Dalili na ishara za shambulio la moyo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili na ishara za shambulio la moyo. Shambulio la moyo huzuia damu yenye oksijeni kufika kwenye moyo hivyo hupelekea tishu kufa. Na Ugonjwa huu mtu akicheleweshewa matibabu huweza kupata mshtuko wa moyo mpaka kifo.
DALILI
1. Shinikizo, kujaa au maumivu ya kufinya katikati ya kifua ambayo hudumu kwa zaidi ya dakika chache
2. Maumivu yanayoenea zaidi ya kifua chako hadi kwenye bega lako, mkono, mgongo, au hata kwenye meno na taya yako
3. Kuongezeka kwa vipindi vya Maumivu ya Kifua
4. Maumivu ya muda mrefu kwenye tumbo la juu
5 Upungufu wa pumzi
6. Kutokwa na jasho kwa wingi sana
7. Kuzimia na kupoteza fahamu.
8. Kichefuchefu na kutapika.
9.kuhisi mapigo ya moyo yanaenda haraka.
10.maumivu ya kichwa.
11.maumivu ya kifua
Namna ya Kuzuia
1.Kuacha kuvuta sigara
2.Kufanya mazoezi ya mara kwa mara
3.Kupunguza unywaji wa pombe
4.Kubadilisha aina ya mlo. Kupunguza mafuta katika mlo na chumvi.
5.Kutumia mafuta ya samaki (omega-3 fatty acids)
6.Kuna utafiti unaosema kuwa uchangiaji damu hupunguza hatari ya magonjwa ya moyo hasa kwa wanaume.
Mambo ya hatari
1.Moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)
2.Matatizo katika mfumo wa mapigo ya moyo ambayo hatimaye hupelekea kifo
3.Shambulizi la moyo kurudia mara ya pili
4.Kifo cha ghafla.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Madrasa kiganjani π2 Dua za Mitume na Manabii π3 kitabu cha Simulizi π4 Simulizi za Hadithi Audio π5 ai web app π6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Njia za kugundua tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu
Post hii inahusu Zaidi njia mbali mbali ambazo uweza kitumiwa na wataalamu ili kuweza kugundua tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.
Soma Zaidi...Kushambuliwa kwa moyo na kupumua
Post hii inahusu zaidi kuhusu kushambuliwa kwa moyo na kupumua, kushambuliwa kwa moyo na kupumua kwa kitaala huitwa (cardiopulmonary Arrest) ni kitendo Cha kusimama ghafla kwa moyo na kupumua.
Soma Zaidi...Kaswende isiyotibiwa: Athari zake kwenye ubongo na moyo.
βKaswende ni ugonjwa wa zinaa (STI) unaosababishwa na bakteria Treponema pallidum. Ingawa ugonjwa huu hupona kirahisi kwa kutumia dawa za antibayotiki (kama Penicillin) katika hatua za awali, kuupuza dalili au kutokumaliza dozi husababisha bakteria kusambaa mwilini na kuathiri mifumo muhimu ya viungo. Makala hii inachunguza hatua ya tatu ya ugonjwa huu (Tertiary Syphilis) na uharibifu wa kudumu inaoweza kusababisha kwenye mfumo wa neva na moyo.
Soma Zaidi...Dalili na namna ya kujizuia na malaria
Postii hii inshusiana na dalili na ishara za kujikinga au kuzuia malaria kwa Njia mbalimbali.
Soma Zaidi...