picha

DUA 21 - 31

21.

DUA 21 - 31


21.Suratul-Ikhlas (112:1-4) Sema, Yeye ni Allah aliye mmoja tu Allah ndiye anayestahiki 475 kukusudiwa (na viumbe vyote). Hakuzaa wala hakuzaliwa. Hakuna hata mmoja anayefanana naye." (112:1-4)

22.Suratul-Falaq (113:1-5) Sema: Ninajikinga kwa Mola wa ulimwengu wote.Na shari ya Alivyoviumba. Na shari ya giza la usiku liingiapo.Na shari ya wale wanaopulizia mafundoni.Na shari ya hasidi anapohusudu. (113:1-5)

23.Suratun-Naas (114:1-6) Sema: Ninajikinga kwa Bwana Mwenye kuwalea watu. Mfalme wa watu. Muabudiwa wa watu. Na shari ya mwenye kutia wasiwasi mwenye kurejea nyuma. Atiaye wasi wasi nyoyoni mwa watu. (Ambaye ni) katika majini na watu." (114:1-6)

24.Kumswalia Mtume Asubuhi na Jioni Mtume (s.a.w) amesema:Mwenye kuniombea rehema asubuhi mara kumi na jioni mara kumi, nitamuombea shufaa (masamaha) siku ya kiyama.

25.“Allahumma swali'alaa Muhammad wa'alaa aali Muhammad, kamaa swallayta 'alaa Ibraahiima wa'alaa aali Ibraahiim, Innaka hamidun majiidu, allahumma baarik-'alaa Muhammad wa-'alaa aali Muhammad, kamaa barak-ta 'alaa Ibraahiima wa-'alaa aalii Ibraahiima, Innaka hamidunmajiidu."

Ee Allah! Mrehemu Muhammad na jamaa zake (wafuasi wake) Muhammad kama ulivyo mrehemu Ibrahiim na jamaa zake (wafuasi wake) Ibrahiim, hakika wewe ni mwenye kusifika mtukufu. Ee Allah! Mbariki Muhammad na jamaa zake Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na jamaa zake Ibrahiim, Hakika wewe ni Mwenye kusifika Mtukufu. Mtume (s.a.w) amesema: "Anayeniswalia mara moja, Allah (s.w) humswalia mara kumi." (Muslimu).

26.Pia Mtume (s.a.w) amesema: “Bahili ni yule ninapotajwa, haniswalii (haniombei rehema na amani kwa Allah)." (Tirmidh) Kumswalia Mtume (s.a.w) kumeamrishwa kwa waumini kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo: “Hakika Mwenyezi Mungu na Malaika wake wanamswalia Mtume (wanamtakia rehema na amani). Basi, enyi mlioamini mswalieni (muombeeni Mtume) rehema na amani." (33:56)

27.Kuomba Msamaha na Kutubia Amesema Mtume (s.a.w): “Naapa kwa Mwenyezi Mungu hakika mimi ninamtaka msamaha Mwenyezi Mungu na ninatubia kwake katika kila siku zaidi ya mara sabini." (Al-Bukhari). 28.“Astagh-firu llaha waatuubu ilahi." (mara mia) “Namuomba msamaha Allah na ninatubia kwake." 29.Pia Mtume (s.a.w) amesema: "Yeyote anayesoma maneno yafuatayo, Mwenyezi Mungu atamsamehe hatakama anamakosa ya kukimbia vitani:

30.“Astagh-firu llaahal-'adhiimal-ladhii laaillaha illahuwalhayyul qayyuumu wa-atuubu ilayhi." “Namuomba msamaha Allah, Mtukufu ambaye hapana Mola ila yeye, aliye Hai, aliyesimama kwa dhati yake na ninatubia kwake."

31.Amesema Mtume (s.a.w): "Hakuna mja yeyote yule anayefanya dhambi kisha akatawadha vizuri na akaswali rakaa mbili, kisha akamtaka Mwenyezi Mungu msamaha ila atasamehewa". (Abu Daud na Tirmidh) 12. Dhikri ya kuleta baada ya kupatwa na janga au balaa “Laailaha illa llahul-'adhwiimul-haliimu, laa ilaha illa llahu r a b b u l - ' a r - s h i l ' a d hwi imi , L a a i l a h a i l l a l l a h u rabbussamaawaat warabbul-ardhwi,warabbul-'ar-shilkariimi.

“Hapana Mola ila Allah, aliye mtukufu mpole, Hapana Mola ila Allah, Mola wa arshi tukufu, Hapana Mola ila Allah, Mola wa mbingu na ardhi na Mola wa arshi tukufu. “Laailaha illaa-anta Sub-hanaanaka inny kuntuminal Dhw- Dhwaalimiina." Hapana Mola ila Wewe, Utukufu ni wako, hakika mimi ni miongoni mwa waliodhulumu nafsi zao. 13.Unapokutana na adui au mtawala dhalimu “Hasbunallahu wani'imal-wakiilu" “Allah anatutosheleza Naye ni mbora wa kutegemewa.


                   

,m

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1017

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 ai web app    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Uandishi wa hadithi wakati wa Matabii tabiina (tabiitabiina)

Hii ni historia ya uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina. Yaani wafuasi wa wale wafuasi wa Masahaba

Soma Zaidi...
Adabu ya kukaa na kula katika nyumba za watu

"Si vibaya kwa kipofu, wala si vibaya kwa kiguru, wala si vibaya kwa mgonjwa, wala kwenu, kama mkila katika nyumba zenu, au nyumba za baba zenu, au nyumba za mama zenu, au nyumba za ndugu zenu, au nyumba za dada zenu, au nyumba za ami zenu, au nyumba za s

Soma Zaidi...
Dua sehemu ya 04

Soma dua mbalimbali za kila siku ambazo unatakiwa uzijuwe. Dua 120 ambazo muislamu anatakiwa kuzijua

Soma Zaidi...
TANZU ZA HADITHI

Tanzu za Hadith(1) Tanzu ya UsahihiKulingana na kiwango cha usahihi wa Hadith, Hadith zimegawanywa katika makundi makuu manne:(a) Sahihi (b) Hasan/Nzuri.

Soma Zaidi...
Adabu za kuomba dua kuifanya dua yako ikubaliwe kwa haraka

Post hii inakwenda kukugundisha adabu zinazotakikana kwa mwenye kuomba dua.

Soma Zaidi...
AL-ARBAUWN AN-NAWAWIYYAH HADITHI YA 4: Uumbwaji wa mwanadamu

HAdithi hii itakufundisha namna ambavyo mwanadamu anapitia hatuwa mbalumbali tumboni mwa mama yake

Soma Zaidi...
Al-Arba uwn An-Nawawiyyah hadithi ya 7: Nasaha katika dini

Post hii itakufundisha umuhimu wa nasaha katika dini

Soma Zaidi...
Maswali juu ya Sunnah na hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...