mwa watu. (Ambaye ni) katika majini na watu." (114:1-6)

24.Kumswalia Mtume Asubuhi na Jioni Mtume (s.a.w) amesema:Mwenye kuniombea rehema asubuhi mara kumi na jioni mara kumi, nitamuombea shufaa (masamaha) siku ya kiyama.

25.“Allahumma swali'alaa Muhammad wa'alaa aali Muhammad, kamaa swallayta 'alaa Ibraahiima wa'alaa aali Ibraahiim, Innaka hamidun majiidu, allahumma baarik-'alaa Muhammad wa-'alaa aali Muhammad, kamaa barak-ta 'alaa Ibraahiima wa-'alaa aalii Ibraahiima, Innaka hamidunmajiidu."

Ee Allah! Mrehemu Muhammad na jamaa zake (wafuasi wake) Muhammad kama ulivyo mrehemu Ibrahiim na jamaa zake (wafuasi wake) Ibrahiim, hakika wewe ni mwenye kusifika mtukufu. Ee Allah! Mbariki Muhammad na jamaa zake Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na jamaa zake Ibrahiim, Hakika wewe ni Mwenye kusifika Mtukufu. Mtume (s.a.w) amesema: "Anayeniswalia mara moja, Allah (s.w) humswalia mara kumi." (Muslimu).

26.Pia Mtume (s.a.w) amesema: “Bahili ni yule ninapotajwa, haniswalii (haniombei rehema na amani kwa Allah)." (Tirmidh) Kumswalia Mtume (s.a.w) kumeamrishwa kwa waumini kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo: “Hakika Mwenyezi Mungu na Malaika wake wanamswalia Mtume (wanamtakia rehema na amani). Basi, enyi mlioamini mswalieni (muombeeni Mtume) rehema na amani." (33:56)

27.Kuomba Msamaha na Kutubia Amesema Mtume (s.a.w): “Naapa kwa Mwenyezi Mungu hakika mimi ninamtaka msamaha Mwenyezi Mungu na ninatubia kwake katika kila siku zaidi ya mara sabini." (Al-Bukhari). 28.“Astagh-firu llaha waatuubu ilahi." (mara mia) “Namuomba msamaha Allah na ninatubia kwake." 29.Pia Mtume (s.a.w) amesema: "Yeyote anayesoma maneno yafuatayo, Mwenyezi Mungu atamsamehe hatakama anamakosa ya kukimbia vitani:

30.“Astagh-firu llaahal-'adhiimal-ladhii laaillaha illahuwalhayyul qayyuumu wa-atuubu ilayhi." “Namuomba msamaha Allah, Mtukufu ambaye hapana Mola ila yeye, aliye Hai, aliyesimama kwa dhati yake na ninatubia kwake."

31.Amesema Mtume (s.a.w): "Hakuna mja yeyote yule anayefanya dhambi kisha akatawadha vizuri na akaswali rakaa mbili, kisha akamtaka Mwenyezi Mungu msamaha ila atasamehewa". (Abu Daud na Tirmidh) 12. Dhikri ya kuleta baada ya kupatwa na janga au balaa “Laailaha illa llahul-'adhwiimul-haliimu, laa ilaha illa llahu r a b b u l - ' a r - s h i l ' a d hwi imi , L a a i l a h a i l l a l l a h u rabbussamaawaat warabbul-ardhwi,warabbul-'ar-shilkariimi.

“Hapana Mola ila Allah, aliye mtukufu mpole, Hapana Mola ila Allah, Mola wa arshi tukufu, Hapana Mola ila Allah, Mola wa mbingu na ardhi na Mola wa arshi tukufu. “Laailaha illaa-anta Sub-hanaanaka inny kuntuminal Dhw- Dhwaalimiina." Hapana Mola ila Wewe, Utukufu ni wako, hakika mimi ni miongoni mwa waliodhulumu nafsi zao. 13.Unapokutana na adui au mtawala dhalimu “Hasbunallahu wani'imal-wakiilu" “Allah anatutosheleza Naye ni mbora wa kutegemewa.


                   

,m

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF Views 1052

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 ai web app     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

DUA DHIDI YA WASIWASI, UCHAWI NA MASHETANI

DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 1.

Soma Zaidi...
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA

SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA.

Soma Zaidi...
Dua ambazo hutumiwa katika swala

Post hii inakwenda kukugundisha dua ambazo itazitumia katika swala yako.

Soma Zaidi...
Maswali juu ya Sunnah na hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Uislamu ni Nasaha (kunasihiana) kwa Mwenyezi Mungu, Kitabu chake Mtume wake , Viongozi na waislamu wote

عَنْ أَبِي رُقَيَّةَ تَمِيمِ بْنِ أَوْسٍ الدَّارِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: "الدِّينُ النَّصِ?...

Soma Zaidi...
Fadhila za udhu yaani faida za udhu

Katika makala hii utajifunza faida za kuwa na udhu

Soma Zaidi...