Nguzo za uislamu,aina za swala (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Rejea Kitabu cha 1, EDK, Shule za Sekondari, Uk. 150-165.
Swala za Sunnah ni nyingi, tutaangalia baadhi tu kama ifuatavyo:
- Huswaliwa rakaa mbili muda wowote mara tu muislamu aingiapo msikitini kabla ya kukaa.
- Hizi huswaliwa kabla (Qabiliyyah) na Baada (Ba’adiyyah) ya swala za Faradh.
- Ziko aina mbili; ‘Mu’akkadah’ (zilizokokotezwa) na ‘Ghairu Mu’akkadah’ (Hazikukokotezwa).
Rejea Kitabu cha 1, EDK, Shule za Sekondari, Uk. 152.
- Huswaliwa rakaa kwa idadi ya witiri; 1, 3, 5, 7, 9 na 11 katika theluthi ya mwisho wa usiku au mara tu baada ya swala ya Ishaa.
- Witiri imekokotezwa mwisho wa usiku zaidi na huambatanishwa kwa dua ya Qunuti katika rakaa ya mwisho.
- Huswaliwa rakaa 8 usiku wa manane kwa rakaa mbili mbili na kumalia 3 za witiri na kutimia rakaa 11.
- Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu cha Qur’an.
Rejea Qur’an (17:79), (25:64), (39:9) na (73:1-4).
- Ni swala ya kisimamo na Kisomo kirefu cha Qur’an, Juzuu 1 kila siku inayoswaliwa mwezi wa Ramadhani tu baada ya Ishaa au kabla ya swala ya Alfajir.
- Kuna hitilafu kwa idadi ya rakaa, kauli zinasema ni rakaa 8, 11, 20, 36, n.k.lakini yenye nguvu ni rakaa 8 na 3 za witiri na kuwa jumla rakaa 11.
- Zote huswaliwa rakaa mbili, Idil-Fitr huswaliwa mwezi 1 Shawwal baada ya kumalizika funga ya mwezi wa Ramadhani.
- Idil-Al-Udhuhaa huswaliwa mwezi 10 Dhul-Hija baada ya kukamilika ibada ya Hija kila mwaka.
- Huswaliwa kila siku baada ya Jua kupanda kiasi cha mita tatu kutoka kuchomoza kwake.
- Huswaliwa rakaa mbili mbili hadi kutimia nane, lakini kwa uchache huswaliwa rakaa mbili.
- Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada na mwongozo kwa Allah juu ya uamuzi au utatuzi wa jambo lolote zuri.
- Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada au utatuzi wa tatizo lililotokea au unalohitajia.
- Huswaliwa rakaa mbili muda wowote kwa ajili ya kutubia baada ya muislamu kufanya kosa.
Rejea Qur’an (3:135-136).
- Huswaliwa kwa jamaa, rakaa mbili, rukuu mbili kwa kila rakaa moja. Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu mpaka Kupatwa kuondoke.
- Ni swala ya rakaa mbili kwa ajili ya kuomba mvua baada ya kuzidi dhiki na ukame, kwa jamaa na uwanjani.
- Swala hii ina khutuba mbili na takbira kama inavyoswaliwa swala za Idi.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Hapa utajifunza nguzo kuu za swaumu. Kama hazitatimia nguzo hizi basi swaumu itakuwa ni batili.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir
Soma Zaidi...Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ya haramu kwa mwenye hadathi kubwa
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf
Soma Zaidi...Kuingizwa au Kutolewa EdaKatika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh.
Soma Zaidi...