picha

Bipolar disorders

Bipolar disorder ni hali ya afya ya akili inayohusisha mabadiliko makubwa katika hisia, nishati, na shughuli za kila siku za mtu. Dalili za bipolar disorder zinaweza kuwa kwenye kipindi cha mania na kipindi cha unyogovu, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa bipolar.

Ugonjwa huu wa bipolar una sehemu tofauti ambapo mgonjwa wa akili anaweza kuwa na furaha kubwa,kukasilika ghafla ,yaani Kwa ujumla anakuwa na pande mbili yaani furaha na huzuni na jinsi tutakavyozifafanua kama ifuatavyo.

Kipindi Cha furaha (mania)

1.Furaha kupita kiasi au msisimko usio wa kawaida, Hasira au kutokuelewana kwa urahisi,Kwa mda huu mgonjwa anaweza kuwa na furaha sana ,akachangamka akacheka ila Kwa mda mfupi tu akawa na Hasira na kutoelewana na mtu yeyote yule.

2.pia na hisia za kuwa na nguvu zisizo za kawaida.

Kwa mfano uongezeka kwa shughuli na uwezo wa kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja pia mgonjwa anaweza kufanya shughuli zote Kwa ukamilifu na Kwa wakati mmoja zote zikaisha na katika kipindi hiki mgonjwa hapendi kuingiliwa kwenye shughuli zake.

3.kufanya mambo haraka haraka

  Akili ya mgonjwa inakuwa inaamua mambo Kwa haraka ambapo mtu anaweza kuhamasika na mawazo mengi kwa wakati mmoja na kuwa na mipango mingi Kwa wakati mmoja,pia hali hii ikimpata mtu akiwa kiongozi wa kundi kabla hajagundulika watu wanapata shida sana Kwa sababu atakuwa na mipango mingi ya haraka Kwa wakati mmoja.

4.Kupuuza kutokea Kwa hatari.

Kutenda bila kufikiri matokeo, kama vile kuwekeza pesa nyingi au kushiriki katika tabia zisizo za kawaida ambazo zinaweza kuleta hatari Kwa mgonjwa,yaani Kila kitu anaweza kufanya bila kufikilia matokeo ya kitu anachokifanya,haogopi mtu,haogopi wakati wa hatari yeye kauli yake ni kwamba Kila kitu ni kawaida tu.

5.Kujiona Mtu anayefaa na mkubwa kuliko yeyote yule.

:Kujiona kuwa na uwezo au nguvu zaidi kuliko kawaida, au kuwa na dhana ya umbo kubwa zaidi wa kibinafsi,yeye anaona anafahamu Kwa Kila kitu bila yeye hakuna kitu ambacho kinaweza kufanya Kwa hiyo anao uwezo wa kuamrisha Kila mtu.

6.Kukosa Usingizi.

Kulala masaa machache tu au kutokulala kabisa kwa sababu yeye anajiona ni mweye nguvu Kwa hiyo atafanys kazi mda wote na pia kuzunguka huku na huku pia hatulii Kwa sababu anaona bila yeye hakuna kitu kinachoweza kufanyika hali ambayo anaona kulala ni kupoteza mda.

Kipindi cha Unyogovu(depression)

1.kuwa na huzuni.

 kukatishwa tamaa, au hisia za kukosa thamani,hali hii umefanya kujisikia kwamba haifai na pia anachokifanya hakina maana hali inayomsukuma kukata tamaa.

2.Kupoteza hamu ya kufanya shughuli nyingine za kijamii 

Kukosa hamu ya kufanya mambo ambayo kawaida yanawafurahisha na pia anashindwa kunifanyia chochote hata mambo ya kawaida anashindwa kabisa.

.3.Kupunguza au kuongezeka Kwa Uzito.

Mabadiliko makubwa katika uzito kutokana na mabadiliko ya hamu ya chakula Kwa sababu anaweza kuamua kula sana na uzito unaongezeka au anaweza kukosa kabisa hamu ya chakula na uzito ukapungua.

4.Kujisikia uchovu

, kuchoka au kuchoka bila sababu .Kipindi cha Unyogovu Kwa hiyo katika kipindi hiki utamkuta jamaa kalala mda wote ukimuuliza kulikoni anakwambia amechoka na huku hajafanya kitu.

 

.kwa hiyo huyu mgonjwa tunafahamu wazi kwamba ana vipindi viwili ,Kipindi cha unyogovu na kipindi cha maania Mchakato wa muda mrefu wa mabadiliko ya hisia kabla ya kuingia kwenye kipindi cha mania au unyogovu.Msaada na Matibabu:Ni muhimu kutafuta msaada wa kitaalam kama unadhani una dalili za bipolar disorder. Matibabu yanaweza kujumuisha dawa na Terapia ya kuzungumza ili kuweze kumsaidia mgonjwa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Salvatory image Tarehe: 2025-09-20 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 464

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Chanzo cha kiungulia

Post hii inahusu zaidi vyanzo vya kuwepo kwa kiungulia, kiungulia ni kitendo cha kupanda kwa gesi kutoka kwenye tumbo mpaka kwenye mdomo,hali uwasumbua wengi na kusababisha hali isiyo rafiki.

Soma Zaidi...
Ishara na dalilili za Mtoto mwenye kuhara

postii hii inazungumzia dalilili za Mtoto mwenye Kuhara. Kuhara maana yake ni kutokwa na kinyesi chenye maji matatu au zaidi, pamoja na au bila damu ndani ya masaa 24. Kuhara kunaweza kusababishwa na maambukizo ya bakteria na virusi, ugonjwa wa matumb

Soma Zaidi...
Kucha langu LA mguu linang'ooka...nini chaweza kuwa tatizo

Je na wewe unasumbukiwa na kunggoka jwa kucha. Tatizo limekunaza una muda gani nalo?

Soma Zaidi...
Msaada kwa aliye na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Posti hii inahusu zaidi msaada kwa aliye na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni huduma maalumu ambayo utolewa kwa mtu ambaye ana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo. Zifuatazo ni huduma maalumu kwa mwenye uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuepuka minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuiepuka minyoo

Soma Zaidi...
Kifuwa kinaniuma katikati kinaambatana nakichwa

Maumivu ya kifuwa yanaweza kutokea baada ya kubeba kitu kizito, ama kupata mashambulizi ya vijidudu vya maradhi. maumivu ya viungo na hata vidonda vya tumbo. Lakini sasa umesha wahi fikiria maumivu ya kifuwa kwa katikati?

Soma Zaidi...
Dalili kuu 7 za malaria na dawa ya kutibu malaria

Makala hii itazungumzia dalili za Malaria, athari za kuchelewa kutibu malaria, na matibabu ya malaria

Soma Zaidi...
Yajue magonjwa ya kurithi.

Posti hii inahusu zaidi Magonjwa vya kurithi ambayo mara nyingi utokea kwenye jamii ni magonjwa ambayo yanaweza kutokea kwenye familia na wanafamilia walio wengi wakaweza kupata ugonjwa huo Magonjwa yenyewe ni kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa kaswende

Post hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kaswende kwa wajawazito, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa watu wote, kwa sababu ugonjwa huu una dalili ambazo upitia kwa hatua mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Naomb niulize ukiingiliana na mwanmke mweny ukimwi unaweza kuambikizwa na kusaambaaa kwa mda gan ndan ya mwil

Muda gani ukimwi huweza kuonekana mwilini ama kugundulika kama umeathirika, ni dalili zipo hujitokeza punde tu utakapoathirika

Soma Zaidi...