Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.
5.2 .Lengo la Kuumbwa mwaanadamu.
- Ni kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) katika kila kipengele cha maisha ya kila siku ya kibinafsi, kifamilia na kijamii.
“Sikuwaumba Majini na Binaadamu ila wapate kuniabudu” (51:56).
- Mwanaadamu yeyote anayetambua lengo hili, na kuishi kwa mujibu wa lengo ndiye mwenye akili.
Rejea Qur’an (3:190-191).
- Kunasibisha ibada maalumu kama ndio lengo kuu la kuumbwa mwanaadamu sio sahihi kwani kila ibada maalumu ina lengo lake maalumu na pia utekelezaji wake ni sehemu ndogo sana katika kumuabudu Allah (s.w).
- Kwa mfano; shahada ina 0%, swala 7% , zaka 2½%, swaum 5% na hija 0% ikiwa ni jumla ya 3% ya utekelezaji wa nguzo zote 5 za Uislamu ndio ziko katika ibada na 97% ni nje ya ibada.
- Hivyo, lengo la kuumbwa mwanaadamu litafikiwa tu kwa kufanya ibada masaa 24 katika kila kipengele cha maisha na sio baadhi ya vitendo fulani tu.
Rejea Qur’an (2:208), (3:102).
- Ni kumtumikia mwanaadamu ili kufikia lengo la kuumbwa kwake kwa kuboresha maisha yake.
- Maumbile na viumbe vyote vinavyomzunguka mwanaadamu vimetiishwa kwake ili aweze kuvitumia katika kutekeleza ibada.
Rejea Qur’an (45:13).
- Akili, elimu, fani, ujuzi na vipawa vya mwanaadamu ndio nyenzo zitakazomuwezesha kuyamiki na kuyamudu mazingira yake na kuendesha ibada ipasavyo.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Ni nini maana ya Elimu na ni nani aliye elimika? Uislamu una mtazamo gani juu ya Elimu?
Soma Zaidi...“Basi vyote hivi mlivyopewa ni starehe ya maisha ya dunia tu, lakini kilicho kwa Mwenyezi Mungu ni bora na cha kudumu (milele).
Soma Zaidi...Waumini wa kweli wa Mitume wa Allah (s.
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi tutajifunza mitazamo ya kikafiri juu ya dini.
Soma Zaidi...Zifuatazo ni njia nyingi za kumjua Mwenyezi Mungu (EDK form 2:dhana ya elimu katika uislamu)
Soma Zaidi...(i) Kutiishiwa Upepo Qur'an inatufahamisha kuwa Nabii Sulaiman alitiishiwa upepo akaweza kuutumia apendavyo kwa amri yake.
Soma Zaidi...