- Uislamu ulieneza nadharia kuwa wanaadamu wote ni sawa na wote ni watumwa mbele ya Mwenyezi Mungu (s.
- Uislamu ulieneza nadharia kuwa wanaadamu wote ni sawa na wote ni watumwa mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w).
- Uislamu ulijenga uhusiano wa udugu na upendo baina ya watu bila kujali hadhi, nafasi, rangi, taifa la mtu.
- Uislamu ulisisitiza kuwa ubora wa mtu unatokana na ucha-Mungu wake na pia mtumwa au mtu huru anastahiki kuwa kiongozi na kutiiwa ipasavyo
Rejea Qur’an (49:13) na (4:25).
- Utumwa katika Uislamu ulikuwa jambo la kupita na sio taasisi ya kudumu inayojenga matabaka ndani ya jamii.
- Uislamu uliweka mikakati ya kulinda haki, utu na hadhi ya watumwa kwa kuwafanyia wema na ihsani kama wanaadamu wengine.
Rejea Qur’an (4:36) na (49:13).
- Watumwa walikuwa na haki ya kuamini na kufuata mila au dini waipendayo bila kushurutishwa.
Rejea Qur’an (2:256).
- Watumwa walikuwa wanapata huduma za kijamii kama mavazi na malazi sawa na mabwana au wanaadamu wengine.
- Mtumwa alikuwa akikosea alisamehewa badala ya kuadhibiwa, Mtume (s.a.w) alisema mtumwa asamehewe hata mara sabini kwa siku.
- Mtumwa alistahiki kuwa kiongozi na kutiiwa ipasavyo maadamu ni muislamu na Mcha-Mungu. Mtume (s.a.w) amesema “msikilizeni na mtiini kiongozi hata akiwa ni mtumwa wa kutoka uhabeshi, maadam anafuata njia ya haki”
- Uislamu unalinda hadhi ya mtumwa kwa kutomuita “Ewe mtumwa wangu” badala yake anaitwa “Ewe kijana wangu”.
- Watumwa walikuwa na haki ya kujikomboa na huru kwa njia mbali mbali zikiwemo:
1. Kulipa kiasi fulani cha pesa au mali yeyote inayokubalika.
2. Kubadilishana na mateka Waislamu waliokamatwa na maadui.
3. Kulipa fidia kwa kufanya jambo fulani lenye manufaa kwa jamii ya waislamu.
Rejea Qur’an (47:4).
- Mtume (s.a.w) na Maswahaba waliwaachia watumwa huru na kuwakomboa wengine kisha kuwaacha huru kama ifuatavyo:
1. Mtume (s.a.w) mwenyewe aliwaacha huru watumwa 63.
2. Bi Aisha (r.a) mkewe Mtume (s.a.w) aliwaacha huru watumwa 67.
3. Ibn Abbas aliwaachia huru watumwa 70.
4. Abdallah bin Umar aliwaacha huru watumwa 1,000.
5. Abdul-Rahman bin Auf alinunua watumwa 30,000 na kuwaacha huru.
Mpaka kufikia mwisho wa uongozi wa Makhalifah wa nne Waongofu, suala la Utumwa lilibakia kuwa historia katika ulimwengu wa Kiislamu.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya jamaa na taratibu zake.
Soma Zaidi...Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Umuhimu wa KusimamishaSwala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha faida na umuhimu wa kijenga uchumi katika jamii ya kiislamu.
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga.
Soma Zaidi...Hili ni somo letu la kwanza kwenye mtiririko huu wa darsa za fiqh. Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya uislamu na nguzo zake.
Soma Zaidi...Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali.
Soma Zaidi...Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?
Soma Zaidi...