image

Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya Jamii

(c) Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya JamiiKimaumbile wanaadam kama walivyo wanyama, wamejaaliwa kuwa na mvuto wa kimapenzi kati ya mume na mke ili kuwawezesha kutekeleza wajibu mkubwa wa kuzaana na kuendeleza kizazi.

Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya Jamii

(c) Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya Jamii
Kimaumbile wanaadam kama walivyo wanyama, wamejaaliwa kuwa na mvuto wa kimapenzi kati ya mume na mke ili kuwawezesha kutekeleza wajibu mkubwa wa kuzaana na kuendeleza kizazi. Wanyama, matamanio yao ya kukutana dume na jike yanakuwa juu kwa kipindi maalum, pale wanapokuwa tayari kuanzisha uzazi. Tofauti na wanyama, matamanio ya mwanadamu ya kukutana kimwii kati ya mwanamume na mwanamke yako juu siku zote alimradi tu vipatikane vishawishi. Kalika hali hii, endapo wanaume na wanawake wataachiwa huru kuchanganyika na kuingiliana pasina kuwekewa mipaka, watakidhi matamanio yao hadharani kama wanyama na pengine zaidi ya wanyama. Hali hii


tumeiona katika jamii za Ulaya na Marekani baada ya kutolewa uhuru kwa wanawake kuchanganyika na kubusiana na wanaume wependavyo na bila ya mipaka. Athari ya uhuru huu kwa jamii ya Ulaya na Marekani tumeiona katika kushamiri kwa umalaya, kuenea magonjwa ya zinaa, kuwa na watoto wa nje ya ndoa, kuvunjika kwa familia, n.k. Lakini aliyeathirika zaidi ni mwanamke ambaye uke wake umefanywa ni bidhaa ya kuuzwa na kununuliwa na urembo wake umefanywa ni chombo cha matangazo ya biashara.



Allah (s.w) hakujaaliwa mvuto wa mapenzi kati ya mwanamume na mwanamke, ili kumdhalilisha mwanamke na kuiangamiza jamii, bali amejaalia mvuto huu wa kimapenzi kati ya mume na mke ili wanadamu waweze kuendeleza kizazi na kuishi maisha ya kijamii yaliyojcngwa juu ya misingi imara ya upendo na ushirikiano;


Na katika ishara Zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu katika jinsia yenu iii mpate utulivu kwao, naye amejaalia mapenzi 'na huruma baina yenu (30:21).
Ili tuweze kufikia lengo hili, Allah (s.w) ametuwekea utaratibu maalum wa mahusiano kati ya wanaume na wanawake. Allah (s.w) ameturuhusu, wanaume na wanawake, tukidhi matashi ya kimaumbile kati ya mwanamke kwa njia ya ndoa na ametuharamishia mahusiano yoyote kati ya mume na mke nje ya mipaka ya ndoa. Ili kurahisisha maisha ya ndoa na kuyafanya mahusiano kati ya mume na mke nje ya ndoa yawe magumu, Uislamu umeweka vipengele kadhaa vya kuihifadhi jamii na zinaa:



(i)Kujitakasa mtu binafsi (ucha-Mungu)
(ii)Kutoa adhabu kali kwa wazinifu
(iii)Kutokomeza vishawishi vya zinaa
(i) Kujitakasa Mtu binafsi (ucha-Mungu)



Ucha-Mungu ni kuishi kwa kuchunga mipaka ya Allah (s.w) kwa unyenyekevu. Imani thabiti ndio nyenzo kubwa ya kumuwezesha mja kuchunga mipaka ya Allah (s.w). Muumini wa kweli ni yule anayefuata kwa ukamilifu sheria ya Kiislamu katika maisha yake yote kwa kuhakikisha kuwa anafuata maamrisho yote ya Allah (s.w) na kuacha makatazo yake yote. Kwa Muumini huyu anachohitajia ni kujua tu Allah (s.w) na Mtume wake wamearisha nini na wamekataza nini. Muislamu mcha-Mungu atakapojua kuwa jambo fulani limekatazwa katika kitabu cha Allah (s.w) kama vile zinaa ilivyoharamishwa katika aya kadhaa (rejea Qur'an: 17:32), hatajiepusha na kulitenda tu bali hata pia kuliwaza.



Miongoni mwa nyenzo zilizowekwa na Uislamu ili kumuwezesha mtu binafsi kuepukana na tendo ovu Ia zinaa ni kuwasisitiza waumini kuwa na haya, kujiepusha na fikra mbaya juu ya wanawake/wanaume, kujiepusha na kutizama kwa matamanio na wanawake kujiepusha na kushawishi kwa sauti kali, kudhihirisha mapambo na kupaka manukato makali.



"Haya" ni msingi wa Imani na ngao ya kumkinga mtu na maovu. llivyo ni kwamba matendo maovu kama vile uzinifu, wizi, uwongo, n.k. ambavyo mwanaadam huyatenda kutokana na msukumo wa matashi ya unyama wake, yanampelekea kwenda kinyume na utu wake. Matendo yote maovu yameelezwa katika Qur'an kwa neno "Munkar" lenye maana "isiyojulikana" au "jambo geni". Vitendo hivi vimeitwa "Munkar' kwa sababu ni vigeni katika utu wa mwanaadam. Mwanaadam ameumbwa na nguvu ya kupigana ndani kwa ndani na maovu. Nguvu hii ni "haya".



Nguvu hii ipo kwa kila mtu lakini inahitaji kuamshwa kwa kupewa mara kwa mara mafundisho ya maadili ya Uislamu. Katika kuonesha nafasi ya "haya" katika maadili ya Uislamu Mtume (s.a.w) amesema: 'Kila dini ma maadili yake na maadili ya Uislam ni 'Haya ". "Haya" ndiyo inayomuwezesha mwanaadam kujiepusha na maovu bila ya nguvu za polisi. Kinyume chake mtu asiye na haya hufanya ovu lolote alitakalo. Mtume (s.a.w) kasema: 'Unapokuwa huna haya unaweza kufanya ulitakalo ".
Muislam katika kujiepusha na matendo maovu na machafu, hawaonei haya wanaadam wenziwe tu bali humuonea haya zaidi Mwenyezi Mungu ambaye yu karibu yake zaidi kuliko mshipa wake mkuu wa damu (Jugular vein). Mtume (s.a.w) amesema: <<Allah (s.w) anahaki zaidi ya kuonewa haya" (Tirmidh). Kama mtu anaona haya kutenda kitendo kiovu mbele ya watu, basi aone haya zaidi kutenda kitendo hicho mbele ya Allah (s.w).




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 292


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Faida na umuhimu wa ndoa katika jamii
Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi Soma Zaidi...

Haki na Wajibu wa mume kwa mkewe na familia
Soma Zaidi...

Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Zijuwe aina za swala za Suna na namna za kuziswaliWitri, Dhuha, Idi, tarawehe, tahajudu na nyingine
Soma Zaidi...

Taratibu za kumiliki hisa na mali ya shirika
Katika Uislamu kuwa na hisa kwenye mali inaruhusiwa. Hapa utajifunza taratibu za kumiliki hisa. Soma Zaidi...

Kutoa vilivyo vizuri
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Swala ya maiti, namna ya kuiswali, nguzo zake, sharti zake na suna zake, hatua kwa hatua
Soma Zaidi...

Ni yapi mambo yanayoharibu Swaumu na Mambo yanayobatilisha funga
Soma Zaidi...

Swala ya ijumaa, nguzo zake, sharti zake na jinsi ya kuiswali
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali. Soma Zaidi...

Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?
Kwa nini Lengo la Zakat na Sadaqat Halijafikiwa katika Jamii yetu? Soma Zaidi...

Hijja na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Jinsi ya kutoa zakat al fitiri na umuhimu wa zakat al fitri kwa waislamu
Hapa utajifunza kuhusu zakat al fitiri, kiwango chake, watu wanaostahili kupewa na kutoa, pia umuhimu wake katika jamii. Soma Zaidi...