Msimamo wa Uislamu juu ya Utumwa
- Watumwa walikuwa wakikamatwa na kutezwa nguvu bila kujali utu na ubinaadamu wao.
Msimamo wa Uislamu juu ya Utumwa.
Hali ya Utumwa kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w).
- Biashara ya utumwa ilidumu na kuenea sana enzi za ujahili takribani nchi na
mabara mbali mbali hasa nchi za Magharibi, Uarabuni, Bara la Asia na kwingineko Duniani.
- Watumwa walikuwa wakikamatwa na kutezwa nguvu bila kujali utu na
ubinaadamu wao.
- Watumwa walimilikiwa kwa kuuzwa na kununuliwa kama bidhaa za biashara
au kwa matumizi mengineyo pia.
- Watumwa walikuwa wakitumika kama sehemu ya starehe na kiburudisho kwa
wakubwa zao.
- Mateso, unyama na ukatili ilikuwa desturi ya kufanyiwa watumwa na mabwana
zao katika kutimiza matashi yao.
- Watumwa walikuwa hawana uhuru wa kufanya na kufuata mila, desturi au dini
waitakayo na waipendayo wao wenyewe bila ruhusa ya wakubwa wao.
- Watumwa walikuwa wakitumikishwa kama wanyama au hata zaidi ya wanyama
kwa kufanyishwa kazi ngumu zilizozidi uwezo wao.
- Kila jaribio la ubaya lilifanywa kupitia watumwa, mfano makali ya kisu, mkuki,
mshale, n.k yalijaribiwa kwa watumwa.
- Watumwa ndio ilikuwa nyenzo pekee ya kufanyia kazi, kubebea na kusafirishia
mizigo mikubwa kwa masafa ya mbali.
- Hadhi na nafasi kati ya mabwa na watumwa ilikuwa na utofauti mkubwa mno,
kiasi kwamba bwana anaweza kumdhalilisha mtumwa kwa namna apendavyo.
- Huduma na misaada ya kiutu kwa watumwa ilikuwa hafifu mno, kiasi kwamba
mtumwa akiugua au kukosa uwezo wa kuzalisha mali alikuwa hana faida tena
kwa bwana.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 web hosting 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Kuenea kwa dhana ya udhibiti uzazi na uzazi wa mpango
Kustawi kwa Kampeni ya Kudhibiti UzaziMiongoni mwa sababu zilizosaidia kustawi kwa kampeni hii ni matokeo ya mapinduzi ya viwanda (Industrial revolution) ya huko Ulaya.
Soma Zaidi...Aina ya biashara zilizo haramu kwenye uislamu
Hapa utajifunza aina za biashara ambazo ni haramu.
Soma Zaidi...Tarstibu za kulipa swaumu ya Ramadhani
Hapa utajifunza namna ambayo utatakiwa kulipa funga ya Ramadhani kwa siku ambazo hukufunga
Soma Zaidi...