picha

Dalili na ishara za shambulio la moyo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili na ishara za shambulio la moyo. Shambulio la moyo huzuia damu yenye oksijeni kufika kwenye moyo hivyo hupelekea tishu kufa. Na Ugonjwa huu mtu akicheleweshewa matibabu huweza kupata mshtuko wa moyo mpaka kifo.

DALILI 

Daliliza na ishara za kawaida za Shambulio la Moyo ni pamoja na:

1. Shinikizo, kujaa au maumivu ya kufinya katikati ya kifua ambayo hudumu kwa zaidi ya dakika chache

2. Maumivu yanayoenea zaidi ya kifua chako hadi kwenye bega lako, mkono, mgongo, au hata kwenye meno na taya yako

3. Kuongezeka kwa vipindi vya Maumivu ya Kifua

4. Maumivu ya muda mrefu kwenye tumbo la juu

5 Upungufu wa pumzi

6. Kutokwa na jasho kwa wingi sana

7. Kuzimia na kupoteza fahamu.

8. Kichefuchefu na kutapika.

9.kuhisi mapigo ya moyo yanaenda haraka.

10.maumivu ya kichwa.

11.maumivu ya kifua

 

Namna ya Kuzuia

Hatua za kujikinga na  kuzuia shambulizi la moyo

1.Kuacha kuvuta sigara

2.Kufanya mazoezi ya mara kwa mara

3.Kupunguza unywaji wa pombe

4.Kubadilisha aina ya mlo. Kupunguza mafuta katika mlo na chumvi.

5.Kutumia mafuta ya samaki (omega-3 fatty acids)

6.Kuna utafiti unaosema kuwa uchangiaji damu hupunguza hatari ya magonjwa ya moyo hasa kwa wanaume.

 

Mambo ya hatari

Madhara ya shambulizi la moyo Ni Kama Yafuatayo

1.Moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)

2.Matatizo katika mfumo wa mapigo ya moyo ambayo hatimaye hupelekea kifo

3.Shambulizi la moyo kurudia mara ya pili

4.Kifo cha ghafla.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2686

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Kupoteza nywele kwa wingi (Hair loss): Sababu na tiba.

​Kupoteza nywele ni jambo linaloweza kuathiri hali ya kujiamini ya mtu yeyote. Ingawa ni kawaida kupoteza nywele 50 hadi 100 kila siku, kupoteza nywele kwa wingi kiasi cha kuacha sehemu wazi kichwani ni ishara kuwa kuna kitu hakiko sawa. Makala haya yanakusaidia kuelewa sababu zinazochochea hali hii na namna unavyoweza kurejesha afya ya nywele zako.

Soma Zaidi...
Dawa za kutibu fangasi sugu za ukeni (Vaginal Candidiasis).

Fangasi wa ukeni (Vaginal Candidiasis) husababishwa na kuzaliana kupita kiasi kwa fangasi aina ya Candida. Ingawa mara nyingi hutibika kwa dozi moja, baadhi ya wanawake hukumbwa na fangasi sugu (recurrent candidiasis)β€”hali inayojitokeza mara nne au zaidi kwa mwaka. Hii si hali ya kawaida na inahitaji mbinu madhubuti za kitabibu badala ya kutegemea dawa za dukani pekee. Makala haya yanakupa mwongozo wa tiba na hatua za kudumu za kuondoa kero hii.

Soma Zaidi...
Matibabu ya vidonda vya kinywa (Canker sores) na nini cha kula.

Vidonda vya kinywa, vinavyojulikana kitaalamu kama aphthous ulcers au canker sores, ni changamoto ya kawaida inayoweza kusababisha maumivu makali na usumbufu wakati wa kula au kuzungumza. Blogu hii inatoa mwongozo wa kina kuhusu mbinu bora za matibabu, vyakula vya kuepuka ili kupunguza maumivu, na vyakula bora vya kuimarisha kinga ili kusaidia uponyaji wa

Soma Zaidi...
Madhara ya maumivu kwenye nyonga na kiuno.

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa matibabu kwenye nyonga na kiuno hayatafanyika.

Soma Zaidi...
Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.

Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo

Soma Zaidi...
Ninashida Kuna mtu anaumwa pressure Kila anap pima Iko juu il mwil aumuumi at kidg n dawa anatumia unawez kunisaidiaj

Kama unasumbuliwa na presha post hii ni kwa ajili yako. Hapa tutakuoatia ushauri kutokana na swali alilouliza mdau wetu.

Soma Zaidi...