picha

Lengo la kuumbwa Mwanadamu ni lipi?

Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.

5.2 .Lengo la Kuumbwa mwaanadamu.

-     Ni kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) katika kila kipengele cha maisha ya kila siku ya kibinafsi, kifamilia na kijamii.

      “Sikuwaumba Majini na Binaadamu ila wapate kuniabudu” (51:56).

 

-     Mwanaadamu yeyote anayetambua lengo hili, na kuishi kwa mujibu wa lengo ndiye mwenye akili.

      Rejea Qur’an (3:190-191).

 

-     Kunasibisha ibada maalumu kama ndio lengo kuu la kuumbwa mwanaadamu sio sahihi kwani kila ibada maalumu ina lengo lake maalumu na pia utekelezaji wake ni sehemu ndogo sana katika kumuabudu Allah (s.w).

 

-     Kwa mfano; shahada ina 0%, swala 7% , zaka 2½%, swaum 5% na hija 0% ikiwa ni jumla ya 3% ya utekelezaji wa nguzo zote 5 za Uislamu ndio ziko katika ibada na 97% ni nje ya ibada.

 

-     Hivyo, lengo la kuumbwa mwanaadamu litafikiwa tu kwa kufanya ibada masaa 24 katika kila kipengele cha maisha na sio baadhi ya vitendo fulani tu.

      Rejea Qur’an (2:208), (3:102).

 

 

-     Ni kumtumikia mwanaadamu ili kufikia lengo la kuumbwa kwake kwa kuboresha maisha yake.

 

-     Maumbile na viumbe vyote vinavyomzunguka mwanaadamu vimetiishwa kwake ili aweze kuvitumia katika kutekeleza ibada.

      Rejea Qur’an (45:13).

 

-     Akili, elimu, fani, ujuzi na vipawa vya mwanaadamu ndio nyenzo zitakazomuwezesha kuyamiki na kuyamudu mazingira yake na kuendesha ibada ipasavyo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021/12/26/Sunday - 01:04:54 am Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 6479

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 web hosting    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Nafasi ya Elimu katika uislamu

Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu.

Soma Zaidi...
jamii muongozo

Haja ya Mwongozo kutoka kwa Allah (s.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kula mali ya Yatima

Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).

Soma Zaidi...
Maswali juu ya mtazamo wa uislamu kuhusu dini

Mtazamo wa uislamu kuhusu dini (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab

Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa

Soma Zaidi...