Dalili za ugonjwa wa schizophrenia
Schizophrenia ni ugonjwa wa akili ambao huathiri jinsi mtu anavyofikiri, kuhisi, na kuamua. Dalili za schizophrenia zinaweza kuwa kama ifuatavyo hapo chini
1.Mawasiliano Kwa ujumla hasa kuhusu hisia zao na kutoziwasilisha Kwa mpangilio.
Watu wenye schizophrenia wanaweza kushindwa kueleweka au kuwasiliana vyema, Hii inaweza kujumuisha mambo kama kuzungumza bila mpangilio au kuacha mazungumzo,au wakati wa kuongea hawezi kuongea jambo akalimaliza vizuri hatua Kwa hatua na likaeleweka na pia hawezi kuielezea hisia yoyote aliyo nayo na ikaeleweka Kwa watu,Kwa hiyo ni vigumu kumwelewa.
2.Mawazo ya Kutosheleza.
Hii inaweza kujumuisha wazo la kutokuwepo na hali halisi, au kutokuwa na muono sahihi wa hali halisi, yaani hawezi kuongea kitu Kwa uhalisia wake mpaka azunguke na pia anaweza akafumba au akaweka story ambayo haiko nauhalisia Kwa wakati huo Kwa ujumla sio rahisi kuwa na mawazo ya kutosheleza katika jambo fulani.
3.Hallucinations.
Hizi ni uzoefu wa kuona, kusikia, kugusa, au kuhisi mambo ambayo hayapo. Mara nyingi, watu wanashuhudia sauti zisizokuwepo.kwa mfano mnaweza kuwa na mgonjwa wa hali hiyo mmekaa akasema naoa nyoka mkubwa akaanza kukimbia,au akasema mnaningenya au mnanitukana na mambo kama hayo ambayo watu wa kawaida wenye afya ya akili huwezi kuyaona.
4 kuwepo na Delusions.
Hizi ni imani zisizo za kawaida na zisizoweza kubadilishwa. Mfano ni kudhani kuwa mtu anafuatwa au kuhitaji watu fulani kuwasaidia kwa njia zisizo za kweli.Kujitenga: Watu wenye szichophrenia wanaweza kuwa na hisia ya kujitenga kutokana na familia na marafiki, na mara nyingi wanaweza kutojihusisha na shughuli za kijamii.
5.Kutokuwepo na hisia
: Hii inaweza kujumuisha kukosa hisia ya furaha, huzuni, au hisia nyingine za kibinadamu,yaani Kwa ujumla mtu haeleweki kama amefurahi,amekasilika au kuwepo Kwa hisia yoyote,Kwa mfano akifurahi ni mda mfupi na ameacha na hisia zozote Kwa kweli hazitabiliki kwake.
: 6.kubadilikabadilika Kwa Tabia
Watu wenye ugonjwa huu wanaweza kuonyesha tabia zisizotarajiwa au za ajabu, kama vile kuzungumza na mtu ambaye hayupo, Kwa hiyo unaweza kukuta mtu yupo busy na kuongea na mtu ambaye alifariki thamani au mtu wa maana Kwa mfano unaweza kukuta mgonjwa anasema nipo naongea na kiongozi wa Nchi Sasa hivi na ukiona alivyojipanga kama anaongea nakiongozi kweli kumbe ni ugonjwa tu.
kuukosa hamu ya kushiriki shughuli za kawaida kwenye jamii.
Wanaweza kuwa na ugumu wa kujihamasisha kufanya kazi au shughuli za kawaida za kila siku Kwa sababu mara nyingi jinsi wanavyowaza wanaona ni watu wa pekee kabisa na wanastahiki kupewe Kila kitu,Kwa hiyo wanajiona hawana haha ya kufanya chochote,Kwa mfano anayejiita kiongozi wa Nchi kadri ya akili yake huyo hatutegemei kabisa kama anaweza kufanya chochote au mwingine anajiita BOT,,na mambo kama hayo yanayoweza kusababisha uvivu katika jamii.
8. Kuhisi sio watu wa muhimu Miongoni mwa Watu
: Wanaweza kuwa na wazo la kujiona kama miongoni mwa watu wasioeleweka au wasio na thamani,Kwa sababu mara nyingi watu hawawaelewi hali hii inatokea pale wagonjwa wa schizophrenia wanapokuwa kero katika jamii Kwa hiyo Kuna kipindi jamiii inaweza kuwatenga Kwa sababu ya halo yao halisi.
ujua dalili hizi ni muhimu kwa sababu ugonjwa wa schizophrenia unahitaji matibabu sahihi. Ikiwa unafikiri kuwa wewe au mtu unayemjua anaweza kuwa na dalili hizi, ni muhimu kutafuta msaada wa kitaalamu. Matibabu yanaweza kujumuisha dawa na terapi ya mwili na kisaikolojia..
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
WAJUE FANGASI, AINA ZAKE, DALILI ZAKE NA MATIBABU YAKE
Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili.
Soma Zaidi...Njia salama za kuongeza uwezo wa kushika mimba.
Kupata ujauzito ni safari inayohitaji maandalizi ya mwili na akili. Kwa wanandoa wengi, mabadiliko madogo lakini yenye tija katika mtindo wa maisha yanaweza kuongeza nafasi za kupata mtoto kwa kiasi kikubwa. Makala hii inaangazia mbinu zilizothibitishwa kisayansi za kuboresha afya ya uzazi na kuongeza nafasi za kushika mimba kwa njia salama na ya asili.
Soma Zaidi...ujuwe ugonjwa wa gout na athari zake mwilini
Post hii itakwenda kuzungumzia ugonjwa wa gout unaosababishwa na ongezeko la asidi mwilini.
Soma Zaidi...Je pumu inaweza kusababishwa na virusi ama bakteria?
Hapa utakwenda kujifunza jinsi ambavyo pumu inaweza kuwa na mahusiano kwa kuwepo kwa aina flani ya bakteria ama virusi.
Soma Zaidi...Dalili kuu 7 za malaria na dawa ya kutibu malaria
Makala hii itazungumzia dalili za Malaria, athari za kuchelewa kutibu malaria, na matibabu ya malaria
Soma Zaidi...Maambukizi kwenye mfumo wa usagaji chakula unaotokea kwenye utumbo mkubwa (diverticulitis)
Posti hii inazungumzia kuhusiana na mifuko midogo midogo, iliyobubujika ambayo inaweza kuunda kwenye utando wa mfumo wako wa usagaji chakula. Wao hupatikana mara nyingi katika sehemu ya chini ya utumbo mkubwa (koloni). Hali hiyo inajulikana kama Divert
Soma Zaidi...