Bipolar disorders

Bipolar disorder ni hali ya afya ya akili inayohusisha mabadiliko makubwa katika hisia, nishati, na shughuli za kila siku za mtu. Dalili za bipolar disorder zinaweza kuwa kwenye kipindi cha mania na kipindi cha unyogovu, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa bipolar.

Ugonjwa huu wa bipolar una sehemu tofauti ambapo mgonjwa wa akili anaweza kuwa na furaha kubwa,kukasilika ghafla ,yaani Kwa ujumla anakuwa na pande mbili yaani furaha na huzuni na jinsi tutakavyozifafanua kama ifuatavyo.

Kipindi Cha furaha (mania)

1.Furaha kupita kiasi au msisimko usio wa kawaida, Hasira au kutokuelewana kwa urahisi,Kwa mda huu mgonjwa anaweza kuwa na furaha sana ,akachangamka akacheka ila Kwa mda mfupi tu akawa na Hasira na kutoelewana na mtu yeyote yule.

2.pia na hisia za kuwa na nguvu zisizo za kawaida.

Kwa mfano uongezeka kwa shughuli na uwezo wa kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja pia mgonjwa anaweza kufanya shughuli zote Kwa ukamilifu na Kwa wakati mmoja zote zikaisha na katika kipindi hiki mgonjwa hapendi kuingiliwa kwenye shughuli zake.

3.kufanya mambo haraka haraka

  Akili ya mgonjwa inakuwa inaamua mambo Kwa haraka ambapo mtu anaweza kuhamasika na mawazo mengi kwa wakati mmoja na kuwa na mipango mingi Kwa wakati mmoja,pia hali hii ikimpata mtu akiwa kiongozi wa kundi kabla hajagundulika watu wanapata shida sana Kwa sababu atakuwa na mipango mingi ya haraka Kwa wakati mmoja.

4.Kupuuza kutokea Kwa hatari.

Kutenda bila kufikiri matokeo, kama vile kuwekeza pesa nyingi au kushiriki katika tabia zisizo za kawaida ambazo zinaweza kuleta hatari Kwa mgonjwa,yaani Kila kitu anaweza kufanya bila kufikilia matokeo ya kitu anachokifanya,haogopi mtu,haogopi wakati wa hatari yeye kauli yake ni kwamba Kila kitu ni kawaida tu.

5.Kujiona Mtu anayefaa na mkubwa kuliko yeyote yule.

:Kujiona kuwa na uwezo au nguvu zaidi kuliko kawaida, au kuwa na dhana ya umbo kubwa zaidi wa kibinafsi,yeye anaona anafahamu Kwa Kila kitu bila yeye hakuna kitu ambacho kinaweza kufanya Kwa hiyo anao uwezo wa kuamrisha Kila mtu.

6.Kukosa Usingizi.

Kulala masaa machache tu au kutokulala kabisa kwa sababu yeye anajiona ni mweye nguvu Kwa hiyo atafanys kazi mda wote na pia kuzunguka huku na huku pia hatulii Kwa sababu anaona bila yeye hakuna kitu kinachoweza kufanyika hali ambayo anaona kulala ni kupoteza mda.

Kipindi cha Unyogovu(depression)

1.kuwa na huzuni.

 kukatishwa tamaa, au hisia za kukosa thamani,hali hii umefanya kujisikia kwamba haifai na pia anachokifanya hakina maana hali inayomsukuma kukata tamaa.

2.Kupoteza hamu ya kufanya shughuli nyingine za kijamii 

Kukosa hamu ya kufanya mambo ambayo kawaida yanawafurahisha na pia anashindwa kunifanyia chochote hata mambo ya kawaida anashindwa kabisa.

.3.Kupunguza au kuongezeka Kwa Uzito.

Mabadiliko makubwa katika uzito kutokana na mabadiliko ya hamu ya chakula Kwa sababu anaweza kuamua kula sana na uzito unaongezeka au anaweza kukosa kabisa hamu ya chakula na uzito ukapungua.

4.Kujisikia uchovu

, kuchoka au kuchoka bila sababu .Kipindi cha Unyogovu Kwa hiyo katika kipindi hiki utamkuta jamaa kalala mda wote ukimuuliza kulikoni anakwambia amechoka na huku hajafanya kitu.

 

.kwa hiyo huyu mgonjwa tunafahamu wazi kwamba ana vipindi viwili ,Kipindi cha unyogovu na kipindi cha maania Mchakato wa muda mrefu wa mabadiliko ya hisia kabla ya kuingia kwenye kipindi cha mania au unyogovu.Msaada na Matibabu:Ni muhimu kutafuta msaada wa kitaalam kama unadhani una dalili za bipolar disorder. Matibabu yanaweza kujumuisha dawa na Terapia ya kuzungumza ili kuweze kumsaidia mgonjwa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Salvatory image Tarehe: 1970-01-01 03:33:45 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 215

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Sababu zinazoweza kumfanya figo kuharibika.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kufanya figo kuharibika.hili ni janga ambalo linawakumba Watu wengi siku hizi na kusababisha kupoteza maisha kwa wagonjwa wa figo hasa hasa kwa wale ambao hawana uwezo wa kulipia hela ya kusafishia figo.

Soma Zaidi...
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces

Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis.

Soma Zaidi...
Dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo

Post hii inahusu zaidi dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ingawa sio watu wote wenye dalili kama hizi Wana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo Ila zikitokea mtu anapaswa

Soma Zaidi...
Dalili za homa ya ini

Kaika post hii utakwenda kujifunz akuhusu dalili za homa ya ini. Dalili hizi sio lazima zitokee zote. Zinaweza zikatokea baadhi tu na ikatosha kuonjesha kuw auna homa ya ini.

Soma Zaidi...
Hatua tatu anazozipitia mgonjwa wa tauni

Posti hii inahusu zaidi njia au hatua tatu muhimu anazopitia Mgonjwa wa gauni, kuanzia kwa Maambukizi mpaka kwenye hatua ya mwisho hasa kama Ugonjwa huu haujatibiwa mapema.

Soma Zaidi...
Matatizo yanayosababisha mshtuko wa moyo.

Mshtuko wa moyo hutokea wakati mtiririko wa damu kwa moyo umezuiwa, mara nyingi kwa mkusanyiko wa mafuta, cholesterol na vitu vingine, ambayo huunda plaque katika mishipa inayolisha moyo (mishipa ya moyo). Mtiririko wa damu ulioingiliwa unaweza kuharibu

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa mshtuko wa sumu.

Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu ni matatizo ya nadra, yanayotishia maisha ya aina fulani za maambukizi ya bakteria. Mara nyingi ugonjwa wa mshtuko wenye sumu hutokana na sumu zinazozalishwa na bakteria.

Soma Zaidi...
Namna ya Kuzuia Mtoto mwenye kifua kikuu (TB).

posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano. Kifua kikuu ni ugonjwa sugu wa kuambukiza na anuwai ya magonjwa ya kliniki yanayosababishwa na Mycobacterium tuberculosis complex.

Soma Zaidi...
Je unaijuwa ugonjwa wa bawasiri

Katika post hii nitakwenda kukujuza kuhusu ugonjwa wa bawasiri

Soma Zaidi...