Ijue timu ya upasuaji
Posti hii inahusu timu ya upasuaji hii ni timu ambayo inahusika katika chumba cha upasuaji, kwa sababu ya kutunza usafi na usalama chumba hiki kinapaswa juwa na timu ya watu wanne na walio na elimu kuhusu kazi hiyo.
Timu ya upasuaji.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa upasuaji ni hali ya kurekebisha sehemu fulani kwenye mwili au kutoa kiungo chochote kwenye mwili au kusafisha kutokana na uchafu ulio kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo kazi hii inahitaji usafi wa hali ya juu kabisa ili kuweza kuepuka Maambukizi kutoka kwenye mwili wa binadamu kwenda kwa mgonjwa kwa hiyo wafuatao ni wahudumu kwenye chumba cha upasuaji.
2. Mhudumu wa kwanza ni yule anayefanya usafi kwenye chumba cha upasuaji.
Huyu mhudumu sifa ya kwanza anapaswa kuwa ni nesi aliyesajiliwa na kupata mafunzo kutokana na kazi hiyo kwa hiyo kazi yake ni kuhakikisha kuwa chumba kinakuwa kwenye hali ya usafi na hakuna vumbi yoyote ambayo inakuwepo kwenye chumba hicho na kuhakikisha kuwa kuna hewa inayopaswa kuwepo kwenye chumba hicho cha upasuaji.
3. Mhudumu mwingine ni msafisha vifaa vya upasuaji.
Tunajua wazi vifaa vinavyotumika kwenye upasuaji ni vifaa ambavyo utumika kwa mgonjwa mmoja na mwingine kwa hiyo mhudumu huyu anapaswa kuwa na elimu ya kutosha kuhusu kusafisha vyombo hivyo kwa hiyo kabla ya kufanya upasuaji anapaswa kuhakikisha kubwa vyombo vyote vipo na vinafanya kazi kwa hiyo vyombo hivyo visiposafishwa vizuri usababisha maambukizi kwa mgonjwa.
4. Mtoa huduma ya usingizi.
Huyu ni mmojawapo ambaye anapaswa kutoa dawa ya usingizi kufuatana na mda ambao dawa inapoisha kwenye mwili wa mgonjwa kwa hiyo huyu ndiye anapaswa kuwaambia wafanya upasuaji kutumia mda ili upasuaji uishe kabla ya dawa kuisha kwenye mwili kwa hiyo huyu pia uhakikisha kuwa mgonjwa anapumua vizuri na mapigo ya moyo yako sawa na kuhakikisha kuwa upasuaji unaenda vizuri.
5. Mfanya upasuaji au kwa jina lingine ni daktari.
Huyu ni mhusika mkuu wa upasuaji ambaye ndiye anakuwa ana utaalamu katika upasuaji kwa sababu anakuwa na ujuzi kwa hiyo wahudumu wengine wanapaswa kumsaidia sana kwa sababu ya shughuli kubwa aliyonayo kwa hiyo huyu anapaswa kuwa na ujuzi wa kutosha kabisa
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 ai web app 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Habari za uzima,nimesoma makala yako tumbo linaniuma upande wa kulia Ila sisikii Sana yenyewe Ila nikibonyeza na mkono ndio inauma yaani ni Kama nimegongwa sehem flani alafu Kuna maumivu lakini ni mpaka upaguse ndio una experience maumivu Kama Kuna namna
Kama unasumbuliwana tumbo upande wa kulia, kushoto, kitomvuni ama kuoande wa kuliavkwachini, basi muulizaji huyu atakupa uelewa.
Soma Zaidi...Fahamu mtindo mzuri wa maisha
Postei hizi inahusu zaidi mtindo mzuri wa maisha, yaani mtu ale ki vipi au afanyeni nini ili kuweza kuboresha afya yake.
Soma Zaidi...AFYA NA MAGONJWA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...