Rangi za majimaji yanayotoka kwenye uke na maana yake kiafya

Rangi za majimaji yanayotoka kwenye uke na maana yake kiafya

Je unajuwa kuwa majimaji yanayotoka ukeni yanatueleza mengi kuhusu afya yako, rangi za majimaji ya ukeni na damu ya hedhi

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Rangi za majimaji yanayotoka kwenye uke na maana yake kiafya

/p>

RANGI ZA MAJIMAJI YANAYOTOKA KWENYE UKE NA MAANA YAKE KIAFYA


Majimaji yanayotoka kwenye uke ikiwemo damu ya hedhi kitaalamu yanajulikana kama vaginal discharge yanaweza kuwa na rangi mbalimbali unaweza pia kujiuliza lamda utakuwa unaumwa, kwani muda mwingine unaweza kuona yanatoka yakiwa na rangi ya tofauti kabisa. Kama ulivyo mkojo hubadili rang halikadhalika hata majimaji yanayotoka ukeni huweza kubadili. Makala hii itakwenda kukueleza maana za kiafya kutokana na rangi za majimaji haya:-


Majimaji haya yana umuhimu mkubwa sana katika kulinda afya ya mwanamke na ujauzito. Miongoni mwa kazi zake ni:-
1.kuondoa uchafu mwilini mwa mwanamke
2.Kuondoa seli zilizokufa mwilini
3.Kulinda mimba dhidi ya bakteria, fangasi na virusi
4.Kulinda mwili wa mwanamke dhidi ya vimelea vya maradhi visiingie kwenye mfumo wa kizazi kwa kupitia ukeni
5.Kuweka mfumo wa kizazi katika usalama na ubora wake.


Kiasi cha majimaji yanayotoka ukei huweza kutofautiana kwa rangi kulingana na siku katika mzunguruko wake wa hedhi. Kwa mfano:-


1.siku ya 1 - 5 hapa ni mwanzo wa hedhi, kwa mwanake aliye katika umri wa kupata hedhi majimaji yanayotoka kwenye uke wake yatakuwa ni mekundu ama yenye damu.
2.Siku ya 6 - 14 hii ni baada ya kukata kwa hedhi, hapa mwanamke hataona majimaji mengi kwenye uke kwake. Ila kadiri siku zinavyoenda yataanza kubadilika na kuwa kama mawingu ama rangi nyeupe pia yanaweza kuwa na rangi ya nnjano na kunatanata.
3.Siku ya 14 - 25 hapa yai linakuwa limesha toka, hivyo majimaji yanaanza kuwa na utelezi mwingi na kufanana na yale majimai meupe ya yai baada ya kulivunja. Na baada yamuda yanarudi kuwa na mawingu, meupe ama njano.
4.Siku ya 25 - 28 majimaji haya ytakuwa mepesi sana na ni machache sana.


Ok tumeshaona mabadiliko hayo ya majimaji yanavyobadilika kulingana na siku. Sasa hebu tuone babadiliko haya ra angi yanatuambia nini kiafya:-


1.rangi nyekundu:-
Hii ni damu ya hedhi, mara nyingi damu hii inakuwa ni anga’vu na yenye kufanana na rangi ya kutu. Hii ni kawaida kwa wanawake wote hivyo inaashiria afya ya kawaida. Na endapo itatoka kwa siku nyingi zaidi ya wiki, kiafya haionyeshi usalama. Ni vyema kumuona daktari aliye karibu nawe.


2.rangi nyeupe
Majimaji meupe yaaweza kuwa na rangi kama ya cream ama njano iliyo pauka. Kama mwanamke hana dalili zozote basi rangi hii inaonyeka mwanamke huyo yupo katika afya njema.


Hata hivyo ikiwa majimaji haya ni meupe na yameshikamana kama maziwa ya mgando au yakiwa yana harufu kali inaweza kuashiria kuna maambukizi ya vimelea vya maradhi kama fangasi na bakteria.


Ila kwa mara nyingi majimaji meupe yakiwa mazito, yana harufu kali hali hii inahusiana na maambukizi ya fangasi. Hali hii inaweza kusababisha miwasho.


3.Rangi ya ngajo na kijani
Kama majmaji haya yana rangi ya njano huenda hakuna tatizo ila yakiwa ni njano iliyowiva ama njano iliyona ukijani ama majimaji haya yakiwa ni ya kijani hii huashiria maambukizi ya bakteria ama magonjwa ya zinaa, fika kituo cha afya kama yatakuwa yanatoa harufu mbaya.


4.rangi ya kahawiya
Majimaji ya rangi hii yanakuwa na damu kwa mbali. Hali hii ni kawaida kama itatokea siku chache kabla ya kuingia hedhi. Pia inaweza kuashiria mimba changa. Na majimaji haya yatakuwa yanatokea baada ya kukutana kimwili, hii inaashiria kuwa kuna michubuko imetokea kwenye uke na kusababisha mipasuko midogo iliyokuwa ikivija damu..


5.majimaji yaliyo safi.
Katika hali ya kawaida majimaji yanayotoka ukeni yana kuwa ni safi na yenye weupe na yenye kuteleza kama vile majimaji meupe yanayotoka baada ya kupasua yai.


6.rangi ya kijivu
Majimaji ya rangi ya ijivu sio ya kawaida hivyo yanaashiria kuwa kuna sida katika afya ya mwanamke na mara nyingi ji maambukizi ya bakteria wanotambulika kama bacterial vaginosis. Dalil nyingine za baktera hawa bi:-
1.Maumivu
2.Miwasho
3.Harufu mbaya
4.Kuwa na wekundu kuzunguka mashavu ya uke na kwenye mlango wa uke.




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 7694

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Dawa ya kiungulia na njia za kuzuia kiungulia
Dawa ya kiungulia na njia za kuzuia kiungulia

utajifunza njia za kuzuia kiungulia, dalili za kiungulia na dawa ya kutibu kiungulia.

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kunywa aji ya moto wakati wa asubuhi
Faida za kiafya za kunywa aji ya moto wakati wa asubuhi

Katika makala hii tutakwenda kujufunza faida za kiafya zinazopatuikana kwa kunywa maji yamoti wakati wa asubuhi

Soma Zaidi...
Faida za kula Nazi
Faida za kula Nazi

Nazi ni katika matunda bora sana kiafya, Soma faida zake kwa afya yako

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula uyoga
Faida za kiafya za kula uyoga

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula uyoga

Soma Zaidi...
Faida za kungumanga/nutmeg
Faida za kungumanga/nutmeg

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula kungumanga

Soma Zaidi...
Nini maana ya protini
Nini maana ya protini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya protini

Soma Zaidi...
Faida za kula Nanasi
Faida za kula Nanasi

Nanasi ni katika matunda matamu lakini mazuri pia kiafya, je unazijuwa faida zake kiafya

Soma Zaidi...
Faida za kula Zaituni
Faida za kula Zaituni

Matunda ya zamani, matunda ya asili, Zaituni tunda lipendezalo, zijuwe faida zake leo

Soma Zaidi...
vitamini B na makundi yake
vitamini B na makundi yake

Makala hii inakwenda kukuletea kazi za vitamini B, pia tutajwenda kuona makundi ya vitamini B na kazi za kila kundi. Pia makala hii inakwenda kukufundisha vyanzo na vyakula vya vitamini B. Utajifunza pia kazi kuu za vitamini B kw

Soma Zaidi...