Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya Jamii

Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya Jamii

(c) Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya JamiiKimaumbile wanaadam kama walivyo wanyama, wamejaaliwa kuwa na mvuto wa kimapenzi kati ya mume na mke ili kuwawezesha kutekeleza wajibu mkubwa wa kuzaana na kuendeleza kizazi.

Download Post hii hapa

Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya Jamii

(c) Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya Jamii
Kimaumbile wanaadam kama walivyo wanyama, wamejaaliwa kuwa na mvuto wa kimapenzi kati ya mume na mke ili kuwawezesha kutekeleza wajibu mkubwa wa kuzaana na kuendeleza kizazi. Wanyama, matamanio yao ya kukutana dume na jike yanakuwa juu kwa kipindi maalum, pale wanapokuwa tayari kuanzisha uzazi. Tofauti na wanyama, matamanio ya mwanadamu ya kukutana kimwii kati ya mwanamume na mwanamke yako juu siku zote alimradi tu vipatikane vishawishi. Kalika hali hii, endapo wanaume na wanawake wataachiwa huru kuchanganyika na kuingiliana pasina kuwekewa mipaka, watakidhi matamanio yao hadharani kama wanyama na pengine zaidi ya wanyama. Hali hii


tumeiona katika jamii za Ulaya na Marekani baada ya kutolewa uhuru kwa wanawake kuchanganyika na kubusiana na wanaume wependavyo na bila ya mipaka. Athari ya uhuru huu kwa jamii ya Ulaya na Marekani tumeiona katika kushamiri kwa umalaya, kuenea magonjwa ya zinaa, kuwa na watoto wa nje ya ndoa, kuvunjika kwa familia, n.k. Lakini aliyeathirika zaidi ni mwanamke ambaye uke wake umefanywa ni bidhaa ya kuuzwa na kununuliwa na urembo wake umefanywa ni chombo cha matangazo ya biashara.



Allah (s.w) hakujaaliwa mvuto wa mapenzi kati ya mwanamume na mwanamke, ili kumdhalilisha mwanamke na kuiangamiza jamii, bali amejaalia mvuto huu wa kimapenzi kati ya mume na mke ili wanadamu waweze kuendeleza kizazi na kuishi maisha ya kijamii yaliyojcngwa juu ya misingi imara ya upendo na ushirikiano;


Na katika ishara Zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu katika jinsia yenu iii mpate utulivu kwao, naye amejaalia mapenzi 'na huruma baina yenu (30:21).
Ili tuweze kufikia lengo hili, Allah (s.w) ametuwekea utaratibu maalum wa mahusiano kati ya wanaume na wanawake. Allah (s.w) ameturuhusu, wanaume na wanawake, tukidhi matashi ya kimaumbile kati ya mwanamke kwa njia ya ndoa na ametuharamishia mahusiano yoyote kati ya mume na mke nje ya mipaka ya ndoa. Ili kurahisisha maisha ya ndoa na kuyafanya mahusiano kati ya mume na mke nje ya ndoa yawe magumu, Uislamu umeweka vipengele kadhaa vya kuihifadhi jamii na zinaa:



(i)Kujitakasa mtu binafsi (ucha-Mungu)
(ii)Kutoa adhabu kali kwa wazinifu
(iii)Kutokomeza vishawishi vya zinaa
(i) Kujitakasa Mtu binafsi (ucha-Mungu)



Ucha-Mungu ni kuishi kwa kuchunga mipaka ya Allah (s.w) kwa unyenyekevu. Imani thabiti ndio nyenzo kubwa ya kumuwezesha mja kuchunga mipaka ya Allah (s.w). Muumini wa kweli ni yule anayefuata kwa ukamilifu sheria ya Kiislamu katika maisha yake yote kwa kuhakikisha kuwa anafuata maamrisho yote ya Allah (s.w) na kuacha makatazo yake yote. Kwa Muumini huyu anachohitajia ni kujua tu Allah (s.w) na Mtume wake wamearisha nini na wamekataza nini. Muislamu mcha-Mungu atakapojua kuwa jambo fulani limekatazwa katika kitabu cha Allah (s.w) kama vile zinaa ilivyoharamishwa katika aya kadhaa (rejea Qur'an: 17:32), hatajiepusha na kulitenda tu bali hata pia kuliwaza.



Miongoni mwa nyenzo zilizowekwa na Uislamu ili kumuwezesha mtu binafsi kuepukana na tendo ovu Ia zinaa ni kuwasisitiza waumini kuwa na haya, kujiepusha na fikra mbaya juu ya wanawake/wanaume, kujiepusha na kutizama kwa matamanio na wanawake kujiepusha na kushawishi kwa sauti kali, kudhihirisha mapambo na kupaka manukato makali.



"Haya" ni msingi wa Imani na ngao ya kumkinga mtu na maovu. llivyo ni kwamba matendo maovu kama vile uzinifu, wizi, uwongo, n.k. ambavyo mwanaadam huyatenda kutokana na msukumo wa matashi ya unyama wake, yanampelekea kwenda kinyume na utu wake. Matendo yote maovu yameelezwa katika Qur'an kwa neno "Munkar" lenye maana "isiyojulikana" au "jambo geni". Vitendo hivi vimeitwa "Munkar' kwa sababu ni vigeni katika utu wa mwanaadam. Mwanaadam ameumbwa na nguvu ya kupigana ndani kwa ndani na maovu. Nguvu hii ni "haya".



Nguvu hii ipo kwa kila mtu lakini inahitaji kuamshwa kwa kupewa mara kwa mara mafundisho ya maadili ya Uislamu. Katika kuonesha nafasi ya "haya" katika maadili ya Uislamu Mtume (s.a.w) amesema: 'Kila dini ma maadili yake na maadili ya Uislam ni 'Haya ". "Haya" ndiyo inayomuwezesha mwanaadam kujiepusha na maovu bila ya nguvu za polisi. Kinyume chake mtu asiye na haya hufanya ovu lolote alitakalo. Mtume (s.a.w) kasema: 'Unapokuwa huna haya unaweza kufanya ulitakalo ".
Muislam katika kujiepusha na matendo maovu na machafu, hawaonei haya wanaadam wenziwe tu bali humuonea haya zaidi Mwenyezi Mungu ambaye yu karibu yake zaidi kuliko mshipa wake mkuu wa damu (Jugular vein). Mtume (s.a.w) amesema: <<Allah (s.w) anahaki zaidi ya kuonewa haya" (Tirmidh). Kama mtu anaona haya kutenda kitendo kiovu mbele ya watu, basi aone haya zaidi kutenda kitendo hicho mbele ya Allah (s.w).




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 803

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰2 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰3 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰5 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Mwenendo wa Mtu aliyetoa Shahada
Mwenendo wa Mtu aliyetoa Shahada

Muislamu aliyetoa shahada ya kweli hanabudiย kumfanya Mtume (s.

Soma Zaidi...
Maana ya hadathi na aina zake
Maana ya hadathi na aina zake

Post hii inakwenda kukugundisha maana ya hadathi pamoja na kutaja aina za hadathi

Soma Zaidi...
Nini kifanyike baada ya mazishi ya kiislamu
Nini kifanyike baada ya mazishi ya kiislamu

Huu ni utaratibu unaotakiwa kufanyika baada ya kuzika.

Soma Zaidi...
Sunnah za swaumu,  sunnah ambazo zinaambatans ns kufungabmwezi wa Ramadhani
Sunnah za swaumu, sunnah ambazo zinaambatans ns kufungabmwezi wa Ramadhani

Yajuwe mambo ambayo yanapendeza kuyafanya wakati ukiwa umefunga Ramadhani.

Soma Zaidi...
Mifano na namna ya kurithisha
Mifano na namna ya kurithisha

Ugawaji wa mirathi-Mume ana nusu (1/2) = 1/2 -Mama ana sudusi.

Soma Zaidi...
JIFUNZE FIQH
JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Fadhila za usiku waalylat al qadir
Fadhila za usiku waalylat al qadir

Zijuwe fadhila za usiku wenye cheo kuliko nyusiku ya miezi 1000.

Soma Zaidi...
Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?
Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?

Kwa nini Lengo la Zakat na Sadaqat Halijafikiwa katika Jamii yetu?

Soma Zaidi...