picha

Madhara kwa wasiofanya mazoezi

Posti hii inahusu zaidi madhara mbalimbali ambayo yanaweza kutokea kwa watu wasiofanya mazoezi, mazoezi ni kama tiba kwa namna Moja au nyingine ila Kuna madhara ambayo yanaweza kutokea kwa wale ambao hawafanyi mazoezi.

Madhara kwa wasiofanya mazoezi.

1. Kuwepo kwa magonjwa mbalimbali ya kuambukizwa.

Kwa sababu ya kutofanya mazoezi Kuna hatari ya kuwepo kwa magonjwa mbalimbali yasiyoambukizwa magonjwa hayo ni pamoja na saratani mbalimbali, mshutuko wa moyo na kisukari hayo ni baadhi ya magonjwa ambayo yanaweza kutokea kwa watu ambao hawafanyi mazoezi.

 

2. Kuwepo kwa Uzito mkubwa na unene wa kupitiliza.

Kwa sababu ya kuwepo kwa mafuta kwenye mwili Kuna hatari ya kuwepo kwa uzito mkubwa na uliopitiliza  kwa sababu kila kitu kinachoingia mwilini ukaa humo humo na hakitoki mwilini hali inayosababisha kuwepo kwa uzito mkubwa na unene wa kupitiliza.

 

3. Pia kutofanya mazoezi usababisha kuwepo kwa presha .

Kwa sababu ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha mafuta kwenye mwili usababisha mishipa kuziba na upelekea kuwepo kwa presha kw watu ambao hawafanyi mazoezi.

 

4. Pia kwa wale wasiofanya mazoezi wanaweza kuwa na matatizo katika upumuaji.

Kwa sababu ya kuwepo kwa mazoezi usaidia vile vile kuweka kifua kwenye hali nzuri na pia mapafu yanakuwa na uwezo wa kupitisha hewa Vizuri kabisa bila shida yoyote, ila kwa wale wasiofanya mazoezi ni vizuri kabisa kufahamu kwamba wanaweza kupata matatizo mbalimbali katika upumuaji.

 

5.vile vile kwa wale wasiofanya mazoezi wanaweza kupata matatizo ya kuwepo kwa cholesterol kwenye mwili kwa sababu cholesterol usababishwa na kuwepo kwa kiwango cha mafuta mwilini kwa hiyo kwa wale wanaofanya mazoezi hawawezi au ni vigumu kupata tatizo hili kwa hiyo ni vizuri kabisa kufanya mazoezi Ili kuepukana na tatizo la kuwepo kwa cholesterol mwilini.

 

6. Pia kwa wale wasiofanya mazoezi Wana uwezekano wa kupata na maradhi ya mara Kwa mara kama vile mafua, kikohozi vi homa homa vya kila wakati na magonjwa madogo madogo kwa hiyo ni vizuri kabisa kufanya mazoezi Ili kujiepusha na matatizo mbalimbali kwenye mwili.

 

7. Pia kwa wale wasiofanya mazoezi miili yao huwa mizito na pia mifsuli pamoja na mifupa huwa laini kwa hiyo ni vizuri kabisa kufanya mazoezi Ili kuweza kujiepusha na hali ya kuwepo kwa ulaini kwenye mifupa na misuli 

 

8 . Kwa wale wasiofanya mazoezi jitahidi walau kutafuta kitu chochote cha kukufanyaa utoe jasho kwa sababu mazoezi ni dawa na pia mazoezi ni kinga ni vizuri kabisa kufanya mazoezi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/07/20/Wednesday - 07:39:54 am Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 3228

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

KWA NINI MBU HAWEZI KUAMBUKIZA HIV (UKIMWI)

Tumekusha kuona na kujua kuwa mbu anaweza kuambukiza maradhi mengi na ya virusi kama zika.

Soma Zaidi...
VIZAZI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Kitabu cha Afya 03

Yajuwe mambo yanayoathiri afya ya miili yetu, jifunze mambo mengi kuhusu afya.

Soma Zaidi...
Namna ya kutunza chumba cha upasuaji

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza chumba cha upasuaji, chumba cha upasuaji ni tofauti na vyumba vingine kwenye hospitali kwa hiyo vinahitaji uangalizi wa hali ya juu sana ili kuepuka aina yoyote ya uchafu kuwepo kwenye chumba hicho, zifuatazo ni na

Soma Zaidi...
AFYA NA MAGONJWA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Kujiandaa kwa ajili ya kumuona daktari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya mambo ya kujiandaa kwa ajili ya kumuona daktari

Soma Zaidi...
Madhara ya kutumia tissue au toilet paper

Post hii inahusu zaidi madhara ambayo tunaweza kuyapata katika matumizi ya toilet paper au tisu kwenye sehemu za siri.

Soma Zaidi...
DARASA LA AFYA, AFYA YA UZAZI, MARADHI NA LISHE BORA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...