Tutazungumzia: Makundi ya vyakula rafiki kwa mgonjwa wa kisukari. Namna ya kuchagua chakula chenye sukari ndogo kwa mwili. Mifano ya vyakula vya kula na vile vya kupunguza.
Mtu mwenye kisukari anahitaji kula vyakula vinavyoleta uwiano mzuri wa sukari kwenye damu, visivyopandisha kiwango cha sukari kwa haraka, na vinavyosaidia mwili kufanya kazi kwa utulivu. Hii huitwa kula vyakula vyenye glycemic index ya chini au ya kati.
Hivi ndivyo vyakula muhimu zaidi kwa mwenye kisukari.
Mfano:
Spinachi
Kabichi
Karoti (kwa kiasi)
Brokoli
Sukuma
Hivi vina nyuzinyuzi nyingi, vitamini na hupandisha sukari polepole sana.
Mfano wa nafaka rafiki ni kama:
brown rice
Oats
Uji wa mtama
Uwele
Ngano nzima (whole wheat)
Nafaka hizi huongeza sukari taratibu kwa sababu ya fiber nyingi.
Protini husaidia kushibisha bila kuongeza sukari.
Zingatia:
Mayai
Samaki
Nyama isiyo na mafuta mengi
Kuku bila ngozi
Maharage, dengu, choroko, kunde
Matunda yana sukari ya asili, hivyo kiasi ni muhimu.
Mifano mizuri:
Tikiti maji (kiasi kidogo)
Embe (kiasi)
Papai
Maembe mabichi
Mapera
Strawberries, blueberries, apples, pears
Epuka kula matunda kwa wingi kwa mara moja. Gawa mara mbili hadi tatu kwa siku.
Mafuta ya asili yana msaada kwa moyo na hupunguza sukari kupanda.
Mzuri kula kwa kiasi:
Avocado
Karanga
Mbegu (chia, maboga, alizeti)
Mafuta ya zeituni
Chagua:
Mtindi usio na sukari
Maziwa fresh bila sukari
Cheese kwa kiasi
Kunywa maji mengi kuliko vinywaji vya sukari. Epuka soda, juisi zilizoongezwa sukari na vinywaji vya kuongeza nguvu.
Kula kiasi na kupanga muda wa kula ni muhimu zaidi kuliko chakula chenyewe? Kwa mfano, mtu akila chakula kizuri lakini kingi kwa mara moja, sukari bado inaweza kupanda.
Vyakula bora kwa mwenye kisukari ni vile vyenye fiber nyingi na sukari ndogo.
Mboga, nafaka nzima, protini nyepesi na matunda kwa kiasi ndizo msingi wa mlo mzuri.
Epuka sukari nyingi, vyakula vilivyosindikwa na mafuta mengi mabaya.
Kila mlo ugawiwe vizuri: mboga nyingi, wanga kidogo, protini kiasi.
Kunywa maji ya kutosha kila siku.
Umeionaje Makala hii.. ?
Je umesha wahi kujiuliza kuwa ni vinywaji vipi mwenye presha ya kupanda anafaha kutumia, Unadhani ni maji, mvinyo wa pombe, chai na kahawa. Bila shaka ungependa kujuwa zaidi kuhusu jambo hili. Makala hii ni kwa ajili yako
Soma Zaidi...Somo hili litakwenda kukueleza kuhusu faida za kula zabibu na umuhimu wake kiafya
Soma Zaidi...Posti hii inaonyesha Faida za kula papai.papai Ni tunda na Lina leta afya,nguvu na kuujenga mwili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Ukosefu wa madini ya Shaba mwilini, ni Ukosefu wa madini ya Shaba mwilini ambao usababisha madhara kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Makala hii inakwenda kukupa elimu juu ya vyakula na vinywaji vilivyo salama kwa mtu mwenye kisukari, na ni vyakula vipi ni hatari kwa mwenye kisukari. Pia utajifunza njia za kujilinda na kupata kisukari.
Soma Zaidi...