picha

Zijue Dalili za hatari kwa Mama mjamzito

Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa Mama mjamzito, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama mjamzito, hizi Dalili zisipofanyiwa kazi mapema zinaweza kuleta shida kwa Mama kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua Dalili hizi na kuchukua hatua endapo zitajio

Dalili za hatari kwa Mama mjamzito 

1. Kutokwa na damu ukeni.

Kutokwa na damu kunaweza kuwa sio dalili mbaya, kwani si jambo la kuogopa na ni hali inayoweza kumtokea mjamzito. Lakini tunatarajia damu hii sio nyingi. Endapo damu hii itaambatana na maumivu makali ya tumbo, ama kizunguzungu ama maumivu makali ya kichwa, ni vyema kufika kituo cha afya. Pia endapo damu hii itakuwa nyingi kiasi cha kuhitaji kujisitiri pia ni vyema kufika kituo cha afya kwa uangalizi.

 

2. Dalili ya hatari nyingine kwa Mama mjamzito ni mtoto kushindwa kucheza tumboni, kwa kawaida uhai wa mtoto akiwa tumboni ni kuhisi kuwa mtoto anacheza pindi mtoto akishindwa kucheza hiyo ni Dalili ya hatari  ,  wakati mwingine ni mabadiliko ya Mama kama vile uchovu na sababu nyingine nyingi, kwa hiyo mama akisikia mtoto amepitisha siku  bila kucheza anapaswa kwenda hospitalini mara moja ili aweze kupata  msaada zaidi.

 

 3. Kuvimba miguu kwa wajawazito.

Na hili ni mojawapo ya Dalili ya hatari kwa Mama , ambapo maji mengi yanayoka kwenye seli yanakuja kwenye tisu na pengine ni kwa sababu ya kupungua kwa protini kwenye mwili na sababu nyingine nyingi kwa hiyo Mama akiona amevimba miguuni anapaswa kwenda hospitalini ili kupata matibabu na maelekezo zaidi kutoka kwa wataalamu wa afya pia wauguzi wanapaswa kuwaambia wakina Mama kuwa pindi waonapo Dalli hizi wanapaswa kwenda moja kwa moja hospitalini.

 

4.Maumivu akali ya kichwa kwa Mama mjamzito.

Mama mjamzito akipatwa na  maumivu makali ya kichwa anapaswa kujua wazi hali yake ya kuwa ni ya hatari kwa hiyo anapaswa kwenda hospitalini kwa sababu kuumwa sana kichwa kunaweza kusababishwa na presha au mabadiliko yoyote ya mwili ambayo yasipotibiwa kwa wakati yanaweza kuleta kitu kingine kisicho cha kawaida. Kwa hiyo wauguzi na wataalam wengine wa afya wanaswa kuwaambia ukweli kuhusu Dalili hizi za hatari.

 

5. Kwa kawaida tunajua wazi kubwa akina Mama wajawazito wanapaswa kutunzwa vizuri na kuhakikisha kubwa wasipatwa na janga lolote ambalo linaweza kumfanya awe dhaifu kwa hiyo tunapaswa kujua Dalili za hatari na kuwapeleka hospitali mara moja bila kuchelewa na pia wanapaswa kwenda kliniki mara kwa mara ili kuweza kujua maendeleo ya afya zao na pia jamii iliyowazunguka inapaswa kujua Dalili hizi na kuwawaisha hospitalini bila kuchelewa 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 3449

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Uhusiano uliopo kati ya Mama Mjamzito na kibofu cha mkojo.

Posti hii inahusu zaidi uhusiano uliopo kati ya Mama Mjamzito na kibofu cha mkojo.ni mwingiliano unaokuwepo ambao usababisha Mama kukojoa sana wakati wa ujauzito.

Soma Zaidi...
Niharisha siku ya pili baada ya tendo. Jana hadi leo sijapata choo inawezakua nimeshika ujauzito?

Hivi unadhani kuharisha ni katika dalili za mimba, vipi kuhusu kutopata choo pia inaweza kuwa ni ujauzito?

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu wakati wa tendo la ndoa

Kama unapata maumivu wakati wa tendo la ndoa, suluhisho lako lipo kwenye makala hii

Soma Zaidi...
Mabadiliko kwenye tumbo la uzazi wa Mama anapobeba Mimba.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye tumbo la uzazi la Mama pindi anapobeba mimba, ni mabadiliko yanayotokea kwa mwanamke anapobeba mimba kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Namna ya kufunga kitovu cha mtoto.

Posti hii inahusu zaidi njia au namna ya kufunga kitovu cha mtoto mara tu anapozaliwa, kwa kawaida tunafahamu kwamba ili mtoto aweze kuishi akiwa tumboni anategemea sana kula na kufanya shughuli zake kwa kupitia kwenye plasenta kwa hiyo mtoto akizaliwa tu

Soma Zaidi...
Vipimo muhimu wakati wa ujauzito

Post hii inahusu zaidi vipimo muhimu wakati wa ujauzito ni vipimo ambavyo vinapaswa kupimwa na Mama ili kuangalia mambo mbalimbali katika damu au sehemu yoyote, pia vipimo hivi umsaidia sana Mama kujua afya yake.

Soma Zaidi...