picha

Aina za swala..

Nguzo za uislamu,aina za swala (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Rejea Kitabu cha 1, EDK, Shule za Sekondari, Uk. 150-165.

Swala za Sunnah ni nyingi, tutaangalia baadhi tu kama ifuatavyo:

 

  1. Swala ya Maamkizi ya Msikiti.

-    Huswaliwa rakaa mbili muda wowote mara tu muislamu aingiapo msikitini kabla ya kukaa.

   

  1. Swala za Qabiliyyah na Ba’adiyyah.

      -    Hizi huswaliwa kabla (Qabiliyyah) na Baada (Ba’adiyyah) ya swala za Faradh.

      -    Ziko aina mbili; ‘Mu’akkadah’ (zilizokokotezwa) na ‘Ghairu Mu’akkadah’ (Hazikukokotezwa).

    Rejea Kitabu cha 1, EDK, Shule za Sekondari, Uk. 152.

 

  1. Swala ya Witiri.

-    Huswaliwa rakaa kwa idadi ya witiri; 1, 3, 5, 7, 9 na 11 katika theluthi ya mwisho wa usiku au mara tu baada ya swala ya Ishaa.

      -    Witiri imekokotezwa mwisho wa usiku zaidi na huambatanishwa kwa dua ya Qunuti katika rakaa ya mwisho.

 

  1. Swala ya Tahajjud (Qiyaamul-layl).

-    Huswaliwa rakaa 8 usiku wa manane kwa rakaa mbili mbili na kumalia 3 za witiri na kutimia rakaa 11. 

-    Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu cha Qur’an.

    Rejea Qur’an (17:79), (25:64), (39:9) na (73:1-4).

 

  1. Swala ya Tarawehe (Qiyaamu Ramadhan).

-    Ni swala ya kisimamo na Kisomo kirefu cha Qur’an, Juzuu 1 kila siku inayoswaliwa mwezi wa Ramadhani tu baada ya Ishaa au kabla ya swala ya Alfajir.

-    Kuna hitilafu kwa idadi ya rakaa, kauli zinasema ni rakaa 8, 11, 20, 36, n.k.lakini yenye nguvu ni rakaa 8 na 3 za witiri na kuwa jumla rakaa 11. 

 

  1. Swala ya Idil-Fitr na Al-Udhuhaa.

-    Zote huswaliwa rakaa mbili, Idil-Fitr huswaliwa mwezi 1 Shawwal baada ya kumalizika funga ya mwezi wa Ramadhani.

-    Idil-Al-Udhuhaa huswaliwa mwezi 10 Dhul-Hija baada ya kukamilika ibada ya Hija kila mwaka.

 

  1. Swalatudh-Dhuhaa.

-    Huswaliwa kila siku baada ya Jua kupanda kiasi cha mita tatu kutoka kuchomoza kwake.

-    Huswaliwa rakaa mbili mbili hadi kutimia nane, lakini kwa uchache huswaliwa rakaa mbili.

 

  1. Swalatul-Istikharah.

-    Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada na mwongozo kwa Allah juu ya uamuzi au utatuzi wa jambo lolote zuri.

 

  1. Swala ya Kukidhi Haja.

-    Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada au utatuzi wa tatizo lililotokea au unalohitajia.

 

  1. Swalatut – Tawbah.

-    Huswaliwa rakaa mbili muda wowote kwa ajili ya kutubia baada ya muislamu kufanya kosa.

    Rejea Qur’an (3:135-136).

 

  1. Swala ya Kupatwa kwa Jua na Mwezi.

-    Huswaliwa kwa jamaa, rakaa mbili, rukuu mbili kwa kila rakaa moja. Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu mpaka Kupatwa kuondoke. 

 

  1. Swala ya Kuomba (Swalatul-Istisqaa).

-    Ni swala ya rakaa mbili kwa ajili ya kuomba mvua baada ya kuzidi dhiki na ukame, kwa jamaa na uwanjani.

-    Swala hii ina khutuba mbili na takbira kama inavyoswaliwa swala za Idi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 2920

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 web hosting     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Hadathi ya kati na kati

Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maswali juu ya haki na uadilifu katika uislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3:Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...