image

Ijue timu ya upasuaji

Posti hii inahusu timu ya upasuaji hii ni timu ambayo inahusika katika chumba cha upasuaji, kwa sababu ya kutunza usafi na usalama chumba hiki kinapaswa juwa na timu ya watu wanne na walio na elimu kuhusu kazi hiyo.

Timu ya upasuaji.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa upasuaji ni hali ya kurekebisha sehemu fulani kwenye mwili au kutoa kiungo chochote kwenye mwili au kusafisha kutokana na uchafu ulio kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo kazi hii inahitaji usafi wa hali ya juu kabisa ili kuweza kuepuka Maambukizi kutoka kwenye mwili wa binadamu kwenda kwa mgonjwa kwa hiyo wafuatao ni wahudumu kwenye chumba cha upasuaji.

 

2. Mhudumu wa kwanza ni yule anayefanya usafi kwenye chumba cha upasuaji.

Huyu mhudumu sifa ya kwanza anapaswa kuwa ni  nesi aliyesajiliwa na kupata mafunzo kutokana na kazi hiyo kwa hiyo kazi yake ni kuhakikisha kuwa chumba kinakuwa kwenye hali ya usafi na hakuna vumbi yoyote ambayo inakuwepo kwenye chumba hicho na kuhakikisha kuwa kuna hewa inayopaswa kuwepo kwenye chumba hicho cha upasuaji.

 

3. Mhudumu mwingine ni msafisha vifaa vya upasuaji.

Tunajua wazi vifaa vinavyotumika kwenye upasuaji ni vifaa ambavyo utumika kwa mgonjwa mmoja na mwingine kwa hiyo mhudumu huyu anapaswa kuwa na elimu ya kutosha kuhusu kusafisha vyombo hivyo kwa hiyo kabla ya kufanya upasuaji anapaswa kuhakikisha kubwa vyombo vyote vipo na vinafanya kazi kwa hiyo vyombo hivyo visiposafishwa vizuri usababisha maambukizi kwa mgonjwa.

 

4. Mtoa huduma ya  usingizi.

Huyu ni mmojawapo ambaye anapaswa kutoa dawa ya usingizi kufuatana na mda ambao dawa inapoisha kwenye mwili wa mgonjwa kwa hiyo huyu ndiye anapaswa kuwaambia wafanya upasuaji kutumia mda ili upasuaji uishe kabla ya dawa kuisha kwenye mwili kwa hiyo huyu pia uhakikisha kuwa mgonjwa anapumua vizuri na mapigo ya moyo yako sawa na kuhakikisha kuwa  upasuaji unaenda vizuri.

 

5. Mfanya upasuaji au kwa jina lingine ni daktari.

Huyu ni mhusika mkuu wa upasuaji ambaye ndiye anakuwa ana utaalamu katika upasuaji kwa sababu anakuwa na ujuzi kwa hiyo wahudumu wengine wanapaswa kumsaidia sana kwa sababu ya shughuli kubwa aliyonayo kwa hiyo huyu anapaswa kuwa na ujuzi wa kutosha kabisa

 

 

 



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/02/05/Saturday - 09:52:34 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1070


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Zijue sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji
Post hii inahusu zaidi sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji, chumba cha upasuaji kina sehemu kuu nne na sehemu hizo ufanya kazi tofauti tofauti kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

ilinde Afya yako
Hiki ni kitabu kilichosheheni masomo zaidi kuhusu Afya yako, vyakula pamoja na maradhi sugu. Soma Zaidi...

dondoo 100 za Afya
Basi tambua haya;- 61. Soma Zaidi...

AFYA NA MAGONJWA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

matunda na mboga
Soma Zaidi...

Dondoo za afya 81-100
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dondoo za afya Soma Zaidi...

kitabu cha afya
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...

kitabu cha afya
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...

darasa la lishe
Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe Soma Zaidi...

Mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji
Posti hii inahusu zaidi mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji ni mambo muhimu ambayo yanapaswa kufanyika kwanza na baadaye upasuaji unaweza kuendelea. Soma Zaidi...

MAGONJWA 7 YALETWAYO NA MBU: MALARIA, DENGUE, HOMA YA ZIKA, HOMA YA MANJANO
Soma Zaidi...

KITABU HA MATUNDA
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...