Dalili za ugonjwa wa schizophrenia
Schizophrenia ni ugonjwa wa akili ambao huathiri jinsi mtu anavyofikiri, kuhisi, na kuamua. Dalili za schizophrenia zinaweza kuwa kama ifuatavyo hapo chini
1.Mawasiliano Kwa ujumla hasa kuhusu hisia zao na kutoziwasilisha Kwa mpangilio.
Watu wenye schizophrenia wanaweza kushindwa kueleweka au kuwasiliana vyema, Hii inaweza kujumuisha mambo kama kuzungumza bila mpangilio au kuacha mazungumzo,au wakati wa kuongea hawezi kuongea jambo akalimaliza vizuri hatua Kwa hatua na likaeleweka na pia hawezi kuielezea hisia yoyote aliyo nayo na ikaeleweka Kwa watu,Kwa hiyo ni vigumu kumwelewa.
2.Mawazo ya Kutosheleza.
Hii inaweza kujumuisha wazo la kutokuwepo na hali halisi, au kutokuwa na muono sahihi wa hali halisi, yaani hawezi kuongea kitu Kwa uhalisia wake mpaka azunguke na pia anaweza akafumba au akaweka story ambayo haiko nauhalisia Kwa wakati huo Kwa ujumla sio rahisi kuwa na mawazo ya kutosheleza katika jambo fulani.
3.Hallucinations.
Hizi ni uzoefu wa kuona, kusikia, kugusa, au kuhisi mambo ambayo hayapo. Mara nyingi, watu wanashuhudia sauti zisizokuwepo.kwa mfano mnaweza kuwa na mgonjwa wa hali hiyo mmekaa akasema naoa nyoka mkubwa akaanza kukimbia,au akasema mnaningenya au mnanitukana na mambo kama hayo ambayo watu wa kawaida wenye afya ya akili huwezi kuyaona.
4 kuwepo na Delusions.
Hizi ni imani zisizo za kawaida na zisizoweza kubadilishwa. Mfano ni kudhani kuwa mtu anafuatwa au kuhitaji watu fulani kuwasaidia kwa njia zisizo za kweli.Kujitenga: Watu wenye szichophrenia wanaweza kuwa na hisia ya kujitenga kutokana na familia na marafiki, na mara nyingi wanaweza kutojihusisha na shughuli za kijamii.
5.Kutokuwepo na hisia
: Hii inaweza kujumuisha kukosa hisia ya furaha, huzuni, au hisia nyingine za kibinadamu,yaani Kwa ujumla mtu haeleweki kama amefurahi,amekasilika au kuwepo Kwa hisia yoyote,Kwa mfano akifurahi ni mda mfupi na ameacha na hisia zozote Kwa kweli hazitabiliki kwake.
: 6.kubadilikabadilika Kwa Tabia
Watu wenye ugonjwa huu wanaweza kuonyesha tabia zisizotarajiwa au za ajabu, kama vile kuzungumza na mtu ambaye hayupo, Kwa hiyo unaweza kukuta mtu yupo busy na kuongea na mtu ambaye alifariki thamani au mtu wa maana Kwa mfano unaweza kukuta mgonjwa anasema nipo naongea na kiongozi wa Nchi Sasa hivi na ukiona alivyojipanga kama anaongea nakiongozi kweli kumbe ni ugonjwa tu.
kuukosa hamu ya kushiriki shughuli za kawaida kwenye jamii.
Wanaweza kuwa na ugumu wa kujihamasisha kufanya kazi au shughuli za kawaida za kila siku Kwa sababu mara nyingi jinsi wanavyowaza wanaona ni watu wa pekee kabisa na wanastahiki kupewe Kila kitu,Kwa hiyo wanajiona hawana haha ya kufanya chochote,Kwa mfano anayejiita kiongozi wa Nchi kadri ya akili yake huyo hatutegemei kabisa kama anaweza kufanya chochote au mwingine anajiita BOT,,na mambo kama hayo yanayoweza kusababisha uvivu katika jamii.
8. Kuhisi sio watu wa muhimu Miongoni mwa Watu
: Wanaweza kuwa na wazo la kujiona kama miongoni mwa watu wasioeleweka au wasio na thamani,Kwa sababu mara nyingi watu hawawaelewi hali hii inatokea pale wagonjwa wa schizophrenia wanapokuwa kero katika jamii Kwa hiyo Kuna kipindi jamiii inaweza kuwatenga Kwa sababu ya halo yao halisi.
ujua dalili hizi ni muhimu kwa sababu ugonjwa wa schizophrenia unahitaji matibabu sahihi. Ikiwa unafikiri kuwa wewe au mtu unayemjua anaweza kuwa na dalili hizi, ni muhimu kutafuta msaada wa kitaalamu. Matibabu yanaweza kujumuisha dawa na terapi ya mwili na kisaikolojia..
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Walio katika hatari ya kupata magonjwa ya ngono
Posti hii inahusu zaidi watu walio kwenye liski ya kupata magonjwa ya ngono, ni watu wanaofanya mambo yanayosababisha kupata magonjwa ya ngono.
Soma Zaidi...Maambukizi ya Kawaida ya zinaa (Chlamydia)
maambukizi ya kawaida ya zinaa (STI), Hujulikana Kama Chlamydia. Huenda usijue una Ugonjwa huu kwa sababu watu wengi hawapati dalili au ishara, kama vile maumivu ya sehemu za siri na kutokwa na uchafu kutoka kwa uke au uume. Maambukizi haya huathiri
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa wa Saratani ya uke
Saratani ya uke ni Saratani adimu inayotokea kwenye uke wako mrija wa misuli unaounganisha uterasi na sehemu zako za siri. Saratani ya uke mara nyingi hutokea katika seli zilizo kwenye uso wa uke wako, ambao wakati mwingine huitwa njia ya uzazi. Wan
Soma Zaidi...Koo langu limekauka yaweza kuwa ni muadhirika?
kuwashwa na koo ni katika dalili za kuwa na maambukizi mwilini. Kuwa na maambukizi haimaanishi ni HIV ama UKIMWI laa hili ni neno pana. Hapa nitakujuza kwa ufupi kuhusu swali hilo la muulizaji kuwa anawashwa na koo.
Soma Zaidi...Athari za ugonjwa wa Dondakoo
Posti hii inahusu zaidi athari za ugonjwa wa Dondakoo,hali hii utokea iwapo ugonjwa haukutibiwa mapema au umetibiwa lakini bado Kuna matokea hasi ambayo yanaweza kujitokeza kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Yajue matatizo yanayosababisha Ugonjwa wa akili.
Madhara ya ugonjwa wa akili yanaweza kuwa ya muda au ya kudumu. Unaweza pia kuwa na zaidi ya ugonjwa mmoja wa afya ya akili kwa wakati mmoja. Kwa mfano, unaweza kuwa na ulegevu na ugonjwa wa matumizi ya madawa ya kulevya.
Soma Zaidi...