Aina za swala..

Aina za swala..

Nguzo za uislamu,aina za swala (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Rejea Kitabu cha 1, EDK, Shule za Sekondari, Uk. 150-165.

Swala za Sunnah ni nyingi, tutaangalia baadhi tu kama ifuatavyo:

 

  1. Swala ya Maamkizi ya Msikiti.

-    Huswaliwa rakaa mbili muda wowote mara tu muislamu aingiapo msikitini kabla ya kukaa.

   

  1. Swala za Qabiliyyah na Ba’adiyyah.

      -    Hizi huswaliwa kabla (Qabiliyyah) na Baada (Ba’adiyyah) ya swala za Faradh.

      -    Ziko aina mbili; ‘Mu’akkadah’ (zilizokokotezwa) na ‘Ghairu Mu’akkadah’ (Hazikukokotezwa).

    Rejea Kitabu cha 1, EDK, Shule za Sekondari, Uk. 152.

 

  1. Swala ya Witiri.

-    Huswaliwa rakaa kwa idadi ya witiri; 1, 3, 5, 7, 9 na 11 katika theluthi ya mwisho wa usiku au mara tu baada ya swala ya Ishaa.

      -    Witiri imekokotezwa mwisho wa usiku zaidi na huambatanishwa kwa dua ya Qunuti katika rakaa ya mwisho.

 

  1. Swala ya Tahajjud (Qiyaamul-layl).

-    Huswaliwa rakaa 8 usiku wa manane kwa rakaa mbili mbili na kumalia 3 za witiri na kutimia rakaa 11. 

-    Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu cha Qur’an.

    Rejea Qur’an (17:79), (25:64), (39:9) na (73:1-4).

 

  1. Swala ya Tarawehe (Qiyaamu Ramadhan).

-    Ni swala ya kisimamo na Kisomo kirefu cha Qur’an, Juzuu 1 kila siku inayoswaliwa mwezi wa Ramadhani tu baada ya Ishaa au kabla ya swala ya Alfajir.

-    Kuna hitilafu kwa idadi ya rakaa, kauli zinasema ni rakaa 8, 11, 20, 36, n.k.lakini yenye nguvu ni rakaa 8 na 3 za witiri na kuwa jumla rakaa 11. 

 

  1. Swala ya Idil-Fitr na Al-Udhuhaa.

-    Zote huswaliwa rakaa mbili, Idil-Fitr huswaliwa mwezi 1 Shawwal baada ya kumalizika funga ya mwezi wa Ramadhani.

-    Idil-Al-Udhuhaa huswaliwa mwezi 10 Dhul-Hija baada ya kukamilika ibada ya Hija kila mwaka.

 

  1. Swalatudh-Dhuhaa.

-    Huswaliwa kila siku baada ya Jua kupanda kiasi cha mita tatu kutoka kuchomoza kwake.

-    Huswaliwa rakaa mbili mbili hadi kutimia nane, lakini kwa uchache huswaliwa rakaa mbili.

 

  1. Swalatul-Istikharah.

-    Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada na mwongozo kwa Allah juu ya uamuzi au utatuzi wa jambo lolote zuri.

 

  1. Swala ya Kukidhi Haja.

-    Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada au utatuzi wa tatizo lililotokea au unalohitajia.

 

  1. Swalatut – Tawbah.

-    Huswaliwa rakaa mbili muda wowote kwa ajili ya kutubia baada ya muislamu kufanya kosa.

    Rejea Qur’an (3:135-136).

 

  1. Swala ya Kupatwa kwa Jua na Mwezi.

-    Huswaliwa kwa jamaa, rakaa mbili, rukuu mbili kwa kila rakaa moja. Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu mpaka Kupatwa kuondoke. 

 

  1. Swala ya Kuomba (Swalatul-Istisqaa).

-    Ni swala ya rakaa mbili kwa ajili ya kuomba mvua baada ya kuzidi dhiki na ukame, kwa jamaa na uwanjani.

-    Swala hii ina khutuba mbili na takbira kama inavyoswaliwa swala za Idi.

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2124

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Nguzo za swaumu (kufinga)
Nguzo za swaumu (kufinga)

Hapa utajifunza nguzo kuu za swaumu. Kama hazitatimia nguzo hizi basi swaumu itakuwa ni batili.

Soma Zaidi...
Swala ya idil fitir na idil haji nanjinsi ya kuziswali
Swala ya idil fitir na idil haji nanjinsi ya kuziswali

Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir

Soma Zaidi...
Sanda ya mtoto
Sanda ya mtoto

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mwenye hadathi kubwa.
Yaliyo haramu kwa mwenye hadathi kubwa.

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ya haramu kwa mwenye hadathi kubwa

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf

Soma Zaidi...
Je inafaha kuingizwa eda na kutolewa?
Je inafaha kuingizwa eda na kutolewa?

Kuingizwa au Kutolewa EdaKatika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh.

Soma Zaidi...