Dalili za saratani (cancer)
Posti hii inahusu zaidi dalili za kansa, ni dalili ambazo utokea kwa mtu Mwenye tatizo la ugonjwa wa Kansa ingawa sio lazima dalili hizi kutokea tukadhani kuwa ni Kansa Ila zilizonyingi huwa ni kweli dalili za kansa.
Dalili za kansa
1.Mabadiliko ya sauti na kikohozi
Mabadiliko ya sauti na kikohozi ni dalili mojawapo ya Kansa ya koo, pengine sauti ugoma kutoka ambayo uandamana na kikohozi Cha mara kwa mara na pengine chakula ushindwa kupitia kwenye Koo.
2.Matatizo ya kutopata choo kwa mda mrefu. Matatizo ya kutopata choo huwa ni mojawapo ya dalili za kansa ya utumbo mkubwa, au pengine choo huwa na damu hali ambayo upelekea choo,kuwa kigumu sana na pengine choo klainika kusiko kwa kawaida ambapo ni viashilia vya Kansa.
3.Mabadiliko kwenye haja ndogo.
Dalili mojawapo ya Kansa ya kibofu Cha mkojo ni pale ambapo mtu uanza kukojoa damu na pengine uchafu kutoka kwenye kibofu Cha mkojo ukiwa na rangi ya njano, hii ni mojawapo ya Kansa ya kibofu Cha mkojo.
4.Maumivu ya mda mrefu kwenye sehemu yoyote kwa mfano maumivu ya kichwa, miguu na sehemu nyingine nyingi ambapo hata ikitumiwa dawa maumivu hayo upoa na kwa mda fulani uanza tena kwa ujumla maumivu ambayo haya sikii dawa na dalili ya ugonjwa wa kwanza
5.Mabadiliko ya uvimbe
Pengine Kuna uvimbe utokea na kupotea na huwa inauma au pengine hauumi, na baadae utokea sehemu mbalimbali kwa mtindo tofauti na kwa mda tofauti,hizi ni dalili za kansa.na ikitokea ukaguswa kwa kupasuliwa ndipo dalili uongezeka zaidi.
6.Kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi na kutokwa damu kwa wale wanawake ambao walishamaliza kipindi Chao Cha hedhi, hii uonesha kuwa na dalili za kansa kwenye kizazi na pengine siku za hedhi ubadilika badilika kuliko kawaida.
7.Kupungua kwa uzito kupitia kiasi
Dalili nyingine ya Kansa ni kupungua uzito kuliko kawaida,hii utokea hasa wakati wa dalili za mwanzoni ambapo uzito wa mgonjwa unapungua hata kama abatumia chakula Cha Aina gani.
Dalili hizo ni za kansa lakini Kuna pangine mtu anaweza kupata dalili kama hizi lakini sio Kansa, Ila kwa uhakika zaidi tunapaswa kwenda hospitalini kuangalia afya zetu zaidi, kwa hiyo sio kila mwenye Dalili za hapo juu ana Kansa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 kitabu cha Simulizi π2 ai web app π3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π4 Kitau cha Fiqh π5 Bongolite - Game zone - Play free game π6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Njia ambazo VVU huambukizwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo VVU huambukizwa
Soma Zaidi...Sababu za homa kwa watoto wachanga
Muhtasari (Executive Summary) βHoma kwa mtoto mchanga si ugonjwa wenyewe, bali ni ishara kwamba mfumo wa kinga ya mwili unapambana na kitu kigeni. Ingawa homa inaweza kuwatia hofu wazazi wengi, mara nyingi husababishwa na maambukizi ya virusi, bakteria, mabadiliko ya mwili kama kuota meno, au matokeo ya kawaida ya chanjo. Makala haya yanachambua sababu hizi kwa kina na kutoa mwongozo wa lini unapaswa kukimbilia hospitali haraka.
Soma Zaidi...Dalili za jeraha kali kwenye ubongo
Posti hii inahusu zaidi dalili za jeraha kali kwenye ubongo, ni majeraha ambayo utokea kwenye ubongo pale ambapo mtu anapata ajali au amepigwa na kitu chochote kigumu kichwni, zifuatazo ni dalili za jeraha kali kwenye ubongo
Soma Zaidi...Homa ya ini Nini Nini, na husababishwa na nini
Katika post hii utajifunza maana ya homa ya ini. Pia utajifunza chanzo kinachosababisha homa ya ini. Makala hii itakuwa endelevu hivyo usikose muendelezo wake.
Soma Zaidi...Kucha langu LA mguu linang'ooka...nini chaweza kuwa tatizo
Je na wewe unasumbukiwa na kunggoka jwa kucha. Tatizo limekunaza una muda gani nalo?
Soma Zaidi...Dalili za Minyoo kwa Watoto
βMinyoo ni tatizo la kawaida kwa watoto ambalo linaweza kuathiri ukuaji na afya zao kwa ujumla. Makala haya yataeleza dalili za kawaida za maambukizi ya minyoo, ukweli muhimu kuhusu tiba yake, na umuhimu wa usafi katika kuzuia tatizo hili.
Soma Zaidi...