Dondoo za afya 41-60

Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya

? DONDOO 41 - 60

Basi tambua haya;-

41.Njia ambazo ugonjwa wa manjano huambukizwa ni sawa na zile za kuambukiza UKIMWI.

42.Dalili za ugonjwa wa manjano huchelewa kuonekana, na huonekana pale mtu anapokuwa ameshaathirika. Dalili hizo ni kama kukojoa mkojo wa rangi nyeusi, macho na ngozi kuwa njano, kichefichefu cha mara kwa mara, kupungua uzuto, homa kali, mwili kuwa dhaifu, kupoteza hamu ya kula na maumivu makali ya tumbo karibu na ini.

43.Ugonjwa huu pia hauna tiba, ila mgonjwa akiwahi hospitali anaweza kupewa dawa za kupambana na virusi hawa. Pia anaweza kubadilishiwa ini.

44.Mgonjwa mwenye ugonjwa wa manyano anatakiwa asinye pombe, madawa ya kulevya n.k

45.Virusi vya ugonjwa huu wa homa ya manjano ni hatari kuliko vya ukimwi maana vinaweza kukaa nje ya mfumo wa damu mpaka siku saba, wakati vya ukimwi haviwezi kufika hata dakika moja.

46.Mbegu za maboga zinaweza kuwasaidia watu wanaoishi na kisukari. Mbegu hizi zimeonekana kuwa na uwezo wa kusaidia kurekebisha kiwango cha insulin.

47.Madini ya zinc yaliyomo kwenye mbegu za maboga husaidia kuboresha afya ya ubongo na utunzaji wa kumbukumbu.

48.Karanga pia husaidi afya ya ubongo na utunzaji wa kumbukumbu. Kuna vitamin E kwenye karanga, hivi ndivyo vina kazi hii.

49.Mshubiri ni katika tiba za asili sana. Husaidia kuondoa miwasho kwenye ngozi. Pia kuponesha vidonda na michubuko kwnye ngozi. Kata jani lake kisha jipake kwenye jeraha, mchubuko au muwasho.

50.Na muarobani nao pia hutibi maumivi ya sikio , maradhi ya macho na miwash ya ngozi. Changanya mwarobaini uliopondwa na asali kisha weka tone moja wenye sikio. Fanya hivyo kwa siku kadhaa utapona.

51.Tende ni katika matunda ya asili na ni katika matunda yanayoweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu kwa njia za asili. Wataalamu wa afya wanazungumza kuwa karibia virutubisho vyote anavyohitajia mwanadamu kuishi vinaweza kupatikana kwenye tende. Pia wataalamu wanaongeza kuwa mtu anaweza kuishi kwa muda mrefu kwa kula tende kokwa chache tu na glas ya maziwa.

52.Maziwa ni katika vinywaji vya asili pia. Maziwa ya mama yanafahamika kwa ubora wake na umuhimu kwa watoto wachanga. Wataalamu wa afya qwanasisitiza kuwanyonyesha watoto kwa muda wa miaka miwili. Halikadhalika maziwa ya ng’ombe na wanyama wengine kama ngamia na mbuzi yamekuwa yakitumiwa sana na watu wazima. Watu wamekuwa wakinywa maziwa kwa ajili ya kuondoa sumu. Halikadhalika maziwa yana virutubisho mauhimu nambavyo mwanadamu anahitajia. Wagonjwa wa vidonda vya tumbo wanashauriwa sana kunywa maziwa.

53.Asali pia ni katika vyakula na vinywaji vya asili. Ukiachilia mbali virutubisho vingi sana vilivyomo kwenye asali, lakini asali pia huweza kutumika kama dawa. Kwa walioungua hupaka asali kwenye jeraha. Asali ina uwezo mkubwa wakuuwa bakteria kwenye kidonda.

54.Nyama ni katika vyakula vyenye protini. Watu wengi hupenda kula vyama. Wapishi wa nyama wanapashwa kuwa makini kwani vyama inatakiwa iiive na kama haitaiva walaji wanaweza kudhurika kama mnyama atakuwa na vijidudu. Vyama vyekundu kama ya ng’ombe na mbuzi zimekuwa zikipatikana zaidi. Lakini wataalamu wa afya wanapendelea zaidi uaji wa nyama nyeupe kama nyama ya samaki, kuku n.k.

55.Samaki ni katika vyakula vya asili pia. Wataalam wa afya wanaeleza kuwa ukuaji salalma wa ubongo kwa mtoto unaweza kuwa maradufu kama mtoto atakuala samaki. Wataalamu wa afya wanasisitika kula samaki akiwa katika supu ama namna ingine. Mafuta ya samaki ni katika sehemu muhimu inayopasa kuliwa kwenye samaki

56.Ni vyema kula matunda ukiwa una vyaa kabla ya kula chakula. Ulaji wa matunda ukiwa na njaa utapelekea mmeng’enyo wa lile tunda kukamilika wote na kuingia kwenye mfumo wa chakula.

57.Ijapokuwa watu wengi hawapendi pilipili ila itambulike kuwa tunda hili ni zuri na lina vitamini anbavyo vinasaidia katika ukuaji wa ubongo.

58.Matunda yenye rangi ya njano kama maembe na machungwa yana kiasi kikubwa cha vitamikni C. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa vitamini hivi ini mujarabu katika kuulinda mwili dhidi ya maradhi mablimbali.

59.Mimea yenye rangi a kijani yaani mboga ina vitamini A. Vitamini hivi pia via kazi ya kuulinda mwili na maradhi. Matatizo ya kutokuona usiku ni kutokana na upungufu wa vitamini hivi.

60.Ni vema kupiga mswaki kabla ya kulala. Ukilala na mabaki ya chakula mdomoni unaweza kukaribisha bakteria kuzaliana kwa kiasi kikubwa kwenye kinywa chako. Hali hii inaweza kuleta madhara katika afya ya meno yako.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Author Tarehe 2021/11/10/Wednesday - 09:31:06 pm     Share On Facebook or WhatsApp Imesomwa mara 1028

Post zifazofanana:-

Dalili za Mgonjwa wa kisukari
Post hii inahusu dalili za mtu Mwenye ugonjwa wa kisukari, dalili hizi zinaweza kujitokeza Moja kwa Moja mtu akagundua kuwa ana Ugonjwa wa kisukari.zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kisukari. Soma Zaidi...

Fida za kula uyoga
Uyoga pia ni katika vyakula vya asili, ijapokuwa upatikanaji wake umekuwa mchache siku hizi. Shukrani ziwaendee wataalamu wa kilimo, kwa sasa tunaweza kuzipata mbegu za uyoga kutoka maabara na kulima uyoga popote pale. Wataalamu wa mimea wanaamini kuwa uyoga si katika mimiea kwani uyoga upo katika kundi la viumbe liitwalo fungi (kingdom fungi). ila tunapozungumzia vyakula uyoga tunauweka kwenye kundi la mbogamboga. Uyoga una virutubisho vingi na vizuri kwa afya. Soma Zaidi...

Makundi ya watu walio katika hatari ya kupata Ugonjwa wa Ukimwi
Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata Maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi,ni kutokana na kazi zao pamoja na mazingira yao kwa hiyo wako kwenye hatari ya kupata Ugonjwa wa ukimwi. Soma Zaidi...

Njia za kujilinda na kujikinga na UTI
Somo hili linakwenda kukuletea njia za kujilinda na kujikinga na UTI Soma Zaidi...

Dalili za mimba yenye uvimbe
Mimba ya tumbo - pia inajulikana kama hydatidiform mole - ni ugumu usiyo na kansa (benign) ambayo hutokea kwenye uterasi. Mimba ya molar huanza wakati yai linaporutubishwa, lakini badala ya mimba ya kawaida, yenye uwezo wa kutokea, plasenta hukua na kuwa wingi wa uvimbe usio wa kawaida. Soma Zaidi...

Vitamini C Ni nini?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana na historia ya vitamin C Soma Zaidi...

Vyakula kwa wagonjwa wa sukari na utaratibu wao wa lishe
Post hii inakwenda kukufundisha utaratibu wa lishe kwa wagonjwa wenye kisukari pamoja na vyakula salamakwao. Soma Zaidi...

Ntajilinda vipi na magonjwa ya meno
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujilinda na magonjwa ya meno Soma Zaidi...

Sababu za ugumba kwa wanawake
Post hii inahusu zaidi sababu za ugumba kwa wanawake, ni sababu ambazo upelekea wanawake wengi kuwa wagumba ukizingatia kuwa wanazaliwa wakiwa na uwezo kabisa wa kupata watoto lakini kwa sababu mbalimbali za kimazingira wanakoswa watoto, zifuatazo ni sababu za ugumba kwa wanawake. Soma Zaidi...

Ujue Ugonjwa wa homa ya ini yenye sumu.
Homa ya ini yenye sumu'ni kuvimba kwa ini lako kutokana na kuathiriwa na vitu fulani ambavyo umeathiriwa navyo. Homa ya ini yenye sumu'inaweza kusababishwa na pombe, kemikali, dawa za kulevya au viongeza vya lishe. Soma Zaidi...

Dalili za mtu aliyekula chakula chenye sumu
Post hii inahusu zaidi mtu aliyekula chakula chenye sumu, chakula chenye sumu ni chakula ambacho kikitumiwa na mtu yeyote kinaweza kuleta madhara kwenye mwili wa binadamu hata kifo. Soma Zaidi...

Asili ya Madini ya shaba
Posti hii inahusu zaidi asili ya madini ya Shaba, ni sehemu ambapo madini ya Shaba yanaweza kupatikana ni katika mimea na wanyama Soma Zaidi...