Schizophrenia ni ugonjwa wa akili ambao huathiri jinsi mtu anavyofikiri, kuhisi, na kuamua. Dalili za schizophrenia zinaweza kuwa kama ifuatavyo hapo chini
1.Mawasiliano Kwa ujumla hasa kuhusu hisia zao na kutoziwasilisha Kwa mpangilio.
Watu wenye schizophrenia wanaweza kushindwa kueleweka au kuwasiliana vyema, Hii inaweza kujumuisha mambo kama kuzungumza bila mpangilio au kuacha mazungumzo,au wakati wa kuongea hawezi kuongea jambo akalimaliza vizuri hatua Kwa hatua na likaeleweka na pia hawezi kuielezea hisia yoyote aliyo nayo na ikaeleweka Kwa watu,Kwa hiyo ni vigumu kumwelewa.
2.Mawazo ya Kutosheleza.
Hii inaweza kujumuisha wazo la kutokuwepo na hali halisi, au kutokuwa na muono sahihi wa hali halisi, yaani hawezi kuongea kitu Kwa uhalisia wake mpaka azunguke na pia anaweza akafumba au akaweka story ambayo haiko nauhalisia Kwa wakati huo Kwa ujumla sio rahisi kuwa na mawazo ya kutosheleza katika jambo fulani.
3.Hallucinations.
Hizi ni uzoefu wa kuona, kusikia, kugusa, au kuhisi mambo ambayo hayapo. Mara nyingi, watu wanashuhudia sauti zisizokuwepo.kwa mfano mnaweza kuwa na mgonjwa wa hali hiyo mmekaa akasema naoa nyoka mkubwa akaanza kukimbia,au akasema mnaningenya au mnanitukana na mambo kama hayo ambayo watu wa kawaida wenye afya ya akili huwezi kuyaona.
4 kuwepo na Delusions.
Hizi ni imani zisizo za kawaida na zisizoweza kubadilishwa. Mfano ni kudhani kuwa mtu anafuatwa au kuhitaji watu fulani kuwasaidia kwa njia zisizo za kweli.Kujitenga: Watu wenye szichophrenia wanaweza kuwa na hisia ya kujitenga kutokana na familia na marafiki, na mara nyingi wanaweza kutojihusisha na shughuli za kijamii.
5.Kutokuwepo na hisia
: Hii inaweza kujumuisha kukosa hisia ya furaha, huzuni, au hisia nyingine za kibinadamu,yaani Kwa ujumla mtu haeleweki kama amefurahi,amekasilika au kuwepo Kwa hisia yoyote,Kwa mfano akifurahi ni mda mfupi na ameacha na hisia zozote Kwa kweli hazitabiliki kwake.
: 6.kubadilikabadilika Kwa Tabia
Watu wenye ugonjwa huu wanaweza kuonyesha tabia zisizotarajiwa au za ajabu, kama vile kuzungumza na mtu ambaye hayupo, Kwa hiyo unaweza kukuta mtu yupo busy na kuongea na mtu ambaye alifariki thamani au mtu wa maana Kwa mfano unaweza kukuta mgonjwa anasema nipo naongea na kiongozi wa Nchi Sasa hivi na ukiona alivyojipanga kama anaongea nakiongozi kweli kumbe ni ugonjwa tu.
kuukosa hamu ya kushiriki shughuli za kawaida kwenye jamii.
Wanaweza kuwa na ugumu wa kujihamasisha kufanya kazi au shughuli za kawaida za kila siku Kwa sababu mara nyingi jinsi wanavyowaza wanaona ni watu wa pekee kabisa na wanastahiki kupewe Kila kitu,Kwa hiyo wanajiona hawana haha ya kufanya chochote,Kwa mfano anayejiita kiongozi wa Nchi kadri ya akili yake huyo hatutegemei kabisa kama anaweza kufanya chochote au mwingine anajiita BOT,,na mambo kama hayo yanayoweza kusababisha uvivu katika jamii.
8. Kuhisi sio watu wa muhimu Miongoni mwa Watu
: Wanaweza kuwa na wazo la kujiona kama miongoni mwa watu wasioeleweka au wasio na thamani,Kwa sababu mara nyingi watu hawawaelewi hali hii inatokea pale wagonjwa wa schizophrenia wanapokuwa kero katika jamii Kwa hiyo Kuna kipindi jamiii inaweza kuwatenga Kwa sababu ya halo yao halisi.
ujua dalili hizi ni muhimu kwa sababu ugonjwa wa schizophrenia unahitaji matibabu sahihi. Ikiwa unafikiri kuwa wewe au mtu unayemjua anaweza kuwa na dalili hizi, ni muhimu kutafuta msaada wa kitaalamu. Matibabu yanaweza kujumuisha dawa na terapi ya mwili na kisaikolojia..
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyanzo m ali mbali vinavyohisiwa kuwa chanzo cha UKIMWI
Soma Zaidi...Posti hii inahusu Maambukizi kwenye tumbo na kwenye utumbo mdogo,ni Maambukizi ambayo uwa kwenye tumbo na utumbo mdogo.
Soma Zaidi...Posti hii inaonyesha mambo mbalimbali yanayoweza kusababisha Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kisukari hurejelea kundi la magonjwa yanayoathiri jinsi mwili wako unavyotumia sukari kwenye damu (glucose). Glucose ni muhimu kwa afya yako kwa sababu ni chanzo muhimu cha nishati kwa seli zinazounda misuli na tishu zako. Pia ndio chanzo ki
Soma Zaidi...Makala hii inakwenda kukupa majibu ya maswali mengi kuhusu VVU na UKIMWI. tutakwenda kuona kwa ufupi historian a chanzo cha VVU na UKIMWI. hatuwa za maambukizi ya VVU na ukimwi na dalili zake za kuonekana toka kupata maambukizi. Pia hapa utajifunza namna
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanaume
Soma Zaidi...Posti hii inahusu sababu za mwanamke kuumwa tumbo chini ya kitovu, ni tatizo ambalo limewapata wanawake wengi na pengine sababu ni vigumu kupata au pengine zinapatikana lakini kwa kuchelewa hali ambayo usababisha madhara mbalimbali kwenye mwili.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ugonjwa wa UTI
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kaswende kwa wajawazito, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa watu wote, kwa sababu ugonjwa huu una dalili ambazo upitia kwa hatua mbalimbali kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...