Tahadhari za ugonjwa wa UTI

Tahadhari za ugonjwa wa UTI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu tahadhari za kuchukua ili kujikinga na UTI

Mtu anaweza kuchukuwa tahadhari dhidi ya ugonjwa huu kwa,;-

1.Jisafishe kutokea mbele kuelekea nyuma baada ya kukidhi haja kubwa (kwa wanawake). Hii husaidia kuzuia bakteria wanaotoka kwenye utumbo mkubwa wasipate nafasi ya kuingia kwenye njia ya haja ndogo.

2.mwaga maji kila uingiapo chooni kwaajili ya nkujisaidia. Kitendo hiki kitaondosha vijidudu vilivyopo pale chini.

3.Jisafishe sehemu za siri kabla ya kuingiliana na baada.

4.Hakikisha unakwenda kutoa haja ndogo (kukojoa) baada ya tendo la ndoa. Kitendo hiki kitasaidia kuondosha vijidudu vilivyoingia wakati wa tendo.

5.Nenda katoe haja ndogo haraka sana baada ya kuhisi.

6.Kunywa maji mengi zaidi. Husaidia kuondowa vijidudu kwa njia ya mkojo.

7.Vaa nguo za ndani za pamba, kavu na zisizobana.nguo za mpira na zinazobana husababisha jasho (majimaji) sehemu za siri. Majimaji haya husaidia bakteria kukuwa na kuishi hivyo wanaweza kuathiri njia ya mkojo.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views: 2325

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Tofauti kati ya homa ya mapafu (Nimonia) na mafua makali.

​Mara nyingi watu huchanganya Nimonia (Pneumonia) na mafua makali kwa sababu yote huathiri mfumo wa upumuaji. Hata hivyo, haya ni magonjwa tofauti kimsingi: mafua husababishwa na virusi na huathiri njia ya juu ya hewa (pua, koo), wakati Nimonia ni maambukizi ya viini (bakteria, virusi, au fangasi) yanayoshambulia mifuko ya hewa ndani ya mapafu (alveoli). Makala hii inaelezea tofauti za kifizikia na umuhimu wa kupata matibabu sahihi.

Soma Zaidi...
Tofauti ya dalili za mafua ya kawaida na COVID-19.

​Katika ulimwengu wa sasa, kuelewa tofauti kati ya mafua ya kawaida (common cold) na COVID-19 ni muhimu kwa ajili ya usalama wako na wa jamii inayokuzunguka. Ingawa magonjwa yote mawili husababishwa na virusi na kushambulia mfumo wa upumuaji, yana tofauti muhimu katika jinsi yanavyoanza, muda wake, na dalili zake mahususi. Makala haya yanakupa mwongozo wa kulinganisha dalili ili uweze kuchukua hatua sahihi za kiafya.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Saratani ya ini.

Saratani ya ini ni Saratani inayoanzia kwenye seli za ini lako.

Soma Zaidi...
dalili za mimba changa ndani ya wiki moja

Je na wewe ni katika ambao wanahitaji kujuwa dalili za mimba ndani ya wiki moja? kama ndio makala hii ni kwa ajili yako. Utakwenda kuona dalili za mwanzo sana za ujauzito toka siku za mwanzoni.

Soma Zaidi...
Sababu za ugonjwa wa mkojo kuwa na damu

Posti hii inaelezea sababu zinazosababisha mkojo kuwa na damu.

Soma Zaidi...
Sababu za kutokea kwa maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kutokea kwa maumivu ya jino

Soma Zaidi...