Ugonjwa wa upele na matibabu yake
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa upele na matatibabu yake, ni ugonjwa unaosabavishwa na mdudu kwa kitaalamu huitwa mites sarcoptes scrabie mdudu huyu usababisha miwasho kwenye ngozi.
Ugonjwa wa upele.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa ugonjwa huu wa upele unashambulia sana watoto na wazee pamoja na wale wenye kinga kidogo mwilini. Kwa sababu ya uangalizi mdogo wa wazee na watoto ndo maana wanakuwa waanga wa kwanza wa ugonjwa huu.
2. Ugonjwa huu unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa kugusana au kutumia nguo Moja yaani mwenye maambukizi ana vaa nguo na asiye na maambukizi naye anavaa kwa kufanya hivyo ugonjwa huu unaweza kusambaa sana, pia kwa wale watu wanaotumia shuka Moja wakati wa kulala wanaweza kupata ugonjwa huo kwa hiyo ni vizuri kuwa makini katika matumizi ya nguo na vitu Ili kuendelea kupambana na ugonjwa huu wa upele.
3. Ugonjwa huu ukitokea unaweza kitibiwa kwa dawa zifuatazo permethrin, parathyroid na pia Kuna dawa ya oral livermectin na yenyewe inasaidia kwenye matibabu, na pia tunaweza kutumia anti histamine Ili kupunguza miwasho kwa sababu Kuna wakati mwingine miwasho inakuwa mingi na yenye nguvu kwa hiyo ni vizuri kutumia dawa hiyo hata kama unatumia zingine walau miwasho ipungue.
4. Pia Kuna wakati mwingine usafi tu ndo dawa kama Kuna upele kwenye familia pamoja na kutumia dawa ni vizuri kabisa kufanya usafi kwa kupga kila siku kwa maji masafi na sababu pia ni lazima kifua nguo na kuzinyoosha na kihakikisha kuwa mashuka nayo yanafuliwa na ikiwezekana kuto vitu nje pamoja na magodoro walau mara Moja kwa wiki Ili kuweza kupunguza na kuondoa maambukizi.
5. Vile vile kwa matumizi ya dawa ni vizuri kabisa kutumia dawa hizo kwa ushauri wa wataalamu wa afya Ili kuepuka matumizi ya kiholela, kwa hiyo ni vizuri kabisa kupambana na ugonjwa huu kwa sababu unaweza kuisha kabisa.
6. Pia kwa wale wenye maambukizi au kinga yao inashuka hata kama wakifanya usafi ni vigumu kupona ugonjwa huu kwa hiyo wanapaswa kuwaona wataalamu wa afya Ili kuweza kupata ushauri na kupima afya zao na kuondokana na ugonjwa huu. Piaa Kuna wale wenye aleji na vitu na wanapata upele na wenyewe wanapaswa kutafuta matibabu Ili kuepuka na ugonjwa huu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Fahamu matatizo ya ini kuwa na kovu
kovu (Fibrosis) ya ini inayosababishwa na aina nyingi za magonjwa na hali ya ini, kama vile Homa ya Ini na unywaji pombe kupita kiasi. Ini hufanya kazi kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na kuondoa vitu vyenye madhara katika mwili wako, kusafisha damu yako
Soma Zaidi...Sababu za maumivu wakati wa kujamiiana
​Maumivu wakati wa kujamiiana (kitaalamu dyspareunia) ni tatizo linalowasumbua wanawake wengi, ingawa mara nyingi halizungumzwi wazi kutokana na unyanyapaa au aibu. Maumivu haya yanaweza kusababishwa na sababu za kisaikolojia, matatizo ya kimwili, au mabadiliko ya kihomoni. Makala haya yanachambua vyanzo vikuu vya maumivu hayo na kutoa ukweli wa kisayansi (Fact Check) ili kukusaidia kujua hatua za kuchukua.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa vidonda vya kitanda (bed sores)
Posti hii inaonyesha dalili za ugonjwa wa Vidonda vya kitanda (bed sores)mara nyingi hukua kwenye ngozi ambayo hufunika sehemu za mifupa ya mwili, kama vile visigino, vifundoni, viuno. Vidonda vya kitanda vinaweza kukua haraka na mara nyingi ni vigumu
Soma Zaidi...Fangasi mdomoni ni dalili ya minyoo aina gani
Zipo aina nyingi za fantasy ambazo ni rahisi kuathiri binadamu. Wipe ambao haiathiri mdomo, nyayo, shemu za siri na kwenye ngozi.
Soma Zaidi...Dalili za Maambukizi kwenye mifupa
Posti hii inahusu zaidi dalili za Maambukizi kwenye mifupa, ni dalili ambazo ukionyesha kwa mtu mwenye Maambukizi kwenye mifupa.
Soma Zaidi...Tatizo la kujaa mate mdomoni nimeambiwa nina minyoo
Mie ni kijana wa kiume umri 33, nna tatizo la kujaa mate mdomoni nimeambiwa nna minyoo lakini hata nikinywa dawa sioni afadhali, niliona labda ni pombe nikapumzika kunywa tatizo lipo pale pale japo nisipokunywa haliwi kwa ukubwa ule ila lipo.
Soma Zaidi...