Dalili za UKIMWI huonekana baada ya muda gani

Hapa utajifunza muda mabao dalili za VVU na UKIMWI huonekana, na kwa muda gani mgonjwa ataishi na UKIMWI bila ya kutumia ARV

Dalili za UKIMWI huonekana baada ya muda gani

Dalili za UKIMWI huonekana baada ya muda gani




VVU na UKIMWI ni mzigo mzito wa siri ambao watu wengi hawataki kutoa siri zao. Hii hupelekea kukaa muda mrefu akiwa na VVU ana UKIMWi bila hata kutumia dawa. Ni athari zipi anazipata. Hili hana haja nalo. Mwisho wa siku anafikia katika hatuwa ambao ni ngumu kurudi katika hali ya kawaida na hatimaye ni kifo.



Je unasubiliwa na mawazo kama umeathiria? Ni muda gani naweza kuishi na VVu na UKIMWI bila ya kupoteza maisha. Je ni zipi hasa dalili za kwanza kama una VVU na UKIMWI. Makala hii ni kwa ajili yako. Hapa tutakwenda kujibu maswali hayo na swali letu kuu lisemalo “ni muda gani naweza kuishi na VVU na UKIMWI bila hata ya kutumia dawa za ARVs?



Dalili za VVU na UKIMWI huweza kujitokeza katika hatuwa kuu tatu. Katika hatuwa hizo tutaendelea kuona je ni muuda gani mtu anaendelea kuishi katika hali hizo bila ya kutumia dawa za ARV?



1.Katika hatuwa ya kwanza wiki ya 2 mpaka ya 4 baada ya kuathirika.
Hii ni hatuwa ya kwanza, punde baada ya kuathirika yaani kupata VVU. Hapa mwanzoni mtu atahidi dalili ambazo zinatokea wiki ya pili mpaka wiki ya nne. Kwa baadhi ya watu inaweza kufika mpaka wiki ya 6. katika kipindi hiki mgonjwa atona dalili kadha zitakazoonyeshwa hapo chini:-



Dalili za VVU ndani ya mwezi mmoja toka kuathirika
1.Homa
2.Maumivu ya viungo na misuli
3.Uchou
4.Kutokwa na jasho jingi usiku
5.Kutokwa na upele au ukurutu kwenye ngozi
6.Kutokwa na vidonda vya mdomo
7.Kuwashwa na koo ama vidonda vya koo
8.Kuvimba kwa tezi za limfu kwenye mapaja (mitoki) kwenye makwapa na kwenye shingo (tonsils)
9.Kichefuchefu na kutapika



Katika kipindi hiki virusi huendelea kuzaliana kwa kasi sana, na kujirundika kwa wingi sana kwenye damu kuliko maeneo mengine. Kipindi hiki huchukuwa wiki 2 mpaka nne ama 6 kwa wastani ni mwezi mmoja. Amam mmoja na nusu. Baada ya hapa mtu hatahisi dalili zingine za VVU wala UKIMWI. Katika kipindi hiki mtu anaweza kuambukiza wengine kwa urahisi.



2.Katika hatuwa ya pili kutoka kwezi mmoja na kuendelea.
Katika kipindi hiki virusi vinaanza kujichimbia ndani zaidi kwenye mwili. Uwingi wa virusi unasambaa maeneo mengine ya mwili na kuendelea kuambukiza wengine. Hatuwa hii mgonjwa kama hatatumia dawa za ARV anaweza kuishi mpaka miaka 10 ama zaidi ya hapo. Endapo mtu atatumia dawa virudi vitaweza kuzuiwakujizalia na hatimaye kupunguwa mwilini na vinawez akufikia katika hatuwa mabayo havionekani kabisa, ila mtu ataendelea kuwa muathirika, na ataendelea kutumia dawa.



Katika hatuwa hii hakuna dalili maalumu za VVU zitakazojitokeza. Yaani hakuna dalili yeyote katika hatuwa hii. Hatuwa hii ni mbaya sana kwani mtu anajihisi yupo sawa kiafya na hana shida yeyote, lakini virusi vinaendelea kuharibu kinga ya mwili kidogo kidogo. Mwishoni mwa hatuwa hii mtu atakuwa kinga yake imeshuka sana. Katika hatuwa hii mi bado haambiwi ana UKIMWI ila bado ni muathirika wa VVU



3.Hatuwa ya tatu, UKIMWI.
UKIMWI hutokea pale virusi vya VVU vinapoharibu kinga ya mtu hadi kufikia CD4 200. ipo hivi; mtu mwenye afya ya kawaida katika kila kipimo kimoja seli zake za CD$ zinakuwa kati ya 500 mpaka 1500. sasa endapo zitashuka na kufika 200 mtu huyu ataambiwa ana upungufu wa kinga mwilii yaani UKIMWI, tu endapo upungufu huu umesababishwa na VVU. Katika hatuwa hii kama mtu hatatumia dawa za ARV anaweza kuishi kwa miaka 3 baada ya hapo huwenda akafariki dunia.



Dalili za UKIMWI
1.Kutokwa na jasho jingi usiku
2.Homa za mara kwa mara
3.Kifua kikavu kisichopona
4.Maradhi ya ngozi na mdomo
5.Maambukizi na mashambukizi ya mara kwa mara
6.Kuharisha kusikokoma
7.Kupunguwa uzito



Kwa nini ni muhimu kutumia ARV?
Kwa kuwa sasa umeshajuwa kuwa usipotumia dawa unaweza kuishi zaidi ya miaka 10.sasa nikujuze faida za kutumia dawa hizi:-
1.Kuzuia uzalishaji wa virusi vya UKIMWi
2.Kuongeza umathubuti wa kinga ya mwili na kurefusha muda wa kuishi
3.Kupunguza uwezekano wa kuambukiza watu wengine.



Je naweza kufanya ngono na aliyeathirika na nisiathirike?
Ndio inawezekana kabisa kwa sababu zifuatazo:-
1.Kama umetumia kinga (kondomu)
2.Kama hakukutokea muchubuko wakati wa tendo la ndoa
3.Kama mgonjwa ametumia ARV kwa muda mrefu angalau kwa miezi 6 na kutumi na hali hiyo kwa muda zaidi hata akafikia kiasi idadi ya virusi haionekani kwenye kipimo.



Dawa ya kuzuia kuathirika kwa walio hatarini zaidi.
Kuna watu wapo hatarini sana kuathirika. Kwa mfano madaktari na wakunga, muda wowote wanaweza kuathirika. Shuikrani ziwaendee wataalamu wa dawa, wametuletea dawa inayotambulikwa kwa PrEP au kwa kirefu pre-exposure prophylaxis. Hii ji dawa inayotumika kwa dharura endapo umepatwa na mazingira hatarishi ambayo yanaweza kukupelekea kuathirika. Dawa hii inafanya kazi ndani ya masaa 72 baada ya kupata virusi. Tafiti zinaonyesha kuwa dawa hii ni bora kwa asilimia 80 inaweza kuzuia kmaambukizi ya muda mfupi.



Utaratibu wa maisha kwa aliyeathirika
1.Jilinde na maambukizi
2.Punguza misongo ya mawazo
3.Tumia kondomu wakati wa kushiriki ngono
4.Fanya mazoezi ya mara kwa mara
5.Kula mlo kamili
6.Wacha kuvuta sigara
7.Wacha ama punguza kutumia vilevi





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 40582

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa

Soma Zaidi...
TIBA YA MINYOO AU DAWA YA MINYOO: praziquantel (biltricide) mebendazole (vermox, emverm) na albendazole (albenza).

TIBA YA MINYOO Moja katika sifa za minyoo ni kuwa wanatibika kwa urahisi pindi mgonjwa akipewa dawa husika.

Soma Zaidi...
Dalili za sukari kupungua mwilini (Hypoglycemia)

sukari kupungua mwilini (Hypoglycemia) huhusishwa kwa kawaida na matibabu ya Kisukari. Hata hivyo, hali mbalimbali, nyingi zikiwa nadra, zinaweza kusababisha sukari ya chini ya damu kwa watu wasio na Kisukari. Kama vile Homa, Hy

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa kula kupindukia

Ugonjwa wa kula kupindukia ni ugonjwa mbaya wa ulaji ambapo mara kwa mara unatumia kiasi kikubwa cha chakula na kuhisi huwezi kuacha kula.

Soma Zaidi...
Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisonono, sababu zake nanjia za kujilinda.

Kisonono husababishwa na bakteria. Bakteria ya kisonono mara nyingi hupitishwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine wakati wa kujamiiana, ikiwa ni pamoja na kujamiiana kwa mdomo, mkundu au uke.

Soma Zaidi...
Fahamu matatizo ya ini kuwa na kovu

kovu (Fibrosis) ya ini inayosababishwa na aina nyingi za magonjwa na hali ya ini, kama vile Homa ya Ini na unywaji pombe kupita kiasi. Ini hufanya kazi kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na kuondoa vitu vyenye madhara katika mwili wako, kusafisha damu yako

Soma Zaidi...
Matibabu ya fangasi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu matibabu ya fangasi

Soma Zaidi...