Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
3.KISUKARI (DIABETES)
Mwili unahitaji nguvu na uwezo wa kufanya kazi, nguvu hii husababishwa na glucose iliyopo ndani ya mwili. glucose ni aina ya sukari ambayo hupatikana kwenye vyakula vya wanga. Mwili hauwezi kutumia glucose bila ya insulin. Insulin ni homoni ambayo inatengenezwa kwenye kongosho. Hii inakazi ya kudhibiti kiwango cha glucose ndani ya mwili. Yaani wakati kwenye damu kukiwa na glucose nyingi insulini huletwa ili kuipunguza na ikiwa ni kidogo insulin hailetwi.
Ikitokea mwili hauna uwezo wa kuzalisha insulini ya kutosheleza mwilini au seli zinashindwa kutumia insulini inayozalishwa hapa kisukari hutokea. Yaani mwili utashindwa kudhibiti kiwango cha glucose. Katika hali hii seli zitashindwa kupata glucose hivyo kusababisha damu kuwa na glucose nyingi na hivyo figo hutowa maji mengi na kusababisha kukojoa mara kwa mara. Katika hali hii tumesema kuwa glucose ni aina ya sukari ambayo inahitajika kwa ajili ya kupata nguvu na uwezo wa kufanya kazi (energy) hivyo mwili utatumia fat na protin kujitengenezea energy hivyo kupelekea kuzalisha sumu ndani ya mwli. Na hali hii ikiendelea mtu aanweza kupoteza fahamu na hali hii huitwa diabetic coma.
AINA ZA KISUKARI
1.Type 1 Diabetes; aina hii huotokea wakati mfumo wa kinga mwilini (immune system) unaposhambulia seli zinazozalisha insulin katika kingosho. Seli hizi zinaposhambuliwa mwili utashindwa kuzalisha insulin. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa aina hii ya kisukari husababishwa na virusi pamoja na kurithi kutoka kwa wazazi.
Aina hii ya kisukari pia huitwa insulin-dependent au juvenile diabees. Hii hutibiwa kwa kutumia dawa na mara nyingi huweza kuonekana kabla ya miaka 18. Dalili za aina hii ni za hatari sana na hutokea kwa ghafla. Miongoni mwazo ni kiu kikali, kuchoka sana na kupunguwa uzito.
2.Type 2 Diabetes; pia aina hii huitwa noninsulin-dependent diabetes na mara nyingi huwapata watu wenye umri wa kuanzia miaka 40 na wale watu ambao wana uzito wa kuzidi.
Katika aina hii ya kisukari mwili unazalisha insulin lakini seli zinashindwa kuitumia insulin inayozaliwa. Miongoni mwa dalili zake ni kukojoakojoa, kiu kikali, kutokuona kwa ufasaha, kuchelewa kupona kwa majeraha na maambukizi ya mara kwa mara.
3.Gestation Diabetes; hii huwatokea sana wajawazito mwishoni mwa mimba na hupotea baada ya mtoto kuzaliwa. Hii huweza kuongeza hatari wakati wa kijifungua na kama mama amerithi kisukari kutoka kwa wazazi hali inaweza kuwa mbaya zaid. Dalili zake ni sawa na zile za hizo aina mbili hapo juu,
KUPAMBANA NA KISUKARI
A)hakikisha una uzito wa kawaida
B)Wacha kutumia bidhaa za tumbaku
C)Punguza misongo ya mawazo
D)Fanya mazoezi ya mara kwa mara
E)Kula mlo kamili
Umeionaje Makala hii.. ?
Ni ngumu kujuwa vidonda vya tumbo uhakika wake bila ya kupata vipimo. Unajuwa ni kwa nini, ni kwa sababu maumivu ya tumbo ni dalili ya shida nyingi za kiafya kama ujauzito, mimba, typhod, na shida kwenye unfumo wa chakula.
Soma Zaidi...Psti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa Maambukizi ya tezi za mate ambao hujulikana Kama MABUSHA (mumps) ni maambukizi ya virusi ambayo kimsingi huathiri tezi mojawapo ya jozi tatu za tezi za mate zinazotoa mate, zilizo chini na mbele ya masikio
Soma Zaidi...Hepatitis B Ni maambukizi ya ini ambayo yamekuwa sugu kuanzia mwezi na kuendelea.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa pumu ni ugonjwa unaoshambulia mfumo wa hewa ambapo mgonjwa hushindwa kupumua vizuri na hupelekea matatizo ya kudumu kama haujatibiwa mapema.
Soma Zaidi...Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji.
Soma Zaidi...Karibia fangasi wote hawa wanatibika bila ya ugumu wowote maka mgonjwa atakamilisha dozi.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo yanayoweza kusababishwa mgongo wAko au kiuno kwa na maumivu, Mgongo ukiwa na maumivu makali Sana yanaweza kusababishwa shida kubwa ata utakapokaa au ukilala au ukitumia bado maumivu yanakuwepo.
Soma Zaidi...Tonsillitis kwa kiswahili hujulikana kama mafundomafundo ambayo hutokea pande mbili karibu na Koo na huwa na uvimbe na zikikaa kwa muda bila matibabu hutoa usaha.Dalili na dalili za ugonjwa wa tonsillitis ni pamoja na
Soma Zaidi...Je unasumbuliwa na maumivuvya tumbo chini ya kitovu upande wa kushito. Post hii itakuletea sababu za maukivubhayo na nini ufanye.
Soma Zaidi...