Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.
5.2 .Lengo la Kuumbwa mwaanadamu.
- Ni kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) katika kila kipengele cha maisha ya kila siku ya kibinafsi, kifamilia na kijamii.
“Sikuwaumba Majini na Binaadamu ila wapate kuniabudu” (51:56).
- Mwanaadamu yeyote anayetambua lengo hili, na kuishi kwa mujibu wa lengo ndiye mwenye akili.
Rejea Qur’an (3:190-191).
- Kunasibisha ibada maalumu kama ndio lengo kuu la kuumbwa mwanaadamu sio sahihi kwani kila ibada maalumu ina lengo lake maalumu na pia utekelezaji wake ni sehemu ndogo sana katika kumuabudu Allah (s.w).
- Kwa mfano; shahada ina 0%, swala 7% , zaka 2½%, swaum 5% na hija 0% ikiwa ni jumla ya 3% ya utekelezaji wa nguzo zote 5 za Uislamu ndio ziko katika ibada na 97% ni nje ya ibada.
- Hivyo, lengo la kuumbwa mwanaadamu litafikiwa tu kwa kufanya ibada masaa 24 katika kila kipengele cha maisha na sio baadhi ya vitendo fulani tu.
Rejea Qur’an (2:208), (3:102).
- Ni kumtumikia mwanaadamu ili kufikia lengo la kuumbwa kwake kwa kuboresha maisha yake.
- Maumbile na viumbe vyote vinavyomzunguka mwanaadamu vimetiishwa kwake ili aweze kuvitumia katika kutekeleza ibada.
Rejea Qur’an (45:13).
- Akili, elimu, fani, ujuzi na vipawa vya mwanaadamu ndio nyenzo zitakazomuwezesha kuyamiki na kuyamudu mazingira yake na kuendesha ibada ipasavyo.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Hili ni swali kutoka katika maarifa ya elimu ya dini ya kiislamu kidato cha kwanza (EDK FORM 1)
Soma Zaidi...“Basi vyote hivi mlivyopewa ni starehe ya maisha ya dunia tu, lakini kilicho kwa Mwenyezi Mungu ni bora na cha kudumu (milele).
Soma Zaidi...Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Ukizingatia maana halisi ya dini, kuwa dini ni utaratibu wa maisha, utadhihirikiwa kuwa umbile la mwanaadamu ni la kidini.
Soma Zaidi...Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?
Soma Zaidi...