Zijuwe aina za minyoo na tiba yake. Dawa 5 za kutibu minyoo ya aina zote
DAWA YA MINYOO
Minyoo ni wadudu aina ya parasite ambao wanaingia kwenye miili ya kiumbe hai kama wanyama na binadamu, na wanajipatia chakula chao humo na kuishi. Kwa binadamu kuna minyoo aiina nyingi sana inayo weza kuwaathiri. Ila zipo aina tatu ambazo zinaonekana ni zaidi kuathiri binadamu. Nazo ni kama:-
1.Minyoo aina ya Roundworms hawa wanaingia kwenye miili yetu kupitia vyakula tunavyokula ama vinywaji endapo hivyo vyakula ama vinywaji vitakuwa na mayai yao. Minyoo hawa wanataga na kuishi kwenye utumbo. Minyoo hawa ni pamoja na threadworm, ascaris, hookworm na trichuris.
2.Minyoo aina ya tapeworm, hawa hishi kwenye tumbo, mara nyingi tunaweza kuwapata minyoo hawa kwa kula chakula ambacho hakikupikwa ama hakikuwiva vyema kama nyama, mihogo mibichi n.k
3.Flukeworms, minyoo hawa huingia mwilini mwetu na kuishi kwenye damu, tumbo, mapafu ama kwenye ini. Unaweza kuwapata minyoo hawa kwa kuogelea ama kuoga kwenye maji yenye minyoo hawa. Mimnyoo hawa husababisha pia ugonjwa ujulikanao kama kichocho (schistosomiasis).
Ni dawa gani hutibu minyoo?
Kwa ufupi tiba ya minyoo hutofautiana kulingana na aina ya minyoo na kiasi cha athari ndani ya mwili. Kwa kiasi kikubwa dawa aina ya Mebendazole imekuwa ikitumika kwa kiasi kikubwa sana maeneo mengi. Na hii ni kwa sababu dawa hii inatumika sana kutibu minyoo aina ya threadworm ambao minyoo hawa ndio wanaathiri watu zaidi. Pia inaweza kutibu aina nyinginyingi za minyoo. Dawa nyingine za kutibu minyoo ni:-
1.Levamisole
2.Tiabendazole
3.Ivermectin
4.Niclosamide
5.Praziquantel
6.Albendazole
7.Diethylcarbamazine
Dawa hizi zinafanyaje kazi?
Yes hili ni swali zuri sana. Sasa inakupasa ujuwe namna ambavyo dawa hizi zitakusaidia kutibu minyoo. Dawa hizi zinafanya kazi kama ifuatavyo:-
A.Mebendazole, albendazole na tiabendazole hizi kuzuia minyoo isifyonze chakul (sugar) kutoka kwenye miili yetu. Hivyo wanaweza kufa kwa njaa. Ila dawa hii itauwa minyoo lakini sio mayai yao ambayo wameyataga tayari.
B.Praziquantel na ivermectin, dawa hizi husaidia kuwazubaisha minyoo kwenye utumbo, hivyo wanaweza kutolewa kwa njia ya haja kubwa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi dawa ya cloxacillin ambayo Iko kwenye kundi mojawapo la penicillin ambalo uzuia enzymes zinazotengenezwa na bakteria.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya propranolol katika matibabu ya magonjwa ya moyo, dawa hii ipo kwenye kundi la beta blockers na ufanya Kazi mbalimbali hasa kwa wagonjwa wa moyo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa mbadala za vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya Acetohexamide kwa matibabu ya sukari, kama tulivyoona katika post iliyopita kwamba kuna kipindi ambacho kongosho linatoa insulini lakini seli haziko tayari kupokea hiyo insulini.
Soma Zaidi...Unapotaka kufanyiwa baadhi ya matibabu unatakiwa kupewa ganzi ama nusu kaput ili kulifanyia usihisi maumivu. Dawa hizi zinajulikana na Anesthesia.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya Sp , kirefu cha dawa hii ni sulphadoxine na pyrimethamine hii dawa ilitumika kutibu malaria kwa kipindi fulani lakini sasa hivi imebaki kutumiwa na wajawazito kama kinga ya kuwazuia kupata malaria.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa za 5-fluorouracil, Tegafur na uracili katika kupambana na kansa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi tiba ya jino,ni tiba ya kawaida kwa watu walio na matatizo ya meno, kwa kawaida tunafahamu kwamba jino huwa halina dawa ila dawa yake huwa ni kungoa lakini Leo nawaletea habari njema kwamba jino sio kungoa tena ila Kuna tiba ambayo
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna au njia ya kufanya Ili kuweza kutumia tiba hii ya jino, kwa sababu ya mchanganyiko ambao umekwisha kuwepo kwa hiyo unachumua mchanganyiko unafanya kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...