Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa Mama mjamzito, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama mjamzito, hizi Dalili zisipofanyiwa kazi mapema zinaweza kuleta shida kwa Mama kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua Dalili hizi na kuchukua hatua endapo zitajio
Dalili za hatari kwa Mama mjamzito
1. Kutokwa na damu ukeni.
Kutokwa na damu kunaweza kuwa sio dalili mbaya, kwani si jambo la kuogopa na ni hali inayoweza kumtokea mjamzito. Lakini tunatarajia damu hii sio nyingi. Endapo damu hii itaambatana na maumivu makali ya tumbo, ama kizunguzungu ama maumivu makali ya kichwa, ni vyema kufika kituo cha afya. Pia endapo damu hii itakuwa nyingi kiasi cha kuhitaji kujisitiri pia ni vyema kufika kituo cha afya kwa uangalizi.
2. Dalili ya hatari nyingine kwa Mama mjamzito ni mtoto kushindwa kucheza tumboni, kwa kawaida uhai wa mtoto akiwa tumboni ni kuhisi kuwa mtoto anacheza pindi mtoto akishindwa kucheza hiyo ni Dalili ya hatari , wakati mwingine ni mabadiliko ya Mama kama vile uchovu na sababu nyingine nyingi, kwa hiyo mama akisikia mtoto amepitisha siku bila kucheza anapaswa kwenda hospitalini mara moja ili aweze kupata msaada zaidi.
3. Kuvimba miguu kwa wajawazito.
Na hili ni mojawapo ya Dalili ya hatari kwa Mama , ambapo maji mengi yanayoka kwenye seli yanakuja kwenye tisu na pengine ni kwa sababu ya kupungua kwa protini kwenye mwili na sababu nyingine nyingi kwa hiyo Mama akiona amevimba miguuni anapaswa kwenda hospitalini ili kupata matibabu na maelekezo zaidi kutoka kwa wataalamu wa afya pia wauguzi wanapaswa kuwaambia wakina Mama kuwa pindi waonapo Dalli hizi wanapaswa kwenda moja kwa moja hospitalini.
4.Maumivu akali ya kichwa kwa Mama mjamzito.
Mama mjamzito akipatwa na maumivu makali ya kichwa anapaswa kujua wazi hali yake ya kuwa ni ya hatari kwa hiyo anapaswa kwenda hospitalini kwa sababu kuumwa sana kichwa kunaweza kusababishwa na presha au mabadiliko yoyote ya mwili ambayo yasipotibiwa kwa wakati yanaweza kuleta kitu kingine kisicho cha kawaida. Kwa hiyo wauguzi na wataalam wengine wa afya wanaswa kuwaambia ukweli kuhusu Dalili hizi za hatari.
5. Kwa kawaida tunajua wazi kubwa akina Mama wajawazito wanapaswa kutunzwa vizuri na kuhakikisha kubwa wasipatwa na janga lolote ambalo linaweza kumfanya awe dhaifu kwa hiyo tunapaswa kujua Dalili za hatari na kuwapeleka hospitali mara moja bila kuchelewa na pia wanapaswa kwenda kliniki mara kwa mara ili kuweza kujua maendeleo ya afya zao na pia jamii iliyowazunguka inapaswa kujua Dalili hizi na kuwawaisha hospitalini bila kuchelewa
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Utajifunza sababu za kuweo kwa maumivu ya uume wbaada ya tendo la ndoa na wakati wa tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo nakiuno kwa mwanamke yanahitaji uangalizi wakina. Kwani kuna sababu nyingi ambazo zinawezakuwa ni chanzo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dalili za mimba kutoka, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa mimba zote ambazo utaka kutoka kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu wakati wa tendo la ndoa na baada
Soma Zaidi...Je, unafahamu dalili za mwanzo za ujauzito? Kutoka kwa kichefuchefu hadi uchovu, ujue nini cha kutarajia.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kujaa tmgesi tumbon
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za PID maana yake ni maambukizi kwenye pelvic kwa kitaalamu huitwa pelvic infection disease, ni ugonjwa unaoshambulia sana wanawake na wasichana
Soma Zaidi...Utajifunza dalili za minyoo, sababu za minyoo na namna ya kujiepusha na minyoo. Dalili kuu 5 za minyoo mwilini
Soma Zaidi...Ujauzito husababisha mabadiliko mengi mwilini, ikiwepo ongezeko la Majimaji ukeni ifikapo tarehe za kukaribia kujifunguwa. Majimaji haya ni muhimu kwa afya ya mtoto aliye tumboni.
Soma Zaidi...