Dalili za ugonjwa wa schizophrenia

Schizophrenia ni ugonjwa wa akili ambao huathiri jinsi mtu anavyofikiri, kuhisi, na kuamua. Dalili za schizophrenia zinaweza kuwa kama ifuatavyo hapo chini

1.Mawasiliano Kwa ujumla hasa kuhusu hisia zao na kutoziwasilisha Kwa mpangilio.

 Watu wenye schizophrenia wanaweza kushindwa kueleweka au kuwasiliana vyema, Hii inaweza kujumuisha mambo kama kuzungumza bila mpangilio au kuacha mazungumzo,au wakati wa kuongea hawezi kuongea jambo akalimaliza vizuri hatua Kwa hatua na likaeleweka na pia hawezi kuielezea hisia yoyote aliyo nayo na ikaeleweka Kwa watu,Kwa hiyo ni vigumu kumwelewa.

 

2.Mawazo ya Kutosheleza.

 Hii inaweza kujumuisha wazo la kutokuwepo na hali halisi, au kutokuwa na muono sahihi wa hali halisi, yaani hawezi kuongea kitu Kwa uhalisia wake mpaka azunguke na pia anaweza akafumba au akaweka story ambayo haiko nauhalisia Kwa wakati huo Kwa ujumla sio rahisi kuwa na mawazo ya kutosheleza katika jambo fulani.

3.Hallucinations.

Hizi ni uzoefu wa kuona, kusikia, kugusa, au kuhisi mambo ambayo hayapo. Mara nyingi, watu wanashuhudia sauti zisizokuwepo.kwa mfano mnaweza kuwa na mgonjwa wa hali hiyo mmekaa akasema naoa nyoka mkubwa akaanza kukimbia,au akasema mnaningenya au mnanitukana na mambo kama hayo ambayo watu wa kawaida wenye afya ya akili huwezi kuyaona.

 

 

4 kuwepo na Delusions.

Hizi ni imani zisizo za kawaida na zisizoweza kubadilishwa. Mfano ni kudhani kuwa mtu anafuatwa au kuhitaji watu fulani kuwasaidia kwa njia zisizo za kweli.Kujitenga: Watu wenye szichophrenia wanaweza kuwa na hisia ya kujitenga kutokana na familia na marafiki, na mara nyingi wanaweza kutojihusisha na shughuli za kijamii.

5.Kutokuwepo na hisia

: Hii inaweza kujumuisha kukosa hisia ya furaha, huzuni, au hisia nyingine za kibinadamu,yaani Kwa ujumla mtu haeleweki kama amefurahi,amekasilika au kuwepo Kwa hisia yoyote,Kwa mfano akifurahi ni mda mfupi na ameacha na hisia zozote Kwa kweli hazitabiliki kwake.

: 6.kubadilikabadilika Kwa Tabia

Watu wenye ugonjwa huu wanaweza kuonyesha tabia zisizotarajiwa au za ajabu, kama vile kuzungumza na mtu ambaye hayupo, Kwa hiyo unaweza kukuta mtu yupo busy na kuongea na mtu ambaye alifariki thamani au mtu wa maana Kwa mfano unaweza kukuta mgonjwa anasema nipo naongea na kiongozi wa Nchi Sasa hivi na ukiona alivyojipanga kama anaongea nakiongozi kweli kumbe ni ugonjwa tu.

kuukosa hamu ya kushiriki shughuli za kawaida kwenye jamii.

Wanaweza kuwa na ugumu wa kujihamasisha kufanya kazi au shughuli za kawaida za kila siku Kwa sababu mara nyingi jinsi wanavyowaza wanaona ni watu wa pekee kabisa na wanastahiki kupewe Kila kitu,Kwa hiyo wanajiona hawana haha ya kufanya chochote,Kwa mfano anayejiita kiongozi wa Nchi kadri ya akili yake huyo hatutegemei kabisa kama anaweza kufanya chochote au mwingine anajiita BOT,,na mambo kama hayo yanayoweza kusababisha uvivu katika jamii.

 

8. Kuhisi sio watu wa muhimu Miongoni mwa Watu

: Wanaweza kuwa na wazo la kujiona kama miongoni mwa watu wasioeleweka au wasio na thamani,Kwa sababu mara nyingi watu hawawaelewi hali hii inatokea pale wagonjwa wa schizophrenia wanapokuwa kero katika jamii Kwa hiyo Kuna kipindi jamiii inaweza kuwatenga Kwa sababu ya halo yao halisi.

ujua dalili hizi ni muhimu kwa sababu ugonjwa wa schizophrenia unahitaji matibabu sahihi. Ikiwa unafikiri kuwa wewe au mtu unayemjua anaweza kuwa na dalili hizi, ni muhimu kutafuta msaada wa kitaalamu. Matibabu yanaweza kujumuisha dawa na terapi ya mwili na kisaikolojia..

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Salvatory image Tarehe: 1970-01-01 03:33:45 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 19

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Dalili za saratani ya mapafu

Saratani ya Mapafu ni aina ya Kansa inayoanzia kwenye mapafu. Mapafu yako ni viungo viwili vya sponji kwenye kifua chako ambavyo huchukua oksijeni unapovuta na kutoa kaboni dioksidi unapotoa nje.

Soma Zaidi...
Swali langu ni hivi ,napata maumivu kwa mbali kwenye njia za mkojo pia napoteza ham na uwezo wa kushiriki tendo la ndoa kadiri siku zinavoenda je,hizi ni dalili za tezi dume?

Hivi umeshawahikujiuliza kuhusu tezi dume. Wacha nikujuze kitu kimoja, ni kuwa tezi dume huwapata watu kuanziamiaka 40 na kuendelea. Na ifahamike kuwa tezi dume sio busha ama ngiri maji. Pia itambulikekuwa rozi dumehutibika.

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia maambukizi kwenye nephroni

Post hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye nephroni, ni njia zinazotumika kuzuia maambukizi kwenye nephroni

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa kula kupindukia

Ugonjwa wa kula kupindukia ni ugonjwa mbaya wa ulaji ambapo mara kwa mara unatumia kiasi kikubwa cha chakula na kuhisi huwezi kuacha kula.

Soma Zaidi...
Aina ya Magonjwa ya akili

Unyogovu (Depression ) ni mojawapo ya ugonjwa wa akili ambao unahusishwa na hisia za huzuni, kukosa matumaini, na kupoteza furaha au shauku katika shughuli za kila siku. Huu si tu hisia ya huzuni iliyokatisha tamaa, bali ni hali sugu inayoweza kuathiri mabadiliko ya mwili, mawazo, na tabia ya mtu. Unyogovu unaweza kutokea kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya kemikali katika ubongo, maumbile, mazingira, na matukio mbali mbali katika maisha ambayo kupelekea mgonjwa kuwa hivyo.

Soma Zaidi...
Je unaijuwa ugonjwa wa bawasiri

Katika post hii nitakwenda kukujuza kuhusu ugonjwa wa bawasiri

Soma Zaidi...
Dalili za kisukari aina ya type 2

Kisukari cha Aina ya 2, ambacho wakati mmoja kilijulikana kama Kisukari cha watu wazima au kisichotegemea insulini, ni ugonjwa sugu unaoathiri jinsi mwili wako unavyobadilisha sukari (glucose), chanzo muhimu cha nishati ya mwili wako.

Soma Zaidi...
Yajue maambukizi kwenye epididimisi kwa kitaalamu huitwa (Epididymitis)

Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye epididimisi, ni maambukizi ambayo hutokea kwenye epididimisi na kusababisha matatizo mengi.

Soma Zaidi...
NJIA ZA KUKABILIANA NA MINYOO: kuosha mikono, kuwa msafi, kuvaa viatu, maji safi, kuivisha nyama vyema

NJIA ZA KUKABILIANA NA MINYOO Kwa kuwa tumekwisha kuona namna ambavyo minyoo huenezwa, hivyo basi ni rahisi sasa kutaja namna ya kubambana na minyoo.

Soma Zaidi...
Sababu za miguu kufa ganzi.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali,za miguu kufa ganzi,ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi na walio wengi hawafahamu kabisa ni sababu zipi ambazo uleta tatizo hili.

Soma Zaidi...