Dawa na matibabu ya presha ya kushuka
Hapa utajifuanza dalili za presha ya kushuka, na dawa ya presha ya kushuka na nJia za kuzuiaama kudhibiti presha ya kushuka
PRESHA YA KUSHUKA NA MATIBABU YAKE
Presha ya kushuka mara nyingi haina dalili za kutisha, pia haina shida sana ukilingnisha na presha ya kupanda. Kama unahisi dalili za presha ya kushuka kama kizunguzungu, kichwa kuwa chepesi wakati unaposimama na kuamka, huku mgandamizo wa damu kupunguwa hii hali inatambulika kama postural hypotension.
Kugundua presha ya kushuka daktari atakupima kwa kipimo maalumu. Pia vipo vipimo vngine kama vitahitajika zaidi, kama vile electrocardiogram (ECG), ultrasound pia kipimo cha damu kuangalia kiwango cha sukari kwenye damu na kuangalia kama kuna upungufu wa damu.
Utaratibu wa kuishi ukiwa na presha ya kushuka.
Ningependa tu kukujulisha kuwa unaweza kuishi vyema ukiwa na presha ya kushuka, hata bila ya kutumia dawa za mahospitali. Kabla hatujaona dawa za mahospitali sasa nanakwenda kukueleza utaratibu wa lishe kwa mwenye prsha ya kushuka.
1.Kula chakula chenye chumvi zaidi
2.Kula vyakula vyenye majimaji mengi kama matunda na mfano wake
3.Punguza kunywa vilevi
4.Kunywa maji mengi hasa wakati wa joto
5.Fanya mazoezi ya mara kwa mara
6.Unapolala tumia mto, yaani sehemu ya kichwa chako iwe juu
7.Jizuie kubeba vitu vizito
8.Washa kukaa maeneo yenye joto sana ma kuoga maji ya moto kwa muda mrefu.
9.Acha kusimama wima sehemu moja kwa muda mrefu.
Dawa zinazotumika kutibu presha ya kushuka (hypotension)
A.Fludrocortisone, zungumza na daktari kabla ya kutumiadawa hii.
B.Midodrine.
Hakikisha dawa hizi humezi kiholela. Kabla ya kutumia dawa yeyote kwanza zungumza na daktari kwanza. Hii ni kwa ajili ya afya yako.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Dawa ya kutibu mapunye
DAWA YA MAPUNYEMatibabu ya mapunye inategemea ni wapi mapunjye yapo.
Soma Zaidi...Ni zipi dawa za Vidonda vya tumbo?
Dawa za vidonda vya tumbo na tiba zake zinapatikana hapa. Soma makala hii kwa ufanisi
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya ketoconazole.
Post hii inahusu zaidi dawa aina ya ketoconazole ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye koo.
Soma Zaidi...Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo Aspirin.
Aspirini Ni dawa ya kutuliza maumivu.Majina yanayoaminika zaidi katika kutuliza maumivu sasa yanapatikana kwa njia mbadala inayookoa gharama kwa kutumia Aspirini. Aspirini inayopendwa na familia kwa miongo kadhaa, mara nyingi hutumiwa kupunguza maumivu y
Soma Zaidi...Ifahamu dawa ya kupunguza maumivu
Post hii inahusu dawa ya aspirin katika kupunguza maumivu,ni dawa ambayo upunguz maumivu ya Kawaida, kushusha homa na pia usaidia kwenye magonjwa ya moyo hasa kuzuia stroke kama imetokea mda ndani ya masaa ishilini na manne
Soma Zaidi...