Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.
Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo
Dalili na ishara za saratani ya utumbo mdogo ni pamoja na:
1. Maumivu ya tumbo
2. Ngozi kuwa na manjano na weupe wa macho (jaundice)
3. Kuhisi udhaifu au uchovu usio wa kawaida
4. Kichefuchefu
5. Kutapika
6. Kupungua uzito
7. Damu kwenye kinyesi, ambayo inaweza kuonekana nyekundu au nyeusi
8. Kuhara kwa maji
Jinsi ya kujizuia na ugonjwa wa Saratani ya utumbo mdogo.
1. Kula aina mbalimbali za matunda, mboga mboga na nafaka. Matunda, mboga mboga na nafaka nzima zina vitamini, madini, nyuzinyuzi ambayo inaweza kusaidia kupunguza hatari ya saratani na magonjwa mengine.
2. Punguza kunywa pombe kupita kuasi ikiwezekana acha kabisa. Ukichagua kunywa pombe, punguza kiwango cha pombe unachokunywa kisizidi kinywaji kimoja kwa siku .
3. Acha kuvuta sigara. Tafuta njia mbadala ambazo zitakutengenezea mazingira ya kuacha kabisa kuvuta sigara au kutumia tumbaku.
4. Fanya mazoezi . Jaribu kupata angalau dakika 30 za mazoezi.
5. Punguza uzito wako kama ni mkubwa kulingana na afya yako. Ikiwa una uzito mzuri, fanya kazi ili kudumisha uzito wako kwa kuchanganya chakula cha afya na mazoezi ya kila siku.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 web hosting ๐2 Madrasa kiganjani ๐3 Kitau cha Fiqh ๐4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) ๐5 Bongolite - Game zone - Play free game ๐6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Dondoo muhimu ya ki afya.
Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu ya ki afya, ni maelekezo ambayo utolewa ili kuweza kuzifanya afya zetu ziwe bora zaidi na kuepuka madhara yoyote ya ki afya
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu magonjwa yasiyoambukizwa
Post hii inahusu magonjwa yasiyo ya kuambukizwa,haya ni magonjwa ambayo hayawezi kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda mwingine
Soma Zaidi...Maumivu Wakati wa Hedhi: Sababu na Suluhisho
Post hii inachunguza hali ya maumivu wakati wa hedhi (dysmenorrhea), ikigusia sababu za kibaolojia zinazosababisha maumivu haya, dalili za kawaida, na mbinu mbalimbali za nyumbani na kitiba za kupunguza usumbufu huo ili kuboresha hali ya maisha ya mwanamke.
Soma Zaidi...Chanzo cha kiungulia
Post hii inahusu zaidi vyanzo vya kuwepo kwa kiungulia, kiungulia ni kitendo cha kupanda kwa gesi kutoka kwenye tumbo mpaka kwenye mdomo,hali uwasumbua wengi na kusababisha hali isiyo rafiki.
Soma Zaidi...Kwa nini kungโatwa na mbu hakuambukizi UKIMWI?
Ingawa mbu hunyonya damu kwa binadamu, hawana uwezo wa kueneza virusi vya UKIMWI (VVU). Sababu ni kwamba virusi vya VVU haviwezi kuishi wala kuzaliana ndani ya mwili wa mbu, na pia mbu hawaingizi damu ya mtu mmoja kwa mwingine wanapongโata.
Soma Zaidi...Dalili za kisukari na njia za kuzuia kisukari
Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisakari, dalili zake,na namna ya kujikinga usipate kisukari au Kama tayari unakisukari ukijikinga madhara yanapungua au kupona kabisa.Kisukari au bolisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwa
Soma Zaidi...