picha

Huduma kwa wanawake wenye mahitaji maalum.

Posti hii inahusu huduma kwa wanawake wenye mahitaji maalum, ni wanawake ambao wana shida ya akili, walionyanyaswa kijinsia, wakimbizi na wote wenye matatizo mbalimbali.

Huduma kwa wanawake wenye matatizo mbalimbali.

1.Tunajua kuwa hawa wanawake wanahitaji uangalizi kwa karibu kwa hiyo tunapaswa kuwasaidia katika kujieleza, katika kutembea labda wengine ni walemavu, katika kujifanyia mambo ya kawaida ya usafi na namna ya kufanya usafi na katika maamuzi maana wengine wana shida ya kutoa uamuzi.

 

2.Pia inabidi kuwasaidia katika wakati uliopo kwa tatizo lililopo kwa mfano kama mama anahitaji huduma za vipimo anapaswa kusaidiwa kwa sababu wakati mwingine hawezi kufika sehemu za vipimo na kuweza kujieleza kwa hiyo anapaswa kusaidiwa na kuhakikisha kuwa anapata kila kitu anachokihitaji.

 

3.Kumsaidia Mama kujua umuhimu wa kupima virus vya ukimwi na magonjwa ya zinaa na namna ya kuzuia magonjwa hayo kwa hiyo hawa akina Mama wanapaswa kupewa elimu ili waweze kupima na kujua afya zao na kama wana Maambukizi wanapaswa kujua namna ya kuwalinda watoto wao na matumizi ya dawa za ARV.

 

4.Kuwasaidia hawa wakina Mama wenye matatizo kuchagua aina bora ya uzazi wa mpango kwa kadiri ya hali yake na kuwasaidia namna ya kutumia njia hizo na kuwa na idadi ya watoto wanaowahifadhi kwa hiyo hawa akina Mama wanapaswa kuwa na uangalizi wa karibu zaidi katika kutumia uzazi wa mpango.

 

5.Pia jamii inapaswa kuwahudumia hawa wajawazito wenye mahitaji maalum ili waweze kujifungua salama na kuepuka imani potovu ya kutoa mimba kwa wajawazito ambao wana kifafa na wenye matatizo kwa kuepuka kulea watoto wao kwa hiyo wanapaswa kutumia njia za uzazi wa mpango ili wasizae sana, kwa hiyo jamii inapaswa kuwapokea watu hawa kwa sababu nao ni binadamu wanahitaji haki zote kama walivyo binadamu wengine.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1654

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Watu walio hatarini kupata ugonjwa wa pumu

Kila mtu anaweza kupata ugonjwa wa pumu, hata hivyo kuna ambao wapo hatarini zaidi kupata pumu.

Soma Zaidi...
Vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
ninasumbuliwa Sana na mapunye ya kichwani nimetumia dawa takribani miaka 3

Habari, samahani ninasumbuliwa Sana na mapunye ya kichwani nimetumia dawa takribani miaka 3 ila yanapona Tena baada ya Muda flani yanatokea.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa Donda koo

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Donda Koo ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea viitwavyo kwa kitaalamu corynebacterium diphtheria, ugonjwa huu ushambulia Koo na unaweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa, mate na

Soma Zaidi...
Je, Fangasi Ukeni Huambukiza?

Maambukizi ya fangasi ukeni (Vaginal Thrush/Yeast Infection) ni changamoto inayowasumbua wanawake wengi, lakini bado kuna mkanganyiko mkubwa kuhusu jinsi ugonjwa huu unavyoenea. Makala haya yanachambua kiundani tabia ya fangasi hawa, kama wanaweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda mwingine, dalili zake, na ukweli wa kisayansi unaofuta dhana potofu zilizopo kwenye jamii.

Soma Zaidi...
Dalili za Kufunga kwa ulimi (tongue tie)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili za Kufunga kwa ulimi (Tongue-tie) kuanzia Mtoto anavyo zalia mpaka navyokua ni hali inayotokea wakati wa kuzaliwa ambayo kitaalamu hujulikana kama ankyloglossia.

Soma Zaidi...