Huduma kwa wanawake wenye mahitaji maalum.
Posti hii inahusu huduma kwa wanawake wenye mahitaji maalum, ni wanawake ambao wana shida ya akili, walionyanyaswa kijinsia, wakimbizi na wote wenye matatizo mbalimbali.
Huduma kwa wanawake wenye matatizo mbalimbali.
1.Tunajua kuwa hawa wanawake wanahitaji uangalizi kwa karibu kwa hiyo tunapaswa kuwasaidia katika kujieleza, katika kutembea labda wengine ni walemavu, katika kujifanyia mambo ya kawaida ya usafi na namna ya kufanya usafi na katika maamuzi maana wengine wana shida ya kutoa uamuzi.
2.Pia inabidi kuwasaidia katika wakati uliopo kwa tatizo lililopo kwa mfano kama mama anahitaji huduma za vipimo anapaswa kusaidiwa kwa sababu wakati mwingine hawezi kufika sehemu za vipimo na kuweza kujieleza kwa hiyo anapaswa kusaidiwa na kuhakikisha kuwa anapata kila kitu anachokihitaji.
3.Kumsaidia Mama kujua umuhimu wa kupima virus vya ukimwi na magonjwa ya zinaa na namna ya kuzuia magonjwa hayo kwa hiyo hawa akina Mama wanapaswa kupewa elimu ili waweze kupima na kujua afya zao na kama wana Maambukizi wanapaswa kujua namna ya kuwalinda watoto wao na matumizi ya dawa za ARV.
4.Kuwasaidia hawa wakina Mama wenye matatizo kuchagua aina bora ya uzazi wa mpango kwa kadiri ya hali yake na kuwasaidia namna ya kutumia njia hizo na kuwa na idadi ya watoto wanaowahifadhi kwa hiyo hawa akina Mama wanapaswa kuwa na uangalizi wa karibu zaidi katika kutumia uzazi wa mpango.
5.Pia jamii inapaswa kuwahudumia hawa wajawazito wenye mahitaji maalum ili waweze kujifungua salama na kuepuka imani potovu ya kutoa mimba kwa wajawazito ambao wana kifafa na wenye matatizo kwa kuepuka kulea watoto wao kwa hiyo wanapaswa kutumia njia za uzazi wa mpango ili wasizae sana, kwa hiyo jamii inapaswa kuwapokea watu hawa kwa sababu nao ni binadamu wanahitaji haki zote kama walivyo binadamu wengine.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 ai web app 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Maambukizi ya tezi za mate
Psti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa Maambukizi ya tezi za mate ambao hujulikana Kama MABUSHA (mumps) ni maambukizi ya virusi ambayo kimsingi huathiri tezi mojawapo ya jozi tatu za tezi za mate zinazotoa mate, zilizo chini na mbele ya masikio
Soma Zaidi...Aina za ajali kwenye kifua,
Post hii inahusu Zaidi aina za ajali kwenye kifua,pamoja na kifua kuwa na sehemu mbalimbali na pia na ajali ambazo utokea Huwa za aina mbalimbali kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu Ugonjwa wa pre - eclampsia
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa pre- eclampsia ni Ugonjwa ambao uwapata wanawake wajawazito uwapata pale mimba inapofikisha umri wa wiki ishilini, utokea pale ambapo Mama mjamzito huwa na kiwango kikubwa cha shinikizo la damu na pia kuwepo kwa protini
Soma Zaidi...Ishara na dalilili za Kichaa Cha mbwa
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kichaa cha mbwa ni virusi hatari vinavyoenezwa kwa watu kutoka kwa mate ya wanyama walioambukizwa. Virusi vya kichaa cha mbwa kawaida hupitishwa kwa kuuma.
Soma Zaidi...Njia za kuzuia uwepo wa ugonjwa wa Bawasili.
Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii, hizi ni njia za awali za kupambana na kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.
Soma Zaidi...