Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa Mama mjamzito, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama mjamzito, hizi Dalili zisipofanyiwa kazi mapema zinaweza kuleta shida kwa Mama kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua Dalili hizi na kuchukua hatua endapo zitajio
Dalili za hatari kwa Mama mjamzito
1. Kutokwa na damu ukeni.
Kutokwa na damu kunaweza kuwa sio dalili mbaya, kwani si jambo la kuogopa na ni hali inayoweza kumtokea mjamzito. Lakini tunatarajia damu hii sio nyingi. Endapo damu hii itaambatana na maumivu makali ya tumbo, ama kizunguzungu ama maumivu makali ya kichwa, ni vyema kufika kituo cha afya. Pia endapo damu hii itakuwa nyingi kiasi cha kuhitaji kujisitiri pia ni vyema kufika kituo cha afya kwa uangalizi.
2. Dalili ya hatari nyingine kwa Mama mjamzito ni mtoto kushindwa kucheza tumboni, kwa kawaida uhai wa mtoto akiwa tumboni ni kuhisi kuwa mtoto anacheza pindi mtoto akishindwa kucheza hiyo ni Dalili ya hatari , wakati mwingine ni mabadiliko ya Mama kama vile uchovu na sababu nyingine nyingi, kwa hiyo mama akisikia mtoto amepitisha siku bila kucheza anapaswa kwenda hospitalini mara moja ili aweze kupata msaada zaidi.
3. Kuvimba miguu kwa wajawazito.
Na hili ni mojawapo ya Dalili ya hatari kwa Mama , ambapo maji mengi yanayoka kwenye seli yanakuja kwenye tisu na pengine ni kwa sababu ya kupungua kwa protini kwenye mwili na sababu nyingine nyingi kwa hiyo Mama akiona amevimba miguuni anapaswa kwenda hospitalini ili kupata matibabu na maelekezo zaidi kutoka kwa wataalamu wa afya pia wauguzi wanapaswa kuwaambia wakina Mama kuwa pindi waonapo Dalli hizi wanapaswa kwenda moja kwa moja hospitalini.
4.Maumivu akali ya kichwa kwa Mama mjamzito.
Mama mjamzito akipatwa na maumivu makali ya kichwa anapaswa kujua wazi hali yake ya kuwa ni ya hatari kwa hiyo anapaswa kwenda hospitalini kwa sababu kuumwa sana kichwa kunaweza kusababishwa na presha au mabadiliko yoyote ya mwili ambayo yasipotibiwa kwa wakati yanaweza kuleta kitu kingine kisicho cha kawaida. Kwa hiyo wauguzi na wataalam wengine wa afya wanaswa kuwaambia ukweli kuhusu Dalili hizi za hatari.
5. Kwa kawaida tunajua wazi kubwa akina Mama wajawazito wanapaswa kutunzwa vizuri na kuhakikisha kubwa wasipatwa na janga lolote ambalo linaweza kumfanya awe dhaifu kwa hiyo tunapaswa kujua Dalili za hatari na kuwapeleka hospitali mara moja bila kuchelewa na pia wanapaswa kwenda kliniki mara kwa mara ili kuweza kujua maendeleo ya afya zao na pia jamii iliyowazunguka inapaswa kujua Dalili hizi na kuwawaisha hospitalini bila kuchelewa
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Kuuma mwa matiti ni moka ya Ichiro kuwa huwenda ni ujauzito. Hii haimaanishi etindio mjamzito, zipo dalili nyingi za ujauzito. Hata hivyo kuona dalili za ujauzito haimaanishi umepata tayari ujauzito. Kwanza fanya vipimondipo Upate uhakika
Soma Zaidi...Kukoma hedhi hufafanuliwa kuwa hutokea miezi 12 baada ya kipindi chako cha mwisho cha hedhi na huashiria mwisho wa mizunguko ya hedhi. Kukoma hedhi kunaweza kutokea katika miaka ya 40 au 50. Kukoma hedhi ni mchakato wa asili wa kibaolojia. Ingawa pia in
Soma Zaidi...Nitakujulisha siku ya kupata mimba na sifa zake, na namna ya kuweza kuitafuta
Soma Zaidi...Kipimo cha mimba kwa mkojo kimekuwa kikitumika sana kuangalia ujauzito. Kipimo hiki kinapotumika vibaya kinaweza kukupa majibu ya uongo. Kuwa makini na ujue muda sahihi.
Soma Zaidi...Ni vyakula gani anapasa kula mjamzito, na utaratibu mzima wa lishe kwa wajawazito
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupima mimba kwa kutumia chumvi sukari na sabuni
Soma Zaidi...Kuunda na kujaa kwa matiti ni miongoni mwa dalili za ujauzito lakini pia ni dalili za kukaribia hedhi kwa baadhi ya wanawake. Posti hii itakwenda kufafanuabutofauti wa dalili hizi na kipi ni sahihibkatibya hedhi ama ujauzito.
Soma Zaidi...Nitakujiza dawa ya chango na maumivu ya tumbo lahedhi, dalili zake na njia za kukabiliana na maumivu ya tumbo la chango.
Soma Zaidi...Uchungu wa uzazi hutokana na kubana nakuachia kwa misuli hii husababishwa kufunhuka kwa mlango wa tumbo la uzazi pamoja na shingo ya kizazi na kumuongezea mama uchungu wakati wa kujifungua(during labour) Pia kubana na kuachia huanza polepole wakati wa
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...