Bipolar disorders

Bipolar disorder ni hali ya afya ya akili inayohusisha mabadiliko makubwa katika hisia, nishati, na shughuli za kila siku za mtu. Dalili za bipolar disorder zinaweza kuwa kwenye kipindi cha mania na kipindi cha unyogovu, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa bipolar.

Ugonjwa huu wa bipolar una sehemu tofauti ambapo mgonjwa wa akili anaweza kuwa na furaha kubwa,kukasilika ghafla ,yaani Kwa ujumla anakuwa na pande mbili yaani furaha na huzuni na jinsi tutakavyozifafanua kama ifuatavyo.

Kipindi Cha furaha (mania)

1.Furaha kupita kiasi au msisimko usio wa kawaida, Hasira au kutokuelewana kwa urahisi,Kwa mda huu mgonjwa anaweza kuwa na furaha sana ,akachangamka akacheka ila Kwa mda mfupi tu akawa na Hasira na kutoelewana na mtu yeyote yule.

2.pia na hisia za kuwa na nguvu zisizo za kawaida.

Kwa mfano uongezeka kwa shughuli na uwezo wa kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja pia mgonjwa anaweza kufanya shughuli zote Kwa ukamilifu na Kwa wakati mmoja zote zikaisha na katika kipindi hiki mgonjwa hapendi kuingiliwa kwenye shughuli zake.

3.kufanya mambo haraka haraka

  Akili ya mgonjwa inakuwa inaamua mambo Kwa haraka ambapo mtu anaweza kuhamasika na mawazo mengi kwa wakati mmoja na kuwa na mipango mingi Kwa wakati mmoja,pia hali hii ikimpata mtu akiwa kiongozi wa kundi kabla hajagundulika watu wanapata shida sana Kwa sababu atakuwa na mipango mingi ya haraka Kwa wakati mmoja.

4.Kupuuza kutokea Kwa hatari.

Kutenda bila kufikiri matokeo, kama vile kuwekeza pesa nyingi au kushiriki katika tabia zisizo za kawaida ambazo zinaweza kuleta hatari Kwa mgonjwa,yaani Kila kitu anaweza kufanya bila kufikilia matokeo ya kitu anachokifanya,haogopi mtu,haogopi wakati wa hatari yeye kauli yake ni kwamba Kila kitu ni kawaida tu.

5.Kujiona Mtu anayefaa na mkubwa kuliko yeyote yule.

:Kujiona kuwa na uwezo au nguvu zaidi kuliko kawaida, au kuwa na dhana ya umbo kubwa zaidi wa kibinafsi,yeye anaona anafahamu Kwa Kila kitu bila yeye hakuna kitu ambacho kinaweza kufanya Kwa hiyo anao uwezo wa kuamrisha Kila mtu.

6.Kukosa Usingizi.

Kulala masaa machache tu au kutokulala kabisa kwa sababu yeye anajiona ni mweye nguvu Kwa hiyo atafanys kazi mda wote na pia kuzunguka huku na huku pia hatulii Kwa sababu anaona bila yeye hakuna kitu kinachoweza kufanyika hali ambayo anaona kulala ni kupoteza mda.

Kipindi cha Unyogovu(depression)

1.kuwa na huzuni.

 kukatishwa tamaa, au hisia za kukosa thamani,hali hii umefanya kujisikia kwamba haifai na pia anachokifanya hakina maana hali inayomsukuma kukata tamaa.

2.Kupoteza hamu ya kufanya shughuli nyingine za kijamii 

Kukosa hamu ya kufanya mambo ambayo kawaida yanawafurahisha na pia anashindwa kunifanyia chochote hata mambo ya kawaida anashindwa kabisa.

.3.Kupunguza au kuongezeka Kwa Uzito.

Mabadiliko makubwa katika uzito kutokana na mabadiliko ya hamu ya chakula Kwa sababu anaweza kuamua kula sana na uzito unaongezeka au anaweza kukosa kabisa hamu ya chakula na uzito ukapungua.

4.Kujisikia uchovu

, kuchoka au kuchoka bila sababu .Kipindi cha Unyogovu Kwa hiyo katika kipindi hiki utamkuta jamaa kalala mda wote ukimuuliza kulikoni anakwambia amechoka na huku hajafanya kitu.

 

.kwa hiyo huyu mgonjwa tunafahamu wazi kwamba ana vipindi viwili ,Kipindi cha unyogovu na kipindi cha maania Mchakato wa muda mrefu wa mabadiliko ya hisia kabla ya kuingia kwenye kipindi cha mania au unyogovu.Msaada na Matibabu:Ni muhimu kutafuta msaada wa kitaalam kama unadhani una dalili za bipolar disorder. Matibabu yanaweza kujumuisha dawa na Terapia ya kuzungumza ili kuweze kumsaidia mgonjwa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Salvatory image Tarehe: 1970-01-01 03:33:45 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 381

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

Nini hasa chanzo cha pumu, na je inarithiwa?

Ugonjwa wa pumu ni moja katika magonjwa hatari yanayoweza kutokea kwa ghafla, na endapo itacheleweshwa kudhibitiwa inaweza sababisha athari mbaya zaidi

Soma Zaidi...
Magonjwa ya moyo

Posti hii inahusu zaidi magonjwa ya moyo, kwa kawaida watu wakisikia habari za magonjwa ya moyo huwa hawaelewi yanakuwaje kuwaje, Leo nataka niwafahamishe kuhusu magonjwa ya moyo na sehemu mbalimbali zinazoathirika.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kushoto

Soma Zaidi...
Kuona damu kwenye mkojo

Kuona damu kwenye mkojo kunaweza kusababisha wasiwasi. Ingawa katika hali nyingi kuna sababu zisizofaa, Damu kwenye mkojo (hematuria) pia inaweza kuonyesha ugonjwa mbaya.

Soma Zaidi...
ugonjwa wa Malaria dalili zake na chanzo chake.

Malaria ni moja ya magonjwa hatari yanayoongoza katika vifo vya watoto wengi duniani walio chni ya umri wa miaka 5. Katika post hii utakwend akujifunza kuhusuugonjwa huu jinsi unavyotokea, hatuwa zake na dalili zake.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za Ugonjwa wa kuambukiza.

Magonjwa ya kuambukiza ni maradhi yanayosababishwa na vijidudu kama vile bakteria, virusi, fangasi au vimelea. Viumbe vingi vinaishi ndani na kwenye miili yetu. Kwa kawaida hazina madhara au hata kusaidia, lakini chini ya hali fulani, baadhi ya viumbe

Soma Zaidi...
Dalili ya pressure ya kupanda

Post ya leo inaenda kufundisha dalili na hatari za presha ya kupanda. Presha ni ugonjwa unaosababishwa na baadhi ya vitu mbalimbali.pressure hujulikana kwa jina lingine ambolo ni hypertension (pressure ya kupanda). presha hugundulika pale ambapo presha ya

Soma Zaidi...
Huduma kwa wenye Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia Watu wale ambao wana Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo.

Soma Zaidi...
Dalili za homa ya ini

Kaika post hii utakwenda kujifunz akuhusu dalili za homa ya ini. Dalili hizi sio lazima zitokee zote. Zinaweza zikatokea baadhi tu na ikatosha kuonjesha kuw auna homa ya ini.

Soma Zaidi...
FAIDA ZA KIAFYA ZA MINYOO: kupunguza aleji, kuchochea utungaji wa mimba, kupona kwa vidonda vya ndani

FAIDA ZA KIAFYA ZA MINYOO Wakati mwingine kuwa na aina flani ya minyoo kunaweza kuwa na faida katika afya.

Soma Zaidi...