Zoezi la 6 kusimamisha swala
Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala.
Zoezi la 6.1
2.(a) Tofautisha kati ya ‘kuswali’ na ‘kusimamisha swala’
(b) Ni upi umuhimu wa kusimamisha swala katika Uislamu?
3.(a) Nini maana ya ‘twahara’ kilugha na kifiqih.
(b) Bainisha makundi ya maji yanayotumika kujitwaharishia.
(c) Orodhesha mambo yanayoweza kuharibu maji machache kutofaa kujitwaharishia.
4.(a) Toa maelezo mafupi juu ya
(i) maji safi (ii) udongo safi (iii) najisi (iv) hadathi
(b) Taja mgawanyo wa najisi na namna ya kujitwaharisha kwa kila aina ya najisi
5.Bainisha kati ya najisi kubwa na najisi ndogo.
- najisi hafifu na najisi ndogo.
- Maji makombo na maji mutlaq
(b) (i) Eleza maana ya hadathi.
(ii) Bainisha mgawanyo wa hadathi na namna (jinsi) ya kujitwaharisha kwazo.
6.(a) Kwa kutumia ushahidi wa aya, orodhesha nguzo za udhu.
(b) Eleza maana ya
(i) Tayammamu (ii) Qibla
(c) Eleza hatua kwa hatua namna ya
(i) kutia udhu (ii) kutayammamu
(iii) kujitwaharisha kutokana na hadath kubwa (janaba).
7.(a) Bainisha mambo yanayotengua udhu.
(b) Taja nguzo na masharti za tayammamu
8.Ainisha mipaka ya sitara ya mwanamume na mwanamke kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah.
9.(a) Taja nyakati zilizoharamishwa kuswali
(b) Tofautisha kati ya ‘adhana’ na ‘iqama’
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Mwenendo wa mwenye kunuia hijjah na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Mafungu ya urithi katika uislamu
Hspa utajifunza viwango maalumu vya kutithi mirathi ys kiislamu.
Soma Zaidi...Ni upi umuhimu wa kufunga katika uislamu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kufunga kiroho, kiafya na kijamii.
Soma Zaidi...Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba
Uislamu umekataza tabia ya kuombaomba kama ndio njia ya kuendesha maisha. Pia ukaweka suluhisho la kukomesha tabia hiyo
Soma Zaidi...