Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)

Kwa tabia zake njema Yusufu(a.

Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)

Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)


Kwa tabia zake njema Yusufu(a.s) alipendwa sana na baba yake. Ndugu zake Yusufu(a.s) wakajawa chuki na husuda wakijadiliana kuwa;


...............Hakika Yusufu na nduguye wanapendwa sana na baba kuliko sisi, hali sisi ni kundi lenye nguvu. Hakika baba yetu yumo katika upotofu ulio wazi.(12:8)



Wakapanga njama za kumhujumu Yusufu (a.s) kwa kumuua ili mapenzi ya baba yao yawageukie wao. Wakapanga na kuazimia kuwa:



Muueni Yusufu au mtupeni nchi za mbali ili uso wa baba yenu ukuelekeeni na baada ya haya mtakuwa watu wema. (12:9)



Hatimaye wakakubaliana kumtumbukiza kisimani badala kumwua,wazo hili lilitolewa na mmoja wao ambaye angalau aliogopa kubeba dhima ya kufanya dhambi kubwa ya kuiua nafsi pasina haki. Akasema;



Msimuue Yusufu lakini mtupeni Yusufu katika(jiwe la ndani) ya kisima kirefu, watamuokota baadhi ya wasafiri, kama ninyi mnataka kufanya kitu.(12:10)



Yusufu anatumbukizwa kisimani

Kutumbukizwa Yusufu(a.s) Kisimani Pamoja na kuwa na dhamira ile mbaya ya kutaka kufanya kosa la kuua mtu asiyekuwa na hatia , wakaongeza kosa lingine la kusema uwongo. Wakasema:


........Ewe baba yetu, mbona hutuamini juu ya Yusufu, hakika sisi ni wenye kumtakia mema. Mruhusu kesho pamoja nasi atakula kwa furaha na kucheza; hakika sisi tutamlinda (12:11-12)



Ingawa mzee Ya'aquub(a.s) alionesha wasiwasi,lakini hatimaye aliwaruhusu waandamane naye. Walimtumbukiza Yusufu(a.s) kisimani kama walivyo dhamiria na wakaichukua kanzu yake na kuipakaza damu za uwongo, kisha wakamuongopea baba yao:



Ewe baba yetu! Hakika sisi tulikwenda kushindana mbio na tukamuacha Yusufu penye vyombo vyetu, basi mbwa mwitu akamla; lakini hutatuamini ingawa tunasema kweli (12:17)

Ya'aquub(a.s.) alikuwa na mategemeo makubwa ya kupata mrithi bora atakayeendeleza kazi yake. Hata hivyo hatumwoni mzee Ya'aquub akikata tamaa kwa kufadhaika au kukufuru. Yeye akawajibu;

......



'..............Nafsi zenu zimekushawishini jambo. Basi (langu mimi ni) subira njema; na Mwenyezi Mungu ndiye aombwaye msaada kwa haya mnayoyasema' (12:18).

Hii ndio tabia ya Muislamu. Kurejea na kumtegemea zaidi Allah(s.w) afikwapo na msiba.



                   

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 168

Post zifazofanana:-

NINI MAANA YA KUSIMAMISHA SWALA, KATIKA UISLAMU (NI YUPI TARQU SWALA) yaani mwenye kuacha swala)
Kusimamisha Swala. Soma Zaidi...

HADITHI YA CHONGO WA TATU MTOTO WA MFALME
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA CHONGO WA TATU MTOTO WA MFALME Mimi ni mtoto wa mfalme kama nilivyotangulia kusema na ni mtoto wa kipekee kwa baba na mama. Soma Zaidi...

Dawa na matibabu ya presha ya kushuka
Hapa utajifuanza dalili za presha ya kushuka, na dawa ya presha ya kushuka na nJia za kuzuiaama kudhibiti presha ya kushuka Soma Zaidi...

hukumu ya ombaomba katika uchumi wa kiislamu
Suala la omba-ombaTukiliangalia suala la omba-omba kwa upana kidogo, ambalo hivi sasa linaongelewa katika vikao mbalimbali vya kitaifa na kimataifa, tutaona kuwa ni Uislamu pekee unaotoa namna bora ya kulishughulikia suala hili. Soma Zaidi...

Haki na wajibu kwa mayatima
Soma Zaidi...

Musa(a.s) Ahamia Madiani
Mchana wa siku moja Musa(a. Soma Zaidi...

Vyakula vyenye vitamini C kwa wingi
Vitamini C kwa wingi hupatikana kwenye machungwa, maembe, mananasi, limao na ndimu Soma Zaidi...

Kitabu Cha Kiapo Cha Mfalme
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Fahamau protini na kazi zake, vyakula vya protini, na athari za upungufu wake.
unayopaswa kuyajuwa kuhusu protini na vyakula vya protini, faida zake na hasara zake. Madhara ya kiafya yanayohusiana na protini pamoja na kuyaepuka madhara hayo Soma Zaidi...

Hoja juu ya hitajio la kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango
Soma Zaidi...

Njia haramu za uchumi
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SULEIMAN
Soma Zaidi...