Eda ya Kufiwa
Eda ni kipindi cha kungojelea mwanamke baada ya kupewa talaka au baada ya kufiwa na mumewe. Katika kipindi cha eda ni haramu mwanamke kuolewa na mume mwingine. Ambapo tumejifunza kuwa eda ya kuachwa inaisha baada ya twahara tatu au miezi mitatu (kwa wale wasiopata hedhi) au baada ya kujifungua (kwa mke aliyeachwa), eda ya kuachwa inachukua miezi minne na siku kumi au siku mia moja thelathini (130).
Hukumu ya Eda ya kufiwa inabainishwa katika Qur-an:
Na wale wanaofishwa (wanaokufa) miongoni mwenu na kuacha wake; hawa (wake) wangoje (wasiolewe) miezi mine na siku kumi. Na wanapofikia muda wao (wa kumaliza eda yao hiyo), basi si dhambi juu yenu kwa yale wanayoyafanyia nafsi zao (hao wanawake) kwa yanayowafiki (kufuata) Sharia. Na Mwenyezi Mungu anazo habari za yote mnayoyatenda. Wala Si dhambi kwenu katika kupeleka habari ya posa kwa ishara tu (Si kwa maneno) kuwaoa wake (walio edani), wala (hapana dhambi pia) katika kutia katika nyoyo zenu azma (za kuwaoa) Mwenyezi Mungu anajua kwamba nyinyi mtawakumbuka.
Lakini msifunge nao ahadi kwa Sifl (ya kuwaoa maadam eda haijesha) isipokuwa mseme maneno yaliyo mazuri. Wala msiazimie kufunga ndoa mpaka muda uliyoandikwa (katika eda) ufike mwisho wake. Na jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo katika nafsi zenu, basi mwogopeni. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, (na) Mpole sana. (2:234-235)
Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa kizuka (mwanamke aliyefiwa na mumewe) anapokuwa katika eda harusiwi kuolewa wala hata kuposwa wala hata kudhihirishiwa nia ya kuolewa baada ya eda. Bali ni ruhusa kuweka azma moyoni na kuongea naye kwa wema bila kuidhihirisha azma hiyo.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inakwenda kukufundisha njia zinazotumika kujitwaharisha.
Soma Zaidi...عَنْ ابْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم "لَا يَحِلُّ دَمُ امْرِئٍ مُسْلِمٍ [ يشهد أن ل?...
Soma Zaidi...Hapa utajifunza muda wa kutia jia katika funga za sunnah. Pia utajifunza kuhusu uhuru ulio nao
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu: Shahada (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Hspa utajifunza viwango maalumu vya kutithi mirathi ys kiislamu.
Soma Zaidi...(ii) Hatua za Kuzuia Uzinzi JamiiUislamu pamoja na kutoa mafunzo ya maadii yanayomuwezesha mtu binafsi ajiepushe kwa hiari yake na kitendo kibaya cha zinaa, umechukua hatua mbali mbali ambazo huifanya zinaa isiwe kitendo chepesi katika jamii.
Soma Zaidi...Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.
Soma Zaidi...Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3:Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...