Madhara kwa wasiofanya mazoezi
Posti hii inahusu zaidi madhara mbalimbali ambayo yanaweza kutokea kwa watu wasiofanya mazoezi, mazoezi ni kama tiba kwa namna Moja au nyingine ila Kuna madhara ambayo yanaweza kutokea kwa wale ambao hawafanyi mazoezi.
Madhara kwa wasiofanya mazoezi.
1. Kuwepo kwa magonjwa mbalimbali ya kuambukizwa.
Kwa sababu ya kutofanya mazoezi Kuna hatari ya kuwepo kwa magonjwa mbalimbali yasiyoambukizwa magonjwa hayo ni pamoja na saratani mbalimbali, mshutuko wa moyo na kisukari hayo ni baadhi ya magonjwa ambayo yanaweza kutokea kwa watu ambao hawafanyi mazoezi.
2. Kuwepo kwa Uzito mkubwa na unene wa kupitiliza.
Kwa sababu ya kuwepo kwa mafuta kwenye mwili Kuna hatari ya kuwepo kwa uzito mkubwa na uliopitiliza kwa sababu kila kitu kinachoingia mwilini ukaa humo humo na hakitoki mwilini hali inayosababisha kuwepo kwa uzito mkubwa na unene wa kupitiliza.
3. Pia kutofanya mazoezi usababisha kuwepo kwa presha .
Kwa sababu ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha mafuta kwenye mwili usababisha mishipa kuziba na upelekea kuwepo kwa presha kw watu ambao hawafanyi mazoezi.
4. Pia kwa wale wasiofanya mazoezi wanaweza kuwa na matatizo katika upumuaji.
Kwa sababu ya kuwepo kwa mazoezi usaidia vile vile kuweka kifua kwenye hali nzuri na pia mapafu yanakuwa na uwezo wa kupitisha hewa Vizuri kabisa bila shida yoyote, ila kwa wale wasiofanya mazoezi ni vizuri kabisa kufahamu kwamba wanaweza kupata matatizo mbalimbali katika upumuaji.
5.vile vile kwa wale wasiofanya mazoezi wanaweza kupata matatizo ya kuwepo kwa cholesterol kwenye mwili kwa sababu cholesterol usababishwa na kuwepo kwa kiwango cha mafuta mwilini kwa hiyo kwa wale wanaofanya mazoezi hawawezi au ni vigumu kupata tatizo hili kwa hiyo ni vizuri kabisa kufanya mazoezi Ili kuepukana na tatizo la kuwepo kwa cholesterol mwilini.
6. Pia kwa wale wasiofanya mazoezi Wana uwezekano wa kupata na maradhi ya mara Kwa mara kama vile mafua, kikohozi vi homa homa vya kila wakati na magonjwa madogo madogo kwa hiyo ni vizuri kabisa kufanya mazoezi Ili kujiepusha na matatizo mbalimbali kwenye mwili.
7. Pia kwa wale wasiofanya mazoezi miili yao huwa mizito na pia mifsuli pamoja na mifupa huwa laini kwa hiyo ni vizuri kabisa kufanya mazoezi Ili kuweza kujiepusha na hali ya kuwepo kwa ulaini kwenye mifupa na misuli
8 . Kwa wale wasiofanya mazoezi jitahidi walau kutafuta kitu chochote cha kukufanyaa utoe jasho kwa sababu mazoezi ni dawa na pia mazoezi ni kinga ni vizuri kabisa kufanya mazoezi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Kitabu cha Afya 03
Yajuwe mambo yanayoathiri afya ya miili yetu, jifunze mambo mengi kuhusu afya.
Soma Zaidi...Jinsi ya kuondokana na uraibu wa mtandao na simu (Digital detox).
Uraibu wa kidijitali unazidi kupoteza umakini, amani ya akili na muda wetu wa thamani. Makala haya yanakupa mbinu madhubuti za kufanya "Digital Detox" (mapumziko ya kidijitali) ili uweze kupunguza matumizi ya simu na kuishi maisha halisi yenye tija.
Soma Zaidi...Jinsi ya kuhesabu siku za hatari za kupata mimba.
Kujua siku zako za hatari (siku ambazo una uwezekano mkubwa wa kupata mimba) ni njia muhimu sana kwa wanandoa wanaopanga kupata mtoto. Siku hizi hutegemea mchakato wa kupevuka kwa yai (ovulation), ambapo yai huachiliwa kutoka kwenye ovari ili kurutubishwa. Makala hii inaelezea mbinu rahisi ya kalenda unayoweza kutumia.
Soma Zaidi...