Tahadhari za ugonjwa wa UTI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu tahadhari za kuchukua ili kujikinga na UTI
Mtu anaweza kuchukuwa tahadhari dhidi ya ugonjwa huu kwa,;-
1.Jisafishe kutokea mbele kuelekea nyuma baada ya kukidhi haja kubwa (kwa wanawake). Hii husaidia kuzuia bakteria wanaotoka kwenye utumbo mkubwa wasipate nafasi ya kuingia kwenye njia ya haja ndogo.
2.mwaga maji kila uingiapo chooni kwaajili ya nkujisaidia. Kitendo hiki kitaondosha vijidudu vilivyopo pale chini.
3.Jisafishe sehemu za siri kabla ya kuingiliana na baada.
4.Hakikisha unakwenda kutoa haja ndogo (kukojoa) baada ya tendo la ndoa. Kitendo hiki kitasaidia kuondosha vijidudu vilivyoingia wakati wa tendo.
5.Nenda katoe haja ndogo haraka sana baada ya kuhisi.
6.Kunywa maji mengi zaidi. Husaidia kuondowa vijidudu kwa njia ya mkojo.
7.Vaa nguo za ndani za pamba, kavu na zisizobana.nguo za mpira na zinazobana husababisha jasho (majimaji) sehemu za siri. Majimaji haya husaidia bakteria kukuwa na kuishi hivyo wanaweza kuathiri njia ya mkojo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 web hosting 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 ai web app 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Matatizo yanayosababisha mshtuko wa moyo.
Mshtuko wa moyo hutokea wakati mtiririko wa damu kwa moyo umezuiwa, mara nyingi kwa mkusanyiko wa mafuta, cholesterol na vitu vingine, ambayo huunda plaque katika mishipa inayolisha moyo (mishipa ya moyo). Mtiririko wa damu ulioingiliwa unaweza kuharibu
Soma Zaidi...Ugonjwa wa mfumo wa kinga ya mwili inavyoshambulia ini.
Ugonjwa huu hupelekea kuvimba kwenye ini yako ambayo hutokea wakati mfumo wa kinga ya mwili wako unaposhambulia ini lako.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kiseyeye na dalili zake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa kiseyeye na dalili zake
Soma Zaidi...VIPIMO VYA MINYOO (UTAJUAJE KAMA UNA MINYOO)? fecal test, blood test, colonoscopy tape test X-ray, MRI na CT scan.
VIPIMO VYA MINYOO Haitoshelezi kuwa na dalili pekee ukathibitisha kuwa una minyoo.
Soma Zaidi...Viungo vinavyoathiriwa na malaria
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya viungo vinavyoathiriwa na ugonjwa wa malaria
Soma Zaidi...Sababu za Kupungua kwa Hamu ya Mapenzi
Makala hii inachunguza kwa kina sababu zinazosababisha kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa (Low Libido). Tutaangalia vipengele vya kimwili, kisaikolojia, na mtindo wa maisha vinavyoweza kuathiri hali hii, pamoja na ukweli wa kisayansi kuhusu tatizo hili na hatua za kuchukua ili kuboresha afya ya mahusiano.
Soma Zaidi...