picha

Bipolar disorders

Bipolar disorder ni hali ya afya ya akili inayohusisha mabadiliko makubwa katika hisia, nishati, na shughuli za kila siku za mtu. Dalili za bipolar disorder zinaweza kuwa kwenye kipindi cha mania na kipindi cha unyogovu, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa bipolar.

Ugonjwa huu wa bipolar una sehemu tofauti ambapo mgonjwa wa akili anaweza kuwa na furaha kubwa,kukasilika ghafla ,yaani Kwa ujumla anakuwa na pande mbili yaani furaha na huzuni na jinsi tutakavyozifafanua kama ifuatavyo.

Kipindi Cha furaha (mania)

1.Furaha kupita kiasi au msisimko usio wa kawaida, Hasira au kutokuelewana kwa urahisi,Kwa mda huu mgonjwa anaweza kuwa na furaha sana ,akachangamka akacheka ila Kwa mda mfupi tu akawa na Hasira na kutoelewana na mtu yeyote yule.

2.pia na hisia za kuwa na nguvu zisizo za kawaida.

Kwa mfano uongezeka kwa shughuli na uwezo wa kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja pia mgonjwa anaweza kufanya shughuli zote Kwa ukamilifu na Kwa wakati mmoja zote zikaisha na katika kipindi hiki mgonjwa hapendi kuingiliwa kwenye shughuli zake.

3.kufanya mambo haraka haraka

  Akili ya mgonjwa inakuwa inaamua mambo Kwa haraka ambapo mtu anaweza kuhamasika na mawazo mengi kwa wakati mmoja na kuwa na mipango mingi Kwa wakati mmoja,pia hali hii ikimpata mtu akiwa kiongozi wa kundi kabla hajagundulika watu wanapata shida sana Kwa sababu atakuwa na mipango mingi ya haraka Kwa wakati mmoja.

4.Kupuuza kutokea Kwa hatari.

Kutenda bila kufikiri matokeo, kama vile kuwekeza pesa nyingi au kushiriki katika tabia zisizo za kawaida ambazo zinaweza kuleta hatari Kwa mgonjwa,yaani Kila kitu anaweza kufanya bila kufikilia matokeo ya kitu anachokifanya,haogopi mtu,haogopi wakati wa hatari yeye kauli yake ni kwamba Kila kitu ni kawaida tu.

5.Kujiona Mtu anayefaa na mkubwa kuliko yeyote yule.

:Kujiona kuwa na uwezo au nguvu zaidi kuliko kawaida, au kuwa na dhana ya umbo kubwa zaidi wa kibinafsi,yeye anaona anafahamu Kwa Kila kitu bila yeye hakuna kitu ambacho kinaweza kufanya Kwa hiyo anao uwezo wa kuamrisha Kila mtu.

6.Kukosa Usingizi.

Kulala masaa machache tu au kutokulala kabisa kwa sababu yeye anajiona ni mweye nguvu Kwa hiyo atafanys kazi mda wote na pia kuzunguka huku na huku pia hatulii Kwa sababu anaona bila yeye hakuna kitu kinachoweza kufanyika hali ambayo anaona kulala ni kupoteza mda.

Kipindi cha Unyogovu(depression)

1.kuwa na huzuni.

 kukatishwa tamaa, au hisia za kukosa thamani,hali hii umefanya kujisikia kwamba haifai na pia anachokifanya hakina maana hali inayomsukuma kukata tamaa.

2.Kupoteza hamu ya kufanya shughuli nyingine za kijamii 

Kukosa hamu ya kufanya mambo ambayo kawaida yanawafurahisha na pia anashindwa kunifanyia chochote hata mambo ya kawaida anashindwa kabisa.

.3.Kupunguza au kuongezeka Kwa Uzito.

Mabadiliko makubwa katika uzito kutokana na mabadiliko ya hamu ya chakula Kwa sababu anaweza kuamua kula sana na uzito unaongezeka au anaweza kukosa kabisa hamu ya chakula na uzito ukapungua.

4.Kujisikia uchovu

, kuchoka au kuchoka bila sababu .Kipindi cha Unyogovu Kwa hiyo katika kipindi hiki utamkuta jamaa kalala mda wote ukimuuliza kulikoni anakwambia amechoka na huku hajafanya kitu.

 

.kwa hiyo huyu mgonjwa tunafahamu wazi kwamba ana vipindi viwili ,Kipindi cha unyogovu na kipindi cha maania Mchakato wa muda mrefu wa mabadiliko ya hisia kabla ya kuingia kwenye kipindi cha mania au unyogovu.Msaada na Matibabu:Ni muhimu kutafuta msaada wa kitaalam kama unadhani una dalili za bipolar disorder. Matibabu yanaweza kujumuisha dawa na Terapia ya kuzungumza ili kuweze kumsaidia mgonjwa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Salvatory image Tarehe: 2025-09-20 01:44:38 Topic: magonjwa Main: Masomo File: Download PDF Views 687

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     ๐Ÿ‘‰2 Dua za Mitume na Manabii     ๐Ÿ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     ๐Ÿ‘‰4 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game     ๐Ÿ‘‰6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Ni zipi dalili za awali za pumu

Kabla ya kubanwa zaidi na pumu, kuna dalili za awali zinzznza kujitokeza, na hapo ndipo utakapoanza kuchukuwa tahadhari. Makala hii itakwenda kukujulisha zaidi kuhusu dalili hizo.

Soma Zaidi...
Dalili za vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Vyakula Bora kwa Mtoto Anayekua

โ€‹Lishe sahihi ni msingi mkuu wa ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili. Makala haya yataangazia vyakula muhimu vinavyopaswa kuwemo katika mlo wa mtoto, jinsi ya kuandaa mlo kamili, na ukweli wa kisayansi kuhusu virutubisho vinavyohitajika katika kila hatua ya ukuaji.

Soma Zaidi...
โ€‹Kupima HIV Nyumbani

Posthii inatoa mwongozo kamili kuhusu upimaji wa HIV nyumbani. Tutachunguza umuhimu wake, jinsi ya kutumia vifaa hivyo, faida zake, na hatua za kuchukua baada ya kupata majibu, ili kukuwezesha kufanya maamuzi sahihi kuhusu afya yako kwa usiri na utulivu.

Soma Zaidi...
Typhoid husabisha mwili kuchoka na maumivu ya kichwa pamoja na joint za miguu kuchoka

Dalili za typhid zinapasa kuangaliwa kwa umakini. Bila vipimo mtu asitumie dawa za tyohod, kwanu dalili za tyohid hufanana na daliki za maradhi mengi.

Soma Zaidi...
Maumivu wakati wa hedhi

โ€‹Maumivu wakati wa hedhi, kitaalamu yakijulikana kama Dysmenorrhea, ni changamoto inayowaathiri mamilioni ya wanawake duniani kote. Wakati maumivu mepesi yakichukuliwa kama hali ya kawaida ya mabadiliko ya mwili, maumivu makali yanayomzuia mwanamke kufanya shughuli zake za kila siku yanaweza kuwa ishara ya matatizo makubwa ya kiafya. Makala haya yanajadili aina za maumivu haya, vyanzo vyake vikuu, njia za nyumbani na za kitabibu za kupata suluhisho, pamoja na ukweli wa kisayansi dhidi ya dhana potofu.

Soma Zaidi...