image

Dalili za saratani kwa watoto.

Posti hii inahusu zaidi Dalili za saratani kwa watoto, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto na ikiwa mlezi au mzazi akiziona tu anaweza kutambua mara moja kwamba hii ni saratani au la na kama bado ana wasiwasi anaweza kupata msaada zaidi kutoka kwa wataa

Dalili za saratani kwa watoto wadogo.

1.Kwanza kabisa mtoto anakuwa na uvimbe usio wa kawaida  na ambao hauna maumivu kwenye sehemu za mashavu,  kwenye shingo, tumbo, miguuni na sehemu zozote za mwili, kwa mara ya kwanza uvimbe huu unakuwa hauna maumivu hata kidogo lakini ikiwa  umetibuliwa au kuchokonolewa uvimbe huu unaweza kubadilika na kutengeneza kitu kingine na kusababisha maumivu kwa mtoto.

 

2. Kwa hiyo baada ya kuona uvimbe wa aina hii na mtoto anaendelea na maisha bila kuonyesha Dalili yoyote ya maumivu kwanza  kabisa mtoto anapaswa kupelekwa kwa wataalamu wa magonjwa ya saratani na epuka kabisa kutingisha uvimbe huu kwa kutumia waganga wa kienyeji ambao hawana utaalamu wowote au mzazi mwenyewe kuamua kuchokonoa uvimbe huu, mpeleke mtoto hospitalini ili aweze kupata utaratibu kutoka kwa wataalamu wa afya.

 

3. Macho ya mtoto kuwa mekundu kuvimba, kuongezeka, au upofu kwa ghafla.

Kwa kawaida kwa upande wa macho ya mtoto yanaanza kidogo kidogo kuwa mekundu na siku kwa siku wekundu unazidi  na hatimaye mtoto anashindwa kuona linaweza kuanza jicho moja na baadae likaingia la pili au yote mawili yanaweza kupata shida kwa wakati mmoja na kama mtoto hajapata huduma mapema upofu unaweza kutokea kwa mtoto .

 

4. Pia kwa wakati mwingine  damu utoka puani na kwenye fizi. 

Na pia hizi ni mojawapo ya Dalili za saratani kwa watoto wadogo kwa sababu damu zikianza kutoka puani uanza kidogo kidogo na uongezeka zaidi pale kama kuna joto la kwenye mazingira likiwa juu na pia mtoto damu uanza kupungua siku kwa siku na hata damu ikiongezwa inapungua na kwa upande wa fizi ikitokea mtoto kama amefikia wakati wa kupiga maswaki akipiga damu utoka kwa wangi kwenye fizi. Kwa hiyo walezi na wazazi wanapaswa kufika kwa wataalamu wa afya ili kupata matibabu zaidi.

 

5. Mtoto kukonda na kupungua uzito bila sababu.

Kwa wakati mwingine mtoto anaanza kukonda na kupungua uzito bila sababu na huku anakuwa anacheza kawaida ila anakonda na uzito unapungua kwa hiyo Mama anapaswa kumpeleka mtoto huyo kwa wataalamu wa afya ili kuweza kujua tatizo ni nini kwa mtoto, na kwa wakati huu hata mtoto akipewa lishe ya aina yoyote anaongezeka kidogo na baadae hali inakuwa kama kawaida yaani kukonds na kupungua uzito.

 

6. Maumivu ya kichwa kwa mda mrefu na kutapika.

Kwa kawaida kwa watoto wale ambao wanaweza kuongea anaweza kukwambia jinsi anavyojisikia mara nyingi utasikia analalamika kuhusu kichwa kwa wale ambao hawajui kuongea atakuwa analia mara kwa mara , na pia kwa upande wa kutapika mtoto anaweza kutapika kwa mda mrefu hata kama hajala lolote anatapika tu na pia kwa wakati mwingine matapishi huwa mengi kuliko chakula ambacho anakula hali ambayo uwatia wasiwasi pia wazazi  wengine wanaweza kuwa na imani potovu kuhusu hilo.

 

7. Mtoto anaweza kudhoofika na kuacha kucheza pamoja na watoto wengine.

Kwa upande mwingine mtoto anakosa raha anaanza kudhoofika na anashindwa kucheza na wengine kwa wakati mwingine Mama au walezi wanaweza kuchukulia kubwa ni sehemu ya maisha kubwa mtoto huwa hachezi kumbe kuna tatizo ndani yake kwa hiyo uchunguzi kwa mtoto ni lazima ili kuweza kuona kuna tatizo gani, kwa hiyo wazazi au walezi wanapaswa kuwa pamoja na watoto ili kuangalia mabadiliko katika makuzi yao.

 

8. Kwa wakati mwingine mtoto akipata ajali kidogo anatokea na damu nyingi ukilinganisha na kidonda chake kwa hiyo unakuta damu inapungua mwilini na kwa mara nyingine Dalili za wazi ujitokeza ambapo mtoto akipata ka jeraha na damu zikitoka anabadilika rangi na kuwa na rangi nyeupe fulani hivi kwenye mwili.

 

9.Kwa hiyo kitu ambacho tunapaswa kuelewa kubwa saratani kwa watoto pengine uonyesha dalili mbalimbali ambazo zinaweza pengine kuleta mashaka kwa wazazi kwa hiyo basi wazazi na walezi wanapaswa kuwa makini ili kuepukana na Imani za kishirikina na kuweza kujua wazi kuwa ni magonjwa ambayo yako kwenye jamii mbalimbali.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1696


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito. Soma Zaidi...

Faida za uzazi wa mpango kwa jamii
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa jamii, tunapaswa kujua kuwa uzazi wa mpango ukitumiwa vizuri na jamii nayo inapata faida kwa hiyo zifuatazo ni faida za uzazi wa mpango kwa jamii. Soma Zaidi...

Jinsi ya kupata mtoto wa kiume
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nadharia ya kupata mtoto wa kiume. Soma Zaidi...

dalili za uchungu kwa mama mjamzito
Makala hii itakwenda kukufundisha baadhi ya dalili za uchungu kwa mama mjamzito. Soma Zaidi...

Namna ya kutunza uke
Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza uke, tunajua wazi kuna magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo uke hautaweza kutunzwa vizuri na pia uke ukitunzwa vizuri kuna faida ya kuepuka maradhi ya wanawake kwa njia ya kutunza uke. Soma Zaidi...

Habari Mimi ni mjamzito was miezi Tisa sasa nimeanza kutokwa na maji kidogo kidogo ukeni bila uchungu na no mimba yangu ya kwanza he Kuna shida?
Ujauzito husababisha mabadiliko mengi mwilini, ikiwepo ongezeko la Majimaji ukeni ifikapo tarehe za kukaribia kujifunguwa. Majimaji haya ni muhimu kwa afya ya mtoto aliye tumboni. Soma Zaidi...

Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.
Posti hii inahusu zaidi huduma muhimu anazopaswa kupewa mama mjamzito wakati akiwa na mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua yaani ndani ya masaa ishirini na manne, tunajua wazi kuwa Mama akiwa mjamzito anaweza kupata matatizo mbalimbali kwa h Soma Zaidi...

siku za hatari
Hizi ni siku za hatari kupata ujauzito.Siku hizi ndio siku za kupata mimba kwa urahisi Soma Zaidi...

dalili za mimba changa ndani ya wiki moja
Soma Zaidi...

Njia za kuongeza uwezo wa kuzaa au kuzalisha.
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuongeza uwezo wa kuzaa au kuzalisha kwa sababu kuna familia nyingi zinakosa watoto sio kwa sababu ni tasa ila kuna njia mbalimbali za kuongeza uwezo wa kuzaa kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Faida za uzazi wa mpango kwa watoto.
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa uzazi wa mpango kwa watoto, sio akina Mama peke yao wanaofaidika na uzazi wa mpango vile vile na watoto wanafaidika na uzazi wa mpango kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Nia za kupima ujauzito ukiwa nyumbani, Njia kuu 10 za kiasili za kupima mimba changa
Kuna njia nyingi zinatajwa zinapima mimba kama chumvi, sukari, mafuta na sabuni. Hata hivyo zipo njia zaidi ya 10 za kiasili za kupima ujauzito. Utajifunza hapa zote Soma Zaidi...