Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
3.KISUKARI (DIABETES)
Mwili unahitaji nguvu na uwezo wa kufanya kazi, nguvu hii husababishwa na glucose iliyopo ndani ya mwili. glucose ni aina ya sukari ambayo hupatikana kwenye vyakula vya wanga. Mwili hauwezi kutumia glucose bila ya insulin. Insulin ni homoni ambayo inatengenezwa kwenye kongosho. Hii inakazi ya kudhibiti kiwango cha glucose ndani ya mwili. Yaani wakati kwenye damu kukiwa na glucose nyingi insulini huletwa ili kuipunguza na ikiwa ni kidogo insulin hailetwi.
Ikitokea mwili hauna uwezo wa kuzalisha insulini ya kutosheleza mwilini au seli zinashindwa kutumia insulini inayozalishwa hapa kisukari hutokea. Yaani mwili utashindwa kudhibiti kiwango cha glucose. Katika hali hii seli zitashindwa kupata glucose hivyo kusababisha damu kuwa na glucose nyingi na hivyo figo hutowa maji mengi na kusababisha kukojoa mara kwa mara. Katika hali hii tumesema kuwa glucose ni aina ya sukari ambayo inahitajika kwa ajili ya kupata nguvu na uwezo wa kufanya kazi (energy) hivyo mwili utatumia fat na protin kujitengenezea energy hivyo kupelekea kuzalisha sumu ndani ya mwli. Na hali hii ikiendelea mtu aanweza kupoteza fahamu na hali hii huitwa diabetic coma.
AINA ZA KISUKARI
1.Type 1 Diabetes; aina hii huotokea wakati mfumo wa kinga mwilini (immune system) unaposhambulia seli zinazozalisha insulin katika kingosho. Seli hizi zinaposhambuliwa mwili utashindwa kuzalisha insulin. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa aina hii ya kisukari husababishwa na virusi pamoja na kurithi kutoka kwa wazazi.
Aina hii ya kisukari pia huitwa insulin-dependent au juvenile diabees. Hii hutibiwa kwa kutumia dawa na mara nyingi huweza kuonekana kabla ya miaka 18. Dalili za aina hii ni za hatari sana na hutokea kwa ghafla. Miongoni mwazo ni kiu kikali, kuchoka sana na kupunguwa uzito.
2.Type 2 Diabetes; pia aina hii huitwa noninsulin-dependent diabetes na mara nyingi huwapata watu wenye umri wa kuanzia miaka 40 na wale watu ambao wana uzito wa kuzidi.
Katika aina hii ya kisukari mwili unazalisha insulin lakini seli zinashindwa kuitumia insulin inayozaliwa. Miongoni mwa dalili zake ni kukojoakojoa, kiu kikali, kutokuona kwa ufasaha, kuchelewa kupona kwa majeraha na maambukizi ya mara kwa mara.
3.Gestation Diabetes; hii huwatokea sana wajawazito mwishoni mwa mimba na hupotea baada ya mtoto kuzaliwa. Hii huweza kuongeza hatari wakati wa kijifungua na kama mama amerithi kisukari kutoka kwa wazazi hali inaweza kuwa mbaya zaid. Dalili zake ni sawa na zile za hizo aina mbili hapo juu,
KUPAMBANA NA KISUKARI
A)hakikisha una uzito wa kawaida
B)Wacha kutumia bidhaa za tumbaku
C)Punguza misongo ya mawazo
D)Fanya mazoezi ya mara kwa mara
E)Kula mlo kamili
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inaelezea namna na jinsi ya kujikinga au kuzuia Ugonjwa wa ini.
Soma Zaidi...Ugonjwa huu hupelekea kuvimba kwenye ini yako ambayo hutokea wakati mfumo wa kinga ya mwili wako unaposhambulia ini lako.
Soma Zaidi...Kaswende ni maambukizi ya bakteria kawaida huenezwa kwa kujamiiana pia ugonjwa huu hujulikana kama syphilis. Ugonjwa huu huanza kama kidonda kisicho na maumivu kwa kawaida kwenye sehemu zako za siri, rektamu au mdomo
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa vericose veini
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za michubuko,kwa Sababu michubuko utokea sehemu tofauti tofauti na pia Kuna aina mbalimbali kama tutakavyoona hapo mbeleni.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi maumivu ya kiuno na dalili zake, ni maumivu ambayo utokea kwenye kiuno na kusababisha madhara mbalimbali katika mwili,
Soma Zaidi...Hapa nitakueleza namna ambavyounaweza kupunguza hatari ya kupata maradhi ya ini. Kwa njia hizi unaweza kujikina wewe na wengineo na maradhi haya hatari ya ini.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ya kushindwa kupitisha mkojo, ni madhara makubwa yanayotokea kwa mtu iwapo akishindwa kupitisha mkojo.
Soma Zaidi...Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi utaziomna hapa. hizi zinaweza kuwa ndio za kwanza kwa ambaye hajapima HIV
Soma Zaidi...