Dalili za kisukari na njia za kuzuia kisukari
Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisakari, dalili zake,na namna ya kujikinga usipate kisukari au Kama tayari unakisukari ukijikinga madhara yanapungua au kupona kabisa.Kisukari au bolisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwa
Kisukari au bolisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwango vikubwa vya glukosi katika damu. Sababu yake ni uhaba wa homoni ya insulini mwilini au upungufu wa uwezo wa mwili wa kukubali insulini.
Kisukari au bolisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwango vikubwa vya glukosi katika damu. Sababu yake ni uhaba wa homoni ya insulini mwilini au upungufu wa uwezo wa mwili wa kukubali insulini.
Dalili za kawaida ni pamoja na:
- Kuhisi kiu sana
- Kukojoa zaidi ya kawaida, hasa usiku
- Kujisikia kuchoka sana
- Kupunguza uzito bila kujaribu
- Thrush ambayo inaendelea kurudi
- Uoni hafifu
- Vidonda ambavyo havitibiki
Watu walio katika hatari zaidi ya aina ya 2 ni zaidi ya umri wa miaka 40 (au 25 kwa watu wa kusini mwa Asia); wenye mzazi au ndugu mwenye kisukari; wenye uzito mkubwa; na wana asili ya Asia Kusini, Wachina, Caribbean au Wenye asili ya Afrika.
Namna ya kujizuia na kisukari.
Ugonjwa wa kisukari hutegemea maumbile na mazingira lakini unaweza kusaidia kuweka viwango vya sukari kwenye damu yako kwa lishe bora na mtindo wa mzuri wa maisha
1.Lishe nzuri yenye afya ni pamoja na mboga mboga, matunda, maharage na nafaka nzima. Pia inajumuisha mafuta yenye afya, karanga na samaki . Ni muhimu kula mara kwa mara na kuacha kula wakati umeshiba.
2.Mazoezi ya mwili pia yanaweza kusaidia kupunguza viwango vyako vya sukari kwenye damu. Ni muhimu kufanya mazoezi angalau kwa masaa 2 na nusu kila wiki
3.Uzito wenye afya utarahisisha mwili wako kupunguza kiwango cha sukari kwenye damu.
4.Ni muhimu pia kutovuta sigara
Mwisho; kisukari Ni ugonjwa ambao isipopata tiba au kuzingatia vitu vya kufanya mtu anaweza kufa basi Ni vizuri Kama mtu akiona dalili za hivyi awahi kwenye kituo Cha afya apate matibabu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitabu cha Afya π2 Simulizi za Hadithi Audio π3 Bongolite - Game zone - Play free game π4 web hosting π5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Dalili za madhara ya figo
Posti hii inahusu dalili za figo.figo husawazisha maji mwilini pamoja na kuchuja mkojo.
Soma Zaidi...Nini husababisha maumivu ya tumbo chini ya kitomvu kwa wanawake na wanaumr?
Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu. Ni katika maumivu amaboyo kwa wanaume mara nyingi huhusishwa an ngiri na kwa upande wa wanawake huhusishwa na chango hasa pale wanapokaribia kuingia katika siku zao. Ma
Soma Zaidi...Akili kuchoka na kushindwa kufanya maamuzi (Decision fatigue).
βMuhtasari βKatika maisha ya kisasa yenye changamoto nyingi, kila siku tunafanya maelfu ya maamuzi, kuanzia yale madogo kama "nivae nini?" hadi makubwa ya kikazi na kifamilia. Hali hii ya kufanya maamuzi mengi mfululizo husababisha hali inayofahamika kama Decision Fatigue (uchovu wa maamuzi). Makala hii inachambua kisaikolojia jinsi hali hii inavyoathiri tija yako, afya ya akili, na inatoa mbinu za kisayansi za kupunguza athari zake ili uweze kufanya maamuzi bora kila siku.
Soma Zaidi...Madhara ya kula vyakula vya kukaanga mara kwa mara.
Chipsi, kuku wa kukaanga, mandazi, na sambusa ni vyakula vinavyopendwa na wengi kutokana na ladha yake na urahisi wa kupatikana. Hata hivyo, kukaanga chakula kwa mafuta mengi (deep-frying) hubadilisha muundo wa kemikali wa chakula hicho, na kukifanya kiwe na kalori nyingi sana, mafuta hatari, na kemikali zinazoweza kudhuru mwili wako kwa muda mrefu. Makala haya yanakupa mwongozo wa kwa nini unapaswa kupunguza tabia hii.
Soma Zaidi...Ni nini husababisha mate kujaa mdomoni, na ni yapi matibabu yake
Hapa tutaangalia baadhi ya sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate na namna ya kutibu tatizo la kujaa kwa mate mdomoni
Soma Zaidi...