picha

Dalili na ishara za shambulio la moyo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili na ishara za shambulio la moyo. Shambulio la moyo huzuia damu yenye oksijeni kufika kwenye moyo hivyo hupelekea tishu kufa. Na Ugonjwa huu mtu akicheleweshewa matibabu huweza kupata mshtuko wa moyo mpaka kifo.

DALILI 

Daliliza na ishara za kawaida za Shambulio la Moyo ni pamoja na:

1. Shinikizo, kujaa au maumivu ya kufinya katikati ya kifua ambayo hudumu kwa zaidi ya dakika chache

2. Maumivu yanayoenea zaidi ya kifua chako hadi kwenye bega lako, mkono, mgongo, au hata kwenye meno na taya yako

3. Kuongezeka kwa vipindi vya Maumivu ya Kifua

4. Maumivu ya muda mrefu kwenye tumbo la juu

5 Upungufu wa pumzi

6. Kutokwa na jasho kwa wingi sana

7. Kuzimia na kupoteza fahamu.

8. Kichefuchefu na kutapika.

9.kuhisi mapigo ya moyo yanaenda haraka.

10.maumivu ya kichwa.

11.maumivu ya kifua

 

Namna ya Kuzuia

Hatua za kujikinga na  kuzuia shambulizi la moyo

1.Kuacha kuvuta sigara

2.Kufanya mazoezi ya mara kwa mara

3.Kupunguza unywaji wa pombe

4.Kubadilisha aina ya mlo. Kupunguza mafuta katika mlo na chumvi.

5.Kutumia mafuta ya samaki (omega-3 fatty acids)

6.Kuna utafiti unaosema kuwa uchangiaji damu hupunguza hatari ya magonjwa ya moyo hasa kwa wanaume.

 

Mambo ya hatari

Madhara ya shambulizi la moyo Ni Kama Yafuatayo

1.Moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)

2.Matatizo katika mfumo wa mapigo ya moyo ambayo hatimaye hupelekea kifo

3.Shambulizi la moyo kurudia mara ya pili

4.Kifo cha ghafla.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2457

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 ai web app     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa UTI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI

Soma Zaidi...
Njia za kupambana na kuzuia gonorrhea

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya njia za kupambana na kuzuia gonorrhea

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo kitovuni

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya tumbo kitovuni

Soma Zaidi...
Ni bakteria gani husababisha ugonjwa wa pumu

Post hii inakwenda kujibu swali linalosema je ni bakteria aina gani husababisha igonjwa wa pumu.

Soma Zaidi...
YAJUE MARADHI YA KISUKARI

Posti hii itakwenda kuelezea mambo machache kuhusu ugonjwa wa kisukari

Soma Zaidi...
Matibabu ya vidonda vya tumbo nyumbani

Post hii inahusu zaidi matibabu ya vidonda vya tumbo nyumbani, ni njia ya kawaida ya kujitibu vidonda vya tumbo kama tulivyoona.

Soma Zaidi...