picha

Ijue timu ya upasuaji

Posti hii inahusu timu ya upasuaji hii ni timu ambayo inahusika katika chumba cha upasuaji, kwa sababu ya kutunza usafi na usalama chumba hiki kinapaswa juwa na timu ya watu wanne na walio na elimu kuhusu kazi hiyo.

Timu ya upasuaji.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa upasuaji ni hali ya kurekebisha sehemu fulani kwenye mwili au kutoa kiungo chochote kwenye mwili au kusafisha kutokana na uchafu ulio kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo kazi hii inahitaji usafi wa hali ya juu kabisa ili kuweza kuepuka Maambukizi kutoka kwenye mwili wa binadamu kwenda kwa mgonjwa kwa hiyo wafuatao ni wahudumu kwenye chumba cha upasuaji.

 

2. Mhudumu wa kwanza ni yule anayefanya usafi kwenye chumba cha upasuaji.

Huyu mhudumu sifa ya kwanza anapaswa kuwa ni  nesi aliyesajiliwa na kupata mafunzo kutokana na kazi hiyo kwa hiyo kazi yake ni kuhakikisha kuwa chumba kinakuwa kwenye hali ya usafi na hakuna vumbi yoyote ambayo inakuwepo kwenye chumba hicho na kuhakikisha kuwa kuna hewa inayopaswa kuwepo kwenye chumba hicho cha upasuaji.

 

3. Mhudumu mwingine ni msafisha vifaa vya upasuaji.

Tunajua wazi vifaa vinavyotumika kwenye upasuaji ni vifaa ambavyo utumika kwa mgonjwa mmoja na mwingine kwa hiyo mhudumu huyu anapaswa kuwa na elimu ya kutosha kuhusu kusafisha vyombo hivyo kwa hiyo kabla ya kufanya upasuaji anapaswa kuhakikisha kubwa vyombo vyote vipo na vinafanya kazi kwa hiyo vyombo hivyo visiposafishwa vizuri usababisha maambukizi kwa mgonjwa.

 

4. Mtoa huduma ya  usingizi.

Huyu ni mmojawapo ambaye anapaswa kutoa dawa ya usingizi kufuatana na mda ambao dawa inapoisha kwenye mwili wa mgonjwa kwa hiyo huyu ndiye anapaswa kuwaambia wafanya upasuaji kutumia mda ili upasuaji uishe kabla ya dawa kuisha kwenye mwili kwa hiyo huyu pia uhakikisha kuwa mgonjwa anapumua vizuri na mapigo ya moyo yako sawa na kuhakikisha kuwa  upasuaji unaenda vizuri.

 

5. Mfanya upasuaji au kwa jina lingine ni daktari.

Huyu ni mhusika mkuu wa upasuaji ambaye ndiye anakuwa ana utaalamu katika upasuaji kwa sababu anakuwa na ujuzi kwa hiyo wahudumu wengine wanapaswa kumsaidia sana kwa sababu ya shughuli kubwa aliyonayo kwa hiyo huyu anapaswa kuwa na ujuzi wa kutosha kabisa

 

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 1868

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Dondoo za afya 41-60

Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya

Soma Zaidi...
Nguo zinazovaliwa kwenye chumba cha upasuaji na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi nguo za kuvaliwa kwenye chumba cha upasuaji na kazi zake, hizi ni nguo ambazo wahudumu wa afya wanapaswa kuzivaa wakati wa upasuaji kwa ajili ya kuwakinga na Maambukizi kati ya wahudumu wa afya na wagonjwa pia

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji, ni mbinu mbalimbali ambazo utumika ili kujaribu kuepuka Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kuvaa nguo za upasuaji.

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa nguo za upasuaji, tunajua wazi kuwa, wakati wa upasuaji tunapaswa kusafisha chumba na mazingira yake lengo ni kuhakikisha kuwa tunazuia wadudu wasisambae au kuingia kwenye mwili wa binadamu.

Soma Zaidi...
AINA ZA VYAKULA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
SHUGHULI ZA KILA SIKU

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...