picha

Dalili na ishara za shambulio la moyo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili na ishara za shambulio la moyo. Shambulio la moyo huzuia damu yenye oksijeni kufika kwenye moyo hivyo hupelekea tishu kufa. Na Ugonjwa huu mtu akicheleweshewa matibabu huweza kupata mshtuko wa moyo mpaka kifo.

DALILI 

Daliliza na ishara za kawaida za Shambulio la Moyo ni pamoja na:

1. Shinikizo, kujaa au maumivu ya kufinya katikati ya kifua ambayo hudumu kwa zaidi ya dakika chache

2. Maumivu yanayoenea zaidi ya kifua chako hadi kwenye bega lako, mkono, mgongo, au hata kwenye meno na taya yako

3. Kuongezeka kwa vipindi vya Maumivu ya Kifua

4. Maumivu ya muda mrefu kwenye tumbo la juu

5 Upungufu wa pumzi

6. Kutokwa na jasho kwa wingi sana

7. Kuzimia na kupoteza fahamu.

8. Kichefuchefu na kutapika.

9.kuhisi mapigo ya moyo yanaenda haraka.

10.maumivu ya kichwa.

11.maumivu ya kifua

 

Namna ya Kuzuia

Hatua za kujikinga na  kuzuia shambulizi la moyo

1.Kuacha kuvuta sigara

2.Kufanya mazoezi ya mara kwa mara

3.Kupunguza unywaji wa pombe

4.Kubadilisha aina ya mlo. Kupunguza mafuta katika mlo na chumvi.

5.Kutumia mafuta ya samaki (omega-3 fatty acids)

6.Kuna utafiti unaosema kuwa uchangiaji damu hupunguza hatari ya magonjwa ya moyo hasa kwa wanaume.

 

Mambo ya hatari

Madhara ya shambulizi la moyo Ni Kama Yafuatayo

1.Moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)

2.Matatizo katika mfumo wa mapigo ya moyo ambayo hatimaye hupelekea kifo

3.Shambulizi la moyo kurudia mara ya pili

4.Kifo cha ghafla.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2581

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni

Somo hili linakwenda kukuletea sababu za maumivu ya tumbo kitovu i

Soma Zaidi...
Vyakula hatari kwa mwenye vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula hatari kwa mwenye vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa pre - eclampsia

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa pre- eclampsia ni Ugonjwa ambao uwapata wanawake wajawazito uwapata pale mimba inapofikisha umri wa wiki ishilini, utokea pale ambapo Mama mjamzito huwa na kiwango kikubwa cha shinikizo la damu na pia kuwepo kwa protini

Soma Zaidi...
DAWA MBADALA ZA VIDONDA VYA TUMBO

DAWA MBADALA ZA VIDONDA VYA TUMBO Dawa za kukabiliana na zaidi ambazo zina calcium carbonate (Tums, Rolaids), zinaweza kusaidia kutibu vidonda vya tumbo lakini hazipaswi kutumiwa kama matibabu ya msingi.

Soma Zaidi...
KAMA UNASUMBULIWA NA FANGASI

Post hii fupi inakwenda kukujuza juu ya tatizo la fangasi na nini ufanye.

Soma Zaidi...