Namna ya kuoga josho, kujitwaharisha damu ya Hedhi, damu ya kuzaa Nifasi na Janaba
Masharti ya Kuoga
Masharti ya kuoga ni sawa tu na yale masharti ya udhu ila hapa yanahusu mwili mzima.
Nguzo za Kuoga
Kwanza, kutia nia moyoni kuwa unaoga kwa madhumuni ya kujitwaharisha, kutokana na janaba, hedhi, au nifasi. Mahali pa nia ni moyoni na wakati wa kunuiwa ni pale unapoanza kuosha kiungo cha kwanza.
Pili, kueneza maji mwili mzima. Ili kuhakikisha kuwa umeeneza maji mwili mzima ni vyema ufuate mafundisho ya Mtume (s.a.w). Mtume katika kuoga alikuwa akianza kwa kuosha sehemu za siri, kisha alikuwa akitia udhu, kisha alikuwa akijimiminia maji kichwani mara tatu, kisha alikuwa akieneza maji mwili mzima kwa kuanzia upande wa kulia na kumalizia upande wa kushoto, pote mara tatu tatu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Vipi utapata uchamungu kupitia funga
Vipi lengo la funga litafikiwa na kumfanya mfungaji awe mchamungu.
Soma Zaidi...Sura zinazosomwa katika Swala ya Dhuha
Swala ya Dhuha ni swala ya sunna inayosaliwa wakati wa asubuhi baada ya jua kuchomoza na kupanda angalau kiasi cha mkuki (takribani dakika 15 baada ya jua kuchomoza) mpaka kabla ya adhuhuri. Ingawa hakuna sura maalum zilizowekwa kisheria, Mtume ﷺ alisoma baadhi ya sura zenye maana ya kuhimiza kheri na shukrani.
Soma Zaidi...