Zoezi la 6 kusimamisha swala
Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala.
Zoezi la 6.1
2.(a) Tofautisha kati ya ‘kuswali’ na ‘kusimamisha swala’
(b) Ni upi umuhimu wa kusimamisha swala katika Uislamu?
3.(a) Nini maana ya ‘twahara’ kilugha na kifiqih.
(b) Bainisha makundi ya maji yanayotumika kujitwaharishia.
(c) Orodhesha mambo yanayoweza kuharibu maji machache kutofaa kujitwaharishia.
4.(a) Toa maelezo mafupi juu ya
(i) maji safi (ii) udongo safi (iii) najisi (iv) hadathi
(b) Taja mgawanyo wa najisi na namna ya kujitwaharisha kwa kila aina ya najisi
5.Bainisha kati ya najisi kubwa na najisi ndogo.
- najisi hafifu na najisi ndogo.
- Maji makombo na maji mutlaq
(b) (i) Eleza maana ya hadathi.
(ii) Bainisha mgawanyo wa hadathi na namna (jinsi) ya kujitwaharisha kwazo.
6.(a) Kwa kutumia ushahidi wa aya, orodhesha nguzo za udhu.
(b) Eleza maana ya
(i) Tayammamu (ii) Qibla
(c) Eleza hatua kwa hatua namna ya
(i) kutia udhu (ii) kutayammamu
(iii) kujitwaharisha kutokana na hadath kubwa (janaba).
7.(a) Bainisha mambo yanayotengua udhu.
(b) Taja nguzo na masharti za tayammamu
8.Ainisha mipaka ya sitara ya mwanamume na mwanamke kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah.
9.(a) Taja nyakati zilizoharamishwa kuswali
(b) Tofautisha kati ya ‘adhana’ na ‘iqama’
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Vipi utapata uchamungu kupitia funga
Vipi lengo la funga litafikiwa na kumfanya mfungaji awe mchamungu.
Soma Zaidi...Taratibu za kumiliki hisa na mali ya shirika
Katika Uislamu kuwa na hisa kwenye mali inaruhusiwa. Hapa utajifunza taratibu za kumiliki hisa.
Soma Zaidi...