Zoezi la 6 kusimamisha swala
Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala.
Zoezi la 6.1
2.(a) Tofautisha kati ya ‘kuswali’ na ‘kusimamisha swala’
(b) Ni upi umuhimu wa kusimamisha swala katika Uislamu?
3.(a) Nini maana ya ‘twahara’ kilugha na kifiqih.
(b) Bainisha makundi ya maji yanayotumika kujitwaharishia.
(c) Orodhesha mambo yanayoweza kuharibu maji machache kutofaa kujitwaharishia.
4.(a) Toa maelezo mafupi juu ya
(i) maji safi (ii) udongo safi (iii) najisi (iv) hadathi
(b) Taja mgawanyo wa najisi na namna ya kujitwaharisha kwa kila aina ya najisi
5.Bainisha kati ya najisi kubwa na najisi ndogo.
- najisi hafifu na najisi ndogo.
- Maji makombo na maji mutlaq
(b) (i) Eleza maana ya hadathi.
(ii) Bainisha mgawanyo wa hadathi na namna (jinsi) ya kujitwaharisha kwazo.
6.(a) Kwa kutumia ushahidi wa aya, orodhesha nguzo za udhu.
(b) Eleza maana ya
(i) Tayammamu (ii) Qibla
(c) Eleza hatua kwa hatua namna ya
(i) kutia udhu (ii) kutayammamu
(iii) kujitwaharisha kutokana na hadath kubwa (janaba).
7.(a) Bainisha mambo yanayotengua udhu.
(b) Taja nguzo na masharti za tayammamu
8.Ainisha mipaka ya sitara ya mwanamume na mwanamke kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah.
9.(a) Taja nyakati zilizoharamishwa kuswali
(b) Tofautisha kati ya ‘adhana’ na ‘iqama’
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina ๐2 Simulizi za Hadithi Audio ๐3 Kitabu cha Afya ๐4 Madrasa kiganjani ๐5 kitabu cha Simulizi ๐6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Maana ya swala
Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno ยSwalaatย lina maana ya ยombi au ยdua.
Soma Zaidi...