picha

Lengo la kuumbwa Mwanadamu ni lipi?

Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.

5.2 .Lengo la Kuumbwa mwaanadamu.

-     Ni kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) katika kila kipengele cha maisha ya kila siku ya kibinafsi, kifamilia na kijamii.

      “Sikuwaumba Majini na Binaadamu ila wapate kuniabudu” (51:56).

 

-     Mwanaadamu yeyote anayetambua lengo hili, na kuishi kwa mujibu wa lengo ndiye mwenye akili.

      Rejea Qur’an (3:190-191).

 

-     Kunasibisha ibada maalumu kama ndio lengo kuu la kuumbwa mwanaadamu sio sahihi kwani kila ibada maalumu ina lengo lake maalumu na pia utekelezaji wake ni sehemu ndogo sana katika kumuabudu Allah (s.w).

 

-     Kwa mfano; shahada ina 0%, swala 7% , zaka 2½%, swaum 5% na hija 0% ikiwa ni jumla ya 3% ya utekelezaji wa nguzo zote 5 za Uislamu ndio ziko katika ibada na 97% ni nje ya ibada.

 

-     Hivyo, lengo la kuumbwa mwanaadamu litafikiwa tu kwa kufanya ibada masaa 24 katika kila kipengele cha maisha na sio baadhi ya vitendo fulani tu.

      Rejea Qur’an (2:208), (3:102).

 

 

-     Ni kumtumikia mwanaadamu ili kufikia lengo la kuumbwa kwake kwa kuboresha maisha yake.

 

-     Maumbile na viumbe vyote vinavyomzunguka mwanaadamu vimetiishwa kwake ili aweze kuvitumia katika kutekeleza ibada.

      Rejea Qur’an (45:13).

 

-     Akili, elimu, fani, ujuzi na vipawa vya mwanaadamu ndio nyenzo zitakazomuwezesha kuyamiki na kuyamudu mazingira yake na kuendesha ibada ipasavyo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 6677

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 web hosting     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Elimu yenye manufaa

Elimu yenye manufaa Ni ipi? (EDK form 1:elimu yenye manufaa)

Soma Zaidi...
Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil

Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.

Soma Zaidi...
Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa

Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...