Changamoto za kwenye ndoa kwa waliotoa mimba mara Kwa mara
Posti hii inahusu zaidi changamoto za kwenye ndoa kwa wale waliotoa mimba mara Kwa mara,hizi ni changamoto za wakati wa kufanya tendo na mme wake au mtu mwingine kwa ajili ya kupata mtoto.
Changamoto za kwenye ndoa kwa wale waliotoa mimba mara Kwa mara.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa wale waliotoa mimba mara Kuna kipindi wakati wakiwa tayari kwenye maisha yao na kutaka kuanza maisha Kuna mambo ambayo wanakutana nayo katika tendo la ndoa changamoto hizo ni kama zifuatazo.
.
2. Uke kuwa mkavu.
Kwa wale waliotoa mimba mara Kwa mara Kuna uwezekano wa uke kuwa mkavu hii inawezekana kwa sababu mbalimbali au ni kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi kwa sababu ya kutembea na waume wengi au pengine ni kwa sababu ya matumizi ya madawa mbalimbali yenye kemikali yanayoingizwa kwenye uke kwa sababu ya kutoa mimba , kwa hiyo mama hawezi kufurahia tendo kwa sababu ya kuwepo kwa uke mkavu na pia mwanaume anaweza kutoka nje ya ndoa kwa sababu ya kukutana na ukavu kila siku.
3. Kuwepo kwa hali ya kupungua kwa hamu ya kushiriki tendo la ndoa.
Kwa Sababu kwenye uke Kuna ukavu na pia wakati wa tendo la ndoa ni lazima kunakuwepo na maumivu makali sana kwa hiyo inakuwa vigumu sana na pia mama au dada anakosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa hali inayopelekea kuwepo kwa kutoelewana katika familia na vile vile usababisha mwanaume kutoka nje ya ndoa hali inayopelekea kuwepo kwa magonjwa mbalimbali kwenye familia , yaani kama vile kisonono, kaswende na magonjwa mbalimbali ya ngono kwa sababu ya kutoka nje ya ndoa.
4. Kwa mara nyingine kunakuwepo na hali ya kushindwa kufika kileleni na pia na kuwepo kwa maumivu wakati wa tendo la ndoa, kwa hiyo ni vizuri kabisa kwa akina dada kuwa makini katika maandalizi ya kuwa Mama kwa sababu kitendo cha siku Moja usababisha matatizo ya kudumu kwa hiyo ni vizuri kabisa walau kitumia niia za uzazi wa mpango kuliko kutumia ngono zembe na kusababisha kujiletea matatizo mbalimbali na kuweza kupata shida na masikitiko maisha Yako yote.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
dalili za uchungu kwa mama mjamzito
Makala hii itakwenda kukufundisha baadhi ya dalili za uchungu kwa mama mjamzito.
Soma Zaidi...Njia za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha.
Posti inahusu zaidi njia maalum za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha,Ni njia za uzazi ambazo wanaonyesha wanatumia kwa sababu kuna njia nyingine zikitumiwa na wanaonyonyesha zinaweza kuleta matatizo kwa watoto au kusababisha maziwa kutokuwa na vitamini v
Soma Zaidi...Madhara ya mwili kushindwa kutengeneza projestron ya kutosha
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo mtu anaweza kupata ikiwa mwili utaeweza kutengeneza progesterone ya kutosha.
Soma Zaidi...Hatari ya kutokwa na damu wakati wa ujauzito
Posti hii inahusu zaidi hatari za kutokwa na damu wakati wa ujauzito, hali hii utokea wakati wa ujauzito ambapo Kuna baadhi ya wajawazito utokwa na damu jambo ambalo hatupaswi kutarajia kwa sababu tunafahamu kabisa mama akishapata ujauzito na damu zinakom
Soma Zaidi...Upungufu wa homoni ya cortisol
Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni hii ya cortisol,hii ni homoni ambayo utokana na tezi glang(adrenal gland) kufanya kazi kupitiliza hali ambayo mara nyingi husababishwa na msongo wa mawazo wa mda mrefu, yaani wale watu ambao mda mwingi huwa wenye
Soma Zaidi...