Fahamu kundi la veta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
Post hii inahusu zaidi kundi la beta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo,hili kundi lina dawa mbalimbali ambazo utumika katika matibabu ya magonjwa ya moyo na kila dawa tutaiongelea tofauti tofauti ili kuweza kujua kazi zake.
Fahamu kundi la Bata blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
1. Kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba hili kundi ambalo usaidia katika matibabu ya magonjwa ya moyo kwa kuwepo dawa tofauti tofauti kwenye kundi hili ambazo nazo uweza kufanya kazi tofauti tofauti kadri ya tatizo la mgonjwa, kwa hiyo kundi hili lina dawa ya atenolo, carvedilo,propanol na labetalolol kwa hiyo dawa hizi kutwa kwenye kundi la beta blockers.
2. Kwa ujumla kundi hili pamoja na kuwepo kwa dawa tofauti usaidia kutibu mapigo ya moyo ambayo siyo ya kawaida, kwa hiyo kuna kipindi mapigo ya moyo yanaweza kubadilika na kuwa na spidi kubwa au wakati mwingine spidi kuwa ndogo, yaani kwa ujumla mapigo ya moyo kutokuwa ya kawaida kwa matumizi ya dawa hii usaidia mapigo ya moyo kuwa ya kawaida.
3. Vile vile dawa hizi ambazo zipo kwenye kundi hili la beta blockers ufanya kazi ya kupanua mishipa ya damu na kusababisha damu iweze kusafiri vizuri, kwa hiyo nazo usaidia kwenye matibabu ya presha ya kupanda, yaani kwa kitaalamu hypertension, na pia usaidia kwa watu wenye matatizo ya heart attack, kwa hiyo dawa hizi ufanya kazi kubwa katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
4. Kwa sababu kundi hili la beta blockers ufanya Kazi mbalimbali na huwa na dawa tofauti tofauti na kila dawa ina matumizi yake ni vizuri kutumia dawa hizi kwa maagizo ya wataalamu wa afya kwa sababu kila dawa kwenye kundi hili huwa na kazi maalumu, kwa hiyo dawa hizi hazitumiki kiholela bali ni kwa utaratibu maalum kadri ya tatizo la mgonjwa.
5. Kwa hiyo kutokana na kuwepo kwa dawa mbalimbali kwenye kundi hili kuna wengine watapaswa kutumia na wengine hapana kwa mfano kwa wale wenye presha ya kushuka hawapaswi kutumia baadhi ya dawa kwenye kundi hili kwa hiyo wataalamu wa afya ni lazima wahusike kwenye matumizi ya dawa hizi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Dawa ya kutibu maumivu ya jino
Utaijuwa Dawa ya maumivu ya jino, sababu za maumivu ya jino na njia za kujikinga na maumivu ya jino
Soma Zaidi...Matumizi ya dawa ya vidonda vya tumbo
Posti hii inahusu zaidi matumizi ya dawa za vidonda vya tumbo, ili kuweza kutumia dawa hizi ni vizuri kabisa kufuata mashariti kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Ifahamu dawa ya furosemide.
Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix
Soma Zaidi...Faida za vidonge vya antroextra
Posti hii inahusu zaidi faida za vidonge vya antroextra, ni vidonge kwa ajili ya mifupa, viungo na gegedu, hivi vidonge vimetumiwa na watu wengi na matokeo yake ni mazuri sana, kwa hiyo zifuatazo ni faida za vidonge hivi.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya Prednisone ambayo usaidia katika kupambana na aleji.
Soma Zaidi...