Ugonjwa wa upele na matibabu yake
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa upele na matatibabu yake, ni ugonjwa unaosabavishwa na mdudu kwa kitaalamu huitwa mites sarcoptes scrabie mdudu huyu usababisha miwasho kwenye ngozi.
Ugonjwa wa upele.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa ugonjwa huu wa upele unashambulia sana watoto na wazee pamoja na wale wenye kinga kidogo mwilini. Kwa sababu ya uangalizi mdogo wa wazee na watoto ndo maana wanakuwa waanga wa kwanza wa ugonjwa huu.
2. Ugonjwa huu unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa kugusana au kutumia nguo Moja yaani mwenye maambukizi ana vaa nguo na asiye na maambukizi naye anavaa kwa kufanya hivyo ugonjwa huu unaweza kusambaa sana, pia kwa wale watu wanaotumia shuka Moja wakati wa kulala wanaweza kupata ugonjwa huo kwa hiyo ni vizuri kuwa makini katika matumizi ya nguo na vitu Ili kuendelea kupambana na ugonjwa huu wa upele.
3. Ugonjwa huu ukitokea unaweza kitibiwa kwa dawa zifuatazo permethrin, parathyroid na pia Kuna dawa ya oral livermectin na yenyewe inasaidia kwenye matibabu, na pia tunaweza kutumia anti histamine Ili kupunguza miwasho kwa sababu Kuna wakati mwingine miwasho inakuwa mingi na yenye nguvu kwa hiyo ni vizuri kutumia dawa hiyo hata kama unatumia zingine walau miwasho ipungue.
4. Pia Kuna wakati mwingine usafi tu ndo dawa kama Kuna upele kwenye familia pamoja na kutumia dawa ni vizuri kabisa kufanya usafi kwa kupga kila siku kwa maji masafi na sababu pia ni lazima kifua nguo na kuzinyoosha na kihakikisha kuwa mashuka nayo yanafuliwa na ikiwezekana kuto vitu nje pamoja na magodoro walau mara Moja kwa wiki Ili kuweza kupunguza na kuondoa maambukizi.
5. Vile vile kwa matumizi ya dawa ni vizuri kabisa kutumia dawa hizo kwa ushauri wa wataalamu wa afya Ili kuepuka matumizi ya kiholela, kwa hiyo ni vizuri kabisa kupambana na ugonjwa huu kwa sababu unaweza kuisha kabisa.
6. Pia kwa wale wenye maambukizi au kinga yao inashuka hata kama wakifanya usafi ni vigumu kupona ugonjwa huu kwa hiyo wanapaswa kuwaona wataalamu wa afya Ili kuweza kupata ushauri na kupima afya zao na kuondokana na ugonjwa huu. Piaa Kuna wale wenye aleji na vitu na wanapata upele na wenyewe wanapaswa kutafuta matibabu Ili kuepuka na ugonjwa huu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 ai web app 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 web hosting 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Msaada kwa wenye Maambukizi kwenye mifupa
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwahudumia wenye Maambukizi kwenye mifupa, ni njia ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuwasaidia wenye Maambukizi kwenye mifupa.
Soma Zaidi...Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Dalili za upungufu wa maji mwilini.
Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji.
Soma Zaidi...Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt
Soma Zaidi...Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.
Soma Zaidi...