picha

Tahadhari za ugonjwa wa UTI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu tahadhari za kuchukua ili kujikinga na UTI

Mtu anaweza kuchukuwa tahadhari dhidi ya ugonjwa huu kwa,;-

1.Jisafishe kutokea mbele kuelekea nyuma baada ya kukidhi haja kubwa (kwa wanawake). Hii husaidia kuzuia bakteria wanaotoka kwenye utumbo mkubwa wasipate nafasi ya kuingia kwenye njia ya haja ndogo.

2.mwaga maji kila uingiapo chooni kwaajili ya nkujisaidia. Kitendo hiki kitaondosha vijidudu vilivyopo pale chini.

3.Jisafishe sehemu za siri kabla ya kuingiliana na baada.

4.Hakikisha unakwenda kutoa haja ndogo (kukojoa) baada ya tendo la ndoa. Kitendo hiki kitasaidia kuondosha vijidudu vilivyoingia wakati wa tendo.

5.Nenda katoe haja ndogo haraka sana baada ya kuhisi.

6.Kunywa maji mengi zaidi. Husaidia kuondowa vijidudu kwa njia ya mkojo.

7.Vaa nguo za ndani za pamba, kavu na zisizobana.nguo za mpira na zinazobana husababisha jasho (majimaji) sehemu za siri. Majimaji haya husaidia bakteria kukuwa na kuishi hivyo wanaweza kuathiri njia ya mkojo.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2150

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 ai web app     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Mimba Changa Hukaa Wiki Ngapi? Fahamu Kipindi Hiki Muhimu

​Neno "mimba changa" hutumiwa sana katika mazungumzo ya kila siku, lakini kitaalamu linawakilisha miezi mitatu ya kwanza ya ujauzito, inayojulikana kama Trimester ya Kwanza. Makala haya yanajadili umri kamili wa mimba changa kwa wiki, mabadiliko makuu yanayotokea kwa mama na kiumbe, ishara za hatari za kuchunguza, na ukweli wa kisayansi dhidi ya dhana potofu kuhusu kipindi hiki.

Soma Zaidi...
Mbinu za kuzuia na kuepukana na maradhi ya uti wa mgongo

Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepukana na tatizo la ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.

Soma Zaidi...
Msaada kwa aliye na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Posti hii inahusu zaidi msaada kwa aliye na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni huduma maalumu ambayo utolewa kwa mtu ambaye ana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo. Zifuatazo ni huduma maalumu kwa mwenye uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Saratani ya ini.

Saratani ya ini ni Saratani inayoanzia kwenye seli za ini lako.

Soma Zaidi...
DALILI ZA SELIMUDU

Posti hii inazungumzia ishara na dalili za SELIMUDU ambao kitaalamu huitwa Sickle cell Anemia.selimudu ni aina ya kurithi ya Anemia — hali ambayo hakuna chembechembe nyekundu za damu zenye afya za kutosha kubeba oksijeni ya kutos

Soma Zaidi...
Bipolar disorders

Bipolar disorder ni hali ya afya ya akili inayohusisha mabadiliko makubwa katika hisia, nishati, na shughuli za kila siku za mtu. Dalili za bipolar disorder zinaweza kuwa kwenye kipindi cha mania na kipindi cha unyogovu, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa bipolar.

Soma Zaidi...